Uzi maalumu kwa ajili nyimbo za injili za zamani(Old school Gospel songs) za Tanzania!

kaka kuna wimbo ka jin animeusahau ila nakumbuka baadhi ya mameno yake tu"alipofika karibu aliuona mji akaulilia akisema watu wa yerusalemu"
 
Nimebalikiwa sana na uzi huu, big up sana uliyeanzisha uzi huu,
kuna wimbo mmoja wa zamani nadhani uliimbwa na Wakenya kama sikosei, nakumbuka title ya wimbo ilikuwa "umejivalia ngozi ya kondoo kumbe ndani ni mbwa mwitu" kama kuna mtu anao naomba atupie hapa.
 
Fahari ya vijana, ni ..........
Fahari ya wazee, ni kichwa chenye mvi
Fahari ya moyo wangu, ni kuyatenda mapenzi yake Mungu

Sauli Sauli mbona waniudhi
Sauli wawatesa watu wangu

Bwana kachukizwa sana, kamwambia Sauli
Mimi ndimi Yesu unayeniudhi
Ole wako wewe, unayemuudhi
Bwana Mungu wako utahukumiwa




"Kwa nini wataka kujiua wewe
Inavyoonesha, umeshakata tamaa. ..

Sikumbuki unavyoendelea wala waimbaji mwee

Naupenda mnoooo



Nimebarikiwa mnoo...


Kuna mwingine pia, naibia ibia tu.

Hata baada ya siku sita mwokozi Yesu,
Alipanda mlimani na wanafunzi wake........

Sauti iii, Sauti iii
Sauti iii, Sauti ikatoka
Huyu ni mwanangu mpendwa msikilizeni, atakayowafundisha nayashikeni

Sijui wametajwa hawa, Bethel Choir walioimba

Wahurumieni
Mungu yu mwema
Sio sisi
Umepoteza Dira
Basi nasema (tunda la roho) etc
Japo melody na sauti siisikii ila hakika maneno Haya yamenibariki.

Thanks Dada mtumishi HS
 
MUNGU akubariki sana umenikumbusha sana,
Pamoja Mkuu!
kaka kuna wimbo ka jin animeusahau ila nakumbuka baadhi ya mameno yake tu"alipofika karibu aliuona mji akaulilia akisema watu wa yerusalemu"
Nakuangalizia,uwe na subira!
Sauli Sauli mbona waniudhi
Sauli wawatesa watu wangu

Bwana kachukizwa sana, kamwambia Sauli
Mimi ndimi Yesu unayeniudhi
Ole wako wewe, unayemuudhi
Bwana Mungu wako utahukumiwa
Naukumbuka Huo Wimbo,uwe na subira!
Fahari ya vijana, ni ..........
Fahari ya wazee, ni kichwa chenye mvi
Fahari ya moyo wangu, ni kuyatenda mapenzi yake Mungu
Just a sec!
 
Nilinunuaga album zao zote 3 ambazo ziko katika video (ULYANKULU). Nilikuwa nawapenda sana hawa, pamoja na wale akina mama "Wa kwa Mungu hakuna mzee" kutoka Shinyanga ... Hawa wa mama walikuwa wana sauti tamu sana.

Nakumbuka Album hizi na nyimbo zake. Ninazo LAKINI nitawawekea majina ya nyimbo ili iwarahisishie kutafuta.

1. KATIKA VIUMBE VYOTE.
-Katika viumbe vyote
-Palikuwa na mtu (Ayubu)
-Bwana ndiye mchungaji wangu
-Neno la Mungu lililomjia Yona
-Wakati ule wa Nuhu
-Vijana tuamke sote
-Alipofika karibu aliuona mji
-Yesu alipokuwa ameketi.

2. MWENYE MAMLAKA (Mapigano)
-Mwenye mamlaka
-Wakati huo
-Yesu katazama
-Wokovu ni lazima
- Fahari ya vijana
-Safari ya wana wa Israeli
-Ombeni nanyi mtapewa (Paulo & Sila)
-Amri mpya nawapeni (upendo)
-Goliathi
-Kama ndugu yako akikosa
-Sisi ni barua

3. SAMSON & DELILA
-Dunia ya shida
-Samson
-Ufunuo wa Yohana
-Nitamwona Yesu
-Basi nasema
-Yusufu
-Nikifikiria
-Kifo cha Yesu
-Ulimkimbilia Mungu

Kuna hawa nao walikuja juu miaka ya 2000 mwanzoni wanaitwa "THE GOSPEL SOUND SINGERS," kutoka EAGT Singida. Album yao ilibamba sana.

Iliitwa "KILA GOTI LITAPIGWA."
Ilikuwa na nyimbo hizi;
-Wathamani
-Dunia hii
-Kabla sijaokoka
-Yesu tusaidie
-Amechukua masikitiko yetu
-Mwanzo na mwisho
-Mimi najivunia
-Bwana Yesu

Nk...

Dah! Those days!
 
Siku ya kutaabika aaaa siku ya kukanyagwa aaaaa siku ya fujo inakuja itokayo kwa bwanaaaa bwana wa majeshi

Katika Bonde la maono linabomoa kuta na kuililia Milima
Tazamaa bwana anakujaa




Kuna huu mwingine unaimba
Mle kaburini Yesu kazikwa alifunikwa na Giza kubwaaaaa na siku ya tatu bwana kafufuka walinda kaburi waliogopaaaa
Walikiri kwamba Yesu yu hai shangilieni Yesu alifufuka
 
Yesu kawaambia

Na kama ndugu yako akikosa muonye
Akitubu msamehe
Kuliko kumkosesha mmoja wapo,
Wa wadogo hawa
Mkuu,nashukuru!ila waweza tuwekea hizo hapa jf?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…