Utitiri wa vyama vya wafanyakazi chanzo cha kukosa umoja wao

Utitiri wa vyama vya wafanyakazi chanzo cha kukosa umoja wao

Retina

JF-Expert Member
Joined
Mar 6, 2015
Posts
1,039
Reaction score
1,163
Kuelekea maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani,wafanyakazi nchini wako kwenye mjadala wa kikokotoo,bima ya afya,nyongeza ya mishahara,kupanda n.k. huku wakikosa umoja na mtetezi atakayesimama kuwasemea ili kufika pale wanapotaka.

Kwa miaka kama tisa au kumi tangu utawala wa Rais Kikwete,wafanyakazi nchini hawajawahi kuongezewa mishahara licha gharama za maisha kuongezeka mara tano zaid ya kipindi cha JK,hakuna anyewasikiliza, hii inatokana na kukosa umoja kutokana na utitiri wa vyama vya wafanyakazi vinavyofikia 33+ ambavyo badala ya kuwatetea,viko kwa ajili ya kuwanyonya wafanyakazi.

Wakati mjadala wa nyongeza ya mishahara ukiendelea likaibuka suala ya bima ya afya kukataliwa kwenye baadhi ya hospital, binafsi sikuona chama cha wafanyakazi kilichosimama kukemea hilo.

Kabla hakujapoa kwenye bima likaibuka Kikokotoo,huu mjadala no moto hauna mwisho lakini ungemalizwa na vyama vya wafanyakazi kama wangekuwa imara ,hatujaona malumbano kati ya Tucta wakiibana serikali kufuta sheria ya kikokotoo ambayo haina maslahi kwa mstaafu.

Wafanyakazi nchini wanapitia kipindi kigumu kutokana kukosekana kwa mtetesi, mtetesi wao wamegawanyika kutokana na utitiri wa vyama huku wengi wa viongoz na makada wa chama tawala na wako kwa ajili ya kuwanyonya wanachama kupitia michango na sio kutetea maslahi ya wanachama.

Yawezekana serikali ikaweka mapandikizi kwenye vyama hivi vya wafanyakazi na ndio maana unaweza ukaona serikali ikiyafumbia madudu yanayofanywa na CWT ambayo yamepelekea uundwaji wa Chama kipya cha walimu,siku hizi kuna vyama vya manesi,najiuliza iko wapi nguvu ya vyama ya vya wafanyakazi?

Nitawashangaa sana kama wataimba ule wimbo wa SOLIDARITY siku ya Mei Mosi.
 
Viongozi wote wa juu wa hivyo vyama wanateuliwa na nani??
 
Hivyo vyama vipo kupiga pesa za mfanyakazi sio kumtetea.
 
Changamoto ya vyama vya wafanyakazi ni viongozi wao kuwa machawa wa CCM na hivyo kutokuwa na nguvu za kusukuma ajenda za wafanyakazi!

Kwa ilivyo sasa vyama vyote ni matawi ya CCM na vipo kwa ajili ya kulinda maslahi ya viongozi wa serikali!

Kwa kifupi vyama vyote vya wafanyakazi havistahili kuendelea kuwepo kwa kuwa ni laana kwa wafanyakazi!
 
Kuelekea maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani,wafanyakazi nchini wako kwenye mjadala wa kikokotoo,bima ya afya,nyongeza ya mishahara,kupanda n.k. huku wakikosa umoja na mtetezi atakayesimama kuwasemea ili kufika pale wanapotaka.
Kwa miaka kama tisa au kumi tangu utawala wa Rais Kikwete,wafanyakazi nchini hawajawahi kuongezewa mishahara licha gharama za maisha kuongezeka mara tano zaid ya kipindi cha JK,hakuna anyewasikiliza,hii inatokana na kukosa umoja kutokana na utitiri wa vyama vya wafanyakazi vinavyofikia 33+ ambavyo badala ya kuwatetea,viko kwa ajili ya kuwanyonya wafanyakazi.
Wakati mjadala wa nyongeza ya mishahara ukiendelea likaibuka suala ya bima ya afya kukataliwa kwenye baadhi ya hospital, binafsi sikuona chama cha wafanyakazi kilichosimama kukemea hilo.
Kabla hakujapoa kwenye bima likaibuka Kikokotoo,huu mjadala no moto hauna mwisho lakini ungemalizwa na vyama vya wafanyakazi kama wangekuwa imara ,hatujaona malumbano kati ya Tucta wakiibana serikali kufuta sheria ya kikokotoo ambayo haina maslahi kwa mstaafu.Wafanyakazi nchini wanapitia kipindi kigumu kutokana kukosekana kwa mtetesi,mtetesi wao wamegawanyika kutokana na utitiri wa vyama huku wengi wa viongoz na makada wa chama tawala na wako kwa ajili ya kuwanyonya wanachama kupitia michango na sio kutetea maslahi ya wanachama.
Yawezekana serikali ikaweka mapandikizi kwenye vyama hivi vya wafanyakazi na ndio maana unaweza ukaona serikali ikiyafumbia madudu yanayofanywa na CWT ambayo yamepelekea uundwaji wa Chama kipya cha walimu,siku hizi kuna vyama vya manesi,najiuliza iko wapi nguvu ya vyama ya vya wafanyakazi?Nitawashangaa sana kama wataimba ule wimbo wa SOLIDARITY siku ya Mei Mosi.
WAGAWE UWATAWALE
Yes, absolutely!
"Divide and Rule" Tactic.

Utitiri huu uliopo wa vyama vya Wafanyakazi umeanzishwa makusudi na Serikali ili kurahisisha Wafanyakazi wasiwe na Umoja madhubuti. Ukisikia 'hila na ghiriba' za kiutawala Ndio hizi.
Utaratibu huu ulianzishwa makusudi kwa 'nia ovu' ya kukidhibiti, kukipunguzia nguvu na kuua kilichokuwa Chama cha Wafanyakazi ambacho kilikuwa na nguvu kubwa zaidi ya ushawishi kwa Wafanyakazi hapa Tanzania kilichoitwa kwa jina la OTTU.
 
Back
Top Bottom