UTT AMIS naona kwenye account yangu ya UTT hela imeongezeka kidogo

UTT AMIS naona kwenye account yangu ya UTT hela imeongezeka kidogo

Came on man..huu ni undezi wa ajabu yani niweke 10m nipata 88k per month..umasikini huu tunautafuta wenyewe huku tukitajirisha wengine.

#MaendeleoHayanaChama
Kwaninukijenga nyumba ya vyumba viwili kodi unachukua ngapi?
Hiyo nyumba ya vyumba viwli ukiweka na kiwanja na gharama zote za ujenzi unaweza ukakuta inazid 10m . Na kodi unapata maximum 120k kwa mwezi. Sasa ndo uwekezaji wa Utt
 
Kwaninukijenga nyumba ya vyumba viwili kodi unachukua ngapi?
Hiyo nyumba ya vyumba viwli ukiweka na kiwanja na gharama zote za ujenzi unaweza ukakuta inazid 10m . Na kodi unapata maximum 120k kwa mwezi. Sasa ndo uwekezaji wa Utt
Bora hata nyumba unaweza ombea mkopo au kuiuza zaidi ya hiyo hela.

Kuliko hela ipo tu haifanyi chochote kisha unapesa 88k per month yani 10m ikupe hiyo hela kwa mwezi sibora mninyonge basi.

Wanaowekeza utt either wazembe na wavivu na waoga..au wanahela nyingi sana hawana pa kuzipeleka au wazee wali staafu wanasubiri kufa.

#MaendeleoHayanaChama
 
Tatizo kubwa la waafrika ni ubishi usiokuwa na maana yotote UTT Wana mifuko sita, thamani ya vipande inatofautiana, mtoa madam amezungumzia Bond fund ambapo bei ya kipande ni sh. 114 , amesema Kila kipande gawio ni sh. 1, sasa inategemea una vipande vingapi. Narudia tena tusiwe wabishi tutafute taarifa sahihi kwenye vyanzo sahihi.
Sasa huoni hata kama una vipande 50000 ambavyo thamani yake ni milioni 70,000 bado utapata nyongeza ya Tsh 50000 pekee kama gawio ndo hilo
 
Milioni 10 gawio ni 88,390/= kwa kila mwezi. Hii ni hela kubwa mno kwa fedha iliyowekwa pending ktk biashara yaani iliyokua haina kazi. Hili gawio kwa cc walala hoi tunalipa bills nyingi sana kwa mwezi[emoji2957][emoji2957][emoji2957]
Uwekezaji wa 10mil kupata gawio la 88,000 unasema inakusaidia lipa bills?
 
Utetezi mkubwa sana

Eti nimeacha kuuza mazao

Eti ndo tumewekeza kwa ajili ya uzee huyu dalali ndo kasema hivi
 
Kuna watu wanaenda kupigwa tena muda si mrefu. Eti sisi sio kama wale
 
Uwekezaji wa 10mil kupata gawio la 88,000 unasema inakusaidia lipa bills?
Milioni 10 hata ukianzisha mpesa kwa mwezi faida ni zaidi ya 500k.

10m ni pesa nyingi sana kupewa gawio la 88k kwa mwezi.

Mimi ni mtaalamu wa haya mambo ya uwekezaji kwenye mifuko ya fedha na UTT. Kwa hapa Tanzania bado soko changa sana hivyo faida ya 88k ni kubwa sana inawezekana kabisa usipate kitu kwa mwezi mzima 😂.

Kwa sasa bora mtu ununue hati Fungani za serikali kuliko kuwekeza kwenye utt ana hisa za haya mabenki.

Kwa watu wenye pesa ya ziada, extra ama excess fund ndio wawekeze huko kwa sababu wanayo hela nyingi ya kufanyia ama kuzungusha na kuishi ila kama una hela ya kubahatisha achana na hayo mambo. Bora kufungua duka la Mangi😂.
 
Shida nnayoona hapa kwa wanaobeza UTT ni hawajui kuhusu kitu kinaitwa compound interest.

Kwanza niseme ndio iwapo una biashara yenye faida basi kupata 100k kwa mwezi kutoka UTT utaona ni jambo dogo. Ila lengo la UTT si kulinganishwa na biashara bali ni kukupa kipato kutoka kwenye pesa ambayo haizalishi kwa muda huo. Hii inaweza kuwa savings ama pesa uliyopata kwa mkupuo na bado haujaipangia matumizi. Badala ya kuweka beki ni vizuri ikae UTT ili angalau ishalishe kitu.

Turudi kwenye compound interest na jinsi ya kuitumia na UTT ili kufanya savings vizuri kwa ajili ya utaporetire.

Tutumie mfano wa jamaa ambaye ameweka 10m. Na tuseme kwa mwaka UTT Inatoa faida ya 10% kwa mwaka. Na pia tuseme jamaa ana mpango wa kuretire baada ya miaka 20. Na mwisho tuseme jamaa kila mwezi ana uwezo wa kuongezea 100k kwenye akaunti yake ya UTT.

Kwa kutumia calculator iliyopo hapa: Compound Interest Calculator | Investor.gov baada ya miaka 20, jamaa atakuwa amechangia jumla ya milioni 32 katika mfuko. Ila salio lake litakuwa milioni 150. Hivyo atakuwa amepata ziada ya milioni 120 kwa ajili ya kuretire huku akichangia 100k tu kwa mwezi.

Mnaweza kutumia calculator hiyo ili kuona jinsi kushiriki katika mfuko wa UTT unaweza kuwa na manufaa kwa savings za muda mrefu.
Thamani ya vipande haishukagi?
Na ukitaka kuchukua hela yako, unauza vipande vyako? Ama unaichukua tu?
 
Wakuu Jana nimefanikiwa kupata gawio la mwezi kwa mara ya kwanza tokea nilipowekeza.

Asante wadau wote mlionipa taarifa kuhusu UTT AMIS. Ndugu wanaosita kuwekeza huko wafanye hivyo kwani hawa jamaa ni real
View attachment 2383160
Duuh labda kama mtu huna mawazo kabisa ya biashara au ni mtu mvivu.

10mil upate elfu 87 kwa mwezi ni bora utafute center nzuri mjini ufungue mpesa na wakala wa crdb/nmb.
 
Back
Top Bottom