Uwezo wa kuongea na wafu: Elimu Iliyoshindikana duniani

Uwezo wa kuongea na wafu: Elimu Iliyoshindikana duniani

mshan jr;
Siamimi habari za mizimu kuwa rafiki ila najua ipo, na inafanya mengi tu. Kwetu tumezaliwa wengi kidogo. Mdogo wangu anayenifuata siku alipofariki ghafula niliona maajab.
Kwanza ilikuwa hivi; Jana yake tuligombana tukapigana ka watoto wafanyavyo. Kwa kuwa nilikuwa sikubali kupigwa na mdogo, nikamshikisha adab. Keshoye kafariki ghafula, japo si kwa kipigo changu kwani naye alinitwanga si kidogo. Ni kwa ugonjwa sikuujua kwani tulikuwa wadogo tu. Umri wa 12 kwa 10.
Cha ajab, usiku wa alipozikwa, nikiwa nimelala kitanda kimoja na baba mzazi, jamaa alikuja, akaniamsha, alianza kunipiga mangumi, mateke mpaka damu zikanitoka puani. Nikapiga yowe, baba akaamka ghafula, akawasha taa. Damu zinatiririka puani, kuuliza kisa nikamwambia kuwa ni jamaa alikuja akanipiga. Baba akaona kuwa ni ndoto. Akaamuru nilale.
Mara tukasikia hodi zinapigwa huko nje. Mama mdogo kamleta mdogo wangu mwingine kutoka kwake, ati alienda kupiga hodi huko anataka chakula. Alipoulizwa amekuja na nani usiku ule, akasema ni huyo jamaa alimfungulia mlango wa chumba cha mama yetu na kumleta huko ili wale chakula.
Je, ni ndoto au ni kweli? Mimi nasema ni kweli kwani nilimwona na alinipiga ngumi ya pua damu zikatoka. Believe it or not, this is a true story

Lakini hapo hebu nambie kuna hiz wanasema misukule yan unaligwa na unakufa gafla lakini kumbe hukufa, labda ukute mdogo wako alifanywa msukule maana misukule waga inasumbua sana, mzim na msukule ni vitu 2 tofaut kabisa,
 
Viko vitatu vinavyotengeneza ID/utambulisho wa kiumbe hai/mwanadamu! Kimoja (mwili)kinaonekana viwili nafsi na roho haionekani
1.mwili ni jumba la kubeba roho/uhai
2.roho ndio inayofanya mwili uwe na uhai
3.nafsi/kujitambua ndio huleta ufahamu kwenye mwili wenye roho

Kuna wakati nafsi inakosekana lakini mwili na roho vina endelea kuwa live, tendo la kukosa fahamu hufanya mtu kukosa kujitambua kuwa yuko wapi na anafanya nini
Kwa kiingereza ni ME, MYSELF and I

mkuu una elimu nyingi sana.
 
Mmh! Kwani watu wakisema 'Mzimu wa marehemu' wanamanisha nini? or Mzimu ni nini?


Kwa kidhungu inaitwa wondering soul/souls ni roho za marehemu zinazotangatanga, wakati majini ni viumbe roho ambavyo havizaliwi na binadamu


Naomba kujuzwa bayana uhalisia wa RED WORDS na tofauti yake uki-include na neno GHOST vina tofauti kati yake kiongozi, ama...?.

Na souls zinatakiwa zi-rest, hizi zinazotanga tanga naweza kupata maelezo juu yake ni zile zilizokufa/uliwa nje ya muda au ni zipi...?.

Extra one : ZOMBIES NA MISUKULE.

THANKS MKUU...!.
 
Hungry ghosts hawana nafasi tena na kama ipo huwachukua kipindi cha KALPA moja kuweza kurudi kuwa binadamu KALPA moja hupimwa kwa kipimo cha jiwe moja la tani tano limegwe kipande kidogo kisochozidi robo kilo kila mwaka maramoja mpaka liishe hiyo ndio KALPA
Tulikuwa tunafanya ibada za kuwalisha kwakuwa wana matumbo makubwa lakini makoromeo yao kila kinachotaka kupita huunguzwa na moto mkali na kuyeyuka hapohapo

Hivyo basi wakati wa chakula tulikuwa tunafanya ibada ya kupoza ule moto ili japo maji na chakula kidogo kipite ndio maana wanaitwa hungry ghost

Kuweza kushuka na kuwa katika kiwango cha mwisho cha u binadamu ni pale mtu anapo fanya matendo ya kinyama na kutisha kabisa kwa viumbe hai ambayo hayasemeki hasa kutoa uhai wa viumbe vingi kwa wakati mmoja

Hapo kama viumbe vipi mana kuna ssmiz tunakanyaga kuna, nyoka tunaua wadudu weng sana tunaua hasa ss binadam mbali nakuua bindama tutapata mateso kwa hawa viumbe tunaoua?
 
mshan jr;
Siamimi habari za mizimu kuwa rafiki ila najua ipo, na inafanya mengi tu. Kwetu tumezaliwa wengi kidogo. Mdogo wangu anayenifuata siku alipofariki ghafula niliona maajab.
Kwanza ilikuwa hivi; Jana yake tuligombana tukapigana ka watoto wafanyavyo. Kwa kuwa nilikuwa sikubali kupigwa na mdogo, nikamshikisha adab. Keshoye kafariki ghafula, japo si kwa kipigo changu kwani naye alinitwanga si kidogo. Ni kwa ugonjwa sikuujua kwani tulikuwa wadogo tu. Umri wa 12 kwa 10.
Cha ajab, usiku wa alipozikwa, nikiwa nimelala kitanda kimoja na baba mzazi, jamaa alikuja, akaniamsha, alianza kunipiga mangumi, mateke mpaka damu zikanitoka puani. Nikapiga yowe, baba akaamka ghafula, akawasha taa. Damu zinatiririka puani, kuuliza kisa nikamwambia kuwa ni jamaa alikuja akanipiga. Baba akaona kuwa ni ndoto. Akaamuru nilale.
Mara tukasikia hodi zinapigwa huko nje. Mama mdogo kamleta mdogo wangu mwingine kutoka kwake, ati alienda kupiga hodi huko anataka chakula. Alipoulizwa amekuja na nani usiku ule, akasema ni huyo jamaa alimfungulia mlango wa chumba cha mama yetu na kumleta huko ili wale chakula.
Je, ni ndoto au ni kweli? Mimi nasema ni kweli kwani nilimwona na alinipiga ngumi ya pua damu zikatoka. Believe it or not, this is a true story


Well, nimesoma hii habari ila staki kusema kuwa aliuliwa kichawi huyu dogo wako coz mara nyingine wachawi huua kupitia sababu ya kitu fulani ili ionekane amekufa kwa kitu fulani.

Lakini pia, nilimuuliza mshana jr kuhusu roho ambazo zimekufa kabla ya muda wake inakuaje zinaitwaje sjajua amejibu vipi ntasoma mbele coz napita post baada ya post.

Ila pia tukumbuke kuwa misukule huwa inaskia njaa kama tuskiavyo tulio hai, sasa suala la yeye kuonba chakula hapa najaribu ku-connect DOTS coz kuna vitu bado naendelea kujifunza. Na mara nyingi napenda kujifanya sijui/kuuliza ili nijue zaidi.

LET ME GO BACK TO CLASS.
 
Last edited by a moderator:
Njaa hoja hujibiwa kwa hoja, kukimbilia tu kutoa conclusion ya uongo bila hoja ni uvivu wa kufikiri au kukwepa ukweli
Hapa kuna vitu vitatu, uhalisia wa nilichoandika, ukweli wa maneno yangu na Kongo uliouona katika post yangu
Labda tu nikwambie kwa upole kwamba hapa si jukwaa la siasa wala mapenzi, hapa kilichopo kipo na kitakuwepo, nimeandika uhalisi wa kile kilichotokea si mara moja au mbili sasa suala la kuamini au kutoamini sio jukumu langu, huo utakuwa mtazamo wako

Haya mambo ni ngumu sana kuwa na ithibati za kisayansi ndio maana wengi wetu tusiopenda kufikirisha bongo zetu, na kufikiri zaidi ya kufikiri huku tukiutazama ulimwengu kwa namna nyingine isiyozoeleka na wengi huja na maneno kama haya ya kwako
Njaa hii dunia ni zaidi ya unavyoiona na kuisoma kwenye zile elimu za kawaida mashuleni, kuna zaidi ya hapo kuna ulimwenguni mwingine kabisa ambao hufanya kazi kwa namna ya tofauti kabisa na ni ulimwengu huo unaofanya maisha yasonge,sio huu ulimwengu wa 1+1=2 THINK BIG rafiki soma elimu ya utambuzi utaona dunia katika mwanga tofauti

Hiz insue bana zinaweza kuwa kweli maana hata mm 24yrs ago nilipozaliwa waliniita jina lakini hii ni maneno ninayoambiwagwa na bb angu mpaka sasa kwamba nililia jina wiki nzima slali naliaga tu, ikafika sehem nikawa sili wala kunyonya, ndipo wakanipeleka hospitali vipimo sina ugonjwa wwte ila kulia kupo pale pale na kula ni kdogo sana ndipo walipo fuatilia ktk matambiko na mizim, ikawa niitwe jina la baba ake na babu yng kizaaa baba yng mm, siku nimeitwa hila jina nililala vibaya sana zaid ya masaa14 na nilikula na kunyonya kama kawida, hivyo mshana yupo sahihi, ndo maana siku hiz mambo yamebadilika sana ktk maisha na majila pia kwa kupuuuza miiko na mizimu ya akina babu zetu hasa kabisa ni ile kuiga mambo ya wazung wakati wao wanamiiko na mzimu wanayoifuata kule ulaya, tutakuwa hivhiv na matatizo hayataisha, hasa kama haya mambo yakuita majina ya kizungu unaacha ya asili ni kosa kubwa sana
 
Last edited by a moderator:
Mh hatateew mgoja nimalizie nyagi kwanza nipate lakuchangia humu jukwaaani


Yeap. Kazi na dawa.

Kwa kuwa nimeamua kushinda kwenye huu uzi leo.

You Made Ma Day Buddy.
 
Wengine ni imaginations tu ambazo zikikomaa kwenye sense ya sita hujenga taswira halisi ya kitu


I wanna go deep down with this pia.

Nafkiri hili somo lina-relate sana kwenye meditation right...?.
 
mshana jr katika ubora Wake

Ni kweli ulilosema na nilishawahi lishuhudia
Maiti kuguna
Kukung'ang'ania
Kukauka
Au kugoma kuingizwa Kwenye nyumba Fulani ambayo aliikataa
 
Last edited by a moderator:
toka lini wafu wakaongea hizo iman haba kwamba wafu huadhibiwa wakiwa kaburin kitu ambacho hakiwazekan ktk hari ya kawaida,nackia hata sanda inachanwa kwenye masikio ili marehem asikie sauti?!

Inawezekana na ndivyo ilivyo
 
Niliwahi hadithiwa na bibi yangu kuwa
Roho hurudi kaburini siku ya alhamisi na huondoka ijumaa jioni

Je kunaukweli
Kwa maana nikienda kaburini jioni ya alhamisi nikiongea watasikia?
Kwanini waislam tunafundishwa kuwa tukikatisha makaburini tutoe salam?
 
Sabrina ni kweli roho huko ziliko ni ready made yani kinachofanyika ni kutafutiwa maumbo tu ya kuingia na utambulisho/nafsi kwamba huyu ni mnyama, mdudu, mwanadamu, nk na hakuna roho inayoangamia hata siku moja bali kinachoangamia ni umbo, utambusho/ID hubaki kama kumbukumbu kwamba 'a'likuwepo mshana jr 'a'kawa hivi au vile 'a'kafariki maiti/mwili 'wake' 'u'kapotea/'u'kazikwa/'u'kaungua na Mungu 'a'ilaze roho yake mahali pema peponi huo ndio utambulisho unaobaki

Kwahiyo mimi ni muunganiko wa vitu vitatu mwili nafsi na roho, nje ya hapo kuna mwili wangu, roho yangu na nafsi yangu


BADO NASOMA.

Ni kama ilivyokwisha semwa hapo nyuma kuwa kuna msemo hutumiwa ujulikanao kama...

ME, MYSELF & I

ME = BODY

MYSELF = NAFSI

I = ROHO


Well, kwenye huo msemo hapo juu tunaweza kujifunza vingi tu, nidokeze kidogo...

ME.

Hii inawakilishwa na mwili ambapo kama tujuavyo kuwa mwili hufa ambalo ndio jumba linalobeba I, hii I ambayo ni ROHO. kwa kawaida hii huwa haifi. Kilichobaki ni...

MYSELF.

Hii ni NAFSI ambayo iko baina ya ME & I ambayo ni MYSELF = NAFSI, sasa kama nilivyosema kuwa ME inakufa ila I huwa haifi.

Kilichobaki ni hii MYSELF = NAFSI inakuaje, inakufa au haifi...?, ni swali ambalo unaweza ukajiuliza na ukajipa jibu mwenyewe ; tujaribu KUSHUGHULISHA bongo zetu angalau.

Lakini pia turudi kwenye msemo ambao umezoeleka sana si mara moja MIMI kupata kuuskia toka kwa watu tafauti, msemo huu unasema hivi...

KULLU NAFSI DHAAHIKATUL MAUT = KILA NAFSI ITAONJA UMAUTI...

Sasa turudi kwenye uhalisia wa kauli hiyo, kwa nini imesemwa kuwa ITAONJA ?, kwa nini isingesemwa kuwa KILA NAFSI ITAKUFA ?, nini mantiki/logic ya kutumiwa neno KUONJA ?, na katika udadisi wangu ni kuwa, hayo maneno yametoka kwenye KITABU KITAKATIFU cha DINI YA KIISLAM tukiaminishwa kuwa ni MANENO YA MUNGU. Sasa kama nafsi ITAONJA UMAUTI it means kuwa ITAKUFA THE ITAENDELEA kuwa HAI kama ilivyokuwa kwa ME & I...?.

TAKE A BRAKE.AND, THINK ABOUT IT | AS A GREAT THINKER.


LET ME GO BACK TO CLASS.
 
Last edited by a moderator:
sante saana mshana jr somo zuri...kama hutajali je tofauti ya roho na nafsi ni nini????,

mtu akifa na nafsi inakufa???..


Anha...!

Kumbe ilishaulizwa huku.

BADO NASOMA.
 
Last edited by a moderator:
Roho ni uhai nafsi ni utambulisho
Nafsi haifi kwakuwa haina uhai bali nafsi hubaki kama utambulisho kinachokufa ni mwili kwa maana ya roho kuuacha mwili milele


Well, hivyo hapa tumeweza kuona kuwa NAFSI NA ROHO huwa hazifi ila kinachokufa ni MWILI PEKEE.

Na ndio mana nikasema kuwa KULLU NAFSI DHAAHIKATUL MAUT = KILA NAFSI ITAONJA UMAUTI.

Nilijiuliza before kuwa kwa nini haikusemwa kuwa KILA NAFSI ITAKUFA, then nikauliza NINI MAANA YA KUONJA ?, KUONJA NI TOFAUTI NA KULA AU KUMEZA coz HUWEZI KULA BILA ya KUMEZA, kitu KINAPOMEZWA ndipo husemwa kuwa KIMELIWA lakini KUONJA ni kitendo cha KUTIA MDOMONI haijalishi kuwa KIMETEMWA AU KIMEMEZWA kinakuwa kipo BAINA NA BAINA ya KATIKATI ya kilipokuwa mwanzo i.e KWENYE SAHANI NA TUMBO kipo KATIKATO.

Na ndivyo ilivyo kwa NAFSI kuwa imesemwa kuwa ITAONJA UMAUTI, sitachelea kusema kuwa HAITAKUFA WALA HAITAKUWA HAI na ndio maana ikawa KATIKATI ya ME & I.

Mkuu watakaelewa watakuwa WAMEELEWA TU na wasioelewa inahitaji kutumia nguvu ya zaida kidogo kuelewa coz HII ILMU NI KUBWA MNO, sasa staki kuwapeleka THAT DEEP tusije tukawachanganya watu ila inahitaji UFAHAM NA UELEWA wa hali ya juu kwa mtu mwenye AKILI YA KAWAIDA kuweza kuelewa haya mambo coz DUNIA NI ZAIDI YA WANAVYOIJUA.


LET ME GO BACK TO CLASS.
 
Duu dagii imekuwaje tena? miss gisenyi ni vema ukayafahamu haya mambo ili siku ukikutana nayo usibabaike, ni vema kujifunza mambo mengi kadiri ya uwezavyo lakini tenda yale yenye manufaa tuu


Heh heh.

Hapa nadhani lilishaanza kukolea mkuu.

Very Funny...!
 
Last edited by a moderator:
Nimekuelewa kaka mshana Jr kwa sisi tunaomini ktk mizimu uwezo wa kumuita mzee wako na kuongea nae upo ila inategemea unamuita kwa kusudio lipi nitakupa mfano Mimi kipindi nazaliwa miaka 25 nyuma ilitokea kukataa jina mana baba yangu alikua mganga mkubwa tu hivyo jina nililopewa mizimu ikakataa wakitka nipewe jina watakalopendeza wao kilichotokea ni kuitwa kwa mizimu ya mababu na majini ya mzee likatoka jina moja kwa mizimu na lingine kwa majini nikawa natumia yote hiyo ndio namna unavyoweza kuita mtu aliyekufa na kuongea nae ila mila nyingi zimehalibiwa na utamaduni wa hizi dini ila kungekuwa na utamaduni wetu kuna vitu watu wangejifunza na kuvijua na kuulewa ulimwengu huu ila wale wanaojua wanatumia na wamenufaika sana ila tutafundishana taratibu na kila mtu atajifunza na kuelewa ili tunufaike wote mana najua kuna watu wangependa kuongea na ndugu zao waliokufa ila hawajui waanzie wapi


Walau nimeweza kukuelewa hapa mkuu.

Education has no boundaries.

LET ME GO BACK TO CLASS | BADO NIPO DARASANI.
 
Roho ni uhai nafsi ni utambulisho
Nafsi haifi kwakuwa haina uhai bali nafsi hubaki kama utambulisho kinachokufa ni mwili kwa maana ya roho kuuacha mwili milele

Mshana nina shida nataka kuonana nawe ninamambo yangu nataka unipe elimu kwa maana nimehangaika sana
 
Mkuu mshana jr unaikumbuka hii, heh heh...


Mshana jr. Unaweza kutafsiri ndoto?


Hapana huo uwezo sina


Sorry kk. Ulishawai kuona saa kwa ndani kuna picha ya mtu au nembo fulani?


Mara nyingi zinakuaga saa za ukutani zile kubwa


Nakusikiliza hebu nifafanulie unacholenga kusema


Kwa mfano ulishai kuona vile saa za sigara aina ya sm au spot? Ambazo kwenye maduka mengi wanazo


Ambazo uwekwa ukutani. Kwa ufupi kabla ya mishale c kunakuwaga na namba za kuonyesha muda 1-12 nyingine zinakua za kirumi. Sasa kwenye zile namba kunakua na picha ya kitu flan au nembo ua kitu flan


Hebu ngoja nitafanya utafiti kwani kuna nini ndani yake?


Ninachotaka kama kuna sehemu wanayo hiyo huduma kwa dsm niwatafute. Ninafunga ndoa hivi muda c mref so nataka kutengeneza hiyo kitu ya picha zetu


Sjacheka the way nilivyocheka kwenye post za jamaa hata skumbuki mara ya mwisho nimecheka hivi ni lini aseee.

Jamaa kaniongezea UHAI leo kiasi flani mkuu dah, NI HATARI SANA.

THAT'S WHY I LOVE THIS PLACE | JF.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom