Uzi Maalum wa maswali na masuala mbalimbali yahusuyo Kodi, ushuru na masuala mengine yanayowahusu TRA

Uzi Maalum wa maswali na masuala mbalimbali yahusuyo Kodi, ushuru na masuala mengine yanayowahusu TRA

Pamoja na kutumia CIF ila kwanini kusiwe na punguzo jinsi gari linavokua jipya. Mfano gari ikizidi miaka kumi kodi ni 90% ya cif na cc zikizidi #### sasa kuwepo pia na punguzo kwa gari iliyo chini ya miaka hata 2 ya 90% ili tuweze kumiliki magari yenye ubora hasa upande wa public transport
Sijui kama nimekuelewa vizuri. Lakini sheria ya kodi inafurahisha saana. Kinachotokea ni kwamba ukinunua gari jipya inamaanisha wewe unakipato kikubwa, hivyo wanakucharge kodi kubwa (japo hulipii uchakavu). Unaponunua gari used la kati ya mwaka mmoja mpaka 10, kulipishwa uchakavu kulingana na uzee wa gari. Ila likizidi miaka kumi, kodi inapungua kidogo, moja ni kwa sababu ya CIF ndogo, pili mfumo wa kodi unakuchukulia kuwa na kipato cha chini. Ndio maana unanunua vitu vizee saana. So wanakuhurumia kidogo.
 
hapa mashaka tupu unawezs ukawa umekadiria gari labda upate kwa 6M kodi nayo labda 4.7M sasa balaa linakuja kodi unaweza kupigwa ndefu mpaka ukashindwa hata kukomboa gari

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Trust me huwa hawafuati kabisaaa.
Kama ukitaka kuamini nenda kaangalie pg 2 ya assessment document yako.
1. Import duty = cif × 25%
2. Excise duty = (import duty + cif) × 5%
3. Excise duty due to age= (import duty + cif) × 30%
4. Vehicle registration = 450000 tsh
5. Railway revi = cif × 1.5%
6. Custom process fee = fob × 0.6 %
7. Vat = (all of taxes above + cif) × 18%

Hayo ndo mahesabu ambayo hata kwenye kikokotozi chao yapo
Nadhani inategemea na uliyekutana naye kwa siku hiyo, mara ya mwisho nilitoa gari mwezi wa pili katka ushuru wao ikaja 7mln wakaona ndogo wakaenda kwenye system ikawa 8.5mln wakaniambia nilipe hiyo ya system
 
Nadhani inategemea na uliyekutana naye kwa siku hiyo, mara ya mwisho nilitoa gari mwezi wa pili katka ushuru wao ikaja 7mln wakaona ndogo wakaenda kwenye system ikawa 8.5mln wakaniambia nilipe hiyo ya system
Upo sahihi mkuu kama cif yako ni ndogo lazima watumie njia nyingine kukuliza.
Ndo maana kuna declared cif na assessed cif. Kwa kesi kama hiyo kwenye declared wanaweka yako ambayo ni ndogo alafu kwenye assessed wanaweka ya calculator ambayo itakua kubwa alafu wanaendelea na mahesabu kwa kutumia assessed cif.
Ila kama yako ni kubwa, kwenye declared na assessed kote wanaweka yako na mahesabu yanaendelea kama kawaida.
Kwa kesi zote hizo unaweza ukalalamika na assessed cif ikashuka na total taxes yako ikashuka vile vile.
 
Wa TRA maskini ya Mungu kachomekewa boko kaingia kichwa kichwa bila kujua,ukute hajala hata buku.ila polisi Mungu anawaona aisee,kumkamata mhalifu mpaka pesa,Duuh!this is too much
 
Kuna watu wakiamoni Watanzania wameacha ujanjaujanja awamu hii ila kiuhalisia ni kama ndiyo wamebuni mbinu kabambe.
 
mkuu njoo inbox nikupe issue ya kufanya, hii sio ya public unless nataka kunyea ndoo
otherwise submit hio invoice ikikupendeza na itakupendeza zaidi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haziendani kabisa mwezi wa 12 niliagiza gari kodi ilikua 8.1m kwenye kulipia mwezi wa kwanza kodi waliniletea ipo 9.1m
 
Haziendani kabisa mwezi wa 12 niliagiza gari kodi ilikua 8.1m kwenye kulipia mwezi wa kwanza kodi waliniletea ipo 9.1m

Hapo ulikosea timing mkuu wakati unaagiza gari yako ilikua haijafikisha miaka kumi ya uchakavuu,lakini wakati unafanya declaration tushaingia 2020,na uchakavu tayari ni zaidi ya miaka kumi ambapo wanakuchaji 30% ya uchakavu tofauti na 15% ikiwa gari halijazidi miaka kumi


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ili uweze kulipa kodi sawa na iliyo kwenye calculator hakikisha CIF yako haizidi ya kwenye calculator, maana sheria inasema ofisa achukue cif iliyo kubwa kati ya uliodeclare na iliyo kwenye calculator


Sent using Jamii Forums mobile app
 
hapa mashaka tupu unawezs ukawa umekadiria gari labda upate kwa 6M kodi nayo labda 4.7M sasa balaa linakuja kodi unaweza kupigwa ndefu mpaka ukashindwa hata kukomboa gari
Haha, unachosema kina ukweli aisee, kuna jamaa aliwahi kuagiza gari, mwenyewe amejiandaa ila kodi kutoka, ikawa tofauti kidogo na alivyokua ametegemea. Sasa kwenye kuhaha huku na huku kutafuta ya kuongezea, muda wa storage nao ukamfikia kidogo.

Bahati nzuri, kwenye kuhangaika akakutana na jamaa ambaye aliagiza gari mbili ila zile gari yeye alilipia tu CIF ushuru akalipia jamaa ambaye huwa anatoa huduma hiyo kisha akamrejeshea kwa awamu mbili. Ila walikua na makubaliano ya kimaandishi.

Basi ndio akamuonganishia hapo, japo anasema haikuwa rahisi jamaa kukubali maana tayari alikua na watu wengi, ila baada ya jamaa kumuomba sana ikabidi akubali.

Amemaliza deni lake mwezi uliopita tu hapo.
 
Hapo ulikosea timing mkuu wakati unaagiza gari yako ilikua haijafikisha miaka kumi ya uchakavuu,lakini wakati unafanya declaration tushaingia 2020,na uchakavu tayari ni zaidi ya miaka kumi ambapo wanakuchaji 30% ya uchakavu tofauti na 15% ikiwa gari halijazidi miaka kumi


Sent using Jamii Forums mobile app
Umemjibu kitaalamu zaidi. Huu ndio ukweli.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Za majukumu wandugu? Bila shaka Mungu anasaidia

Niliagiza mizigo Ali express order zilikua 6 mwezi Desemba mwaka Jana. Ila kutokana na janga la Corona mizigo ikachelewa na nikajua imepotea sababu ndani ya mwezi tu huwa unapokea ila this time ilivuka muda inaonekana imewaasili lakini sjapewa taarifa na Posta na corona ipo high nikaona nishapoteza.

Tarehe 30 mwezi huu wa Machi ikafika, Posta walinitumia text. Nimeenda Posta wakasema mzigo mmoja upo TRA nenda kaufuate ila hii mingine wameiruhusu chukua.

Nikaenda mpaka TRA sehemu husika incharge nilimkuta jamaa mmoja nikamsalimu nikampa maelezo. Akaniambia ni kweli mzigo upo ila niliuzuia inabidi ulipe kodi kisha uchukue. Ilikua ni mini sewing machine yaani kimashine cha kushonea unashika mkononi. Akaniuliza hii mashine ulinunua bei gani? Nikamwambia Tshs. 5,000 akaguna. Akauliza na zile memory nikamwambia moja Tshs. 4500 so pale zipo 2 jumla Tshs. 9,000.

Akaendelea kuuliza "Zina ukubwa gani?" Nikamwambia GB 16. Akauliza "kwanini usinunue hapa mpaka ununulie China?" Nikamwambia bei ni ndogo, hiyo Tshs. 4,500 Tanzania huwezi kupata memory card ya GB 16, hata GB 2 hupati. Akasema sawa, sasa iyo mashine inabidi ulipe kodi. Nikamuuliza kiasi akasema lipia Tshs. 35,000.

Nikamwambia kitu cha Tshs. 5,000 kodi yake Tshs. 35,000, cha laki si itakua laki 5? Akasema yani iyo ni nje ya mfumo tukiingiza kwenye system hapa inazidi hiyo. Nikamuuliza kodi mnakata asilimia ngapi? Akasema hawezi kusema hadi auone mzigo. Nikamuuliza tena, mfano naagizia kitu cha Tshs. 70,000 kodi ni kiasi gani na inakatwa kwa asilimia ngapi? Akasema dogo mpaka tuone mzigo maana kuna VAT na vitu gani sijui.

Ila nahisi kengele iligonga kichwani make kwamba huyu dogo anaelewa hizi vitu kutokana na maswali yangu. Akaniambia kwahiyo lipia basi nina ishu nyingi za kufanya. Nikamwambia bro sina hela halafu kama ni kodi inabidi nilipe chini ya iyo pesa niliyonunulia nahisi ata elfu moja haifiki.

Akatulia akanicheki then akasema fungua simu yako nicheki hiyo bei, bahati mbaya simu haikuwa na chaji ilikuwa 4% tu. Akanipa charger yake nikafungua Ali Express nikamuonesha akacheki akaona ni sahihi sjadanganya. Akatoa karatasi akaandika realese statement akanipatia kamzigo kangu.

Ila nilipanga asiponipa naenda uongozi wa juu, potela mbali hata kama ni cha 5,000 ni pesa yangu.

Nimejifunza kitu, TRA inachafuka kutokana na watu waliopewa usimamizi kwa tamaa zao. Ukiwa muoga wanakupiga hasa au huo mzigo wako utaacha na hupati kitu. Wajuzi mnisaidie kodi ya vitu kama hivyo ni asilimia ngapi inakatwa ili nitakapoagiza mzigo mkubwa nijue kabisa naenda lipa kodi kiasi gani maana yule jamaa alishindwa kuniambia ukweli.

Sijawahi kutana na TRA Posta ila sasa ndio wameanza kukagua na wanafungua ndani wanacheki kuna nini japo sijajua mikoa mingine ipoje na kama haipo basi jiandaeni mi nipo mkoani.


Screenshot_2020-04-02-00-19-38.png
.
 
Back
Top Bottom