Uteuzi wa Makamba kama Waziri wa Nishati na aliyofanya alipoteuliwa umenifanya niwakataze watoto wangu kuchukua masomo ya Sayansi

Badala ya makamba ulitaka nani awe waziri wa nishati?
Sina mtu ninaemtaka bali nina sifa - ateuliwe mtu anaejua mambo ya sera na utawala wa nishati, na ana uzoefu wa kazi. Wapo Watanzania wenye hizo sifa mara kumi ya Makamba, au kwa sababu wao sio watoto wa Katibu Mkuu wa CCM mstaafu au hawakuwahi kuwa waandishi wa hotuba za raisi?
 
lakin kwa tz hili swala km la makamba sio round ya kwanz kufanyik tkea enzi za zaman yamefanyika ... kiufup tuyazoee tu
Aaah Mkuu, ndio maana hatuendi popote, umeme toka enzi na enzi na unashindwa kuzalisha umeme wa kutosha nchi yenyewe ndogo hivi na vyanzo vya umeme kibao, gesi, maji, makaa, upepom jua! Tatizo tunafikiri kama mtu aliandika hotuba nzuri basi ataweza kuwa waziri mzuri, hata kama wizara ni ya nishati inayohitaji mtu mahili. Mtu mwenye sifa zake kama ni lazima awe waziri, basi si wampe uwaziri wa elimu hivi? Kwani atakuwa waziri nusu akiwa elimu?
 
hii africa haiwez kuendelea km tutakuw na viongoz sampe hii labda kizazi hiki chote kife kizaz kijach uend kikalet mabadiliko
 
Hawa nguini silaha yao Ni uchawa ama kujipendekeza Ina Mana kwa huyo wanayejipendekeza kwake angetaka mlango wowote kuingiza foreign invader mwilini mwake nadhani asingekataliwa.


Africa Ni siasa ndio ama uswahili ndio unaongoza nchi.
 
Yote haya yana mwisho wake.Umeandika vizuri sana ndugu yangu na kwa hisia.Mm huwa namlaumu sana Nyerere katika mambo haya yote yanayotokea Tanzania.Mwalimu Julius Nyerere alikuwa na mazuri yake ,lakini pia alikuwa na mabaya yake.Ingawa yeye alisema Kama Kuna mabaya mnisamehe.Wakati mwalimu anaondoka madarakani ,alitakiwa kutupatia katiba mpya .Na suala la katiba wapinzani wengi wa CCM wamekuwa wanalichukulia tu kuwa ni suala la kubali mifumo ya serikali ya CCM.Lakin katiba mpya ni kuwa na mifumo mizuri ya serikali na hata vyama kubadilika kabisa.Kama Mwalimu angetusaidia kuwa na katiba nzuri sana.Vyama vya upinzani viwe vya public visiwe vya watu .Hakika tusingekuwa na vilaza wengi ,kuongoza wasomi wazuri.Ila kila Jambo lina mwisho wake kwa njia yeyote tu watatoka na watafilisiwa.Angalia Angola.Nchi imeongozwa kwa miaka 38 na mtu mmoja.Lakin kwa sasa utawala ule haupo tena .Mungu ibaliki Tanzania.
 
Kweli kabisa ndugu yangu, maana hadi sasa maendeleo ya Tanzania yanafanyika kwa hulka ya kiongozi aliyeko madarakani, sio kwa mfumo ambao raisi yeyote atakaekuwapo ataufuata. Kila raisi anakuja na mambo yake na watuwake na interest zake.
 
Autopilot, kwakweli maana hata nchini kwenyew haonekanini safari kila kukicha[emoji1787]
 
Janabi.......???
 
Mpaka sasa bado sijapata mtu mwenye fact kuonesha makamba hafai ukilinganisha na watungulizi wake.Wengi wenu mnaleta hoja zisizo na fact yoyote.

Wakati fulani kuna watu walimzodoa makamba kwenye issue ya crane iliokua inahitajika kwenye mradi wa umeme wa Mwl Nyerere kwamba crane anayoeleza inapatikana nchini tena kutoka kwa makampuni ya kawaida,baada yakufuatilia kwa undani nilichokuja kubaini watu wengi huwa wanaleta hoja pasipo kupata fact zakutosha.

Hawa wanasansi wetu humu waliowengi wanachojua ni kuziba viraka tu tunawaona sehemu kibao lakini impact kwa nchi huwa ni zero.

Ukienda pale DIT kule nyuma karibu na makaburi ya kisutu utawakuta wanachuo wanajisomea huku wanavuta bangi maana yake hawa ndio sehemu ya hawa wanasayansi mnaowaona wa maana hapa.
 
Nchi inaharibiwa beyond repair.
 
Katika Historia ya sekta ya Nishati,ni January peke yake kama Waziri ambaye ameacha majukumu ya kusimamia sera za Nishati na kuwa Marketing Manager wa TaifaGas.
Lakini achilia mbali tuhuma za kuiba mituhani akiwa shule,iyo ni tisa; kumi ni kumuondoa Engineer Tito Kama DG wa TANESCO na kumpa shavu muuza vifurushi vya DSTv na mwisho kuondoa Bodi ya wataalaamu na kuteua Bankers kuwa wajumbe wa Bodi ya TANESCO.
Ila tuache masiala ili hii nchi ikae sawa lazima JWTZ walinde katiba na TISS wapoteze baadhi ya watu.
Otherwise,wacha tuendelee kuimba Iyenaiyena....
 
Lack of proper nutrition leads to mental retardation hence poor intelligence thinking!
Mkuu jitahidi kula vyakula vyenye lishe ya kutosha na vilevile kama unatumia jani,jaribu kulikausha kwanza.Asante!
 
Lack of proper nutrition leads to mental retardation hence poor intelligence thinking!
Mkuu jitahidi kula vyakula vyenye lishe ya kutosha na vilevile kama unatumia jani,jaribu kulikausha kwanza.Asante!
Dogo, sijaona hoja yoyote yenye mashiko hapa zaidi ya blah blah blah!
Pole.
 
Kwa hiyo suluhisho ni kupachika mtu yeyote kwenye wizara nyeti kama Nishati, kama Makamba?

Kama ambavyo ninapinga Makamba kwekwa Nishati, ndivyo ambavyo nilipinga Mwigule Nchemba kuwewa Mambo ya Ndani. Na ukimwondoa mtu kama Mwigulu pale fedha unkamweka Makamba nitakuona una ulevi wa namna fulani

Kuna wizara ambazo lazima uwe makini unamweka nani, mfano

  • Nishati,
  • Madini
  • Fedha
  • Sayansi na Technolojia
  • Afya
 
Elimu ya chuo kikuu inatakiwa iwape uwezo wa kufikiri na kupambanua mambo. Uwaziri na uongozi katika serikali unahitaji mtu anayesikiliza vizuri, anayeweza kuwasiliana na kueleweka vizuri na wananchi, vile vile awe mtu anayeweza kutatua matatizo ya wananchi. Uwaziri hauhitaji mtu kipanga shuleni au alisomea masomo gani- wananchi wanataka matatizo yatatuliwe. Tatizo la wasomi wengi wanakuwa na kiburi, hawasikilizi watu wasio wasomi wakifikiri kuwa wao wanajua kila kitu. Katika Wizara kuna wataalamu waliobobea ambao kama waziri akiwatumia na kuwaongoza vizuri watamsaidia kutatua matatizo. Tumeona madaktari wakipewa kuongoza wizara ya afya na kuboronga vibaya sana. Uongozi ni somo lingine kabisa ni mchangayiko wa sayansi , ungwini na kipaji.
 
Kwa hiyo tumweke Msukuma akaongoze wizara ya fedha basi. Anajua sana kusikiliza watu na kuwasiliana na wananchi, zaidi ya Mwigulu Nchemba.
 
Makamba anapiga kazi nzuri mno. Akimaliza mtamkumbuka kama mnavyomkumbuka kwenye viroba na mifuko ya plastic
.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…