Uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu Mpya wa TISS, Said H. Masoro, na Mtazamo wangu

Uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu Mpya wa TISS, Said H. Masoro, na Mtazamo wangu

Kiukweli Bwana Yericko lazima nikupe hongera kwa kuandika kitabu maana kuandika kitabu siyo mchezo. Lakini kwa sababu kitabu chako hukuandika kama matokeo ya utafiti kwa ajili ya taaluma, maelezo yako hayajasanifiwa (hayana peer review ya wataalam wa somo hilo). Kwa hiyo kitabu chako ni kama barua kwa wasomaji. Hii haina ubaya wo wote ila tu usitegemee kitabu kitumike kufanya mabadiliko makubwa.
Kwanza, suala la Usalama, ni suala la utawala. Kwa bahati mbaya sheria hiyo ilipotungwa uwezo unaotokana na uzoefu wa kiutawala katika ngazi za juu sana ulikuwa umeshatutoka. Pili, baada ya Siasa ya Vyama vingi kuanzishwa mwaka 1992, malengo ya kitaifa ya muda mrefu hayapewi kipaumbele na unajua suala la Usalama wa Taifa linahusu mstakabali waTaifa; ni la muda mrefu, si suala la kushinda uchaguzi ujao. Tatu, Usalama wa Taifa unahusu kuwa na mipango, mbinu za muda mrefu za, kulinda, kudumisha na ustawi wa nchi na watu wake. Sasa mambo muhimu hapo ni mengi: mipaka, afya ya jamii, elimu na vipaji vya jamii, sayansi na kuangalia masuala ya sasa yatakavyoathiri Taifa baadaye na kupendekeza mikakati. Nne, utaona hapo kuwa kila nchi usalama wake utatokana na historia ya nchi na taifa lilivyozuka, umakini wa watawala kuhusu mustakabali wa Taifa na uwezekano wa kuwa na uongozi, uendeshaji na zana ambazo ni zaidi ya wastani wa Taifa katika Idara yenyewe. Mwisho, itategemea hao viongozi wa kisiasa wa awamu mbalimbali wamejaliwa vipi katika kuelewa na kutambua masuala haya ya muda mrefu.
Kwa hiyo uchumi ni kipengele kimoja cha kati. IQ ya Mtanzania inashuka au inapanda pengine ndiyo suala la kwanza; na kama haipandi sababu ni nini? lishe, elimu, uongozi au hujuma!?
SAHIHI.

Na >'jicho la kuona kote na mote'< ni kitu chenye nasibu ya 'kucheza Mungu'...

Ndiyo maana taasisi zote za namna hii duniani huvutia watu wema na wabaya; na wetu wengi wangalipenda kuwa taasisini kwa ajili ya 'mambo ya upendeleo' kwa wale watu walio nyuma ya pazia...

Siku za mbele, ushamba wa 'usiri wa mambo' na 'siasa za nyuma ya pazia' vitakoma. Kuna mambo yamekuwa ni sanaa na taaluma za >'Taasisi Jicho--Taasisi Mwewe'<--vile kuona mapana na vipenyo kana vile kutoka juu, isivyo wa wengi walio tambarareni; tena juu ya sera za nchi zenye kutawala uhai wa taifa, yatakuwa maarifa ya kawaida ya kila mtu, kila raia, kila 'mja mwema'...

Tupo kwenye >zama mpya< ya maendelo na hatua za kibinadamu ambamo 'tabia za kishirika' zenye kufanyakazi na kustawi kwa 'sanaa na usiri/siri' zitakuwa si zenye 'manufaa' ya ukweli ila 'mning'inio' wa vilevi vya kizamani...

Kwa hivyo ni kweli, suala la maendeleo yakweli na bora--pia makusudi kwa stawi za mapana ya jamii ni hitaji kwa dhamira ya dhati katika kujipambanua kutoka kwenye 'siasa za tawala' kuelekea kwenye 'uongozi wa kweli' wa jamii...

Amerika, Merekani, wametaasisha idara zao za uono mifumo kwa alama ya >'Tai' na 'Nyota'<, lakini hiyo ni duru ya kwanza ya uhai wa mjumuiko wa 'taasisi ya akili-dola' kujihami na mataifa mengine yenye kustawi--na kila baada ya mapana fulani ya maendeleo na ustawi, wao huongeza idara...

Afrika bado kidogo taasisi-jicho zetu zinaushamba wa kuiga na kuzuga; hili linakwenda kubadilika siku za usoni.

Kwa hiyo tuzungumze na kujadili juu ya mifumo na huku tukitafuta kuelimishana zaidi, na basi mengi yanaweza kubayanishwa na kuleta chachu ya mageuzi--na mageuzi yana kitovu cha utashi, pia ushawishi, kote kote katika umma na pia watawala...

Kwa muktadha huu, jambo adhimu linalosubiri ni utashi wa umma juu ya mifumo, na kwa watawala-- hitaji kwa maarifa sahihi na upeo kwa 'machaguo ya kitaasisi' yaliyobora katika kujinasibu na mageuzi ya kijamii kwa kupitia 'fanusi-jamii' za namna mpya...

Pasipo taasisi imara za jicho--zenye kukomaa na 'kumbukumbu/uzoefu' na tena upeo na maarifa ya nyongeza kwa sura na mienendo ya jamii, tutaishi na kadiri ya >watawala na si viongozi<... Basi, taasisi jicho zinahitaji 'kuzaliwa upya' ili zisiishie tu kuwa 'mikondo ya taarifa-kisogo' kwa ajili mifumo mibovu ya tawala na utumishi...

Hii inawezekana kupitia jitihada sahihi za >ELIMU 2.0 na ELIMU 3.0<
 
Pengine huu ni mwanzo mpya wa mageuzi ya Idara ya Usalama wa Taifa. Mabadiliko haya ya uongozi yana maana kubwa sana kwa Idara yetu, ni matumaini yangu kwamba mabadiliko yatakwenda mbali zaidi kuguza muundo wa idara, mfumo wa idara, sheria na kanuni za idara ili kuendana na ulimwengu mpya wa dunia ya sayansi na teknolojia.

DGIS mpya Ndugu Said Masoro si mtu maarufu katika korido za Ujasusi Dar es Salaam ukimlinganisha na mtangulizi wake Athuman Diwani ambae umaarufu wake ulijengwa akiwa Intelijensia ya Polisi, DCI na katibu Tawala, Masoro anaweza kuwa chachu ya magezi ya chombo hiki muhimu na uti wa mgongo wa taifa letu ikiwa hataruhusu kumezwa na siasa chafu za Dar na Dodoma.

Moja ya Sababu kuu mimi kuamua kuandika kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi, ilikuwa ni "kuhimiza mageuzi ya idara ya Usalama Tanzania na mfumo mzima wa ulinzi na Usalama nchini".

Nilifanya hivyo baada ya utafiti mkubwa nilioufanya na kujiridhisha kwamba mfumo uliopo hauwezi kulisaidia taifa katika ulimwengu huu mpya zaidi ya kulirudisha nyuma na kudumaza utu na fikra za kijamii huku dunia ikisonga mbele katika mageuzi ya kilimwengu.

Katika kitabu, nimeeleza mageuzi makuu matatu ya muhimu na ya lazima kwa Idara ya Usalama wa Taifa kama tunalitakia mema taifa hili. Mageuzi hayo ni; kwanza yaanze kwenye Sheria iliyounda chombo hiki, pili ni Muundo wa Chombo hiki, na tatu ni Sera ya chombo hiki adhimu kwa uhai wa taifa letu.

Kwa mjibu wa Katiba ya Tanzania ya 1977 Idara ya Usalama haitajwi moja kwa moja kwenye katiba hii tofauti na majeshi mengine yote ya Nchi. Yaani Katiba ya Tanzania haitambuwi uwepo wa Idara ya Usalama wa Taifa.

Badala yake Chombo hiki kinatambuliwa na sheria ya Usalama wa Taifa ya 20 January 1997 iliyosainiwa na Benjamin William Mkapa, Rais wa Tanzania. Kwa maoni yangu hili ni moja ya makosa, Katiba Mpya inatakiwa kutambua na kuipa nguvu idara/taasisi hii pamoja na kwamba Chombo chochote cha usalama kinachoanzishwa kwa mjibu wa sheria ya Tanzania au katiba ya Tanzania, chombo hicho kitakuwa mali ya Tanzania na kitafanya kazi kwa maslahi ya Taifa na si vinginevyo.

Katika Kitabu cha Ujasusi nimeainisha mapendekezo yangu kwenye sheria ya Usalama wa Taifa ambayo nafikiri kwasasa sheria hiyo ni lazima ifanyiwe marekebisho ili kuendana na mageuzi ya dunia ya leo, tuko karne ya 21 sio enzi za zamadamu.

Moja ya vifungu katika Sheria ya Usalama wa Taifa iliyosainiwa 20 January 1997 na Rais Hayati Benjamiji W. Mkapa ambavyo ni muhimu sana kufanyiwa marekebisho ni. Mfano, kifungu 14 -(1), (2),(3), (4)-(a) na (b). Kifungu cha 15 -(1),(2), (3) -(a) na (b). Kifungu cha 16-(1) (a)na (b), (2) na (3).

Katika kitabu nimehimiza muundo wa Idara ambao umepitwa na wakati ubadilike, muundo huu unahusu kuanzia uajiri (recruiting) na mengineyo, Mfumo wa chama kimoja wa 1962 ulikuwa ndio mfumo wa uajiri wa vyombo vyote vya ulinzi na usalama, na ndio ulikuwa mfumo wa ajira zingine, ilikuwa huwezi kuingia katika vyombo vya ulinzi na usalama bila kupita TANU YOUTH League/UVCCM.

Hadi ilipofika 1992 ndipo mfumo huo ulianza kutoweka katika sekta zingine, lakini katika vyombo vya dola haukutoweka kabisa, Hivi leo watumishi wa vyombo vya dola wengi walioingia kazini kuanzia 1992 kurudi nyuma hadi 1962, hawa ni makada wa chama cha mapinduzi 100%.

Wengi wao leo ni watu wazima ndio ma RPC, OCD na wakuu wa vitengo mbalimbali katika vyombo vya utumishi na vya dola, Hivyo ukimuona RPC anashangilia ccm ikishinda sio kosa lake bali itikadi kwake imekolea na aliingia jeshini kwa tiketi ya chama na sio professional yake.

Kizazi kilichoingia kwenye vyombo vya ulinzi na Usalama miaka ya karibuni angalau hiki msingi wa kuingia kwao ni elimu, undugulaizesheni na kuipenda kazi husika, japo ukada bado una nguvu ndani ya vyombo hivyo, kwamba leo unaweza kuona maajabu RPC anastaafu leo na kesho akagombea uenyekiti wa ccm mkoa au Ubunge utajiuliza lini aliuwa mwanachama kama katiba ya ccm inavyotaka awe mwanachama angalau miaka miwili.

Sera ama Malengo makuu ya Ujasusi Tanzania yanatakiwa kujikita katika Uchumi kwakuwa hakuna njia ya mkato ya kufikia mafanikio ya Taifa kiuchumi bila kuruhusu uchumi wetu uongozwe katika misingi ya Idara ya Usalama wa Taifa na Jeshi la Wananchi Tanzani (TISS na MI).

Hapa ieleweke sana, sina maana biashara na makampuni ya uwekezaji yawe ya vyombo hivyo vya ulinzi, au yawe ya serikali, la hasha, nina maana pana zaidi kwamba ushughulikiaji wa taarifa za biashara na uchumi utiliwe mkazo zaidi kuliko ilivyo sasa taarifa za kisiasa ndizo zenye nguvu ya nchi, Mapendekezo ni TIFF itilie mkazo taarifa za uchumi na biashara zaidi na kuzipa ulinzi shughuli na biashara zote za uwekezaji wa ndani na nje na wawekezaji wake. Hawa waitwe rasmi kuwa ni (asset).

Tanzania iwe na shirika la Ujasusi linaloangalia siasa kama njia tu, na sio msingi imara wa kulinda TAIFA, wanausalama watakao kuwa makini kuona kofia ya siasa haizidi kofia ya nguvu ya umma au TAIFA. Ni wakati mwafaka wa kutambua NCHI ndio nguzo ya UTAIFA na sio siasa kuwa ndio UTAIFA wenyewe.

Kusimamia Demokrasi kwa jicho la ndani na sio jicho la upendeleo wa kiitikadi bali kuongozwa na kusimamia maadilli ya NCHI dhidi ya siasa. Inatakiwa Shirika ambalo halitatumika kwa faida ya chama, Mtu au kikundi cha watu bali ukweli uwe Taifa lianitaji nini kutoka kwenye siasa. Nchi inaishi katika lindi la unafi hasa vijana.

Kwa undani zaidi, soma kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi popote ulipo duniani.


View attachment 2468554
Tapeli tu wewe
 
Ukiangalia mataifa yote, Usalama wa Taifa una play part kubwa sana kwenye uchumi wa nchi bila wao ni kazi bure View attachment 2468361

Mkuu umenena vizuri! Baadhi ya tradition thinkers wao wanadhani ujasusi wa kiuchumi sio sehemu ya TISS ! ni kama ideology flani ya Wajamaa, ila wale wanao enda na “upepo wa mageuzi ya kiuchumi” hutumia taasisi hizi kuzinufaisha nchi zao kiuchumi na kiteknolojia!
 
Jibidiishe kusoma maandiko mbali mbali utaelewa na Kukubaliana na mtoa uzi.

Idara Ya Usalama wa Taifa ina cover almost sector zote ambazo zinafanya Ustawi wa Taifa na zinazochangia Maendeleo na au "Stability" ya Taifa.

Mkuu kuna Wakati nenda dm uulize. Unaweza kuwa unabishana na Bosi wa TISS na wewe unatoa nadharia na mwenzako anatoa uhalisia.
 
Mkuu umenena vizuri! Baadhi ya tradition thinkers wao wanadhani ujasusi wa kiuchumi sio sehemu ya TISS ! ni kama ideology flani ya Wajamaa, ila wale wanao enda na “upepo wa mageuzi ya kiuchumi” hutumia taasisi hizi kuzinufaisha nchi zao kiuchumi na kiteknolojia!
Wengi wanafikiri Usalama wa Taifa hauhusiani na uchumi basi hata hawakumbuki Magu akiwa anasisitiza vita vya kiuchumi ni mbaya ?

Wapeni elimu zaidi mkuu
 
Tindo umeathiriwa sana na propaganda za uvyama mpaka inafikia mahala watu wakijadili mpira wewe unaingiza uvyama, wakijadili mziki wewe unaingiza uvyama, wakijadili mambo mengine ya taifa vilevile unakimbilia kuingiza uvyama.

Kwa aina hii ya maisha unayoishi, usipokuwa makini ipo siku utakuja kujiuwa kisa chama chako kimeshindwa uchaguzi fulani, afu wale walioshindwa kwenye chama chako husika wakiendelea na maisha yao ya kula bata.

Hii inanikumbusha baba yangu mdogo fulani (ambae sasa ashafariki) alitakaga kuchoma nyumba yake mwenyewe na yeye mwenyewe akiwa ndani, kisa team yake ya Simba imefungwa na Yanga miaka ya 90.
Isingekuwa watu kuwahi kuuzima moto na kuvunja mlango ili wamtoe, jamaa angekuwa amewahi kujiuwa kabla ya muda wake wa kufa haujafika. Wakati huo huo viongozi wa team ya Simba na wachezaji wao walikuwa wanaendelea na maisha yao ya kula bata bila kujali kufungwa kwao.
Hili ninalokwambia ulitafakari, bila hivyo kwa aina hii ya wanasiasa wetu wa bongo waliojaa janja janja ya kupiga pesa za umma, au kulamba asali ili kujiandalia maisha yao na ya vizazi vyao kuna siku utakuja kuumia, au kupata ugonjwa wa moyo ambao haukuwa nao before.

Lazima ujue kuna maisha nje ya siasa na mtu ukaishi vizuri tu bila presha wala shutuma kwa mtu mungine.
Alichosema Tindo ndio hali halisi yenyewe
 
Pengine huu ni mwanzo mpya wa mageuzi ya Idara ya Usalama wa Taifa. Mabadiliko haya ya uongozi yana maana kubwa sana kwa Idara yetu, ni matumaini yangu kwamba mabadiliko yatakwenda mbali zaidi kuguza muundo wa idara, mfumo wa idara, sheria na kanuni za idara ili kuendana na ulimwengu mpya wa dunia ya sayansi na teknolojia.

DGIS mpya Ndugu Said Masoro si mtu maarufu katika korido za Ujasusi Dar es Salaam ukimlinganisha na mtangulizi wake Athuman Diwani ambae umaarufu wake ulijengwa akiwa Intelijensia ya Polisi, DCI na katibu Tawala, Masoro anaweza kuwa chachu ya magezi ya chombo hiki muhimu na uti wa mgongo wa taifa letu ikiwa hataruhusu kumezwa na siasa chafu za Dar na Dodoma.

Moja ya Sababu kuu mimi kuamua kuandika kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi, ilikuwa ni "kuhimiza mageuzi ya idara ya Usalama Tanzania na mfumo mzima wa ulinzi na Usalama nchini".

Nilifanya hivyo baada ya utafiti mkubwa nilioufanya na kujiridhisha kwamba mfumo uliopo hauwezi kulisaidia taifa katika ulimwengu huu mpya zaidi ya kulirudisha nyuma na kudumaza utu na fikra za kijamii huku dunia ikisonga mbele katika mageuzi ya kilimwengu.

Katika kitabu, nimeeleza mageuzi makuu matatu ya muhimu na ya lazima kwa Idara ya Usalama wa Taifa kama tunalitakia mema taifa hili. Mageuzi hayo ni; kwanza yaanze kwenye Sheria iliyounda chombo hiki, pili ni Muundo wa Chombo hiki, na tatu ni Sera ya chombo hiki adhimu kwa uhai wa taifa letu.

Kwa mjibu wa Katiba ya Tanzania ya 1977 Idara ya Usalama haitajwi moja kwa moja kwenye katiba hii tofauti na majeshi mengine yote ya Nchi. Yaani Katiba ya Tanzania haitambuwi uwepo wa Idara ya Usalama wa Taifa.

Badala yake Chombo hiki kinatambuliwa na sheria ya Usalama wa Taifa ya 20 January 1997 iliyosainiwa na Benjamin William Mkapa, Rais wa Tanzania. Kwa maoni yangu hili ni moja ya makosa, Katiba Mpya inatakiwa kutambua na kuipa nguvu idara/taasisi hii pamoja na kwamba Chombo chochote cha usalama kinachoanzishwa kwa mjibu wa sheria ya Tanzania au katiba ya Tanzania, chombo hicho kitakuwa mali ya Tanzania na kitafanya kazi kwa maslahi ya Taifa na si vinginevyo.

Katika Kitabu cha Ujasusi nimeainisha mapendekezo yangu kwenye sheria ya Usalama wa Taifa ambayo nafikiri kwasasa sheria hiyo ni lazima ifanyiwe marekebisho ili kuendana na mageuzi ya dunia ya leo, tuko karne ya 21 sio enzi za zamadamu.

Moja ya vifungu katika Sheria ya Usalama wa Taifa iliyosainiwa 20 January 1997 na Rais Hayati Benjamiji W. Mkapa ambavyo ni muhimu sana kufanyiwa marekebisho ni. Mfano, kifungu 14 -(1), (2),(3), (4)-(a) na (b). Kifungu cha 15 -(1),(2), (3) -(a) na (b). Kifungu cha 16-(1) (a)na (b), (2) na (3).

Katika kitabu nimehimiza muundo wa Idara ambao umepitwa na wakati ubadilike, muundo huu unahusu kuanzia uajiri (recruiting) na mengineyo, Mfumo wa chama kimoja wa 1962 ulikuwa ndio mfumo wa uajiri wa vyombo vyote vya ulinzi na usalama, na ndio ulikuwa mfumo wa ajira zingine, ilikuwa huwezi kuingia katika vyombo vya ulinzi na usalama bila kupita TANU YOUTH League/UVCCM.

Hadi ilipofika 1992 ndipo mfumo huo ulianza kutoweka katika sekta zingine, lakini katika vyombo vya dola haukutoweka kabisa, Hivi leo watumishi wa vyombo vya dola wengi walioingia kazini kuanzia 1992 kurudi nyuma hadi 1962, hawa ni makada wa chama cha mapinduzi 100%.

Wengi wao leo ni watu wazima ndio ma RPC, OCD na wakuu wa vitengo mbalimbali katika vyombo vya utumishi na vya dola, Hivyo ukimuona RPC anashangilia ccm ikishinda sio kosa lake bali itikadi kwake imekolea na aliingia jeshini kwa tiketi ya chama na sio professional yake.

Kizazi kilichoingia kwenye vyombo vya ulinzi na Usalama miaka ya karibuni angalau hiki msingi wa kuingia kwao ni elimu, undugulaizesheni na kuipenda kazi husika, japo ukada bado una nguvu ndani ya vyombo hivyo, kwamba leo unaweza kuona maajabu RPC anastaafu leo na kesho akagombea uenyekiti wa ccm mkoa au Ubunge utajiuliza lini aliuwa mwanachama kama katiba ya ccm inavyotaka awe mwanachama angalau miaka miwili.

Sera ama Malengo makuu ya Ujasusi Tanzania yanatakiwa kujikita katika Uchumi kwakuwa hakuna njia ya mkato ya kufikia mafanikio ya Taifa kiuchumi bila kuruhusu uchumi wetu uongozwe katika misingi ya Idara ya Usalama wa Taifa na Jeshi la Wananchi Tanzani (TISS na MI).

Hapa ieleweke sana, sina maana biashara na makampuni ya uwekezaji yawe ya vyombo hivyo vya ulinzi, au yawe ya serikali, la hasha, nina maana pana zaidi kwamba ushughulikiaji wa taarifa za biashara na uchumi utiliwe mkazo zaidi kuliko ilivyo sasa taarifa za kisiasa ndizo zenye nguvu ya nchi, Mapendekezo ni TIFF itilie mkazo taarifa za uchumi na biashara zaidi na kuzipa ulinzi shughuli na biashara zote za uwekezaji wa ndani na nje na wawekezaji wake. Hawa waitwe rasmi kuwa ni (asset).

Tanzania iwe na shirika la Ujasusi linaloangalia siasa kama njia tu, na sio msingi imara wa kulinda TAIFA, wanausalama watakao kuwa makini kuona kofia ya siasa haizidi kofia ya nguvu ya umma au TAIFA. Ni wakati mwafaka wa kutambua NCHI ndio nguzo ya UTAIFA na sio siasa kuwa ndio UTAIFA wenyewe.

Kusimamia Demokrasi kwa jicho la ndani na sio jicho la upendeleo wa kiitikadi bali kuongozwa na kusimamia maadilli ya NCHI dhidi ya siasa. Inatakiwa Shirika ambalo halitatumika kwa faida ya chama, Mtu au kikundi cha watu bali ukweli uwe Taifa lianitaji nini kutoka kwenye siasa. Nchi inaishi katika lindi la unafi hasa vijana.

Kwa undani zaidi, soma kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi popote ulipo duniani.


View attachment 2468554
Mi nirifikili unamchambua boss mpya wa TISS,uwezo wake,katoka wapi,kasoma wapi,CV yake,
Kumbe una promote kitabu chako!!
Unatembelea kwenye fulsa,
Hii ni opportunisticim ya hali ya juu
 
Magu alikuwa na kamsemo kake " hakuna vita mbaya kama vita ya uchumi". TISS wangelikuwa makini na hiyo kauli, jamaa tungekuwa naye hadi sasa.

Kifo cha Magu kinaonesha wazi kwamba TISS wako sharrow kwenye ujasusi wa kiuchumi na wamejikita zaidi kwenye ujasusi wa kisiasa. Magu ali out smart hiyo taasisi kwani maamuzi ya Magu yalikuwa mbele zaidi ya TISS.

CIA, M16, MOSSAD, KGB , etc ndo taasisi zinazofanya biashara kubwa duniani kama madini, mafuta, madawa e.t.c. hawa jamaa wanatoa funds kwa local private companies ili ziweze kuwapatia data za kibiashara. TISS yetu imelala usingizi wa pono kwenye upande wa uchumi ila wako active kuwakamata wanasiasa na kulinda chama.

Projects kama Kabanga Nickel, SGR na Bwawa la nyerere zikisimamiwa vizuri zitaleta impact kubwa kwenye uchumi wa nchi ila zinaendeshwa kisiasa na sidhani kama zitatoboa.

Kiukweli hii nchi ili iweze kusonga mbele, TISS inabidi wabadilike, wajikite zaidi kwenye uchumi. Waende sambamba na tech startup companies zenye innovations ila hazina mitaji wazisimamie ziweze kwenda na vizuri na kasi ya dunia.

Rwanda na Kenya wanajitahidi katika ujasusi wa kiuchumi ndiyo maana wanapeta kwenye nyanja za kimataifa.
 
TISS na Jeshi hawawezi kuukwamua uchumi wetu, hakuna maendeleo yoyote duniani ya kiuchumi yamepatikana kwa njia hii.
Huo wizi ulioiutaja hapa hauhusiani na uchumi. Maendeleo ya uchumi yanahitaji uongozi na mfumo mzuri wa kisiasa pamoja wachumi nguli wanaopewa uhuru kutimiza majukumu yao.
Umeamua maksudi kutoelewa?
Ni namna gani unaweza kutofautisha mfumo wa intelligentsia wa nchi na uchumi wa nchi?
Kila nchi inayojielewa hapa duniani inaimarisha sana Intelligence Agency zao:

Mossad wapo busy pamoja na mambo yite wanayoyafanya kuimarisha diplomasia ya kimataifa ili products za Israeli ziuzike duniani kote.

Tawi la CIA, yaani USAID wapo busy kuanzisha miradi inayoonekana (au kuaminika) ya kijamii yaani humanitarian lakini ajenda nyuma na kuexplore dunia yote na kupenyeza influence ya Marekani kiuchumi duniani kote.

Ndivyo wanavyofanya nchi zote duniani zenye maono.

Ni kweli Benki Kuu na taasisi zinginezo zina nafasi yake katika uchumi wa nchi. But nafasi yao I think ni kuregulate, kupredict na kuconsult on fiscal policies na macro/microeconomics za nchi husika.

Lakini linapokuja suala la kuwa na uchumi shindani, kuwa wa kwanza on the market, kupenya na kuteka masoko mbalimbali asee njia intelligence system ya nchi ambayo nikiri inapaswa kuwa system tambuka lakini coordinated, lazima ihusike.

Vinginevyo mtabaki na TISS yenu inayohangaika na wenyeviti wa vijiji na makatibu kata ili CCM ishinde na kujizolea asilimia 100. Japo kuna njia bora za kushinda uchaguzi bila kuwa na mawazo ya kitoto namna hiyo.
 
Pengine huu ni mwanzo mpya wa mageuzi ya Idara ya Usalama wa Taifa. Mabadiliko haya ya uongozi yana maana kubwa sana kwa Idara yetu, ni matumaini yangu kwamba mabadiliko yatakwenda mbali zaidi kuguza muundo wa idara, mfumo wa idara, sheria na kanuni za idara ili kuendana na ulimwengu mpya wa dunia ya sayansi na teknolojia.

DGIS mpya Ndugu Said Masoro si mtu maarufu katika korido za Ujasusi Dar es Salaam ukimlinganisha na mtangulizi wake Athuman Diwani ambae umaarufu wake ulijengwa akiwa Intelijensia ya Polisi, DCI na katibu Tawala, Masoro anaweza kuwa chachu ya magezi ya chombo hiki muhimu na uti wa mgongo wa taifa letu ikiwa hataruhusu kumezwa na siasa chafu za Dar na Dodoma.

Moja ya Sababu kuu mimi kuamua kuandika kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi, ilikuwa ni "kuhimiza mageuzi ya idara ya Usalama Tanzania na mfumo mzima wa ulinzi na Usalama nchini".

Nilifanya hivyo baada ya utafiti mkubwa nilioufanya na kujiridhisha kwamba mfumo uliopo hauwezi kulisaidia taifa katika ulimwengu huu mpya zaidi ya kulirudisha nyuma na kudumaza utu na fikra za kijamii huku dunia ikisonga mbele katika mageuzi ya kilimwengu.

Katika kitabu, nimeeleza mageuzi makuu matatu ya muhimu na ya lazima kwa Idara ya Usalama wa Taifa kama tunalitakia mema taifa hili. Mageuzi hayo ni; kwanza yaanze kwenye Sheria iliyounda chombo hiki, pili ni Muundo wa Chombo hiki, na tatu ni Sera ya chombo hiki adhimu kwa uhai wa taifa letu.

Kwa mjibu wa Katiba ya Tanzania ya 1977 Idara ya Usalama haitajwi moja kwa moja kwenye katiba hii tofauti na majeshi mengine yote ya Nchi. Yaani Katiba ya Tanzania haitambuwi uwepo wa Idara ya Usalama wa Taifa.

Badala yake Chombo hiki kinatambuliwa na sheria ya Usalama wa Taifa ya 20 January 1997 iliyosainiwa na Benjamin William Mkapa, Rais wa Tanzania. Kwa maoni yangu hili ni moja ya makosa, Katiba Mpya inatakiwa kutambua na kuipa nguvu idara/taasisi hii pamoja na kwamba Chombo chochote cha usalama kinachoanzishwa kwa mjibu wa sheria ya Tanzania au katiba ya Tanzania, chombo hicho kitakuwa mali ya Tanzania na kitafanya kazi kwa maslahi ya Taifa na si vinginevyo.

Katika Kitabu cha Ujasusi nimeainisha mapendekezo yangu kwenye sheria ya Usalama wa Taifa ambayo nafikiri kwasasa sheria hiyo ni lazima ifanyiwe marekebisho ili kuendana na mageuzi ya dunia ya leo, tuko karne ya 21 sio enzi za zamadamu.

Moja ya vifungu katika Sheria ya Usalama wa Taifa iliyosainiwa 20 January 1997 na Rais Hayati Benjamiji W. Mkapa ambavyo ni muhimu sana kufanyiwa marekebisho ni. Mfano, kifungu 14 -(1), (2),(3), (4)-(a) na (b). Kifungu cha 15 -(1),(2), (3) -(a) na (b). Kifungu cha 16-(1) (a)na (b), (2) na (3).

Katika kitabu nimehimiza muundo wa Idara ambao umepitwa na wakati ubadilike, muundo huu unahusu kuanzia uajiri (recruiting) na mengineyo, Mfumo wa chama kimoja wa 1962 ulikuwa ndio mfumo wa uajiri wa vyombo vyote vya ulinzi na usalama, na ndio ulikuwa mfumo wa ajira zingine, ilikuwa huwezi kuingia katika vyombo vya ulinzi na usalama bila kupita TANU YOUTH League/UVCCM.

Hadi ilipofika 1992 ndipo mfumo huo ulianza kutoweka katika sekta zingine, lakini katika vyombo vya dola haukutoweka kabisa, Hivi leo watumishi wa vyombo vya dola wengi walioingia kazini kuanzia 1992 kurudi nyuma hadi 1962, hawa ni makada wa chama cha mapinduzi 100%.

Wengi wao leo ni watu wazima ndio ma RPC, OCD na wakuu wa vitengo mbalimbali katika vyombo vya utumishi na vya dola, Hivyo ukimuona RPC anashangilia ccm ikishinda sio kosa lake bali itikadi kwake imekolea na aliingia jeshini kwa tiketi ya chama na sio professional yake.

Kizazi kilichoingia kwenye vyombo vya ulinzi na Usalama miaka ya karibuni angalau hiki msingi wa kuingia kwao ni elimu, undugulaizesheni na kuipenda kazi husika, japo ukada bado una nguvu ndani ya vyombo hivyo, kwamba leo unaweza kuona maajabu RPC anastaafu leo na kesho akagombea uenyekiti wa ccm mkoa au Ubunge utajiuliza lini aliuwa mwanachama kama katiba ya ccm inavyotaka awe mwanachama angalau miaka miwili.

Sera ama Malengo makuu ya Ujasusi Tanzania yanatakiwa kujikita katika Uchumi kwakuwa hakuna njia ya mkato ya kufikia mafanikio ya Taifa kiuchumi bila kuruhusu uchumi wetu uongozwe katika misingi ya Idara ya Usalama wa Taifa na Jeshi la Wananchi Tanzani (TISS na MI).

Hapa ieleweke sana, sina maana biashara na makampuni ya uwekezaji yawe ya vyombo hivyo vya ulinzi, au yawe ya serikali, la hasha, nina maana pana zaidi kwamba ushughulikiaji wa taarifa za biashara na uchumi utiliwe mkazo zaidi kuliko ilivyo sasa taarifa za kisiasa ndizo zenye nguvu ya nchi, Mapendekezo ni TIFF itilie mkazo taarifa za uchumi na biashara zaidi na kuzipa ulinzi shughuli na biashara zote za uwekezaji wa ndani na nje na wawekezaji wake. Hawa waitwe rasmi kuwa ni (asset).

Tanzania iwe na shirika la Ujasusi linaloangalia siasa kama njia tu, na sio msingi imara wa kulinda TAIFA, wanausalama watakao kuwa makini kuona kofia ya siasa haizidi kofia ya nguvu ya umma au TAIFA. Ni wakati mwafaka wa kutambua NCHI ndio nguzo ya UTAIFA na sio siasa kuwa ndio UTAIFA wenyewe.

Kusimamia Demokrasi kwa jicho la ndani na sio jicho la upendeleo wa kiitikadi bali kuongozwa na kusimamia maadilli ya NCHI dhidi ya siasa. Inatakiwa Shirika ambalo halitatumika kwa faida ya chama, Mtu au kikundi cha watu bali ukweli uwe Taifa lianitaji nini kutoka kwenye siasa. Nchi inaishi katika lindi la unafi hasa vijana.

Kwa undani zaidi, soma kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi popote ulipo duniani.


View attachment 2468554
Naona umeamua kutulazimisha kurejea kitabu chako bila kugusa serious analysis as the title claims

don’t be a trumpet, be the brains
 
Magu alikuwa na kamsemo kake " hakuna vita mbaya kama vita ya uchumi". TISS wangelikuwa makini na hiyo kauli, jamaa tungekuwa naye hadi sasa.

Kifo cha Magu kinaonesha wazi kwamba TISS wako sharrow kwenye ujasusi wa kiuchumi na wamejikita zaidi kwenye ujasusi wa kisiasa. Magu ali out smart hiyo taasisi kwani maamuzi ya Magu yalikuwa mbele zaidi ya TISS.

CIA, M16, MOSSAD, KGB , etc ndo taasisi zinazofanya biashara kubwa duniani kama madini, mafuta, madawa e.t.c. hawa jamaa wanatoa funds kwa local private companies ili ziweze kuwapatia data za kibiashara. TISS yetu imelala usingizi wa pono kwenye upande wa uchumi ila wako active kuwakamata wanasiasa na kulinda chama.

Projects kama Kabanga Nickel, SGR na Bwawa la nyerere zikisimamiwa vizuri zitaleta impact kubwa kwenye uchumi wa nchi ila zinaendeshwa kisiasa na sidhani kama zitatoboa.

Kiukweli hii nchi ili iweze kusonga mbele, TISS inabidi wabadilike, wajikite zaidi kwenye uchumi. Waende sambamba na tech startup companies zenye innovations ila hazina mitaji wazisimamie ziweze kwenda na vizuri na kasi ya dunia.

Rwanda na Kenya wanajitahidi katika ujasusi wa kiuchumi ndiyo maana wanapeta kwenye nyanja za kimataifa.
Be positive mkuu

Hata hizo investments unazozitaja ziko supported na hao unaowakandya
 
Hiki ulichoandika hapa sio kazi kuu za Idara za Usalama wa Taifa/Ujasusi duniani. Kazi za majususi ni ulinzi na usalama wa nchi masuala ya uchumi na biashara yataingizwa huko katika majuku yao kama ni kitisho cha usalama wa nchi zao au kama yataleta matokeo fulani kiusalama.

Hizi kazi za uchumi na biashara katika nchi ni kazi kuu za Wizara ya Fedha na Benki Kuu.
Yoda bwana! Unafikir vita nyingi duniani husabanishwa na nini? Nyingi ni uchimi, Ukraine, Ghuba, Syria kote huko ni uchumi.
Lakini pia kumbuka mtu mmoja alitangaza vita ya kiuchumi hakutoboa, laiti tungekuwa na taasisi iliyojiimarisha huko ingesaidia.

Sent from my Infinix X693 using JamiiForums mobile app
 
Lakini linapokuja suala la kuwa na uchumi shindani, kuwa wa kwanza on the market, kupenya na kuteka masoko mbalimbali asee njia intelligence system ya nchi ambayo nikiri inapaswa kuwa system tambuka lakini coordinated, lazima ihusike.
Jamaa umetema madini sana
 
Pengine huu ni mwanzo mpya wa mageuzi ya Idara ya Usalama wa Taifa. Mabadiliko haya ya uongozi yana maana kubwa sana kwa Idara yetu, ni matumaini yangu kwamba mabadiliko yatakwenda mbali zaidi kuguza muundo wa idara, mfumo wa idara, sheria na kanuni za idara ili kuendana na ulimwengu mpya wa dunia ya sayansi na teknolojia.

DGIS mpya Ndugu Said Masoro si mtu maarufu katika korido za Ujasusi Dar es Salaam ukimlinganisha na mtangulizi wake Athuman Diwani ambae umaarufu wake ulijengwa akiwa Intelijensia ya Polisi, DCI na katibu Tawala, Masoro anaweza kuwa chachu ya magezi ya chombo hiki muhimu na uti wa mgongo wa taifa letu ikiwa hataruhusu kumezwa na siasa chafu za Dar na Dodoma.

Moja ya Sababu kuu mimi kuamua kuandika kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi, ilikuwa ni "kuhimiza mageuzi ya idara ya Usalama Tanzania na mfumo mzima wa ulinzi na Usalama nchini".

Nilifanya hivyo baada ya utafiti mkubwa nilioufanya na kujiridhisha kwamba mfumo uliopo hauwezi kulisaidia taifa katika ulimwengu huu mpya zaidi ya kulirudisha nyuma na kudumaza utu na fikra za kijamii huku dunia ikisonga mbele katika mageuzi ya kilimwengu.

Katika kitabu, nimeeleza mageuzi makuu matatu ya muhimu na ya lazima kwa Idara ya Usalama wa Taifa kama tunalitakia mema taifa hili. Mageuzi hayo ni; kwanza yaanze kwenye Sheria iliyounda chombo hiki, pili ni Muundo wa Chombo hiki, na tatu ni Sera ya chombo hiki adhimu kwa uhai wa taifa letu.

Kwa mjibu wa Katiba ya Tanzania ya 1977 Idara ya Usalama haitajwi moja kwa moja kwenye katiba hii tofauti na majeshi mengine yote ya Nchi. Yaani Katiba ya Tanzania haitambuwi uwepo wa Idara ya Usalama wa Taifa.

Badala yake Chombo hiki kinatambuliwa na sheria ya Usalama wa Taifa ya 20 January 1997 iliyosainiwa na Benjamin William Mkapa, Rais wa Tanzania. Kwa maoni yangu hili ni moja ya makosa, Katiba Mpya inatakiwa kutambua na kuipa nguvu idara/taasisi hii pamoja na kwamba Chombo chochote cha usalama kinachoanzishwa kwa mjibu wa sheria ya Tanzania au katiba ya Tanzania, chombo hicho kitakuwa mali ya Tanzania na kitafanya kazi kwa maslahi ya Taifa na si vinginevyo.

Katika Kitabu cha Ujasusi nimeainisha mapendekezo yangu kwenye sheria ya Usalama wa Taifa ambayo nafikiri kwasasa sheria hiyo ni lazima ifanyiwe marekebisho ili kuendana na mageuzi ya dunia ya leo, tuko karne ya 21 sio enzi za zamadamu.

Moja ya vifungu katika Sheria ya Usalama wa Taifa iliyosainiwa 20 January 1997 na Rais Hayati Benjamiji W. Mkapa ambavyo ni muhimu sana kufanyiwa marekebisho ni. Mfano, kifungu 14 -(1), (2),(3), (4)-(a) na (b). Kifungu cha 15 -(1),(2), (3) -(a) na (b). Kifungu cha 16-(1) (a)na (b), (2) na (3).

Katika kitabu nimehimiza muundo wa Idara ambao umepitwa na wakati ubadilike, muundo huu unahusu kuanzia uajiri (recruiting) na mengineyo, Mfumo wa chama kimoja wa 1962 ulikuwa ndio mfumo wa uajiri wa vyombo vyote vya ulinzi na usalama, na ndio ulikuwa mfumo wa ajira zingine, ilikuwa huwezi kuingia katika vyombo vya ulinzi na usalama bila kupita TANU YOUTH League/UVCCM.

Hadi ilipofika 1992 ndipo mfumo huo ulianza kutoweka katika sekta zingine, lakini katika vyombo vya dola haukutoweka kabisa, Hivi leo watumishi wa vyombo vya dola wengi walioingia kazini kuanzia 1992 kurudi nyuma hadi 1962, hawa ni makada wa chama cha mapinduzi 100%.

Wengi wao leo ni watu wazima ndio ma RPC, OCD na wakuu wa vitengo mbalimbali katika vyombo vya utumishi na vya dola, Hivyo ukimuona RPC anashangilia ccm ikishinda sio kosa lake bali itikadi kwake imekolea na aliingia jeshini kwa tiketi ya chama na sio professional yake.

Kizazi kilichoingia kwenye vyombo vya ulinzi na Usalama miaka ya karibuni angalau hiki msingi wa kuingia kwao ni elimu, undugulaizesheni na kuipenda kazi husika, japo ukada bado una nguvu ndani ya vyombo hivyo, kwamba leo unaweza kuona maajabu RPC anastaafu leo na kesho akagombea uenyekiti wa ccm mkoa au Ubunge utajiuliza lini aliuwa mwanachama kama katiba ya ccm inavyotaka awe mwanachama angalau miaka miwili.

Sera ama Malengo makuu ya Ujasusi Tanzania yanatakiwa kujikita katika Uchumi kwakuwa hakuna njia ya mkato ya kufikia mafanikio ya Taifa kiuchumi bila kuruhusu uchumi wetu uongozwe katika misingi ya Idara ya Usalama wa Taifa na Jeshi la Wananchi Tanzani (TISS na MI).

Hapa ieleweke sana, sina maana biashara na makampuni ya uwekezaji yawe ya vyombo hivyo vya ulinzi, au yawe ya serikali, la hasha, nina maana pana zaidi kwamba ushughulikiaji wa taarifa za biashara na uchumi utiliwe mkazo zaidi kuliko ilivyo sasa taarifa za kisiasa ndizo zenye nguvu ya nchi, Mapendekezo ni TIFF itilie mkazo taarifa za uchumi na biashara zaidi na kuzipa ulinzi shughuli na biashara zote za uwekezaji wa ndani na nje na wawekezaji wake. Hawa waitwe rasmi kuwa ni (asset).

Tanzania iwe na shirika la Ujasusi linaloangalia siasa kama njia tu, na sio msingi imara wa kulinda TAIFA, wanausalama watakao kuwa makini kuona kofia ya siasa haizidi kofia ya nguvu ya umma au TAIFA. Ni wakati mwafaka wa kutambua NCHI ndio nguzo ya UTAIFA na sio siasa kuwa ndio UTAIFA wenyewe.

Kusimamia Demokrasi kwa jicho la ndani na sio jicho la upendeleo wa kiitikadi bali kuongozwa na kusimamia maadilli ya NCHI dhidi ya siasa. Inatakiwa Shirika ambalo halitatumika kwa faida ya chama, Mtu au kikundi cha watu bali ukweli uwe Taifa lianitaji nini kutoka kwenye siasa. Nchi inaishi katika lindi la unafi hasa vijana.

Kwa undani zaidi, soma kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi popote ulipo duniani.


View attachment 2468554
Wewe ni mtu feki tu! Unaleta hadithi za kutunga ili ziendeshe nchi?
 
Back
Top Bottom