UTEUZI: Rais Samia Suluhu amteua Balozi Hussein A. Kattanga kuwa Katibu Mkuu Kiongozi, Dkt. Bashiru Ali ateuliwa kuwa Mbunge

Nimekuelewa mkuu[emoji122][emoji122]
 
Mama sio strong enough ku-deal na hawa watu.Huyu alipaswa kuachwa kam alivyo tu na si kupewa ubunge.

Msishangae akampa uwaziri.

Huyu mama sijui kama ataweza kulipiga chini lile kundi la SUKUMA GANG.
Bado wanacontrol wizara zile - Nishati na Madini
 
Mkuu kwa nini unatutusi, kwani sisi sio wa tz,?acha ubaguzi bwana
 
Kifupi Bashiru Ali katolewa kwenye Chama na Magufuli aachie chama wengine wenyewe wenye chama Na Raisi Samia kamtupa nje ya serikalu aende huko bungeni . now Case closed.Thanks Mama Samia

Watanzania tuko fit
 
Mkuu kwa nini unatutusi, kwani sisi sio wa tz,?acha ubaguzi bwana
Hapana Mkuu, ninyi ni watu wazuri sana waungwana mno sema yale mambo ya mpe mruke mpe mruke ndiyo ninayochukia.Ila sina tatizo kabisa na Wahaya
 
Ila siasa zinahitaji uvumilivu sana.Yaani kazi yake imeishia kuandaa kiapo cha makamu wa raisi na kutupwa nje kabisa ya mfumo.Maana kuna watu aliwapiga biti sana ndani ya serikali akiwa katibu mkuu.
 
Mkuu Katiba inatakiwa ibadirishwe yote siyo marekebisho..
Unaweza kumzomea mgombea urais wa chama furani kwenye kampeni, siku akishinda anakutafuta alikulipizie.
Utakula makonzi mpaka kichwa kichakae
Uko sahihi mkuu katiba hii ni mbovu sana
 
Watanzania usiwaone kimya sio wajinga kama nchi nyingi za jirani na nje wanavyotuona ukiona kobe kainama sio kalala au mjinga anatunga sheria au anawaza namna gani akutandike!
 
Mnisaidie tutaendelea kumuita Balozi Bashiru Ally au tutamuita mheshimiwa Bashiru Ally.
 
Kutoka Katibu Mkuu wa CCM, Katibu Mkuu Kiongozi hadi mbunge wa kuteuliwa hii inaitwa from GLORY to ASHES!
Wenzio wanaangali mpunga wewe unaangalia jina la cheo!

Tena hapo alipo ni mwendo wa mpunga hadi 2025
 
Bashiru mwezi wa 2 alikuwa anaishi nyumba ya Katibu mkuu CCM ya chama, mwezi wa 3 akahamia nyumba ya Katibu mkuu kiongozi na leo anahamia nyumbani kwake Msewe barabara ya chuo kikuu😂😂😂 Hakika huu ni utalii wa ndani.
 
Duh.....Yaani jamaa amedumu wiki 3 tu kwene nafasi hii ya KMK..!!!!!
Something big is being cooking!!! Kuna 2 things hapa:
  1. Yawezekana Bushiri Ali anatupwa Japan...!!
  2. Reshuffle ya Baraza la Mawaziri inanukia na huyu Bushiri akapachikwa kwenye Uwaziri au PM....???
Let's wait and see.......!!?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…