Uwanja wa Benjamin Mkapa | Ligi ya Mabingwa Afrika, Simba SC Vs Plateau United

Uwanja wa Benjamin Mkapa | Ligi ya Mabingwa Afrika, Simba SC Vs Plateau United

Wazalendo wa nchi tu ndo tukutane hapa, cha kushangaza kenge kibao watajoin na dua zao mbaya kwa taifa. Haya mautopolo ni kama machadema tu asee.
Mkuu acha kufananisha Utopolo na akili kubwa!
Hujui kuwa Chama chako kina unasaba na Utopolo,!
 
Nimesikitishwa na kitendo cha utopolo kwenda kuipokea Plateau airport. TfF iwafungie waliohusika kujihusisha na masuala ya soka maisha yao yote.

Hii ni picha mbaya sana kwa shirikisho letu la soka. Fungia utopolo hao.
 
Mabingwa wa Nchi Simba SC, Mnyama Mkali Kuliko Wote Mwituni Jumamosi ya leo Disemba 5, 2020 watakuwa uwanja wa Benjamin Mkapa kupapatuana na Plateau United, kutoka nchini Nigeria kwenye mchezo wa marudiano Ligi ya Mabingwa Barani Afrika.

Mchezo wa leo unatarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua kwa muda wote wa dakika 90 huku Simba SC wakipewa nafasi nzuri ya kushinda kutokana na kupata ushindi ugenini wa bao moja bila majibu kwenye mchezo wa kwanza uliopigwa nchini Nigeria kwenye uwanja wa New Jos matokeo ambayo Plateau United wakitaka kuweka rekodi ya kupindua matokeo.

Kocha wa Simba SC, Sven Vanderbroeck kuelekea mchezo wa leo amesema " Utakuwa mchezo mgumu, na mchezo ambao tumepishana kwa goli moja, hivyo lazima tuwe makini na natarajia mashabiki watajitokeza kwa wingi kushangilia. Timu yao ni nzuri hivyo tunahitaji kila aina ya nguvu ambayo tunayo ili tuweze kupata matokeo mazuri" amesema Vanderbroeck

Kulipewa Mwana... Kulitaka Mwana

Kumbuka mtanange huu wa kombe la Mabingwa Afrika ni kuanzia saa 11:00 jioni. Azam Sports 1 HD Live na Ghazwat na Jopo zima la JF litakuwa hapa Mubashara kukuletea mtanange huu kinagaubaga.

Usikose Ukasimuliwa..View attachment 1642028
Mkuu upo vizuri Sana kwa kuanisha nyuzi za mechi ya moja kwa moja...nashauri update kama hizi uwe unaziweka kwenye uzi wetu Rasmi wa Simba sports maana uzi wetu umedumaa wanatuzidi hata UTOPOLO kuwa na comments nyingi angalau tumewazidi Kila kitu na sisi tunavyovingi vya kujivunia...sehemu nyingine ya mitandao ya kijamii tumewaacha mbali Ila humu wametuzidi
 
Mkuu upo vizuri Sana kwa kuanisha nyuzi za mechi ya moja kwa moja...nashauri update kama hizi uwe unaziweka kwenye uzi wetu Rasmi wa Simba sports maana uzi wetu umedumaa wanatuzidi hata UTOPOLO kuwa na comments nyingi angalau tumewazidi Kila kitu na sisi tunavyovingi vya kujivunia...sehemu nyingine ya mitandao ya kijamii tumewaacha mbali Ila humu wametuzidi
Kuna application za kuongeza comments, download ziwe nyingi

Sent from my Nokia 1 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu upo vizuri Sana kwa kuanisha nyuzi za mechi ya moja kwa moja...nashauri update kama hizi uwe unaziweka kwenye uzi wetu Rasmi wa Simba sports maana uzi wetu umedumaa wanatuzidi hata UTOPOLO kuwa na comments nyingi angalau tumewazidi Kila kitu na sisi tunavyovingi vya kujivunia...sehemu nyingine ya mitandao ya kijamii tumewaacha mbali Ila humu wametuzidi
Tutawaeleza Mods waunganishe nyuzi zetu zoooote za VPL uzi wetu utakuwa na posts mara 100 ya Utopolo usijali.
 
Mkuu upo vizuri Sana kwa kuanisha nyuzi za mechi ya moja kwa moja...nashauri update kama hizi uwe unaziweka kwenye uzi wetu Rasmi wa Simba sports maana uzi wetu umedumaa wanatuzidi hata UTOPOLO kuwa na comments nyingi angalau tumewazidi Kila kitu na sisi tunavyovingi vya kujivunia...sehemu nyingine ya mitandao ya kijamii tumewaacha mbali Ila humu wametuzidi
Mkuu fanya research fupi kwenye huo uzi wa yanga kisha uniambie ni comments za namna gani zilizojaza uzi

Uzi ule umejaa comments za lawama na manung'uniko wakiwashutumu viongozi wao. Angalia katika sakata la morrison jinsi mashabiki wa yanga walivyojawa na gubu


Fatilia siku ile tuliyowapiga goli nne, wana yanga wote waliususa ule uzi wa updates kisha waka-switch a side kwenda kwenye uzi wao kila mmoja kutoa la moyoni

hii ni siku ambayo comments zilitolewa na wadau kwa wingi sana, huku katika hizo comments hakuna comment ambayo ilikua ina positive contents

Sasa simba haina migogoro wala inferior kama yanga na ndio maana uzi wetu umetulia tu hakuna mabishano wala maombolezo kwasababu timu inafanya vizuri
 
Back
Top Bottom