Ligi ya Mabingwa barani Afrika kuendelea kupigwa leo November 29, 2020 ambapo, Klabu ya Plateau United, inawakaribisha Mabingwa nchini Tanzania Simba SC, Mnyama kunako dimba la New Jos nchini Nigeria.
Mchezo unatarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua kwa muda wote wa dakika 90 hasa ukizingatia kwamba kila timu inataka kuanza vema kwenye michuano hii ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Kocha wa Simba SC, Sven Vanderbroeck amesema " Hatuna taarifa kuhusu wao lakini mwanzoni tutaanza kwa kuimarisha eneo la ulinzi na kuangalia uimara na udhaifu wao upo eneo gani na baada ya hapo tutaangalia cha kufanya.
" Kila kitu kipo sawa na kila mmoja yupo tayari kwa mchezo na wana furaha kwa hilo, tulichofanyia kazi kwa wiki kadhaa inabidi tukitumie leo, mipango yetu imejikita zaidi upande wetu ili kuhakikisha tunapa ushindi" amesema Sven Vanderbroeck
Kulitaka Mwana, Kulipewa Mwana
Kumbuka mtanange huu wa kombe la Klabu Bingwa Afrika ni kuanzia saa 10: 00 za huko, saa 12: 00 kwa za Tanzania. Usikose Ukaambiwa..!
Update:
=======
Klabu ya Plateau United imezuia kuonyesha matangazo ya moja kwa moja (mubashara) mchezo huu, hata hivyo viongozi wetu chini ya mtendaji mkuu Barbara Gonzalez wanapambana ili mchezo huu uwe Live kwenye Runinga
View attachment 1637428