Uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu Mpya wa TISS, Said H. Masoro, na Mtazamo wangu

Uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu Mpya wa TISS, Said H. Masoro, na Mtazamo wangu

Pengine huu ni mwanzo mpya wa mageuzi ya Idara ya Usalama wa Taifa. Mabadiliko haya ya uongozi yana maana kubwa sana kwa Idara yetu, ni matumaini yangu kwamba mabadiliko yatakwenda mbali zaidi kuguza muundo wa idara, mfumo wa idara, sheria na kanuni za idara ili kuendana na ulimwengu mpya wa dunia ya sayansi na teknolojia.

DGIS mpya Ndugu Said Masoro si mtu maarufu katika korido za Ujasusi Dar es Salaam ukimlinganisha na mtangulizi wake Athuman Diwani ambae umaarufu wake ulijengwa akiwa Intelijensia ya Polisi, DCI na katibu Tawala, Masoro anaweza kuwa chachu ya magezi ya chombo hiki muhimu na uti wa mgongo wa taifa letu ikiwa hataruhusu kumezwa na siasa chafu za Dar na Dodoma.

Moja ya Sababu kuu mimi kuamua kuandika kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi, ilikuwa ni "kuhimiza mageuzi ya idara ya Usalama Tanzania na mfumo mzima wa ulinzi na Usalama nchini".

Nilifanya hivyo baada ya utafiti mkubwa nilioufanya na kujiridhisha kwamba mfumo uliopo hauwezi kulisaidia taifa katika ulimwengu huu mpya zaidi ya kulirudisha nyuma na kudumaza utu na fikra za kijamii huku dunia ikisonga mbele katika mageuzi ya kilimwengu.

Katika kitabu, nimeeleza mageuzi makuu matatu ya muhimu na ya lazima kwa Idara ya Usalama wa Taifa kama tunalitakia mema taifa hili. Mageuzi hayo ni; kwanza yaanze kwenye Sheria iliyounda chombo hiki, pili ni Muundo wa Chombo hiki, na tatu ni Sera ya chombo hiki adhimu kwa uhai wa taifa letu.

Kwa mjibu wa Katiba ya Tanzania ya 1977 Idara ya Usalama haitajwi moja kwa moja kwenye katiba hii tofauti na majeshi mengine yote ya Nchi. Yaani Katiba ya Tanzania haitambuwi uwepo wa Idara ya Usalama wa Taifa.

Badala yake Chombo hiki kinatambuliwa na sheria ya Usalama wa Taifa ya 20 January 1997 iliyosainiwa na Benjamin William Mkapa, Rais wa Tanzania. Kwa maoni yangu hili ni moja ya makosa, Katiba Mpya inatakiwa kutambua na kuipa nguvu idara/taasisi hii pamoja na kwamba Chombo chochote cha usalama kinachoanzishwa kwa mjibu wa sheria ya Tanzania au katiba ya Tanzania, chombo hicho kitakuwa mali ya Tanzania na kitafanya kazi kwa maslahi ya Taifa na si vinginevyo.

Katika Kitabu cha Ujasusi nimeainisha mapendekezo yangu kwenye sheria ya Usalama wa Taifa ambayo nafikiri kwasasa sheria hiyo ni lazima ifanyiwe marekebisho ili kuendana na mageuzi ya dunia ya leo, tuko karne ya 21 sio enzi za zamadamu.

Moja ya vifungu katika Sheria ya Usalama wa Taifa iliyosainiwa 20 January 1997 na Rais Hayati Benjamiji W. Mkapa ambavyo ni muhimu sana kufanyiwa marekebisho ni. Mfano, kifungu 14 -(1), (2),(3), (4)-(a) na (b). Kifungu cha 15 -(1),(2), (3) -(a) na (b). Kifungu cha 16-(1) (a)na (b), (2) na (3).

Katika kitabu nimehimiza muundo wa Idara ambao umepitwa na wakati ubadilike, muundo huu unahusu kuanzia uajiri (recruiting) na mengineyo, Mfumo wa chama kimoja wa 1962 ulikuwa ndio mfumo wa uajiri wa vyombo vyote vya ulinzi na usalama, na ndio ulikuwa mfumo wa ajira zingine, ilikuwa huwezi kuingia katika vyombo vya ulinzi na usalama bila kupita TANU YOUTH League/UVCCM.

Hadi ilipofika 1992 ndipo mfumo huo ulianza kutoweka katika sekta zingine, lakini katika vyombo vya dola haukutoweka kabisa, Hivi leo watumishi wa vyombo vya dola wengi walioingia kazini kuanzia 1992 kurudi nyuma hadi 1962, hawa ni makada wa chama cha mapinduzi 100%.

Wengi wao leo ni watu wazima ndio ma RPC, OCD na wakuu wa vitengo mbalimbali katika vyombo vya utumishi na vya dola, Hivyo ukimuona RPC anashangilia ccm ikishinda sio kosa lake bali itikadi kwake imekolea na aliingia jeshini kwa tiketi ya chama na sio professional yake.

Kizazi kilichoingia kwenye vyombo vya ulinzi na Usalama miaka ya karibuni angalau hiki msingi wa kuingia kwao ni elimu, undugulaizesheni na kuipenda kazi husika, japo ukada bado una nguvu ndani ya vyombo hivyo, kwamba leo unaweza kuona maajabu RPC anastaafu leo na kesho akagombea uenyekiti wa ccm mkoa au Ubunge utajiuliza lini aliuwa mwanachama kama katiba ya ccm inavyotaka awe mwanachama angalau miaka miwili.

Sera ama Malengo makuu ya Ujasusi Tanzania yanatakiwa kujikita katika Uchumi kwakuwa hakuna njia ya mkato ya kufikia mafanikio ya Taifa kiuchumi bila kuruhusu uchumi wetu uongozwe katika misingi ya Idara ya Usalama wa Taifa na Jeshi la Wananchi Tanzani (TISS na MI).

Hapa ieleweke sana, sina maana biashara na makampuni ya uwekezaji yawe ya vyombo hivyo vya ulinzi, au yawe ya serikali, la hasha, nina maana pana zaidi kwamba ushughulikiaji wa taarifa za biashara na uchumi utiliwe mkazo zaidi kuliko ilivyo sasa taarifa za kisiasa ndizo zenye nguvu ya nchi, Mapendekezo ni TIFF itilie mkazo taarifa za uchumi na biashara zaidi na kuzipa ulinzi shughuli na biashara zote za uwekezaji wa ndani na nje na wawekezaji wake. Hawa waitwe rasmi kuwa ni (asset).

Tanzania iwe na shirika la Ujasusi linaloangalia siasa kama njia tu, na sio msingi imara wa kulinda TAIFA, wanausalama watakao kuwa makini kuona kofia ya siasa haizidi kofia ya nguvu ya umma au TAIFA. Ni wakati mwafaka wa kutambua NCHI ndio nguzo ya UTAIFA na sio siasa kuwa ndio UTAIFA wenyewe.

Kusimamia Demokrasi kwa jicho la ndani na sio jicho la upendeleo wa kiitikadi bali kuongozwa na kusimamia maadilli ya NCHI dhidi ya siasa. Inatakiwa Shirika ambalo halitatumika kwa faida ya chama, Mtu au kikundi cha watu bali ukweli uwe Taifa lianitaji nini kutoka kwenye siasa. Nchi inaishi katika lindi la unafi hasa vijana.

Kwa undani zaidi, soma kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi popote ulipo duniani.


View attachment 2468314
Wabongo Sasa hivi mnapenda credit uchwara.

Huyo ameteuliwa kama Marais wengine walivyoteua huko nyuma. Hakuna jipya.
 
Huu ni mtazamo wako, ngoja tusubiri na mtazamo wa mkongwe Pascal Mayalla ili kujua na yeye atakuja na mtazamo gani kuhusu mkuu huyu wa idara nyeti.

Hakuna mzee mwenye mtazamo tofauti na uliomkuza. Yeye anaamini CCM itatawala milele. Mtu kama huyo hana mtazamo tofauti na huo. Sana sana ataishia kuleta porojo.
 
Pengine huu ni mwanzo mpya wa mageuzi ya Idara ya Usalama wa Taifa. Mabadiliko haya ya uongozi yana maana kubwa sana kwa Idara yetu, ni matumaini yangu kwamba mabadiliko yatakwenda mbali zaidi kuguza muundo wa idara, mfumo wa idara, sheria na kanuni za idara ili kuendana na ulimwengu mpya wa dunia ya sayansi na teknolojia.

DGIS mpya Ndugu Said Masoro si mtu maarufu katika korido za Ujasusi Dar es Salaam ukimlinganisha na mtangulizi wake Athuman Diwani ambae umaarufu wake ulijengwa akiwa Intelijensia ya Polisi, DCI na katibu Tawala, Masoro anaweza kuwa chachu ya magezi ya chombo hiki muhimu na uti wa mgongo wa taifa letu ikiwa hataruhusu kumezwa na siasa chafu za Dar na Dodoma.

Moja ya Sababu kuu mimi kuamua kuandika kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi, ilikuwa ni "kuhimiza mageuzi ya idara ya Usalama Tanzania na mfumo mzima wa ulinzi na Usalama nchini".

Nilifanya hivyo baada ya utafiti mkubwa nilioufanya na kujiridhisha kwamba mfumo uliopo hauwezi kulisaidia taifa katika ulimwengu huu mpya zaidi ya kulirudisha nyuma na kudumaza utu na fikra za kijamii huku dunia ikisonga mbele katika mageuzi ya kilimwengu.

Katika kitabu, nimeeleza mageuzi makuu matatu ya muhimu na ya lazima kwa Idara ya Usalama wa Taifa kama tunalitakia mema taifa hili. Mageuzi hayo ni; kwanza yaanze kwenye Sheria iliyounda chombo hiki, pili ni Muundo wa Chombo hiki, na tatu ni Sera ya chombo hiki adhimu kwa uhai wa taifa letu.

Kwa mjibu wa Katiba ya Tanzania ya 1977 Idara ya Usalama haitajwi moja kwa moja kwenye katiba hii tofauti na majeshi mengine yote ya Nchi. Yaani Katiba ya Tanzania haitambuwi uwepo wa Idara ya Usalama wa Taifa.

Badala yake Chombo hiki kinatambuliwa na sheria ya Usalama wa Taifa ya 20 January 1997 iliyosainiwa na Benjamin William Mkapa, Rais wa Tanzania. Kwa maoni yangu hili ni moja ya makosa, Katiba Mpya inatakiwa kutambua na kuipa nguvu idara/taasisi hii pamoja na kwamba Chombo chochote cha usalama kinachoanzishwa kwa mjibu wa sheria ya Tanzania au katiba ya Tanzania, chombo hicho kitakuwa mali ya Tanzania na kitafanya kazi kwa maslahi ya Taifa na si vinginevyo.

Katika Kitabu cha Ujasusi nimeainisha mapendekezo yangu kwenye sheria ya Usalama wa Taifa ambayo nafikiri kwasasa sheria hiyo ni lazima ifanyiwe marekebisho ili kuendana na mageuzi ya dunia ya leo, tuko karne ya 21 sio enzi za zamadamu.

Moja ya vifungu katika Sheria ya Usalama wa Taifa iliyosainiwa 20 January 1997 na Rais Hayati Benjamiji W. Mkapa ambavyo ni muhimu sana kufanyiwa marekebisho ni. Mfano, kifungu 14 -(1), (2),(3), (4)-(a) na (b). Kifungu cha 15 -(1),(2), (3) -(a) na (b). Kifungu cha 16-(1) (a)na (b), (2) na (3).

Katika kitabu nimehimiza muundo wa Idara ambao umepitwa na wakati ubadilike, muundo huu unahusu kuanzia uajiri (recruiting) na mengineyo, Mfumo wa chama kimoja wa 1962 ulikuwa ndio mfumo wa uajiri wa vyombo vyote vya ulinzi na usalama, na ndio ulikuwa mfumo wa ajira zingine, ilikuwa huwezi kuingia katika vyombo vya ulinzi na usalama bila kupita TANU YOUTH League/UVCCM.

Hadi ilipofika 1992 ndipo mfumo huo ulianza kutoweka katika sekta zingine, lakini katika vyombo vya dola haukutoweka kabisa, Hivi leo watumishi wa vyombo vya dola wengi walioingia kazini kuanzia 1992 kurudi nyuma hadi 1962, hawa ni makada wa chama cha mapinduzi 100%.

Wengi wao leo ni watu wazima ndio ma RPC, OCD na wakuu wa vitengo mbalimbali katika vyombo vya utumishi na vya dola, Hivyo ukimuona RPC anashangilia ccm ikishinda sio kosa lake bali itikadi kwake imekolea na aliingia jeshini kwa tiketi ya chama na sio professional yake.

Kizazi kilichoingia kwenye vyombo vya ulinzi na Usalama miaka ya karibuni angalau hiki msingi wa kuingia kwao ni elimu, undugulaizesheni na kuipenda kazi husika, japo ukada bado una nguvu ndani ya vyombo hivyo, kwamba leo unaweza kuona maajabu RPC anastaafu leo na kesho akagombea uenyekiti wa ccm mkoa au Ubunge utajiuliza lini aliuwa mwanachama kama katiba ya ccm inavyotaka awe mwanachama angalau miaka miwili.

Sera ama Malengo makuu ya Ujasusi Tanzania yanatakiwa kujikita katika Uchumi kwakuwa hakuna njia ya mkato ya kufikia mafanikio ya Taifa kiuchumi bila kuruhusu uchumi wetu uongozwe katika misingi ya Idara ya Usalama wa Taifa na Jeshi la Wananchi Tanzani (TISS na MI).

Hapa ieleweke sana, sina maana biashara na makampuni ya uwekezaji yawe ya vyombo hivyo vya ulinzi, au yawe ya serikali, la hasha, nina maana pana zaidi kwamba ushughulikiaji wa taarifa za biashara na uchumi utiliwe mkazo zaidi kuliko ilivyo sasa taarifa za kisiasa ndizo zenye nguvu ya nchi, Mapendekezo ni TIFF itilie mkazo taarifa za uchumi na biashara zaidi na kuzipa ulinzi shughuli na biashara zote za uwekezaji wa ndani na nje na wawekezaji wake. Hawa waitwe rasmi kuwa ni (asset).

Tanzania iwe na shirika la Ujasusi linaloangalia siasa kama njia tu, na sio msingi imara wa kulinda TAIFA, wanausalama watakao kuwa makini kuona kofia ya siasa haizidi kofia ya nguvu ya umma au TAIFA. Ni wakati mwafaka wa kutambua NCHI ndio nguzo ya UTAIFA na sio siasa kuwa ndio UTAIFA wenyewe.

Kusimamia Demokrasi kwa jicho la ndani na sio jicho la upendeleo wa kiitikadi bali kuongozwa na kusimamia maadilli ya NCHI dhidi ya siasa. Inatakiwa Shirika ambalo halitatumika kwa faida ya chama, Mtu au kikundi cha watu bali ukweli uwe Taifa lianitaji nini kutoka kwenye siasa. Nchi inaishi katika lindi la unafi hasa vijana.

Kwa undani zaidi, soma kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi popote ulipo duniani.


View attachment 2468314
Dahh . Ila we jamaa unaandika ww!!🤣🤣🤣
 
TISS na Jeshi hawawezi kuukwamua uchumi wetu, hakuna maendeleo yoyote duniani ya kiuchumi yamepatikana kwa njia hii.
Huo wizi ulioiutaja hapa hauhusiani na uchumi. Maendeleo ya uchumi yanahitaji uongozi na mfumo mzuri wa kisiasa pamoja wachumi nguli wanaopewa uhuru kutimiza majukumu yao.
Nimesema ni kazi yao mojawapo. Hakuna nchi inatenganisha intelligence services na uchumi.
Kwani kipi hakihitaji uongozi na mfumo mzuri wa kisiasa, ni michezo, utalii au nini. Au kipi hakihitaji wasomi nguli wa fani hiyo kupewa uhuru wa kutimiza majukumu, tuseme afya, elimu au jeshi. Au kitu gani TISS ikiwa strong kinaharibika. Kwanza TISS haifanyi kazi yoyote ikiwa yenyewe bali inasaidiana na wizara au taasisi nyingine, kama kuna kesi ya rushwa TAKUKURU watahusika, kama kuna taarifa za kijasusi juu ya mgeni fulani mwenye hatari Uhamiaji watahusika. Sasa iweje unataka tuitenge na uchumi.

"An intelligence agency is a government agency responsible for the collection, analysis, and exploitation of information in support of law enforcement, national security, military, public safety, and [foreign policy objectives]"

Hizo foreign policy objectives hata uchumi upo, kama mfano tunataka kuwa vinara kwenye biashara ya korosho, tunataka kuwa soko la chai Afrika Mashariki hizo ni agenda ambazo intelligence agency inatakiwa ihusike.

Mojawapo ya kazi ni "Covertly influence the outcome of events in favor of national interests, or influence international security".
Hiyo influence in favour of national interests hata uchumi unahusika. Unless useme kama Tanzania haina mpango wowote kiuchumi inazubaa tu.
 
Hiki ulichoandika hapa sio kazi kuu za Idara za Usalama wa Taifa/Ujasusi duniani. Kazi za majususi ni ulinzi na usalama wa nchi masuala ya uchumi na biashara yataingizwa huko katika majuku yao kama ni kitisho cha usalama wa nchi zao au kama yataleta matokeo fulani kiusalama.

Hizi kazi za uchumi na biashara katika nchi ni kazi kuu za Wizara ya Fedha na Benki Kuu.
Hujui ukisemacho Mkuu.Ndani ya TISS kuna Dawati la Uchumi unadhani linafanyakazi gani? Hivyo hivyo BCI ya Polisi kuna dawati la uchumi.
 
TISS na Jeshi hawawezi kuukwamua uchumi wetu, hakuna maendeleo yoyote duniani ya kiuchumi yamepatikana kwa njia hii.
Huo wizi ulioiutaja hapa hauhusiani na uchumi. Maendeleo ya uchumi yanahitaji uongozi na mfumo mzuri wa kisiasa pamoja wachumi nguli wanaopewa uhuru kutimiza majukumu yao.

Hakuna uchumi bila ujasusi.

Uongozi mzuri unapatikanaje?
Au unafikiri vitu vizuri vinapatikana kienyeji?

Kama ulivyosema moja ya Malengo makuu ya ujasusi ni ishu za ulinzi na usalama.
Sasa sijui unaelewaje kuhusu Ulinzi na usalama.

Ulinzi na usalama unajumuisha mfumo mzima wa Maisha ya binadamu,
Masuala ya kijamii, kiuchumi, kisiasa, kiutamaduni n.k.

Sasa utawezaje kuwa na ulinzi na usalama katika uchumi bila ya ujasusi?
Utawezaje kuwa na ulinzi na usalama katika utamaduni pasipo ujasusi?

Hakuna Uongozi mzuri au Maendeleo ya uchumi pasipo ujasusi.
Kama wewe ni mfanyabiashara mkubwa huwezi kuwa mfanyabiashara mkubwa pasipo ujasusi.
 
Nimesema ni kazi yao mojawapo. Hakuna nchi inatenganisha intelligence services na uchumi.
Kwani kipi hakihitaji uongozi na mfumo mzuri wa kisiasa, ni michezo, utalii au nini. Au kipi hakihitaji wasomi nguli wa fani hiyo kupewa uhuru wa kutimiza majukumu, tuseme afya, elimu au jeshi. Au kitu gani TISS ikiwa strong kinaharibika. Kwanza TISS haifanyi kazi yoyote ikiwa yenyewe bali inasaidiana na wizara au taasisi nyingine, kama kuna kesi ya rushwa TAKUKURU watahusika, kama kuna taarifa za kijasusi juu ya mgeni fulani mwenye hatari Uhamiaji watahusika. Sasa iweje unataka tuitenge na uchumi.

"An intelligence agency is a government agency responsible for the collection, analysis, and exploitation of information in support of law enforcement, national security, military, public safety, and [foreign policy objectives]"

Hizo foreign policy objectives hata uchumi upo, kama mfano tunataka kuwa vinara kwenye biashara ya korosho, tunataka kuwa soko la chai Afrika Mashariki hizo ni agenda ambazo intelligence agency inatakiwa ihusike.

Mojawapo ya kazi ni "Covertly influence the outcome of events in favor of national interests, or influence international security".
Hiyo influence in favour of national interests hata uchumi unahusika. Unless useme kama Tanzania haina mpango wowote kiuchumi inazubaa tu.

Huyo anafikiri ujasusi kazi yake ni mambo ya upolisi Polisi pekee.
Hapo ndipo anapokwama,
 
Nimesema ni kazi yao mojawapo. Hakuna nchi inatenganisha intelligence services na uchumi.
Kwani kipi hakihitaji uongozi na mfumo mzuri wa kisiasa, ni michezo, utalii au nini. Au kipi hakihitaji wasomi nguli wa fani hiyo kupewa uhuru wa kutimiza majukumu, tuseme afya, elimu au jeshi. Au kitu gani TISS ikiwa strong kinaharibika. Kwanza TISS haifanyi kazi yoyote ikiwa yenyewe bali inasaidiana na wizara au taasisi nyingine, kama kuna kesi ya rushwa TAKUKURU watahusika, kama kuna taarifa za kijasusi juu ya mgeni fulani mwenye hatari Uhamiaji watahusika. Sasa iweje unataka tuitenge na uchumi.

"An intelligence agency is a government agency responsible for the collection, analysis, and exploitation of information in support of law enforcement, national security, military, public safety, and [foreign policy objectives]"

Hizo foreign policy objectives hata uchumi upo, kama mfano tunataka kuwa vinara kwenye biashara ya korosho, tunataka kuwa soko la chai Afrika Mashariki hizo ni agenda ambazo intelligence agency inatakiwa ihusike.

Mojawapo ya kazi ni "Covertly influence the outcome of events in favor of national interests, or influence international security".
Hiyo influence in favour of national interests hata uchumi unahusika. Unless useme kama Tanzania haina mpango wowote kiuchumi inazubaa tu.
Nchi ikitaka kuwa kinara wa korosho, chai, tumbaku au bidhaa nyingine yoyote katika masoko ya nchi nyingine kinachotakiwa ni kuzalisha na kufikisha bidhaa bora zinazokidhi hayo masoko kwa gharama za chini kuliko wazalishaji wengine, sera nzuri za biashara na kodi ambazo zina support biashara za kimataifa na mahusiano mazuri ya kidiplomasia kati ya nchi. Huhitaji TISS au chombo cha ujasusi kufanikisha haya, ni mambo basics kabisa. Labda kama taifa linataka kupora uranium au mafuta kutoka taifa lingine au kuuza silaha ndio litahitaji majasusi rogue wanaofadhiliwa na corporations katika uhalifu huo.
 
DGIS mpya Ndugu Said Masoro si mtu maarufu katika korido za Ujasusi Dar es Salaam ukimlinganisha na mtangulizi wake Athuman Diwani ambae umaarufu wake ulijengwa akiwa Intelijensia ya Polisi, DCI na katibu Tawala, Masoro anaweza kuwa chachu ya magezi ya chombo hiki muhimu na uti wa mgongo wa taifa letu ikiwa hataruhusu kumezwa na siasa chafu za Dar na Dodoma.
 
Kwa kifupi elewa hivi Kazi kuu ya ujasusi ni kusaidiq kuweka mazingira salama ya raia kufanya maisha yao kwa ufanisi, iwe biashara au jambo lingine lolote, sio kazi ya taasisi za ujasusi kutuoa muelekeo wa uchumi, kuelekeza au kuingilia jinsi uchumi wa nchi unavyopaswa kwenda. Hii ni kazi ya wanasiasa viongozi na watunga sera.
Kufikiria kwamba taasisi ya ujasusi inaweza kuwa mwarobaini katika kuukwamua uchumi wa nchi ndio kituko kikubwa zaidi.

Zipo models nyingi za maendeleo duniani ila hakuna hata model moja ya maendeleo ya uchumi kutokana na nguvu ya spy agency.
Hakuna uchumi bila ujasusi.

Uongozi mzuri unapatikanaje?
Au unafikiri vitu vizuri vinapatikana kienyeji?

Kama ulivyosema moja ya Malengo makuu ya ujasusi ni ishu za ulinzi na usalama.
Sasa sijui unaelewaje kuhusu Ulinzi na usalama.

Ulinzi na usalama unajumuisha mfumo mzima wa Maisha ya binadamu,
Masuala ya kijamii, kiuchumi, kisiasa, kiutamaduni n.k.

Sasa utawezaje kuwa na ulinzi na usalama katika uchumi bila ya ujasusi?
Utawezaje kuwa na ulinzi na usalama katika utamaduni pasipo ujasusi?

Hakuna Uongozi mzuri au Maendeleo ya uchumi pasipo ujasusi.
Kama wewe ni mfanyabiashara mkubwa huwezi kuwa mfanyabiashara mkubwa pasipo ujasusi.
 
Kwa kifupi elewa hivi Kazi kuu ya ujasusi ni kusaidiq kuweka mazingira salama ya raia kufanya maisha yao kwa ufanisi, iwe biashara au jambo lingine lolote, sio kazi ya taasisi za ujasusi kutuoa muelekeo wa uchumi, kuelekeza au kuingilia jinsi uchumi wa nchi unavyopaswa kwenda. Hii ni kazi ya wanasiasa viongozi na watunga sera.
Kufikiria kwamba taasisi ya ujasusi inaweza kuwa mwarobaini katika kuukwamua uchumi wa nchi ndio kituko kikubwa zaidi.

Zipo models nyingi za maendeleo duniani ila hakuna hata model moja ya maendeleo ya uchumi kutokana na nguvu ya spy agency.

Upo sahihi Kabisa.

Hata uongozi Bora pekee sio mwarobaini as kuikwamua nchi kiuchumi.
Siku zote mambo yanategemeana
 
Hiki ulichoandika hapa sio kazi kuu za Idara za Usalama wa Taifa/Ujasusi duniani. Kazi za majususi ni ulinzi na usalama wa nchi masuala ya uchumi na biashara yataingizwa huko katika majuku yao kama ni kitisho cha usalama wa nchi zao au kama yataleta matokeo fulani kiusalama.

Hizi kazi za uchumi na biashara katika nchi ni kazi kuu za Wizara ya Fedha na Benki Kuu.
Hahaha kasome tanzania intelligence and security service Act 1996. Ujue kazi za hii idara ni nn... Nandomana Kuna kitengo kinaitwa FIU(financial intelligence unit) Kipo BOT kama left wing ya TISS na uzijue kazi za hii FIU hasa ni nn

Sent from my 701SO using JamiiForums mobile app
 
Alichoandika sio kazi kuu ya usalama wa taifa, ila ni kazi mojawapo. Mambo mengine yanafanyika, ulinzi na usalama wanafanya bado ujasusi wa kiuchumi.
Hao unaosema BoT na Finance hawawezi kufanya crandestine operations.

Wasovieti walioiba blueprints za atomic bomb kutoka Los Alamos pale Marekani sio wanasayansi wala watumishi wa jeshi, serikali ya Stalin ingeamua kusubiri jopo la wanasayansi lifanye testing na kila kitu wangetumia gharama kubwa mno na muda mwingi zaidi kupata breakthrough.

Wamarekani walioiba Lunik ya USSR ikiwa kwenye world tour hawakuwa wanasayansi wa NASA, walipiga picha na kukamilisha kazi yao kisha NASA wakatumia hizo taarifa.

Basically TISS isingekuwa na maana kama haitakiwi kufanya kazi fulani maana kila kazi ina wizara. Ulinzi na usalama si zina wizara zake, mambo ya ndani na ile ya ulinzi. TISS kamilifu inatakiwa iweze kusaidia popote pale, hata kampuni ya hapa nchini ikitaka kutengeneza pikipiki ikakwama kutengeneza injini, TISS inabidi iwe na uwezo wa kupata wapi la kupata ujuzi wa kutengeneza injini kwa namna yoyote ile. Ndio vitu duniani wanafanya, China mara nyingi tu unasikia wameiba TB za data kuhusu kitu fulani. Survival of the fittest
Kudos 👌
 
Back
Top Bottom