Tetesi: Uwazi wa RC Makonda na StarTv siri hii hapa nje ndani

Tetesi: Uwazi wa RC Makonda na StarTv siri hii hapa nje ndani

Huyu Makonda anawahangaisha sana.
Sasa kama walikutana wawili kwa siri haya yote umeyapata wapi au ndio m'mbea mpe picha story ataandika mwenyewe..?
Mlisema hamtaangalia kipindi chake sasa haya yote ya nin..?
Huko huko Malaika mlisema Alivamia kipindi XXL wapo kwenye show mpaka watangazaji wakakesha ili tu wasidhurike leo mnasema alikuja mapema tu na kuonana na Dialo.
Mbona mnasahau mliloongea juzi kila siku mnakuja na jipya?
Hawa watu wanachekesha sana, kama bado kunamtu anawaamini aisee hospital ya wale jamaa zetu pale Dodoma inawahusu, walisema alikuwa Mwanza bottom (night club), leo wanasema alikuwa Malaika, eti kampuni imefirisika mpaka Samwel Nyalla kaamua kuondoka, mtu alikuwa mahututi India kwa matibabu washenzi wanakuja kudanganya malofa wenzao, mwafa.
 
Ni vyema taarifa hii angeliileta mdokezaji,vinginevyo ni uzushi.
 
Napata tabu sana kuuamini huu uzi moja kwa moja, sjui kwanini. Hayo mazungumzo ya siri kati ya Makonda na Dialo kayaskiaje ilihali kasema walikuwa wawili?. Duu hiyo inshu ya kupewa ukatibu sasa ndio kaniacha hoi, Ccm ni taasisi kubwa, hata kama ni Manyumbu ukatibu hauwezi kuuzwa kijinga hivyo, Tena na Makonda? Hapana nakataa, mleta Uzi mi nipo neutral ila nimeshindwa kuelewa na kuamini
Baki tu njia kuu Mkuu.

''Lisemwalo........"
 
Mamlaka za juu hata ziwe juu vipi haziwezi zidi vichwa vya watu hasa watu werevu na wenye utambuzi wa baya na zuri,kama watu hawa wamekataa hata sura yako itokee juu ya Maji jua wamekataa tu. Tatizo kubwa la Makonda hana kauli nzuri,kiburi na majivuno kwa Sana'a kiasi kwamba wnafikia mpaka kuwaona Binadamu wote wanaomzunguka ni wajinga na wanastahili kuchapwa viboko kama alivyosema kwenye speech yake ya mwisho hivyo sitashangaa hata akionekana huko Star tv akaendelea kuongea mbovu mbovu

Ifike mahali tuache kumshangaa Makonda, tumpuuze! Hapo yy ndipo mwisho wa uelewa wake, na anajiona yuko pouwa tu! Rejea Askofu Gwajima "zero on paper translate zero in brain!! Na wale wanaocheza kila wimbo wake kumbuka hii" Birds of the same feather flock/tweet together"
 
Umenikumbusha,diallo pia aliwahi kumiliki kampuni ya ndege,leo kafilisika,kafulia,kawa masikini wa kutupwa,kweli maisha yanakimbia,kwa kasi ya Ussain Bolt!!
mmh mkuu umeshadadia kufulia kwa Diallo, lazima kuna kitu alikutenda si bure
 
Ni vyema taarifa hii angeliileta mdokezaji,vinginevyo ni uzushi.
Mleta habari mwenyewe anasema "inasemekana" mara eti sasa hiyo habari niyakuaminika kweli!!!? Ama yakusadikika tu.hahaha na kuna watu wametoa povu hilo mpaka mishipa ya shingo imewasimama jamani.
 
Huyu hahitaji kusamehewa maana hadi sasa hayuko tayari. Msimlazimishe aombe msamaha. Aliomba msamaha kanisani na msikitini. 😉😉😉😀😀
 
Kipindi ni lini na saa ngapi? TEF Hawako fair, wanatunyima habari kwa sababu ya ugomvi wao na kiongozi. Eti wanadai(TEF) uhuru wa habari wakati wanambania mwenye habari..

Una u ndugu na bashite au ndiyo uelewa wako juu ya uhuru wa habari ulipoishia?
 
UWAZI WA MAKONDA STAR TV SIRI HII HAPA NJE NDANI!

Baada ya Paul Makonda hali yake kisiasa kuchafuka kutokana na matendo yake hivi karibuni alikuja Mwanza na kubaini kuwa kwa sasa amepoteza mvuto Kabisa kutokana na kukosa kiki kwenye vyombo vya habari na baadhi ya marafiki zake kuanza kumkimbia.


Inasemekana ujio wa Makonda Mwanza ilikuwa ni Kwa ajili ya kuweka mambo sawa na Mkurugenzi wa Star Tv ndugu Antony Dialo, ambaye walikutana Kwa siri na Mkurugenzi huyo.

Imebainika kuwa Makonda alikuja Kwa malengo matatu la kwanza ni kujaribu kuweka mambo sawa na Dialo ambaye pia ni mwenyekiti wa chama mkoa wa Mwanza ambaye anaunga mkono tamko la Jukwaa la wahariri kutokurusha habari za Makonda.

Imefahamika katika lengo la kwanza walimtisha mzee Dialo kama atashindwa kufanya kazi pamoja na Makonda watamuondoa mara moja ndani ya chama Kwa kumvua nyadhifa zote za uongozi.

Jambo la pili tulilodokezwa ni kwamba Hali ya uchumi ni mbaya katika kampuni ya Sahara iliyopelekea MD wake ndugu Sammy Nyala kuondoka kutokana kushuka sana kibiashara katika kampuni hiyo inayomilikiwa na Mzee Dialo siku hizi hawafanyi vizuri kibiashara na ukichangia na Deni la zaidi ya shilingi bilioni nne kutoka TRA.

Makonda alimuhaidi atamsaidia kuongea na mamlaka za juu kumpatia TAX HOLIDAY endapo atakubali kufanya naye kazi na kurusha taarifa zake Yeye Makonda.

Makonda katika safari ya Mwanza aliambatana na Ray pamoja JB ambaye hivi karibuni amemteua kuwa mhamasishaji wa wasanii katika kusambaza taarifa za Makonda mitandaoni.

Katika Siku ya Pili pale Malaika Resort Makonda alisikika akiongea kwenye simu na mtu ambaye alionekana kumtii sana ndani ya chama na kumpatia taarifa juu ya adhima ya Antony Dialo kuifikiria zaidi nafasi ya Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi.

Jioni walipokutana Katika hotel ya Malaika Resort Majira ya Jioni Gari ya mzee Dialo ilifika, Makonda na Dialo walizungumza tena Kwa kirefu na kupanga jinsi gani wataweza kufanya kazi pamoja mojawapo ni kujisafisha kuhusu uvamizi wa Clouds Media ili kuizima ishu ya Uvamizi mipango ipangwe haikuwa ishu ya Gwajima bali tetesi za uwepo wa Dawa za kulevya rejea tamko aliloliandika Mzee Dialo.

Pia wakati wanazungumza na Mzee Dialo, Makonda alimjulisha kuwa tayari mipango ya kumuandalia nafasi ya Ukatibu mkuu ndani ya chama CCM Taifa imekwishaiva hivyo asiwe na wasiwasi pale Mkutano Mkuu Taifa utakapoitishwa muda wowote kuanzia sasa kumjadili Nape Nnauye basi ndiyo utakuwa muda muafaka wa jambo lake kuingizwa kwenye ajenda ya Mkutano Mkuu.



Chanzo kilidokeza kuwa Makonda alimuhaidi kumpatia Dialo Kiasi cha fedha ambacho atachukua kutoka kwa Wafanyabiashara marafiki zake wa Dar kwa ajili ya kumsaidia kulipa madeni na Mishahara kwa wafanyakazi wake Kwa mwezi wa 3 hadi wa 6 kwani inasemeka wafanyakazi hao wengi wao bado hawajalipwa Mishahara yao isipokuwa posho ndogo zilizopo Kwa ajili ya kujikimu kwa kuwa hali ya Uchumi kwenye kampuni hiyo ni Mbaya sana.

Kingine Makonda amehaidi kumsaidia Anthony Dialo kwa kumpatia ulinzi kwa kipindi Chote watakachokuwa wanafanya kazi pamoja kumlinda na hasira kutoka Kwa waandishi wasio unga mkono harakati za Makonda.

Baada ya kumaliza Maongezi na na Makonda inasemekana Dialo aliwaita wafanyakazi wake na kujadiliana wajipange jinsi gani ya kufanya kazi na Makonda kitu ambacho Wafanyakazi wametafsiri kuwa ni ishara mbaya kwa kituo hicho cha habari hasa ikichangiwa na uhusiano mbovu na dharau alizozionyesha Makonda kipindi cha nyuma kwa wafanyakazi wa kituo hicho.

Unaambiwa Baada ya Antony Dialo kumaliza kile kikao aliwashinikiza wafanyakazi wake kuwa asiyetaka aondoke akatafute kazi sehemu nyingine Kwa kuwa tayari ajenda pekee alizobaki nazo kwa siri kichwani ni Ukatibu Mkuu wa chama na kusamehewa madeni anayodaiwa.

Kwa Taarifa zilizopo mzee Dialo alikwenda South Africa haijulikani alikwenda kufanya nini, nitaendelea kuwajuza kwa kadri iwezekanavyo juu ya ziara hiyo na kila kitu kitakuwa wazi.

Hii sasa ni kufuru kama Paul Makonda ataendelea kutumia ukaribu wake na Mamlaka za juu ili tu aendelee kujinufaisha Kwa maslahi yake binafsi.
Asante kwa taarifaa mkuu
 
UWAZI WA MAKONDA STAR TV SIRI HII HAPA NJE NDANI!

Baada ya Paul Makonda hali yake kisiasa kuchafuka kutokana na matendo yake hivi karibuni alikuja Mwanza na kubaini kuwa kwa sasa amepoteza mvuto Kabisa kutokana na kukosa kiki kwenye vyombo vya habari na baadhi ya marafiki zake kuanza kumkimbia.


Inasemekana ujio wa Makonda Mwanza ilikuwa ni Kwa ajili ya kuweka mambo sawa na Mkurugenzi wa Star Tv ndugu Antony Dialo, ambaye walikutana Kwa siri na Mkurugenzi huyo.

Imebainika kuwa Makonda alikuja Kwa malengo matatu la kwanza ni kujaribu kuweka mambo sawa na Dialo ambaye pia ni mwenyekiti wa chama mkoa wa Mwanza ambaye anaunga mkono tamko la Jukwaa la wahariri kutokurusha habari za Makonda.

Imefahamika katika lengo la kwanza walimtisha mzee Dialo kama atashindwa kufanya kazi pamoja na Makonda watamuondoa mara moja ndani ya chama Kwa kumvua nyadhifa zote za uongozi.

Jambo la pili tulilodokezwa ni kwamba Hali ya uchumi ni mbaya katika kampuni ya Sahara iliyopelekea MD wake ndugu Sammy Nyala kuondoka kutokana kushuka sana kibiashara katika kampuni hiyo inayomilikiwa na Mzee Dialo siku hizi hawafanyi vizuri kibiashara na ukichangia na Deni la zaidi ya shilingi bilioni nne kutoka TRA.

Makonda alimuhaidi atamsaidia kuongea na mamlaka za juu kumpatia TAX HOLIDAY endapo atakubali kufanya naye kazi na kurusha taarifa zake Yeye Makonda.

Makonda katika safari ya Mwanza aliambatana na Ray pamoja JB ambaye hivi karibuni amemteua kuwa mhamasishaji wa wasanii katika kusambaza taarifa za Makonda mitandaoni.

Katika Siku ya Pili pale Malaika Resort Makonda alisikika akiongea kwenye simu na mtu ambaye alionekana kumtii sana ndani ya chama na kumpatia taarifa juu ya adhima ya Antony Dialo kuifikiria zaidi nafasi ya Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi.

Jioni walipokutana Katika hotel ya Malaika Resort Majira ya Jioni Gari ya mzee Dialo ilifika, Makonda na Dialo walizungumza tena Kwa kirefu na kupanga jinsi gani wataweza kufanya kazi pamoja mojawapo ni kujisafisha kuhusu uvamizi wa Clouds Media ili kuizima ishu ya Uvamizi mipango ipangwe haikuwa ishu ya Gwajima bali tetesi za uwepo wa Dawa za kulevya rejea tamko aliloliandika Mzee Dialo.

Pia wakati wanazungumza na Mzee Dialo, Makonda alimjulisha kuwa tayari mipango ya kumuandalia nafasi ya Ukatibu mkuu ndani ya chama CCM Taifa imekwishaiva hivyo asiwe na wasiwasi pale Mkutano Mkuu Taifa utakapoitishwa muda wowote kuanzia sasa kumjadili Nape Nnauye basi ndiyo utakuwa muda muafaka wa jambo lake kuingizwa kwenye ajenda ya Mkutano Mkuu.



Chanzo kilidokeza kuwa Makonda alimuhaidi kumpatia Dialo Kiasi cha fedha ambacho atachukua kutoka kwa Wafanyabiashara marafiki zake wa Dar kwa ajili ya kumsaidia kulipa madeni na Mishahara kwa wafanyakazi wake Kwa mwezi wa 3 hadi wa 6 kwani inasemeka wafanyakazi hao wengi wao bado hawajalipwa Mishahara yao isipokuwa posho ndogo zilizopo Kwa ajili ya kujikimu kwa kuwa hali ya Uchumi kwenye kampuni hiyo ni Mbaya sana.

Kingine Makonda amehaidi kumsaidia Anthony Dialo kwa kumpatia ulinzi kwa kipindi Chote watakachokuwa wanafanya kazi pamoja kumlinda na hasira kutoka Kwa waandishi wasio unga mkono harakati za Makonda.

Baada ya kumaliza Maongezi na na Makonda inasemekana Dialo aliwaita wafanyakazi wake na kujadiliana wajipange jinsi gani ya kufanya kazi na Makonda kitu ambacho Wafanyakazi wametafsiri kuwa ni ishara mbaya kwa kituo hicho cha habari hasa ikichangiwa na uhusiano mbovu na dharau alizozionyesha Makonda kipindi cha nyuma kwa wafanyakazi wa kituo hicho.

Unaambiwa Baada ya Antony Dialo kumaliza kile kikao aliwashinikiza wafanyakazi wake kuwa asiyetaka aondoke akatafute kazi sehemu nyingine Kwa kuwa tayari ajenda pekee alizobaki nazo kwa siri kichwani ni Ukatibu Mkuu wa chama na kusamehewa madeni anayodaiwa.

Kwa Taarifa zilizopo mzee Dialo alikwenda South Africa haijulikani alikwenda kufanya nini, nitaendelea kuwajuza kwa kadri iwezekanavyo juu ya ziara hiyo na kila kitu kitakuwa wazi.

Hii sasa ni kufuru kama Paul Makonda ataendelea kutumia ukaribu wake na Mamlaka za juu ili tu aendelee kujinufaisha Kwa maslahi yake binafsi.
rubbish, uongo mtupu. mnafiki sana wewe kiumbe
 
Mleta habari mwenyewe anasema "inasemekana" mara eti sasa hiyo habari niyakuaminika kweli!!!? Ama yakusadikika tu.hahaha na kuna watu wametoa povu hilo mpaka mishipa ya shingo imewasimama jamani.
Suala LA Makonda na vyombo vya habari linapofanywa kama siasa linaviharibu vyombo vya habari.
Sidhani kama kufungia habari za Makonda kutajustify weledi wa vyombo vya habari.
Jukwaaa LA wahariri na vyombo vya habari wanapaswa kubadilika kwani kwa kufanya hivyo wanawanyima watu uhuru wa kupata habari.
Vilevile si busara kwa wana habari /wanasiasa kutunga tunga habari bila ushaidi wowote kwa kutumia maneno "tetesi,inasemekana,nimedokezwa,nimetonywa n.k" ili eti kupima upepo au kuleta mijadala inayoharibu habari/taswira ya cho/vyombo cha/vya habari.
 
  • Thanks
Reactions: nao
Back
Top Bottom