Uwe maarufu au la, usijifanye una hela wakati huna! Utakuja umbuka msibani

Uwe maarufu au la, usijifanye una hela wakati huna! Utakuja umbuka msibani

Mambo ya familia ni changamoto hasa kwenye Mali. Nilikarabati nyumba ya familia na wazazi kuhamia kwangu nilipojenga. Nyumba ina wapangaji na hela inaingia Kwa ajili ya kuendesha familia. Cha ajabu ikitakiwa ukarabati naangaliwa Mimi. Ni ngumu jamani sababu Ile ni Mali ya familia sio ya MTU mmoja na mara nyingi wale ndugu wajanja wajanja wasiochangia kitu huwa Wana Fujo Sana wazazi wakitangulia.Ndio maana watu wanajitenga na Mali za familia.
 
Leo narudi kwa Babu yangu Kariakoo Mtaa wa Kariakoo kufungua juzuu na kupata mawaidha kuhusu husda.

Naomba msikilizeni Sheikh akitoa mawaidha dhidi ya husda, na mjiondoe kwenye kufanya dhambi ya husda mpaka misibani.

To be sure, mimi sina dini lakini mafunzo mazuri yaliyomo katika dini nayapenda.

Karibuni.


Nimepata darsaa murwaa

Mkuu Kiranga nimefurahi kuona ni mfuatiliaji wa mawaidha ya kiislamu

Karibu kwenye dini ya uislamu nawe uwe muislamu!
 
Wanaotaka makuu hata sio wazazi, ni watu tofauti ambao hata hawakuwepo wakati unahangaika kutafuta maisha
Kuwatunza wazazi Ni jukumu lako kijana. Usijisahau kwa hizo hips za mkeo ambae hathamini wazazi wako Tena anasukuma ndinga lako huku wazazi wako wanakwea usafiri wa mshkaki. Huko kijijini nyumba haielewek ninyi mmekalia picha za insta
 
Tutafute pesa, tupendezeshe kwetu (zikiwemo nyumba za ibada wanapoabudu wazazi nyumbani). Wenzetu wachaga wanachangia hata wakiwa huku mijini. Sisi toka Singida sijui tunakwama wapi?
**Haifurahisi unaendesha Gari Kali (Range Rover, VW, Ford au BMW) halafu home picha za kuibia, unavizia palipopambwa tu!
Naona umeitaja homecity ayee
 
Nimepata darsaa murwaa

Mkuu Kiranga nimefurahi kuona ni mfuatiliaji wa mawaidha ya kiislamu

Karibu kwenye dini ya uislamu nawe uwe muislamu!
Nashukuru kwa kufuagukia mawaidha.

Mimi ni mfuatikiaji mzuri wa mawaidhq na hata Quran ninayo naisoma.

Kuna sehemu ina mawaidha mazuri sana tu.

Kwa leo niishie hapo kuongelea upande huo.
 
Mambo ya familia ni changamoto hasa kwenye Mali. Nilikarabati nyumba ya familia na wazazi kuhamia kwangu nilipojenga. Nyumba ina wapangaji na hela inaingia Kwa ajili ya kuendesha familia. Cha ajabu ikitakiwa ukarabati naangaliwa Mimi. Ni ngumu jamani sababu Ile ni Mali ya familia sio ya MTU mmoja na mara nyingi wale ndugu wajanja wajanja wasiochangia kitu huwa Wana Fujo Sana wazazi wakitangulia.Ndio maana watu wanajitenga na Mali za familia.
Nakazia hapa
 
Heri ya mwaka mpya 2021 tuweke malengo ya kupaendeleza kwetu. Aibu ya 2020 tusiihamishie 2021. Hela unapata ila wazee wako umewasahau mpaka litokee tukio ndo tujue ulivyo.
 
Back
Top Bottom