Uzalendo wa ajabu wa Watanzania: Nchi inatukanwa, Rais anatukanwa, tumenyamaza. Huu ni Uzalendo gani?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi,

Makala za Kwa Maslahi ya Taifa na Pascal Mayalla
Naendelea na Makala zangu ziitwazo Kwa Maslahi ya Taifa, ambazo huchapishwa kwenye gazeti la Raia Mwema toleo la kila siku za Jumatatu. Hizi Makala zitafuatiwa na Kipindi cha TV chenye jina hilo hilo ambacho kitaanza kutoka kwenye vituo kadhaa vya TV hivi karibuni baada ya taratibu za udhamini kukamilika, vikiangazia hoja mbalimbali muhimu kwa maslahi ya taifa letu la Tanzania.

Hoja ya Udikiteta Tanzania
Kwa wiki kadhaa sasa nimekuwa nikijadili hoja ya Udikiteta Tanzania. mada ya leo ni kuhusu uzalendo wa ajabu wa Watanzania kuunyamazia uongo unaoenezwa kimataifa kuhusu huu udikiteta Tanzania. Jee Sisi Watanzania, Tuna Uzalendo Gani Kunyamazia Huu Uongo Unaonezwa Kimataifa Kuwa Rais wa Tanzania ni Dikiteta na Tunatawaliwa Kidikiteta?. Au Kwa Kunyamaza Huku Ndio Kukubali Kwenyewe Kuwa ni Kweli Taifa Letu Tanzania Tuko Kwenye Udikiteta?

Kama ni Kweli Tanzania Tuna Udikiteta na Sisi Wenyewe Tumeukubali, Kwa Nini Watuingilie?.
Kama ni kweli rais wetu Magufuli anatenda kinyume cha katiba na sheria, na taratibu za kumshughulikia zipo lakini sisi Watanzania wenyewe tumeridhika naye na utendaji wake huo huo, hivyo hivyo anavyotenda iwe kwa kuvunja katiba au kinyume cha sheria, Watanzania wenyewe tumeridhika na kukubali, who the hell is jirani yasiyomhusu, anayekuja kutusemea kwenye media yao kuwa rais wetu amekosea? Kama wenyewe tumekubali na tumeridhika, huyu jirani anamsemea nani? Kwa nini Watanzania tunanyamasia uongo huu?

Wiki ijayo, nitakuja na set ya maswali kuhusu hoja za udikiteta ambayo nitayaelekeza kwa Waziri wa Sheria na Katiba. Prof. Palamagamba Kabudi.

Jumamosi Njema.

Paskali
Update
Nitauapdate uzi huu kwa michango michache objective.

 
Kwa taarifa yako, nchi ambazo mwananchi anaweza kumtukana rais bila kupatwa na shda yoyote zime endelea kuliko nchi ambazo zinalazimishwa rais aheshimiwe kama vile mfalme.

Sheria ni ile ile, ukiwakera watu unatukanwa tuu. Usje ukadhani kwa kuwa wewe ni rais watu watavunga. Anatukanwa Trump sembuse JPM!
Si sapoti matusi ila pia wanaotukana waachwe wana toa frastresheni zao.

Jambo la msingi ni kuepuka kusema jambo lolote linalo hatarisha uhai au usalama wa rais hili siungi mkono.
 
Ndio ujuwe kuwa tumefika kubaya inamaana kwa upeo rahisi wakiusalama yani watanzania wapo tayari kuuza nchi yao ili rais wao auwawe. Kiukweli kabisa tuna hali mbaya sana kama taif nakama tusipo kitokomeza kizazi hiki cha wasio wazalendo usalama wetu upo ktk hatari. Mtu amekuwa na nafasi kubwa ya kitaifa anavujisha siri za taifa kwa kisingizio cha upinzani bado yupo mjini anavuta hewa nakupata kahawa hapana we need to act now. Inatisha ndugu zangu
 
Mkuu Pascal Mayalla sio kwamba hatuna uzalendo tatizo ni yeye mwenyewe ndiye anajidhalilisha, unaendaje mahali ambapo watu wamepatwa na tetemeko la ardhi wamefiwa, wana uchungu wa kupoteza nyumba na mali zao halafu unakurupuka na kuwambia wafanye kazi Serikali haitatoa msaada wowote, asiyefanya kazi na asile na asipokula afe, haya ni maneno ya hovyo sana
 
Mbona Rais wako anafurahia Watanzania kuuwawa na kutekwa na tena ndiye anaratibu huu upuuzi na wewe unakuja hapa jukwaani kuandika kitu usiokijua siju unatafuta ukuu wa wilaya

Wacha kujipendekeza huku ukijua rais wako ndie anayeminya democracy na kuratibu huu upuuzi.

Nchi imemshinda na sasa anaratibu upuuzi

Swissme
 
Uzalendo ni kutokubali na kutonyamaza kimya wakati rais wako anaposemwa vibaya kwa hoja za uongo
Pascal Mayalla hivi unajua matendo ya mtu ndio huwa yanampa mtu jina, mfano nikikuita wewe pascal kuwa ni mwandishi wa habari unayefaa kwanini niseme hivyo maana yake naona unachokiandika ni kizuri na kina wafanya wengi wakubali uandishi wako. hapa unanielewa sijui.
 
Ngoja nami niwe mzalendo lakini twende kwanza taratibu!

Mosi, nitamtetea Rais kwa nguvu zote pakiwa na hoja za kumdhalilisha manake, udhalilishaji ni kwenda beyond political civilization.

Kwangu Rais kuitwa au kunasabishwa na udiktea haiwezi kuwa ni udhalilishaji kwa sababu; dictatorship is one of the known leadership style!

Nitakachofanya hapo ni kuangalia Udikteta ni nini na dikteta ni mtu wa aina gani na kisha kuangalia ikiwa Rais wetu ana-fit kwenye hizo sifa za udikteta!!

Hiyo ndiyo changamoto ambayo pia nimekuwa nikiitoa mara kwa mara kwamba; badala ya kuhangaika na akina The Economist; wale "WAZALENDO" wachambue kuonesha ni namna gani Rais wetu sio dikteta!

Wazalendo wamwage nondo kuonesha ni namna gani Rais wetu anavyo-promote demokrasia, utawala bora na jinsi anavyohakikisha taasisi zetu zinavyo-enforce elements za kidemokrasia!!

Aidha, ndugu Pascal Mayalla naomba niongee jambo moja! Sina shaka wewe mwenyewe utakuwa unafahamu lakini kwa staili ya uandishi wako, watu wanaweza kumeza kila ulichoandika kama kilivyo!

Je, ni wananchi wa taifa husika peke yake ndio wana haki ya kumsema rais wao?!

Jibu ni NDIYO & HAPANA!

Zipo issues zinazohitaji kuheshimu mamlaka za nchi kwa sababu ni mambo ya ndani!!

Lakini pia HAPANA kwa sababu kuna issue zinakuwa na Global Impact!!

Dictatorship ina global impact na kwahiyo inapaswa kukemewa na Global Citizens!

Global Citizens hawana mipaka. Global Citizens wanaunganishwa na itikadi!

The Economist ni Classical Liberals! Na misingi ya Classical Liberals ni social liberty and economic freedom!

Hapo ndipo ilipo tofauti ya msingi kati ya The Economist na JPM!

Jana nimeona makala ya "Mwingereza" iliyoletwa hapa JF na kuungwa mkono na JPM!

Mzungu yule (soma Mzungu Fake) anahoji ni kwa vipi The Economist hawaoni jitihada za JPM za kuleta maendeleo wakati wao ( The Economist) ni pro-development!!

Maskini "Mbelgiji" yule ameshindwa kutofautisha kati ya maendeleo na vile unavyoweza kufikia maendeleo husika!

For classical liberals, it's not about the level or degree of development but how did you or do you plan to reach there!

Kama unaleta maendeleo huku unakiuka haki za binadamu, unakiuka utawala wa sheria, unaminya demokrasia, social liberty inakuwa abused; then maendeleo ya aina hiyo (kama yapo) katu hayawezi kuwa commended na Classical Liberals!

Hayawezi kuwa commended kwa sababu nyuma ya hayo maendeleo kuna mambo mengi yanakuwa yamejificha... mambo kama corruption! Na kv no free speech, maovu kama hayo yanakuwa hayafahamiki kwa sababu hata taasisi za umma kama bunge zinakosa guts za kuelezea maovu ya serikali waziwazi!
 
Kuambiwa kwake ukweli na wakosoaji ndio Uzalendo wenyewe mkuu kuliko wanafiki wanaoshindwa kumshauri vyema pale anapokuwa anakwenda mrama.

Ukiongoza kwa mihemko na mikurupuko bila tafakuri ya Kina lazima wenye upeo wao watasema kitu,na kama upo na IQ njema weaknesses zako ndizo unatakiwa uzifanyie kazi na mwisho wa siku ziwe opportunities na sio kuwakandamiza wanaokwambia ukweli,huo ndio ustaarabu, usitake kuonekana malaika wakati sio
 
Rubbish,Hamna kitu we mnafiki mkubwa na mlamba viatu,mikutano ya kisiasa iko wap kama sio udikteta??unatumia tumbo kufikiri,within few months to came utapoteza heshima yote kwa mwendo huu Wa kutetea ujinga usiohitaji maelezo
Haipo na ndio maana jamaa anawapiga kijembe kiaina kama kweli ni uongo wajitokeze wakanushe kitu ambacho serikali haijafanya mpaka leo.

Ulitaka na yeye asimame aseme serikali ya Tanzania ni ya kimabavu, kidikteta, na hayo majina anayopewa raisi yanamfaa? Saivi naye tungesha ambiwa kajiteka!

Unahitajika umakini wa hali ya juu kuelewa mada hizi
 
mbaya zaidi uongo huo ulianzishwa na mleta mada!!ha ha ha unafiki ni mbaya sana
Comment yako hii imenivuta kuchangia huu mjadala, hebu iweke vizuri na kwa uwazi tuweze kupambanua

Mimi sina tatizo na member kama wewe kwakuwa unajulikana wazi umesimama upande gani.Lakini Paskali huwa anakuwa haeleweki kabisa. Na hili si jambo jema
 
Rubbish,Hamna kitu we mnafiki mkubwa na mlamba viatu,mikutano ya kisiasa iko wap kama sio udikteta??unatumia tumbo kufikiri,within few months to came utapoteza heshima yote kwa mwendo huu Wa kutetea ujinga usiohitaji maelezo
@Moderator tafadhalini hii ni JF si FB au mitandao mingine ambayo matusi ni ruksa. Humu lazima staha iwepo si matusi namna hii. Hawa madogo hawajielewi kabisa, unadai demokrasia lakini huwezi kumvumilia mwenzako akitoa hoja tofauti. Ndio maana wengine tumeamua kuwanyoosha ili upinzani na mashabiki wake wabadilike na tujifunze namna ya kujenga hoja huku tukilinda maslahi ya taifa na kuwa na staha kwa viongozi wetu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…