Uzi maalumu wa kuweka tetesi na Taarifa za usajili Ligi Kuu ya NBC kwa msimu ujao 2022/2023

Uzi maalumu wa kuweka tetesi na Taarifa za usajili Ligi Kuu ya NBC kwa msimu ujao 2022/2023

Mchukue huyo kelvin Nashon halafu utakuja kunishukuru baadae

Huyo ndo kile kizazi cha akina Job,kibwana,Mshery,Kibabage,kabwili........kiungo mkabaji wao alikuwa Kelvin Nashon ile U-17 ya coach Kim Poulsen

Hivi "Ali Ng'azi" yuko wapi?
 
Mchukue huyo kelvin Nashon halafu utakuja kunishukuru baadae

Huyo ndo kile kizazi cha akina Job,kibwana,Mshery,Kibabage,kabwili........kiungo mkabaji wao alikuwa Kelvin Nashon ile U-17 ya coach Kim Poulsen
Kuna huyo aziz anacheza beki na kiungo mkabaji kama uliangalia game Yanga na mbeya city kwa mkapa alikichafua sana
 
Unasajili vp bila kocha?

Bongo bhana, hata huko Ulaya Kocha akitimuliwa yule anayeletwa huwa anakuja kunusuru timu, na hatua ya kwanza ni kuwajengea wachezaji imani tu wapambane na sio mbinu zake.

Mbinu huendana na aina ya Wachezaji, mfano Kibu Denis kwa namna anavyocheza, kujiposition unaina kabisa kwa Nabi hawezi cheza kabisa, pia ukija kwa Pablo ukimchukua Kiungo kama Aucho au Chama kwa kocha kama Pablo hawezi kitoboa maana Pablo anapenda viungo wenye kuwa na speed na nguvu nk.

Hivyo Simba wangeanza na Kocha kisha kocha, aingalie Simba katika angle zote, yaan ile Simba ambayo inafungwa kizembe, na ile ambayo inapambana kwa jasho na damu, kupitia hapo kocha atajua ni wachezaji gani wanabaki katika kiwango chao, iwe wamefungwa au kushinda. Hapo ndipo maboresho ya kikosi hutokea.

Kwa usajili huu ni wazi sasa Simba inarudi ilipotoka Yanga ambapo walikuwa wanasajili kwa mihemko, msimu unaoisha huu Yanga imesajili wachezaji ambao sio tu kocha alijaribu kuwaona bali alipendekeza kutoka ukanda wetu huu huu wa Afrika Mashariki.

Simba wasisajili kama Ndondo Cup, watulie, natamani sana kuona Simba na Yanga zote zikifika hatua ya Makundi this time na ikiwezekana Nusu Fainali ya CCL. Ila mikurupuko hii naona kabisa Jwaneng wanakuja kutufumua hapa hapa tena.
Na Rivers wakija kutufumua tena.
?
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na Rivers wakija kutufumua tena.
?
Sent using Jamii Forums mobile app
Honest, this time Yanga wana wachazaji wenye ushindani mkubwa mno. Sioni tatizo kabisa kwenye kikosi kile, Nafasi ya Saido/Yacouba yuko Kambole, Upande wa Moloko yuko pia Ki Aziz.

Beki wa kushoto amepatikana yule Kutoka Uganda. Waboreshe kidogo mno pale katikati maana, Aucho huwa yuko jirani na majeraha mara kwa mara.

Tungiweka ushabiki Pembeni, YANGA ni BORA kuizidi SIMBA karibu katika idara zote, na Kama utachukua vikosi vyote viwili kuunda timu 1 basi Yanga itatoa wachezaji kufikia 9 kwenye hiko kikosi cha Pamoja. Hata kocha aje nani atafanya hivyo.
 
View attachment 2248313

Vyanzo vinadai kwamba Al Ahly wanataka kumtoa Miquisone kwa mkopo. Simba wameonesha nia ya kutaka kumchukua ingawa inaelezwa pia Kaizer Chiefs wanamtolea macho. Kwa sasa Miquisone ni majeruhi.

Kazi itabaki mikononi mwa viongozi wa Simba.
kijana lazima arudi unyamani,Kaizer Chiefs hawapo mashindano Caf
 
Honest, this time Yanga wana wachazaji wenye ushindani mkubwa mno. Sioni tatizo kabisa kwenye kikosi kile, Nafasi ya Saido/Yacouba yuko Kambole, Upande wa Moloko yuko pia Ki Aziz.

Beki wa kushoto amepatikana yule Kutoka Uganda. Waboreshe kidogo mno pale katikati maana, Aucho huwa yuko jirani na majeraha mara kwa mara.

Tungiweka ushabiki Pembeni, YANGA ni BORA kuizidi SIMBA karibu katika idara zote, na Kama utachukua vikosi vyote viwili kuunda timu 1 basi Yanga itatoa wachezaji kufikia 9 kwenye hiko kikosi cha Pamoja. Hata kocha aje nani atafanya hivyo.
Ngoja msimu wa CACL uanze tuone, maana sidhani kama inaweza kuwa kikosi imara kuliko Mamelod ambayo kwa miaka kadhaa imeshindwa kutoboa kwenda nusu fainali tangu ichukue kombe 2016.

Mashindano ya CAFCL& CAFCC sio tu kuwa na kikosi bora.
 
Ngoja msimu wa CACL uanze tuone, maana sidhani kama inaweza kuwa kikosi imara kuliko Mamelod ambayo kwa miaka kadhaa imeshindwa kutoboa kwenda nusu fainali tangu ichukue kombe 2016.

Mashindano ya CAFCL& CAFCC sio tu kuwa na kikosi bora.
Kwanza uwe na kikosi bora halafu bahati na mambo mengine ndio yanafuata......uwe na quality ya kutosha kwenye kikosi chako kwanza

Huwezi kwenda kucheza na Wydad na kikosi chako cha Nyanya halafu utegemee huo uchawi wenu...........hata uchawi huwa unadunda dhidi ya quality players
 
Ahmed Ally kaongea shombo kuwa hawasajili mchezaji ambae hajafika Robo Fainal CAF,watu wakamuuliza wakina Kibu,Gadiel,Mhilu na wengineo walifika Robo final ipi ya CAF,kakimbia akaunti yake.
Kajamaa kataahira sana kale!
 
1655814899207.png


Rasmi: Habib Kyombo ni Singida BIG STAR🌻😃🔥

Karibu fundi wa mpira uitumikie klabu yako pendwa katika msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara (NBC Premier League 2022/2023).
 
Unaambiwa wachezaji hawa wanaweza kuiacha simba msimu ujao

Players who could leave 🇹🇿 Simba SC at the end of the season:

🇲🇼 Banda
🇨🇮 Wawa
🇺🇬 Lwanga
🇷🇼 Kagere
🇨🇩 Mugalu
🇹🇿 Kibu
🇰🇪 Onyango
🇬🇭 Morrison (gone already)

Source: Mickyjnr
Kibu anaenda wapi tena ..... Kibu diii kibu deeee.....
 
Viungo wa kati.!
-Kelvin Nashon
-Azeez Andambwile
-Baraka Majogoro
--Hassan Nassoro
-Gustapha Simon

Mchezaji gan ungetamani timu yako imsajili
Kwa namna Kelvin Nashon anavyocheza, akisajiliwa Yanga, atafit kwenye mfumo wa uchezaji wa timu kwa 100%.

Dogo ana kipaji kikubwa sana cha kiungo mkabaji.
 
View attachment 2248313

Vyanzo vinadai kwamba Al Ahly wanataka kumtoa Miquisone kwa mkopo. Simba wameonesha nia ya kutaka kumchukua ingawa inaelezwa pia Kaizer Chiefs wanamtolea macho. Kwa sasa Miquisone ni majeruhi.

Kazi itabaki mikononi mwa viongozi wa Simba.
Hivi mchezaji akitokewa kwa mkopo, anayemlipa ni yupi kati ya timu ya iliyompeleka mkopo au iliyomchukua kwa mkopo?
 
View attachment 2267699

Rasmi: Habib Kyombo ni Singida BIG STAR🌻😃🔥

Karibu fundi wa mpira uitumikie klabu yako pendwa katika msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara (NBC Premier League 2022/2023).
Huku ataimarika walau kwa msimu mwingine tena. Baada ya hapo, labda anaweza kurudi katika enzi zake zile akiwa Mbao Fc.

Angeenda simba, angejichimbia kaburi.
 
Hivi mchezaji akitokewa kwa mkopo, anayemlipa ni yupi kati ya timu ya iliyompeleka mkopo au iliyomchukua kwa mkopo?
Kunakuwepo na makubaliano ya pande 2! Umlipe wewe unaye mmiliki, alipwe na timu inayomchukua kwa mkopo, au mchangie kumlipa wote wawili.
 
1655824036103.png


TETESI

Baada ya dili la Simba na mshambuliaji wa Vipers United , Caesar Manzoki kusuasua .Klabu ya Simba imeonesha nia ya umsajili mshambuliaji wa Ashanti Gold ya Ghana, Yaw Annor ambaye amemaliza akiwa mfungaji bora ya Ligi Kuu ya Ghana akiwa na magoli 22 , msimu wa 2021/22.

Mpango wa Simba sc kumsajili Manzoki unatajwa kuwa bado upo ila Annor ni chaguo la pili kwa mahitaji ya kikosi chao cha msimu ujao.

Je, ni Manzoki au Annor , tuendelee kula mtori
 
Back
Top Bottom