Utofauti wa mishahara katika Utumishi wa umma, kunavunja moyo na kusababisha watu kubeza kusoma sana

Roho mbaya ni pamoja na kufurahia ubaguzi wa mishahara unaofanya wengine waishi kama wafalme na wengine waishe kama vijakazi wa mfalme ili hali wote wana elimu inayofanana.
Ila wabongo kwa ubinafsi ni kwamba aliye kwenye advantaged position anachoweza kukufanyia ni kejeli tu 🤣!
Ni busara hata kukaa kimya tu maana hamna la kufanyika ila atakukejeli juu!
 
Kuna siku nimetamani kulia aisee. Nipo na kadegree kangu niko halmashauri XYZ nawasiliana na jamaa angu yupo TAWA ananiuliza je una mpango gani nijikwamue kutoka kwenye ka mshahara haka kadogo nilikonako. Nikamwambia nataka mwaka huu nikasome masters aisee ili nione kama nitapata promoshen ya cheo na mshahara pia ili niweze kuwa na take home ya laki 9plus.
Jamaaa akanichekaa sanaa. Akanambia huko kwenye halmashaur mwenye masters anafukuzia take home ya laki 9 wakati sisi huku kwenye mamlaka au mashirika ya umma mwenye masters anakuja 5M.
Nilichoka aiseeeee
 
Halmashauri ni kubovu sana ndio maana watu wanazikimbia kazi za serikali. Kuna watu wanamenya jamani..imagine unakunja 5M una credibility ya kukopesheka.
 
Ila wabongo kwa ubinafsi ni kwamba aliye kwenye advantaged position anachoweza kukufanyia ni kejeli tu [emoji1787]!
Ni busara hata kukaa kimya tu maana hamna la kufanyika ila atakukejeli juu!
Brother classes never end. Na kupanga ni kuchagua [emoji3]

Degree niliyosoma Mimi kunawatu wanakula tgsd, Kuna watu wanakula 1.6m na Kuna watu wanakula 3m

Kuna wenzetu walikuwa wanasoma Sana tukawakejeli Sana kwamba tutaajiriwa sawa tu mwisho wa siku Ila saiv tuko tofauti.
 
Huu ubaguzi mbaya sana, halafu unaleta dharau kwa wale wanaolipwa mishahara kama manamba ila jamii imeridhika tu.
 
Kuna mzee mmoja sasa ni mstaafu alifanya kazi nsssf tangu miaka ya 80 amekuja kustaafu miaka ya 2015 anakwambia hata naibu waziri alikuwa hamkaribii kwa mshahara. Na alikuwa hajui mshahara unatoka lini. Yy akiangalia mshahara tarehe 24 mwezi wa 5 atakuja kuangalia tena tarehe 24 mwezi wa 10 hukooooo. Hana wasi wasi bahasha za ofisini posho ndo zinaendesha familia kusomesha na kujenga. Aiseee nilichoka zaidi nakujiona sisi wa halmashauri tutaenda mbinguni kama ndo kigezo.
 
Inategemea na ulipo yani
 
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] aisee
 
Uko vizuri. Salute kwako.
 
Inategemea na ulipo yani
Yes inategemeana na ulipo, Ila kwangu Mimi siwezi kumuonea wivu mtu anayepata salary kubwa kuliko Mimi kwa sababu nazijua hastle za kuipata hiyo mishahara. Kwa mfano huyu wa 3m, tuliitwa watu 280 kwenye interview na anatakiwa mtu mmoja tu.
Mwamba anayepata hapo unamuoneaje wivu ?
 
Yes inategemeana na ulipo, Ila kwangu Mimi siwezi kumuonea wivu mtu anayepata salary kubwa kuliko Mimi kwa sababu nazijua hastle za kuipata hiyo mishahara. Kwa mfano huyu wa 3m, tuliitwa watu 280 kwenye interview na anatakiwa mtu mmoja tu.
Dah hizo kazi zina changamoto sana
 
Mkuu, hujanishawishi. Na unaweza kukuta huyo jamaa aliyeshinda hakutoa jasho hata nukta, jina lake lilikuwa limeshaandikwa nyie kwenye interview mlikwenda KUJILA tuu
 
Yah hii itasaidia pia hata kupunguza nyodo makazini sababu wengine huona wenzao kama takataka tu sababu ya mishahara ya ajabu ajabu.
 
Mkuu, hujanishawishi. Na unaweza kukuta huyo jamaa aliyeshinda hakutoa jasho hata nukta, jina lake lilikuwa limeshaandikwa nyie kwenye interview mlikwenda KUJILA tuu
Sawa ila hayo Mambo ya nyuma ya pazia hakuna anayeyajua lakini Mimi naongelea jinsi zile kazi zilivyo chache na zilivyo special kiasi kwamba hata Leo mtu akiniambia anapata mshahara 5m siwezi kuufikiria kwa sababu najua hizo kazi ni finyu Sana.
 
Kuelimika ni kujiajiri au kutengeneza ajira kwa wengine........
 

Attachments

  • ttt.jpg
    5.5 KB · Views: 11
Kiufupii Kama mtu haridhikii hukoo stoke awapishee wengine waingieee hukoo
 
Nasoma comments hapa ili nipate kujua ukweli wa hili.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…