Uthubutu: Kijana atakayeelezea jinsi atakavyoizalisha elfu 50 ndani ya mwezi mmoja nitamkopesha bila riba

Uthubutu: Kijana atakayeelezea jinsi atakavyoizalisha elfu 50 ndani ya mwezi mmoja nitamkopesha bila riba

Broo m naomba kufaham viungo wanavyoweka kwa mishkak iwe mitam na ilolainika
Mkuu kwa sasa nafikiria kupata fedha kiasi kadhaa niboreshe hilo wazo,

Kwanza nataka niuze mishikaki vizuri siyo local tena kama mwanzo,
Nataka nitafute sehemu nzuri niweke meza flani hivi nilishadizine,
Then kwa juu naweka katent flani hivi na bango kubwaa,

Hapo itakuwa ni mishikaki ya Nundu plus Nyama ,
Then pembeni kutakuwa na ndizi za kuchoma pamoja na kukaanga ,chachandu flani hivi ya kuvutia,

Mavazi ,nitakuwa na mavazi flani special Tshirt ya kuprint yenye logal mbele na maandishi Nyuma,chini laba flani hivi na jinsi Nyeusi ya kuchomekea(lengo kuwa Nadhifu muda wote wa kazi)

Nje ya meza kutakuwa na Viti vya kudizine vitakavyowezesha kukaa watu nane tu (kila upande watu wanne,)

Yaani nataka niifanye kiaina flani hivi ambayo ata wewe mwenye Suti yako usione Aibu kushuka kwenye gari yako kuja kununua mishikaki ,

hapo kwa haraka haraka mchanganuo wangu mpaka sasa ulikuwa hivi.

Hiyo meza niliyodizine nilishaongea na fundi inacost kama 300k (ni ya chuma alafu itakuwa na umbo kama L )

Carpet yake ya kutandika meza (vile ninavyotaka mimi)35.

Majiko mawili 80k (kubwa 45k, dogo la karahi 35k)

Karahi 1. 9k

Meza na viti vile navyotaka kudizine vitanicost 150k,


Chuma nne za kusimama 120k (kila moja 30k)
Za juu 40k ,turubahi la kuweka 30k (hapo tent ) fundi sijajua bado

So hapo kwa haraka haraka 800k - 900k inatosha Biashara itakuwa kama vile ninavyotaka mimi,

Nilishaweka kiasi kadhaa na bado nazidi kuweka Akiba, wazo langu halina haraka sana nategemea kuanza ikifika mwezi wa Sita hivi ,

Eneo ninalotegemea kuweka ni mapito ya watu wa aina tofauti

Biashara yenyewe.
Nitakapoanza biashara nategemea kuanza kwa bei ya kawaida tu ,
Kila mshikaki utauzwa shilingi 500,
Ndizi ya kuchoma shilingi 500,
Na ndizi ya kukaanga shilingi 400,

Pembeni ya jiko kutakuwa na mishikaki pia midogo ya shilingi mia 2, mia 2 kwa ajiri ya wanafunzi na watoto.

Ongezeko la bidhaa itaongezeka kulingana na ongezeko la wateja watakaokuwa wanakuja mfano.

Naweza kuweka mihogo,maziwa fresh kwa Jioni, maini na firigisi za kuku Nk.

ila tu sitaweka chipsi nataka nidili na hivyo Vitu tu na nitasimamia mwenyewe.

Nb.
Kwenye banda langu la kiepe kama kawa watu wapo wa kufanya kazi mimi binafsi nataka nigeukie huko kwanza


Cc Zero IQ

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna biashara ya kuuza kuni visiwani(wavuvi)wanaoweka kambi kwa ajili ya kuvua dagaa nikitulia ntakuja niitolee mchanganuo ila 50 ndogo kwa wazo hili

Biashara hii iko hivi,,

Pesa ya kununulia miti( inategemeana bei ya mti na kijiji ulipo) nilipo miti ni kwa 10000 mpaka 20000

Gharama za kukata miti na kuichana ili kupata vipande vya kuni(kama mtu yuko njema kimwili anaweza kufanya mwenyewe ama kutumia mashine yako binafsi kama unayo ni) njia rahisi waweza kukodi mashine (bei ya hapa siijui ila kwa kukadiria haiwezi kuzidi 50,000) kwa miti 50
Mashine nayoizungumzia hapa ni zile zinazokata miti na kuchana mbao zipo ndogo kati na kubwa sina uzoefu na hizi mashine ila naamini wengi tunazifahamu hasa wanaoishi kwenye miji midogo

Gharama nyingine ni ya kusafirisha kuni kwa gari/pikipiki kutokea zilipo mpaka kwenye mwalo tayari kupakia tena kwenye boti mpaka kisiwa husika,, hapa ukipachungulia kuna usafiri mara mbili kwa gari na boti pia kupakia na kupakua( kwa sehemu nilipo zote hizi ni shilingi elfu 80,,,, yaani usafiri tu pasipo ununuzi wa miti ama kukata na kuchana)

Kadirio ni mti mmoja kutoa vipande 50 vya kuni, kwa kuanzia ili kuweza kujaza canter ni wastani wa miti 50 ambapo ukizidisha hapo utapata jumla ya vipande 2500 vya kuni ( wazoefu mnisaidie kujua kama canter kwa pisi 2500 ni mkubwa, mdogo au saizi halisi)

Bei ya kipande kimoja cha kuni visiwani ni shilingi 700-1000

mzigo kama huu kuwa umeisha ni siku 7-10 (ukizoeleka au ukawa na kambi nyingi za kuuzia siku zinapungua hapa nimehesabia siku hizo kwa kambi moja kubwa ama ndogo ndogo 3)

Gharama jumla ni mil 1.3

Mauzo kwa shilingi 700 kwa kipande kimoja kuzidisha 2500= 1,750,000 kuna faida ya shilingi 620,000
Mara nyingi malipo hufanyika mwisho wa giza ama papo hapo inategemea na mazungumzo yako wewe na mteja wako

NB; Kama mashine ni yako gharama zinapungua vilevile faida inapanda

Kama ni nguvu zako mwenyewe kukata mti na kupasua hizi kuni kutokana na wingi basi itakuchukua muda mrefu kuweza kumaliza kazi hivyo kupunguza faida njia hii ni ngumu kuliko ugumu wenyewe

Siko vizuri katika kuandika hesabu za kwenye karatasi tuvumiliane
Kisiwa kipo boss

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi si tajiri ila nataka kuwafundisha utu na ubinadamu matajiri walioko JF.

Nataka kijana mwaminifu mmoja kutoka Jf nimwazime 50 na airejeshe baada ya mwezi mmoja au miwili ili nimwazime mwingine.

Changanua wazo lako na weka namba ya simu kama utapenda kuiweka hapa Kisha members wengine watanisaidia kumchagua mtu sahihi.

Please huu sio mkopo kwa wanaojiweza kwa sababu hauna riba na utakuwa umedhulumu haki ya mwingine.

Masharti na vigezo vitazingatiwa. Mshindi atatakiwa kusubmit some of his/ her details PM.

Pesa nitamtumia au kumkabidhi Ijumaa 21/ Febuari/2020.

Shindano litadumu kwa siku 3 tu.


UPDATES
23:15 Jumatano, nimefunga shindano
Nashukuru kwa mliojitokeza kuwania hichi kiasi kidogo cha 50.
Niko busy kidogo na majukumu na washiriki ni wengi.
Ninaomba Jumamosi weekend ndio nipitie post to post ili kuleta haki.
Mshindi atatangazwa na nitampa pesa mkononi kama yuko Dar na kama yuko mkoani nitamtumia na ya kutolea.
Kila mwezi nitafanya kitu hichi na atakayetengeneza faida kubwa zaidi nitampa Pesa nyingi zaidi.

UPDATES
JUMAMOSI SAA 2:50 ASUBUHI
Nimeanza kufanya sorting, niko page number 3. Leo hii hii mshindi atatangawa.

UPDATES
09:15 AM
Nimemaliza uchambuzi wa awali na kupata post 22 zenye nguvu zaidi.
Nakunywa chai kisha nimalizie kusort na kupata vijana 3 nitakaowaleta mbele yenu, asanteni.

Updates
09:48 am
Saturday
Nimepata watu hawa, na uchambuzi unaendelea miongoni mwao.
Kama kuna mtu hajatendewa haki anaruhusiwa kuleta malalamiko within one hour.
Walioingia kwenye kinyang'anyiro ni;
1.Zero IQ post no.29
2.Zwenge Ndaba post no.
3.Noelia, post no.170
4.CONTROLA post no.175
5.Davie post no.236
6.Naipenda Familia yangu, post.#57
7.Peramiho Yetu post #30
8.FK21 post #147.

Updates
1930 hrs
Ninaomba radhi kwa kuchelewesha matokeo ya mwisho.
Sikuwa hewani kwasababu zilizo nje ya uwezo.
But nikitulia nitamaliza kazi leo hii hii na mhusika atapewa chake kwa kadri tutakavyokubaliana njia ya kumfikishia Pesa yake.

Updates
23: 50
Nawashukuru washiriki wote wa shindano hili dogo.
Ninatamani kila mshiriki nimpe pesa nyingi kwaajili ya wazo lake ila kamba yangu ni fupi.
Nawashukuru pia wasomaji na wachangiaji wa Uzi huu.
Washindi ni hawa wafuatao;
3: Zwenge Ndaba, katika post yake #208 inayoelezea biashara ya maziwa kutoka Chalinze kwenda Kibaha au Dar es salaam.
2.Peramiho Yetu, katika post yake #30 anaelezea biashara ya Mahindi mabichi ya kuchoma kutoka Stereo Temeke .
1:Napenda Familia Yangu, katika post yake #57 ameelezea biashara ya maandazi na half cake .
Mimi kwasasa nitaanza na kutoa zawadi kwa mshindi nambari 1.
Kwa atakayekuniunga mkono anaweza kuungana nami kuwapa mtaji washindi nambari 2 & 3 au kumwongezea mtaji mshindi nambari moja.

Note:
Nitaendeleza hili jambo kila baada ya mwezi mmoja na ninawashauri watakaokosa wajaribu tena.
Mshindi anione pm

Hongera sana kuna siri kubwa kwenye kutoa[emoji1376]
 
hv kwa nn most of forex traders u dont talk about ur loss. yaan mnavomotivate watu as if hyo bussness hainaga loss...asee tell them the truth
Sisi wa Forex ngoja tukae kimya maana huwa mnatutukana. Ngoja nimalixe UE nitafute laki niweke itakuwa inanilisha nikirudi semester ijayo. Sahivi nimetoa hela yote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa kijana yoyote ambae ramani hazijakaa sawa namshauri afwate huu ushauri kwa moyo wote na akili zote na kama ataona aibu ahame mkoa akaifanye mkoa mwingine kwa uhuru.kwani ni biashara ya mtaji mdogo na yenye faida kubwa.

Mimi ni shuhuda wa hii biashara na sijaiacha hadi leo.nilipomaliza college na kielimu cha diploma ya pharmacy nimedispense dawa kwenye maduka makubwa ya wahindi kwa miezi 3 tu nikiwa nalipwa laki 5 na nusu.
Nkaacha kazi nkasepa chuga kuuza mishkaki! Wazaz,ndugu na jamaa wacha wanilaumu mno hakuna hata mmoja alienisupport ila sasa hivi wananipongeza!

Yani watanzania wengi sijui tukoje,mtu yupo radhi afanye kazi ya heshima ila haina maslahi makubwa kuliko kazi isiyo na hadhi yenye faida lukuki.ndani ya mwezi wa kwanza tu niliingiza faida ya m1.2!sasa ndugu zangu wana jf kipi kilikua bora kati ya kugawa dawa huku ukiwa na clinical coat ndani ya kiyoyozi mhindi anakupelekesha siku nzima kafunga na camera kabisa kila kona ukichat au ukisinzia ni msala,kazi unaingia saa 1.30 hadi saa 2-3 usiku kila siku huku upande wa mishkaki nilikua nadaamka saa10 kwenda machinjioni kununua nyama kwa bei chee narudi naandaa saa12 niko shule ya msingi naanza kuwachomea madogo saa 6 mchana nshamaliza naingia mtaani kuangalia mishe nyingine,jioni tena huyo maeneo ya stendi kuchoma mishkaki.

Najua ni ngumu sana kwa msomi ila toka mkoa uliopo wanakujua nenda sehemu ambayo hakuna hata anaejua kama ulifika hata la 7!

Nilianza hivyo taratibu hatimae nkaweka vijana waaminifu niliowatoa vijijini huko na hivi nnavyoandika,naingiza si chini ya laki mbili faida kila siku ya Mungu bila pua za TRA wala cha Halmashauri
uko vzuri mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
hv kwa nn most of forex traders u dont talk about ur loss. yaan mnavomotivate watu as if hyo bussness hainaga loss...asee tell them the truth

Sent using Jamii Forums mobile app
Kama sasahivi nimechoma. Ngoja Corona iishe maana ndo imenisababishia hivi. Kupata loss ni kawaida na unawekeza kile ulicho tayari kupoteza.
 
hii post nimeisoma mara mbili mbili ,,,,mpaka nkarud kusoma na ile ya Zero IQ ,,,ukiangalia wale wauza mishkaki waweza ona kama wanapata faida kdogo sana almost 4000 tu per day kumbe they are making a lot duhh asanten wakuu.
Kwa kijana yoyote ambae ramani hazijakaa sawa namshauri afwate huu ushauri kwa moyo wote na akili zote na kama ataona aibu ahame mkoa akaifanye mkoa mwingine kwa uhuru.kwani ni biashara ya mtaji mdogo na yenye faida kubwa.

Mimi ni shuhuda wa hii biashara na sijaiacha hadi leo.nilipomaliza college na kielimu cha diploma ya pharmacy nimedispense dawa kwenye maduka makubwa ya wahindi kwa miezi 3 tu nikiwa nalipwa laki 5 na nusu.
Nkaacha kazi nkasepa chuga kuuza mishkaki! Wazaz,ndugu na jamaa wacha wanilaumu mno hakuna hata mmoja alienisupport ila sasa hivi wananipongeza!

Yani watanzania wengi sijui tukoje,mtu yupo radhi afanye kazi ya heshima ila haina maslahi makubwa kuliko kazi isiyo na hadhi yenye faida lukuki.ndani ya mwezi wa kwanza tu niliingiza faida ya m1.2!sasa ndugu zangu wana jf kipi kilikua bora kati ya kugawa dawa huku ukiwa na clinical coat ndani ya kiyoyozi mhindi anakupelekesha siku nzima kafunga na camera kabisa kila kona ukichat au ukisinzia ni msala,kazi unaingia saa 1.30 hadi saa 2-3 usiku kila siku huku upande wa mishkaki nilikua nadaamka saa10 kwenda machinjioni kununua nyama kwa bei chee narudi naandaa saa12 niko shule ya msingi naanza kuwachomea madogo saa 6 mchana nshamaliza naingia mtaani kuangalia mishe nyingine,jioni tena huyo maeneo ya stendi kuchoma mishkaki.

Najua ni ngumu sana kwa msomi ila toka mkoa uliopo wanakujua nenda sehemu ambayo hakuna hata anaejua kama ulifika hata la 7!

Nilianza hivyo taratibu hatimae nkaweka vijana waaminifu niliowatoa vijijini huko na hivi nnavyoandika,naingiza si chini ya laki mbili faida kila siku ya Mungu bila pua za TRA wala cha Halmashauri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yale matank ili maziwa yasigande
Asante mkuu,ila mshindi sio Mimi,Mimi nimeingia kwenye tatu bora tu.maziwa nimeshafanya research,unauza kwa order,unavyotoa unapeleka moja kwa moja kwa wateja kwa order.order ni nyingine Sana ,maziwa ni deal mjini.hayawezi kubaki.usichanganye na maji tu ,utajiharibia soko.pia in case yakibaki unazalisha ya mgando.nayo Ni bei kuliko fresh.mtaji ukiwa mkubwa unafungua kifrem kabisa.na unanunua vifaa Kama Yale matank ili maziwa yasigande
yakoje haya??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sio kwamba unataka kuiba wazo la watu? Kama ulichoandika ndio nia yako hongera sana maana hata wenye mitaji lakini ni wavivu wa kufikiri watafaidika
Ndo ananunua idea kwa 50000
 
FK21 nmekuchek inbox but hujajbu chochote
WAZO HILI HAPA

Kwa mtaji wa elfu 50 nitaenda kariakoo kununua tishirt za shilingi elfu 4 classic kwa bei ya jumla tishirt 13 zitagharimu shilingi Elfu 48

( siongei theoretical hii biashara nina experience nayo kuna mda nilikuwa naagizwa na mtu kumchukulia mzigo tishirt ni classic kweli.)

baada ya hapo nitakuja kuziuza kwa bei ya TSH 800 kwa kila tishirt ambapo kwa tishirt 13 nitapata elfu 96000
Note: hizo tishirt nitaziuza kwa mda wa one week only.


Baaada yahapo nitarudisha nilichikuwa nimekopeshwa na kusimama mwenyewe .



Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom