Uzi maalumu kwaajili ya maombi ya Alfajiri

Ombi Langu Kwako - Rose Muhando. This melodious song is a blessing to my soul; and a powerful prayer. Hebu Mungu wetu na Akatutendee 🙏🏿🙏🏿🙏🏿

Your browser is not able to play this audio.
 
Bwana Yesu asifiwe
Wiki hili tutaomba kwa ajili ya wenzetu walioteza maisha kwa ajali ya jengo la kariakoo tumhimidi Mungu kwaajili ya wote ambao wamepona katika ajali hii iliyotokea kariakoo
Waliopoteza wapendwa wao Bwana awape tumaini kipindi hichi kigumu
 
Roho Mtakatifu ananisemesha nakuniambia kuwa kuomba kwa ajili ya watu waliopo katika majanga ni fursa kubwa
Hauhitaji sasa mafuta ya nabii ili kupona ugonjwa wako au upate mafanikio

Ukiamka asubuhi omba rehema
Ombea watu waliopata majanga mbalimbali
Ombea amani katika taifa lako ili lisiingie katika vita
Peleka hitaji lako sasa kwa Mungu akutendee miujiza
Zaburi 86:10
Kwa kuwa ndiwe uliye mkuu,
Wewe ndiwe mfanya miujiza,
Ndiwe Mungu peke yako.

Biblia inatukumbusha tuombeane

Yakobo 5:16
[16]Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii.
 
Afadhali nimepata sehemu ya kupokea faraja baada ya hawa kenge wa CCM kunitibua. Shukrani sana na barikiwa
 
Amen
 
Bwana Yesu asifiwe ni siku nyingine tena Mungu ametupa kibali cha kukutana jukwaa hili

Leo tena tunakutana hapa kuombea taifa majanga yasiendelee kutokea
 
Jifunze namna ambavyo Mungu anavyojibu maombi kwa haraka sana itakushangaza sana watu wengi wamekuwa wanaingia faragha katika maombi wanatumia muda mwingi kuombea shida zao na kukemea mapepo ni jambo zuri pia

Mungu huwa anashusha baraka nyingi sana kwa taifa zima lakini ni kwanini sio kila mtu anazipata baraka hizo kwa wakati shida ipo hapa

Sababu Mungu anashusha baraka kwa taifa hivyo baraka zinakwenda kimakundi makundi ya watu wengi wanaoteseka au kulia na jambo Fulani sasa vile vilio vikiwa vingi hapo ndio sauti huwa inamfikia Mungu na kutuma malaika zake kuja kutoa baraka vilio vya watu wengi Bwana alisikia vilio vya wana wa Israel

Kutoka 3:7
BWANA akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao;

Watu zaidi ya 600000 walikuwa wakimlilia Mungu sababu ya kupata mateso ya farao

Hivyo kumbe tunajifunza inatunapasa kuombea makundi ya watu wanaoteseka na jambo Fulani na kuombea jambo fulani linalofanywa na wengi mana Mungu anayasikia zaidi makundi ya watu wanaoteseka malaika wanavyotumwa kushusha baraka watu wote walioshiriki kuombea kundi hilo nao wanabarikiwa kwa haraka

Utatoka kwenye magonjwa na umasikini sababu tu umeombea amani na utulivu uwepo duniani umeombea amani na utulivu uwepo katika katika kipindi hichi tunaelekea kwenye uchaguzi unaohusisha watu wengi ombea nchi zenye vita zinazotuzunguka kama Congo mabala duniani yote ombea amani

Yakobo 5:16
Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii.

1 Timotheo 2:1
Basi, kabla ya mambo yote, nataka dua, na sala, na maombezi, na shukrani, zifanyike kwa ajili ya watu wote;
 
Amen
 
Bwana Yesu asifiwe
Ni siku nyingine tena tunakutana jukwaani hapa Mungu ametupa kibali kukutana jukwaa hili kwa ajili ya maombi .

Unavyoingia katika maombi kila jambo unalo omba jifunze kumuachia Mungu akujibu kwa wakati wake utaona maajabu makubwa jinsi Mungu atavyokutendea makubwa neno linasema hivi

Isaya 55:8
Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu; asema BWANA.
Kwa maana kama vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zangu zi juu sana kuliko njia zenu, na mawazo yangu kuliko mawazo yenu..
 
AMINA MUNGU WA UPENDO BADO ANATUPENDA JAPO TUNATANGA MBALI NA UPENDO WAKE TUSEME NINI ZAIDI YA ASANTE
 
Amina hakika Mungu ni wa upendo,tumechagua kuwa wake na tutasubiri atupe/atujibu kwa wakati wake.
Tusichoke kumtumaini yeye pekee.
 
Siku nyingine Mungu ametupa kibali Cha kukutana asubuhi ya Leo
Tupo kipindi ambacho tunaelekea kipindi Cha uchaguzi Tuombee sana amani na utulivu uendelee kudumu katika taifa Letu
1 Timotheo 2:1-2
[1]Basi, kabla ya mambo yote, nataka dua, na sala, na maombezi, na shukrani, zifanyike kwa ajili ya watu wote;

kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, tuishi maisha ya utulivu na amani, katika utauwa wote na ustahivu.
 
Ufunuo wa Yohana 3:2-3

[2]Uwe mwenye kukesha, ukayaimarishe mambo yaliyosalia, yanayotaka kufa. Maana sikuona matendo yako kuwa yametimilika mbele za Mungu wangu.
Be watchful, and strengthen the things which remain, that are ready to die: for I have not found thy works perfect before God.

[3]Basi kumbuka jinsi ulivyopokea, na jinsi ulivyosikia; yashike hayo na kutubu. Walakini usipokesha, nitakuja kama mwivi, wala hutaijua saa nitakayokuja kwako.
Remember therefore how thou hast received and heard, and hold fast, and repent. If therefore thou shalt not watch, I will come on thee as a thief, and thou shalt not know what hour I will come upon thee.
 
Bwana Yesu asifiwe nimekuja ujumbe kutoka kwa Bwana

Ikiwa unapita wakati mgumu katika biashara/kazi yako unakutana na ugumu wateja wamepungua au uchumi umeyumba, madeni usiache kumtumaini Mungu usirudi nyuma simama endelea kwenda katika viwango vingine katika huduma

Soma biblia mistari hii katika biblia Kuna jambo Mungu atakupa majibu kwa haraka Nini ufanye

Luka 5:1-7
Mathayo 11:28-29
1 Wafalme 18:30-42

3×7
 
Shalom shalom wapendwa Bwana Yesu asifiwe Ni siku nyingine tena Mungu ametupa kibali Cha kukutana hapa
Nimekuja na ujumbe huu kutoka kwa BWANA siku zote ukitaka kupiga hatua kubwa kwenye jambo unalolifanya hakikisha kila changamoto inayokuja mbele yako unaiona ni nyepesi sana kwako

Kila changamoto unayokutana haijalishi ni jambo gumu kiasi gani wewe jiambie maneno haya kila unapoamka asubuhi

"Jambo hili ni jepesi sana kwangu Mungu yupo pamoja nami"

"Jambo hili ni rahisi sana kwangu Mungu yupo pamoja nami"

Soma Neno kutoka vitabu hivi
Yeremia 32:17
Aa! Bwana MUNGU, tazama, wewe umeziumba mbingu na nchi, kwa uweza wako mkuu na kwa mkono wako ulionyoshwa; hapana neno lililo gumu usiloliweza;
Yeremia 1:5-8
Kutoka 3:10-14
Malaki 4-2
Yohana 8-31-32

3×7
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…