UTEUZI: Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Prof. Mohamed Yakubi Janabi kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Muhimbili.
Prof. Janabi alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI)
Prof. Janabi anachukua nafasi ya Prof. Lawrence Maseru ambaye amestaafu.
Aidha Rais Samia amemteua Dkt. Peter R. Kisenge kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete.
Dkt. Kisenge anachukua nafasi ya Prof. Janabi.
Kabla ya uteuzi, Dkt. Kisenge alikuwa Mkurugenzi wa Tafiti na Mafunzo wa (JKCI).
View attachment 2361054