Uwezo wa kuongea na wafu: Elimu Iliyoshindikana duniani

Uwezo wa kuongea na wafu: Elimu Iliyoshindikana duniani

Braza mshana jr ni MTU muhimu sana hapa jukwaani...ukianza kusoma thread zake huwez acha
Tumuombee long life anatusaidia sana
Be lessed kaka
 
Elimu ya kuongea na wafu ipo na inafanya kazi vizuri sana. Tanzania nina mfahamu mtu mmoja mwenye elimu hiyo. Elimu hiyo kwa kitaalamu inaitwa Necromancy ama kwa lugha ya kiswahili unaweza kuiitwa RITIFAA. Nikipata nafasi nitakuja hapa na maelezo ya kina kuhusu MWENYE HEKIMA huyo mwenye uwezo wa kuzungumza na nafsi za watu walio fariki.
 
Dunia imekuwa kama kijiji kutokana na uwezo mkubwa aliounyesha mwanadamu wa kugundua hata ambavyo vilifikirika kwamba haviwezekani

Elimu na ufahamu kuhusu mwili wa mwanadamu kuanzia kuumbwa tumboni kuzaliwa hadi kufa umetafitiwa na kunyumbulishwa kwa mapana yake na wengi wamepata elimu ya juu kabisa PhD kwenye hili eneo, lakini wakashishindwa kitu kimoja tuu!!! Uwezo wa kumuita marehemu na kuongea naye

Zamani kabla ya dini za kigeni hazijaja Africa tulikuwa kwa kiasi fulani tuna uwezo wa kuwaita marehemu kwa njia ya matambiko na kuwaomba hili au lile, lakini ikumbukwe kwamba hawakuja live bali dalili na ishara kadha zilionyesha uwepo wao na kukubali au kukataa ombi husika

Tumekuwa tunaondokewa na wapendwa wetu na watu tunaowahitaji mno katika maisha yetu, tumekuwa na vipindi vigumu kabisa ambapo tunawahamu na kuwahitaji japo wajitokeze kwa dakika chache tu lakini haikuwezekana kabisa

Mfu ni mfu na hatuna uwezo wowote iwe wa kimwili au wa kiroho kuweza kumuita na kuongea naye lolote, hii ni kwakuwa roho inapotengana na mwili hakuna tena huyo MTU bali kunatokea vitu vitatu visivyoweza kuungana tena na kutengeneza kitu kimoja. vitu hivyo ni roho mwili na nafsi, vitatu hivi ndio vinatengeneza MTU nje ya hapo kuna 'mwili wake', 'roho yake' au 'nafsi yake'

Watu wamejaribu kutoa shuhuda nyingi za kutokewa na marehemu, hili linawezekana kwasababu baada ya kifo kuna roho huwa zinawayawaya duniani, zipo tu na hizi ndizo ambazo hugeuka mizimu mizuri au mibaya

Wakati mmoja tu marehemu anaweza kusikia sauti ya mwanadamu na kuitii ni pale tu anapoandaliwa kwa safari yake ya mwisho kaburini, hasa kwenye ishu ya kumsafirisha au kumvalisha nguo

Nikiwa mtu ambaye nilidili na miili ya marehemu kwa miaka mitatu mfululizo nilikutana mara nyingi tu na hizi hali, marehemu hataki dharau ubishi au kufokewa nguo hata iwe inamtosha Siku hiyo itakataa mpaka mumbembeleza

Tuna wajuaji wengi Siku hizi wanaojifanya wametokewa na marehemu fulani na kumpa maagizo Fulani hizi kwa asilimia 90 ni story tu kwakuwa hatujakuwa na uwezo wa kuwaita au wao kututokea tu na uchafu wote huu tulionao

Mkuu wapo watu wenye uwezo wa kuongea na wafu. Kuna mtoto wa Mfalme wa Norway anaitwa Märtha Louise Harald. Huyu ana uwezo wa kuongea na watu live. Mwaka 2008, aliiomba Serikali ya nchi hiyo kuanzisha shule kwa ajili ya kufundisha watoto na watumbali mbali namna ya kuwasiliana na wafu moja kwa moja. Ila serikali haikukubaliana na hoja yake hiyo kwa madai kuwa hakuna tija yoyote kuongea au kuwasiliana na wafu. Ila kiukweli watu hawa wapo
 
Mkuu wapo watu wenye uwezo wa kuongea na wafu. Kuna mtoto wa Mfalme wa Norway anaitwa Märtha Louise Harald. Huyu ana uwezo wa kuongea na watu live. Mwaka 2008, aliiomba Serikali ya nchi hiyo kuanzisha shule kwa ajili ya kufundisha watoto na watumbali mbali namna ya kuwasiliana na wafu moja kwa moja. Ila serikali haikukubaliana na hoja yake hiyo kwa madai kuwa hakuna tija yoyote kuongea au kuwasiliana na wafu. Ila kiukweli watu hawa wapo
Walikosea sana kumkatalia hii elimu ingetatua vitendawili vingi vya vifo vyenye utata
 
Imani zingine hazina ukweli ila zipo kutia watu hofu tu.We mwenyewe unaweza kuunda uoga au ujasiri.Jinsi uonavyo ndiyo jinsi ulivyo.Unaongozwa na akili yako.
 
Mshana jr asome sana BIBLIA ili awe na rejea nyingi na Mungu amtie nguvu aweze kutuletea mada nyingi humu ndani.
 
Mshana jr asome sana BIBLIA ili awe na rejea nyingi na Mungu amtie nguvu aweze kutuletea mada nyingi humu ndani.
Biblia pekee haitoshi bali lazima na kupata mtazamo wa upande mwingine ile kuweza kupata mizania ya kile unachotaka kukijengea hoja
 
uongo mtupu kudadeki
binadamu akifa yan hapo no connection no converstion no communication kwamba kinachobaki pale ni mwili tu.. na ayo mambo ya roho na nafsi vnakwenda wap tunamuachia SIR GOD

ayo mamvo mengine mnayosema ni swwaga za kale walikua wanazitumia mababu zetu pasipo kumjua MUNGU
 
uongo mtupu kudadeki
binadamu akifa yan hapo no connection no converstion no communication kwamba kinachobaki pale ni mwili tu.. na ayo mambo ya roho na nafsi vnakwenda wap tunamuachia SIR GOD

ayo mamvo mengine mnayosema ni swwaga za kale walikua wanazitumia mababu zetu pasipo kumjua MUNGU
Marehemu huwa anaskia mkuu amini
 
Vuta kumbu kumbu zake kwa yale yote mema alokufanyia na unapolala sema kimoyo moyo nataka kuongea na wewe baba Mara 3 alafu taja kile kitu unachotaka kumuuliza alafu lala hakika atakujia na kukupa majibu stahiki
 
Ni hakika hata mimi mama alifarki mda mrefu ila napokuwa na jambo ambalo nataman kumuuliza huwa nafanya ivo
Pia napotaman kumuona huwa nafanya ivo nae hunitokea na huwa hunieleza mengi mkuu
 
Shetani ana njia nyingi na mbinu za kuwahadaa binadamu. Anaweza akajibadili akakujia katika ndoto katika umbo la marehemu fulani, wewe ukakurupuka kuwa marehemu kakutokea katika ndoto! Watu wa Mungu mtaangamia kwa ukosefu wa maarifa yake
 
Back
Top Bottom