UTU: Ubalozi wa Marekani wasaidia ujenzi wa vyoo vya kisasa kwenye shule za Iringa na Morogoro

UTU: Ubalozi wa Marekani wasaidia ujenzi wa vyoo vya kisasa kwenye shule za Iringa na Morogoro

Ni lini sisi dona kantri tutaanza wajengea vyoo mabeberu, maana hii ni dharau sasa.
Kwani tukiuza v8 moja tu ya mkurugenzi tutajenga vyoo vingapi?
 
Miongoni mwa Watu ambao huwa nakubali pale Waafrika tukidhihakiwa Wapumbavu na Wazungu ni Mimi. Karne hii bado pia tunajengewa Vyoo?
JE HOTUBA ALIYOITOA RAISI TRUMP SEPTEMBER 2018 JUU YA AFRIKA KATIKA MKUTANO WA UMOJA WA MATAIFA NI MATUSI AU NDO UKWELI?


Haya ni mambo yaliyonukuliwa katika hotuba ya Raisi Trump akiongelea bara la Afrika. Naomba usome na utoe maoni yako. Akiwa anawasuta viongozi wa Afrika, Trump anahoji kwamba:
  • lkiwa sasa imefika miaka 50 ya uhuru na bado viongozi wengi wa Afrika wameshindwa kuwa na miundo mbinu thatbiti kwa ajili ya watu wao, je hao viongozi ni binadamu kweli?
  • Anaendelea kusema kuwa ikiwa ninyi viongozi mnakalia dhahabu, almasi, mafuta na uranium na watu wenu wanakosa chakula, je ninyi viongozi wa afrika ni watu kweli?
  • Kama mnakaa kwenye madaraka na kununua silaha kutoka kwa wageni na kuua watu wenu, je ninyi ni binadamu kweli?
  • Kama mnawaza kukaa madarakani mpaka mwisho wa maisha yetu, je ninyi ni binadamu kweli?
  • Ikiwa mnatumia maliasili ya nchi zenu kwa maendeleo ya familia zenu, je ninyi ni watu kweli?
  • lwapo hamjali kuweka miundo mbinu ya afya za watu wenu na badala yake mkiugua mnaenda kutibiwa nchi za nje, Je ninyi ni binadanu kweli?
  • Mtaheshimikaje katika mataifa yenu wakati mnapiga risasi raia wenu kama vile ni mchezo?
*Amemalizia kwa kusema kuwa viongozi wa Afrika wataendelea kuwa kama wanyama hadi watakapo badili mtazamo wao na kuheshimu watu wanaowaongoza.

NB: Hadi kufikia hapo, unadhani Raisi Trump inatakiwa alaumie kutokana na tabia zake za kutukana waafrika, au labda anachosema ni kweli tukubaliane na yeye?
Una maoni gani kutokana na hotuba aliyoitoa huko kwenye kikao cha umoja wa mataifa? Hizi ni dharau za wazungu au kuna ukweli ndani yake?
.
 
Hela moja tu ya kumnunua Diwani wa chadema Ili aunge juhudi inatosha kujenga vyoo kwa kutumia nguvu Kazi ya wananchi wa eneo husika.
 
JE HOTUBA ALIYOITOA RAISI TRUMP SEPTEMBER 2018 JUU YA AFRIKA KATIKA MKUTANO WA UMOJA WA MATAIFA NI MATUSI AU NDO UKWELI?


Haya ni mambo yaliyonukuliwa katika hotuba ya Raisi Trump akiongelea bara la Afrika. Naomba usome na utoe maoni yako. Akiwa anawasuta viongozi wa Afrika, Trump anahoji kwamba:
  • lkiwa sasa imefika miaka 50 ya uhuru na bado viongozi wengi wa Afrika wameshindwa kuwa na miundo mbinu thatbiti kwa ajili ya watu wao, je hao viongozi ni binadamu kweli?
  • Anaendelea kusema kuwa ikiwa ninyi viongozi mnakalia dhahabu, almasi, mafuta na uranium na watu wenu wanakosa chakula, je ninyi viongozi wa afrika ni watu kweli?
  • Kama mnakaa kwenye madaraka na kununua silaha kutoka kwa wageni na kuua watu wenu, je ninyi ni binadamu kweli?
  • Kama mnawaza kukaa madarakani mpaka mwisho wa maisha yetu, je ninyi ni binadamu kweli?
  • Ikiwa mnatumia maliasili ya nchi zenu kwa maendeleo ya familia zenu, je ninyi ni watu kweli?
  • lwapo hamjali kuweka miundo mbinu ya afya za watu wenu na badala yake mkiugua mnaenda kutibiwa nchi za nje, Je ninyi ni binadanu kweli?
  • Mtaheshimikaje katika mataifa yenu wakati mnapiga risasi raia wenu kama vile ni mchezo?
*Amemalizia kwa kusema kuwa viongozi wa Afrika wataendelea kuwa kama wanyama hadi watakapo badili mtazamo wao na kuheshimu watu wanaowaongoza.

NB: Hadi kufikia hapo, unadhani Raisi Trump inatakiwa alaumie kutokana na tabia zake za kutukana waafrika, au labda anachosema ni kweli tukubaliane na yeye?
Una maoni gani kutokana na hotuba aliyoitoa huko kwenye kikao cha umoja wa mataifa? Hizi ni dharau za wazungu au kuna ukweli ndani yake?
.
Sasa kama Vyoo tu tunajengewa nao Wazungu na bado tena Mikopo ya Fedha tunawaomba kila Uchao Wakitutukana na Kutudhihaki wanakosea?
 
Hii ni aibu Sana kwa awamu chakavu inayotumia gharama kubwa Sana za kodi yetu kupambana na upinzani badala ya maendeleo. Hicho choo hata milioni 30 haifiki kwa kutumia nguvu za wananchi.
 
Hii ya leo, misaada ya kibinadamu itaendelea tu.

Inji hii buana...mbwembwe mingi, kelele saana lkn vyoo tu vinatushinda. Hao hao wana approve manunuzi ya gari 470m kwa wakurugenzi just sababu wanasaidia kuiba kura !!
Then uchaguzi umeisha wanawageuka..

Eti serikali ya wanyonge..
 
Hivi kuna misaada ambayo si ya kibinadamu? Hata ujenzi wa barabara unalenga kuhudumia binadamu. Sijui ni misaada ipi ambayo si ya kibaindamu?
Hawana nyimbo hao wamebakia kudandia dandia vitu vidogo vidogo tu
 
Taarifa inayosambaa inaonyesha kwamba maboresho hayo yamefanyika kwanye shule 25 za Mikoa ya Iringa na Morogoro , ambapo wanafunzi elfu 14 wametajwa kunufaika na mpango huo.

Mojawapo ya choo kilivyoonekana kabla ya Maboresho.

View attachment 1656831

Hapa chini ni muonekano mpya baada ya Maboresho.

View attachment 1656832

Mungu wabariki Wazungu
Mkurugenzi wa wilaya kilichopo hiki choo anatembelea gari ya mil400+.
Hii inawezekana tu Afrika
 
Hii ya lini kwani? Si mlisema mabeberu wamekataa kutoa msaada kwa ajili ya Lissu kushindwa uchaguzi?
Mnataka msaidiwe kujenga hadi mashimo ya choo

Kweli serikali chini ya ccm ya inashindwa kuwaletea maendeleo wananchi wake...
 
Sijui tumelaaniwa na nani yarabi! Hata vyoo? How comes choo cha shule kinaachwa hadi kifikie hali inayoonekana kwenye picha ya kwanza? Mkuu wa wilaya yupo; afisa elimu wilaya yupo; DED yupo; mbunge yupo; (wote hao ni mwendo wa VX-R V8); maafisa kata wapo; kamati za shule zipo; wazazi wapo; mwalimu mkuu yupo; walimu wapo; tatizo nini? Kazi yao nini? Kula mishahara?

Hadi beberu atoke maelfu ya maili huko kugundua kuna vyoo vya shule nchini Tanzania vimechoka? Nchi hii haina tatizo la fedha tena; lilishakuwa historia tangu awamu ya tano iingie madarakani! Wapinzani walokuwa wanatuchelewesha hawapo tena!
Kweli ni ajabu mno.
 
Back
Top Bottom