Uzi maalumu wa Mimea Tiba inayotuzunguka majumbani

Ukilikausha then ukalivuta...hapo vipi
 
Mzizi ya mbaazi, ukichanganya na kifumbazi ukachanganya nusu kwa nusu, ukakausha kivulini utapata unga laini, tumia kijiko kidogo kwenye uji kwa siku 30, hata uwe umerogwa vipi uchawi wote utakufilia mbali na utakuwa huru.
 


Unaitwa Mgalagala na Paka na leo nimeshuhudia live Paka anavyogalagala 😂😂😂😂
Haya sasa kwa wale Mnaosumbuliwa na kupigwa chini na Wapendwa mnaowapenda. Practice this.

hii kiboko ya mapenzi sharti lake kubwa ukichuma funga mtupie paka agalegale nao huku wewe ukivuta na kunuia wewe mgalagala na paka kama paka anavyokulilia wewe ndivyo ninavyotaka fulani binti fulani au fulani bin fulani na yeye anililie.
 
Wakuu Kuna mmea unaitwa mtambaza ninaomba picha yake na matumizi yake
 
View attachment 2894441Mchunga ( Dandelion) ni mmea wenye faida nyingi sana Binadam. Hapa Tanzania unapatikana porini na majumbani kama maua.
MCHUNGA ni mmea unafaha na kutibu maradhi mbalimbali kama vile;
  • Matatizo ya mifupa
  • kukosa damu
-matatizo ya mkojo
-kisukali
- Figo
-Ini
-Kansa ya damu
  • kansa ya umbo
  • kansa ya kongosho
  • kansa ya matiti

MATUMIZI
Tengeneza chai kutokana na Mizizi yake na kunywa mara 2 kwa siku.
Tumia Unga wa Mizizi kupaka kwenye ngozi yenye shida.
Kunywa kinywaji cha juice ya majani au Mizizi ya MCHUNGA.
 
Dandelion sidhani kama ni mchunga.

Hebu check , Eruca vesicaria (Arugula)
 
Huo mti naufahamu, muegeya. Hii inasaidia kupona uchawi kwa kuondosha uchawi mwilini au tiba ya stroke?
 
Mkuu ndio wenyewe huo nyakati za zamani sana mtu akiumia jeraha kubwa kwa vyuma vyenye kutu alikuwa anaweka utomvu wake sijui tetenas sijui nini haimpati kamwe na anapona salama.
Sasa mtetenasi na mziwa ziwa unachanganya? Majani, mizizi au maganda?
Na unafanyaje, na dozi ikoje.
 
Leo naielezea nchi yangu Tanzania, kwa kutumia namba na unajimu. Tanganyika imepata Uhuru 9/12/1961. Hapa tunaangalia destini au maisha ya watanzania na Tanzania yao kwa ujumla. Tanganyika imepata Uhuru 9/12/1961, hii Ni sawasawa na 9+12+1961=1982, 1982=1+9+8+2=20, 20=2+0=2. Mapitio ya Tanganyika yapo chini ya namba 2. Hii inamaanisha ya kwamba, Tanganyika Ni sehemu ambayo watu wake wanapenda kushirikiana (ujamaa), lakini pia watanganyika Ni watu wenye amani na upendo, hizi zote Ni sifa za namba mbili. Hivyo basi tuna amani kwa sababu haya ndio mapitio yetu tuliyochaguliwa na mungu.

Tanganyika imepata Uhuru wake tarehe 9, namba tisa Ni namba ya mapambano, ndio maana tuna jeshi zuri katika serikali yetu. Ikumbukwe Napoleon bonaparte aliwachukua watu wenye namba tisa akawaingiza kwenye jeshi lake la ufaransa, akawa na jeshi imara Sana. Namba tisa Ni namba inayohusu Mambo ya kijeshi na mapambano. Lakini pia Namba tisa Ni namba ya Siasa, Sanaa na michezo, hii inatufanya watanganyika tupende siasa, Sanaa na michezo.

Namba tisa ni namba ya kutoa msaada kwa watu wenye shida na majanga. Hii inaifanya Tanzania tuwe miongoni mwa wanachama wa umoja wa mataifa, lengo Ni kusaidiana katika serikali zetu. Ikumbukwe, serikali ya Tanzania ishatoa jeshi lake kwenda kutoa msaada kwenye nchi tofauti tofauti barani Afrika, mfano nchi ya sudani, Ethiopia na zinginezo. Hapa nimeielezea Tanzania kwa kutumia namba.

Tukiielezea Tanzania kwa kutumia nyota, ukiiangalia Tanganyika wakati inapata Uhuru, sayari ya Mercury, Venus na jua zote zilikuwa kwenye nyota ya mshale. Mercury ni sayari inayohusu Mambo ya mawasiliano, Mercury ikiwa kwenye nyota ya mshale ambayo Ni nyota inayohusu Mambo ya kigeni na dini, hii inamaanisha ya kwamba, watanzania tunapenda kuzungumzia Mambo ya kigeni kwenye mitandao ya kijamii, ni wafuatiliaji wazuri Sana, ni watu tunaofikiria au tunapenda Mambo ya dini.

Wakati Tanganyika inapata Uhuru wake, sayari ya Venus ilikuwa kwenye nyota ya mshale, Venus ni sayari inayohusu Mambo ya Sanaa, Mambo ya pesa, Mambo ya urembo, pamoja na masuala yote ya mapenzi. Hii inatufanya watanganyika tupende Mambo ya ugenini, lakini pia, watu kutoka mataifa tofauti tofauti wanaipenda nchi yetu. Watanzania tunapenda dini za kigeni, tunapenda Sanaa za kigeni kuliko za nyumbani kwetu. Na mamodo wetu wapo ugenini, wakina Rambo, van Damme, Rihanna, christiano Ronaldo, Lionel Messi nakadhalika.

Wakati Tanganyika inapata Uhuru wake, jua lilikuwa kwenye nyota ya mshale. Jua Ni nyota inayohusu umaarufu wa mtu au kitu, Sanaa hususani filamu na maigizo, lakini pia Mambo ya uongozi. Hii inatufanya watanzania tukiwa ugenini tujulikane Sana, nenda Kenya, Afrika ya kusini na nchi nyinginezo, zinatufahamu vizuri watanzania. Lakini pia hii inafanya serikali yetu iendeshwe kwa kutumia mifumo ya kigeni, mfano Mwl Julius nyerere alikopi na kupesti mfumo wa ujamaa kutoka China na USSR (Urusi).

Lakini pia wakati Tanganyika inapata Uhuru wake, sayari ya satani na mwezi vyote vilikuwa kwenye nyota ya mbuzi. Sayari ya satani ikiwa kwenye nyota ya mbuzi inakuwa na nguvu Sana. Moja ya sifa ya satani ikiwa na nguvu, inakuwa haipendi mabadiliko, inapenda Mambo ya kizamani au mifumo ya zamani, ndio maana ukiiangalia serikali yetu Ni ileile, suala la mabadiliko linapingwa vikali. Ukitaka uonekane mbaya zungumzia mabadiliko hapa lazima uonekane mpinzani.

Satani ikiwa kwenye nyota ya mbuzi, kupata mafanikio Ni suala la muda mrefu Sana, mafanikio kuyafikia kunakuwa na changamoto nyingi Sana, sio rahisi Kama tunavyofikiria. Watanzania tutapata mafanikio lakini itachukua miaka mingi Sana, Ni suala la muda na wakati. Lakini pia sifa nyingine, satani ikiwa nguvu, inakuwa inazingatia maadili kuliko kitu kingine. Ndio maana watanzania tukiona maadili yanakiukwa lazima tusema, hatumuogopi mtu kwenye suala la maadili.

Sehemu ambayo ina changamoto kubwa kwenye nchi yetu ya Tanzania Ni sekta ya kilimo. Satani ikiwa kwenye nyota ya mbuzi, inamaanisha vikwazo, changamoto, kuchelewa kwenye shughuli za nyota ya mbuzi, moja wapo Ni kilimo.

Mambo ambayo watanzania tunapata mafanikio kiurahisi kupitia nyota ya nchi yetu Ni Sanaa, siasa, kwenda kufanya kazi kwenye nchi za kigeni na biashara za kigeni.
By magical power
 

Attachments

  • Screenshot_20240209-093037.jpg
    32.4 KB · Views: 27
Je mnajua kupitia majina yenu mnaweza mkajua Nani mna bahati nae katika maisha yenu? Jina lako linaweza likawa sababu ya kupendwa au kuwa karibu na bosi wako au mzazi wako, au kuwa na bahati kubwa kwenye mahusiano yako.

Kwa kutumia herufi za kiingereza abcdefghijklmnopqrstuvwxyz, unaweza ukajua Nani una bahati nae katika maisha yako.

A, j na s Ni namba 1
B, k na t Ni namba 2
C, l na u Ni namba 3
D, m na v Ni namba 4
E, n na w Ni namba 5
F, o na x Ni namba 6
G, p na y Ni namba 7
H, q na z Ni namba 8
I na R Ni namba 9

Katika kujua Nani ana bahati nani, tunajumlisha jina la mtu na mtu. Mfano tunajumlisha jina la Zeno na Hawa.
Z. E. N. O
8+5+5+6=24
24=2+4=6
Jina la Zeno Lina namba 6.

H. A. W. A
8 +1+ 5+1=15
15=1+5=6
Jina la Hawa Lina namba 6.

Tunajumlisha namba ya jina la Zeno na namba ya jina la Hawa tuone tutapata namba ngapi.
Zeno =6, Hawa=6, hivyo 6+6=12, 12=1+2=3.
Tumejumlisha jina la Zeno na Hawa tumepata namba 3. Namba 3 Ni namba ya bahati. Hivyo basi Zeno na Hawa watakuwa na bahati kubwa katika mahusiano yao ya kikazi au ya kimapenzi. Mfano, Kama Hawa Ni bosi wa Zeno, Zeno atakuwa na bahati kubwa ya kukubalika na kupendwa na bosi wake mwenye jina la Hawa.
By magical power
 
Leo tunaendelea na majina ya namba zilizobaki tuone zikiwa kwenye mahusiano zinakuwaje. Majina ya watu Yana nguvu kubwa Sana katika mahusiano ya mtu na mtu, hivyo yanaweza yakapelekea watu wakawa kwenye mahusiano ya aina Fulani kulingana na namba za majina yao. Tunaangalia namba za majina kwa kutumia alfabeti za kiingereza A mpaka Z.

A, j na s Ni namba 1
B, k na t Ni namba 2
C, l na u Ni namba 3
D, m na v Ni namba 4
E, n na w Ni namba 5
F, o na x Ni namba 6
G, p na y Ni namba 7
H, q na z Ni namba 8
I na R ni namba 9

Mfano tunachukua jina la John na Fatuma tuone wakiwa kwenye mahusiano wataishi maisha gani.

J. O. H. N
1 +6 +8 +5=20
20=2+0=2
Jina la John Lina namba 2.

F. A. T. U. M. A
6+1+2+3+4 +1=17
17=1+7=8
Jina la Fatuma Lina namba 8.

Baada ya kupata namba za majina ya John na Fatuma, tunajumlisha namba zao 2+8=10, 10=1+0=1. Hivyo basi, mahusiano ya John na Fatuma yatakuwa Chini ya namba 1.

Sifa ya namba 1 Ni kujiongoza yenyewe, namba 1 Ni namba yenye ubinafsi. Hivyo basi, mahusiano ya John na Fatuma yatakuwa na ubinafsi ndani yake, kila mmoja atakuwa anaangalia upande wake. Lakini pia, kutakuwa na mabishano katika mahusiano yao, kwa sababu kila mmoja hatopenda kupelekeshwa na mwenzake. Mahusiano yao yatakuwa na majivunia ndani yake, kila mmoja atajiona Bora kwa mwenzake.

Ingekuwa namba 4, mahusiano yao yangekuwa kwenye wakati mgumu Sana. Namba 4 Ni namba ya upinzani. Hivyo kila mmoja angekuwa mpinzani kwa mwenzake, vurugu na kupigana ingekuwa Ni Jambo la kawaida. Lakini pia, katika mahusiano yao wangekuwa Wana panda na kushuka kwenye kipato chao.

Ingekuwa namba 5, mahusiano yao yangekuwa rahisi kuachana na kutengana. Mahusiano ya namba 5 yanaenda kwa kutumia akili nyingi. Jambo la kuachana na kurudiana Ni Jambo la kawaida kwenye mahusiano ya namba tano. Namba 5 inataka tuishi nao kwa akili, sio kuangalia hisia ya mtu. Uzuri wa namba 5 upo kwenye mahusiano ya kibiashara, Ni rahisi kufanikiwa, kwa sababu namba 5 Ni namba ya biashara.

Ingekuwa namba 7, mahusiano yao yangekuwa ya Siri au mmoja wapo angekuwa msiri kwa mwenzake. Siri zipo nyingi, inawezekana ikawa mmoja wapo anamficha mwenzake Kama ana biashara, nyumba, pesa au ana mwanamke au mwanaume wa pembeni. Angalizo, usije ukamuhesabia mume wa mtu au mke wa mtu alafu ikaja namba 7, utajiingiza kwenye matatizo, maana Cha mtu sumu.

Ingekuwa namba 8, John au Fatuma, mmoja wapo angechelewa kumpenda mwenzake. Hapa ingechukuwa muda mrefu mmoja wapo kumkubalia mwenzake kuingia kwenye mahusiano. Ila mahusiano yakianza kunakuwa na heshima kubwa Sana kwenye mahusiano, kila mmoja anamuheshimu mwenzake.

Namba zingine nilishazielezea huko nyuma, hivyo leo nilikuwa namalizia namba 1, 4, 5, 7 na namba 8. Watu wengi wametaka nizielezee namba zote, Nami nikaona Ni Bora nizimalizie.
By magical power
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…