Uwepo wa Mungu unadhihirika kwa alama zake na viumbe vyake

Mkuu unajaribu kucheza na maneno tu, kwenye milango mitano ya fahamu , hayupo waamini wanadai yupo beyond apo , ukiambiwa dhibitisha unarukaruka nidhibitishe hayupo

Kama hauwezi dhibitisha potezea tu kuliko kuchochora vijineno vyako vya uswahilini.
 
Sija kushikia bastora ili umuamini Allah Fanya kinacho kufaa
 
Labda nikuulize na wewe Wanadamu tumetoka wapi,
Vitu vyote duniani asili yake ni nini pls katika majibu yako usiweke hoja yoyote ya kisasnsi...
......... Ni ngumu kutofautisha sayansi na mantiki... Tena kwa vitu ambayo ni empirical /phyisical... Otherwise na wewe hutakuwa na tofauti watu wa imani...
 
Labda uniambie wewe nikuthibitishie mara ngapi. Isiwe hujaona ushahidi kwa ujinga wako au unakataa.

Nilikwambia ya kuwa kuwepo kwako wewe kunathibitisha wazi ya kuwa Mungu yupo. Halafu unakuja tena kutaka ushahidi. Una akili kweli kijana ? Lakini kuwepo kwa Ulimwengu na vilivyomo Kuna thibitisha uwepo wa Mungu.

Labda utuambie uthibitisho kwako wewe una sifa gani ? Usiseme hujathibitishiwa.
 
Labda nikuulize na wewe Wanadamu tumetoka wapi,
Kwa nini unadhani kuna sehemu binadamu tumetokea?

Kuna ulazima upi wa kwamba binadamu tumetokea sehemu fulani?

Kama kila kitu kilichopo lazima kiwe kimetokea, Hata Mungu lazima awe ametokea.

Mungu huyo hawezi kuwepo hivi hivi tu pasipo kutokea sehemu fulani.

Ili muundo mzima wa kutokea sehemu fulani, ufuatwe na vitu vyote.

Pasiwepo kitu chochote kile kilicho jitokeza chenyewe tu pasipo kutokea sehemu fulani.
Vitu vyote duniani asili yake ni nini pls katika majibu yako usiweke hoja yoyote ya kisasnsi...
Hakuna asili yeyote ya vitu vya Dunia.

Kama asili hiyo lazima iwepo,

Je Asili ya "Asili ya Dunia" itakuwa ni ipi?

Hapo kutakuwa na Asili nyingi zisizo na mwisho.
......... Ni ngumu kutofautisha sayansi na mantiki... Tena kwa vitu ambayo ni empirical /phyisical... Otherwise na wewe hutakuwa na tofauti watu wa imani...
 

Kuwepo kwa vitu vya wizi ndani kwangu hakuwezi kuwa ushahidi wa moja kwa moja kwamba mimi ni mwizi .

Kuna kusngiziwa na kuwekewa vitu ndan kama mtego tu .

Uwepo wa binadamu na dunia haviwezi kuwa kama ushahidi wa Mungu kuwepo .

Ndio maana uwepo wa mungu umeegemea kwenye imani zaidi

Uwanja mpana kama huu ndio umetufanya mimi na wewe tupo apa tunatilia mashaka uwepo wa Mungu .
 
Sayansi imeshaelezea uumbaji wa vitu vyote ulivotaja hapo. Ni swala la muda tu lakini sayansi inatoa majibu ya vitendawili vingi anavyojiuliza mwanadamu. Imagine maswali waliyokuwa wanajiuliza mababu zetu miaka ya zamani leo hii yashapatiwa ufumbuzi
 
Sayansi imeshaelezea uumbaji wa vitu vyote ulivotaja hapo. Ni swala la muda tu lakini sayansi inatoa majibu ya vitendawili vingi anavyojiuliza mwanadamu. Imagine maswali waliyokuwa wanajiuliza mababu zetu miaka ya zamani leo hii yashapatiwa ufumbuzi
Yah kuna vitabu vya dini vilidai ukoma ni laana kutoka kwa Mungu ,baadae ukoma sio issues tena na kila mtu ameelewa ukoma upoje na unaweza ukajinga vpi.
 
Jifunze kutoa mifano sahihi, hili ni tatizo kubwa sana ambalo mko nalo.

Mashaka yenu yamekuja kutokana na ujinga wenu na kutofatilia mambo na kyyafikiria kwa usahihi, nyinyi mnafikiria kwa mtindo wa kifalsafa na mantiki mitindo ambayo msingi wake mkuu ni akili ya mwanadamu ambayo ni dhaifu.

Sasa onyesha ya kuwa kuwepo kwa mwanadamu si ushahidi wa uwepo wa Mungu. Hili ndio ulitakiwa ulionyeshe, kwa maana utuambie kwa ushahidi ilikuwaje mwanadamu akawepo na hii Dunia ilikuwaje ikawa hivi ilivyo. Endapo ukishindwa kufanya hivyo utakuwa huna haki ya kujadili mjadala huu, na tutakuuliza ujasiri wa kupinga kitu ambacho huna elimu nacho umeipata wapi ?

Sasa ukiegemea kwenye Imani shida Iko wapi ? Unajua maana ya imani ?
 
Sayansi imeshaelezea uumbaji wa vitu vyote ulivotaja hapo. Ni swala la muda tu lakini sayansi inatoa majibu ya vitendawili vingi anavyojiuliza mwanadamu. Imagine maswali waliyokuwa wanajiuliza mababu zetu miaka ya zamani leo hii yashapatiwa ufumbuzi
Kama maswali gani hayo ? Unaamini kweli kwa akili ya kawaida uwepo wa Dunia ni matokeo ya Big Bang ? Hivi unaijua kweli Sayansi ?

Kitu nilichokiona humu, ni kuwa watu wengi wanaegemeza mambo yao au wanaipa Sayansi kazi ambayo haiwezi kuifanya, kwa kuona ya kuwa Sayansi ndio kila kitu, aisee bado mpo gizani.

Inaonekana hamjishughulishi au hamna msingi ya Sayansi au hamuhoji kuhusu Sayansi, kwahiyo mmebakia ushabiki.

Sayansi haijawahi kutoa majibu ya ukweli kuhusu uumbaji.
 
Imani ni hali ya kuamini au kutegemea jambo fulani pasipo na ushahidi wa moja kwa moja au thibitisho .

Thibitisha Mungu yupo ili niamini Leo vijembe havitakusaidia kudhibitisha.
 
Wewe mwanao uliemzaa akikukosea huwezi ku



Nawewe si ulijua utazaa watoto, watoto wako wakikukosea huwezi kuwaazibu kwa maneno au kwa vitendo?
Wewe hujawahi piga hata mtoto wako?
Watoto wanaokufa kwenye matetemeko na mafuriko.

Mfano mzuri ni kule Hanang..

Je ni namna ya Mungu kutoa adhabu ama?
Waweza nielezea hapo?
 
Sioni hata sababu ya kusema dunia imeumbwa iwe kwa mungu ama kwa sayansi bado hakuna udhibitisho ila miaka ijayo sayansi inaweza fanikisha hilo kwa sababu inakua nakubadilika na kujirekebisha kila siku.
 
Hoja yako ni dhaifu sana Mkuu.
 
Mkuu achana na hawa watu kisanga na nduguye ni wapotoshaji tuu. Ukweli wanaujuwa fika usipoteze muda wako hawata kuelewa nyoyo zao zishakufa
 
Hujajibu swali...Allah anatofauti gani na miungu mingine ambayo umeamua kuamini...umeleta hoja mezani unaulizwa swali unakimbia
Unafikiri sina shughuli za kufanya kutwa ni shinde kwenye mitandao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…