mkuu mark my word gharama ya hiyo kiwanja haiwez kuzid 1m usd tatizo ni hiyo chain ya kuanzia mwenye kiwanja ,dalali, mkurugenzi , nadhani hata katibu mkuu wa fedha anahusika hapoKiwanja ni kikubwa sana zamani kulikuwa na kampuni ya kufyatua matofali pale... Kwa eneo lile dola milion 8 siwezi kubisha
Alafu wenye viwanja na nyumba za kawaida ukanda ule watakuja piga hela sana, maana ule ukanda utakuja kuwa wa magorofa mpaka huku TCRA.Kiwanja ni kikubwa sana zamani kulikuwa na kampuni ya kufyatua matofali pale... Kwa eneo lile dola milion 8 siwezi kubisha
Sana si umeona pale jirani landmark anajenga showroom ya maduka ya kisasa... Within 10yrs hili eneo litakuwa juu sanaAlafu wenye viwanja na nyumba za kawaida ukanda ule watakuja piga hela sana, maana ule ukanda utakuja kuwa wa magorofa mpaka huku TCRA.
Vipi wewe umepanga hapo au ndo wale wanaovuta pumzi waje uza nyumba/ viwanja vyao mabilioni ya hela?Sana si umeona pale jirani landmark anajenga showroom ya maduka ya kisasa... Within 10yrs hili eneo litakuwa juu sana
Sisi tuna nyumba ya familia maeneo hayo... Wengi hawajauza maeneo yao hapoVipi wewe umepanga hapo au ndo wale wanaovuta pumzi waje uza nyumba/ viwanja vyao mabilioni ya hela?
Ndugu zangu, hii si siri ila nimeamua tu kuwanong'oneza tu, sio tetesi ni taarifa za kweli na zinazoweza kuthibitishwa kwa nyaraka, vielelezo pia ushahidi.. Plz naomba msininukuu vibaya.. sijasema hili ni jipu, tezi, busha wala uvimbe.. hamkawii kunisingizia..
Ni taarifa zenye mapana ya ukweli unaoweza kuthibitishwa kuwa Mfuko wa Pensheni wa Mashirika ya umma japo kwa sasa wahusika na kuhifadhi na kulipa pensheni kwa sekta binafsi na zisizo rasmi.. Katika mipango mikakati ya kuwekeza michango ya wanachama wake kupitia sekta ya ujenzi wa nyumba, majumba n.k hivi karibuni mfuko umenunua kiwanja pembezoni mwa barabara ya Sam Nujoma {Mwenge-Ubungo} toka kwa kampuni binafsi kwa bei ya Dola za Kimarekani Milioni 8 sawa na zaidi ya bilioni 16.
Kwa ufahamu wangu mdogo sana, hizi ni pesa nyingi sana kutumika kununua kiwanja pakee katika maeneo husika.. Yamkini huu ni muendelezo wa maamuzi yasio na weredi, uzalendo, harufu ya ubadhirifu, kujinufaisha na tuhuma za wizi, ufisadi pia matumizi mabaya ya madaraka toka kwa viongozi/wafanyakazi/watumishi wanaopewa dhamana husika.
Kumekuwepo na kawaida yenye mizizi kwa wafanya manunuzi toka taasisi za Serikali {Mashirika ya Umma,Wizara na Wakala} kuweka cha juu mbali na asilimia 10 ambayo wamekuwa wakipata kwa lazima toka kwa wazabuni wenye kufanya kandarasi ktk taasisi husika.. Mzabuni asietoa asilimia 10 huyo amekuwa akikanwa, nyanyapaliwa, tengwa na zabuni zake kutupwa ama malipo yake kucheweleshwa kwa makusudi kabisa.
Kwa hili la PPF yamkini na taasisi zingine zenye kufanana na hii, Michakato ya manunuzi ya viwanja vya uwekezaji imekuwa ikihusisha idara zaidi ya moja katika kufikia maamuzi kama Miradi /Uwekezaji,Manunuzi {PMU}, Masoko {Marketing}, Sheria, Uhasibu na Utawala..
Hivyo basi kwa kuwa roho ya urafi, tamaa, wizi, ubadhirifu imekuwa mtambuka kwa kila mmoja kwa nafasi yake kushiriki {Mbuzi hula majani kwa urefu wa kamba yake} vivyo hivyo mapana ya chajuu huwa makubwa zaidi ili kukonga nyoyo za washiriki.
Hili laweza kuthibitishwa na ukweli wa mali wanazomiriki wahusika wakuu wa hii michakato kutofautiana mno na uhalisia wa vipato vyao halali na pia mapato yao ,vitega uchumi vyao kuongezeka mara tu malipo yanapofanywa kwenda kwa wazabuni walio katika miradi dili .
Uchunguzi mahsusi waweza baini taarifa za kina kwenye miradi yote mikubwa inayohusisha matumizi ya mabilioni ya kodi, michango, misaada, ruzuku kama Ujenzi wa Bomba la gesi, Ununuzi wa Vivuko, TPA, RITA, TCRA, UTT, NSSF, PSPF, SUMATRA, DART, TANESCO, TFDA, MSD, VETA, Gaming Board, NMB, EPZA, TANROADS, TBA, REA, WMA, TANAPA, NFRA, MNH, TPF, TPDC, TPDEF, UDSM, DIT, TAMISEMI {Halmashauri, DAWASA, Mamlaka za maji, Wizarani...n.k.
Uchunguzi uende mbele zaidi hata kuwabana wafanyabiashara wasio na maadiri wanaofanya biashara na serikari..
Mfano ktk hili la PPF je baada ya malipo nani na nani waligawiwa,walitumiwa fedha,walilipwa,walitafunishwa mishkaki ama kuyweshwa mvinyo wa ushindi...yale ya Mkombozi na Tegeta Escrow yaweza jitokeza ama la ya viroba, lumbesa, Visandarusi {Stanbic}
Nakiri mimi si mtakatifu, Si msafi, Si Mzalendo wa kutukuza... Tanzania inapaswa kufanyiwa kupasuliwa na kutakaswa kweli kweli... Mwenyezi Mungu awatie nguvu na maarifa viongozi wetu wenye kiu na nia ya dhati kurejesha heshima, utu, usawa na heshima kwa wote.
Kana unapajua, unafikiri pana thamani gani?? Kile kiwanja kama sio ukubwa wa football pitch nasi ni heka moja za mraba!Hapo mahali hakuna uwanja wa thamani hiyo.
Ukishaona hako kajina kwenye nyanja ya ujenzi basi hata usiulize tena ufisadi, muda utasema ukweli!ni hapa ambapo wanajenga estim floor 38 karibu na shell?
halafu nyie acheni kutetea wezi mkishaa kula MLUNGULA mnakimbilia huku kuja kupima upepo watu wanasema nin. ilo eno limeshaakuwa juu sikunyingi tu hata bila kuwepo hiyo landamark maduka ya kisasa kama unavyodai na uwekezaji wa namna hiyo ni wa kijinga ni sawa na wale wa mahotel wanaotegemea wafanye biashara na serikali kwenye kumbi zao za mahotel lakin kutoa 16bilion kwa ajili ya kununua kiwa kiasichozidi 4000sqm ni matumizi mabaya ya pesa za umma nadhani hatua sahihi zitachukuliwa na DR JPMSana si umeona pale jirani landmark anajenga showroom ya maduka ya kisasa... Within 10yrs hili eneo litakuwa juu sana
Wee unaongelea kiwanja gani?? Hiki kipp pale nafikiri kituo cha basi kivulini kwa wale wa kina sisi wa daladala, utaona kimezungusjiwa uzio na nondo zimetanda na mawinch yako juu.Ngoja wanaokijua hicho kiwanja waje watueleze vizuri, huwezi jua labda ni eneo lote linalopakana na barabara ya Sam Nojuma kutoka pale njia ya kwenda TRA-Mwenge mpaka kwenye taa za njia ya kuelekea Sinza makaburini!
Tupeni ushahidi ya dau ushahidi upo ni audit report ya 2014/14 sasa mkianza kuchokonoa tutaweka na Picha za nyumba anazomiliki TZ na londondah umemaliza mkuu, hutowaona wale waliokuwa wakimkandia dr dau humu, wanachungulia tu
Nasikia ukiona Estim au Alpha.... ni shida hawa jamaa!Ukishaona hako kajina kwenye nyanja ya ujenzi basi hata usiulize tena ufisadi, muda utasema ukweli!
Kiwanja chochote maeneo hayo japo sipafahamu vizuri hakiwezi kufikia bei hiyo, labda kama UDSM wameamua kukumilikisha nusu ya eneo lao lote. Ndio maana nikasema labda kama ni kutoka kwenye traffic light za kwenda Sinza makaburini mpaka round about ya Mwenge njia panda ya kwenda TRA/NMB.Wee unaongelea kiwanja gani?? Hiki kipp pale nafikiri kituo cha basi kivulini kwa wale wa kina sisi wa daladala, utaona kimezungusjiwa uzio na nondo zimetanda na mawinch yako juu.
Mkuu kisiwa gani hicho?Hata yule mwekezaji sijui wa South Africa anayesemekana kauziwa kisiwa hajalipa hiyo hela ,16B ?? Haki ya Mungu Tanzania tuna safari ndefu