ELIMU YA BURE..VYAKULA (TIBA).. TOA ADHABU..wabaya wataanza kukukwepa.
Hivi ni baadhi ya vyakula muhimu sana katika tiba asili. Wakati maisha yakiendelea kama kawaida, utumiapo vyakula hivi utajikuta UKIJITIBU mwenyewe bila kufahamu ama KUJIKINGA na majanga ya kishetani na kichawi automatically.
Kama si hivo basi UTAWAHANGAISHA walozi wako na KUWAADHIBU VIKALI masheitwan walioko mwilini mwako au katika makazi yako kwani hutumia makazi na mwili wako kama
makao yao huku ukiwahifadhi, kuwatunza, kuwalinda na kuwatumikia bila ya wewe kufahamu, wakati huo huo wakikuharibia kila kitu japo utaona kana kwamba unajiharibia mwenyewe (self destruction) huku wakikulia timing ya kukuteketeza mazima (total destruction) .. Sasa kabla ya total destruction JIFAHAMU VEMA.
1. Chumvi ya mawe, wakati mwingine pikia chumvi mawe katika mapishi yako ya kila siku. Pia ukiona kitu usichokielewa, mimina au nyunyiza chumvi mawe kwenye hicho kitu.. Alafu chukua hatua.
2. Pilau, Mara moja moja pika pilau kwako. Faida ya kitiba IPO katika vile viungo vyake bila kusahau kitunguu saumu.
3. Pika mbaazi, choroko, kunde nk bila kusahau ufuta, ubuyu na ukwaju.
4. Pendelea kutumia vyakula vya baharini. Hata kama si mpenzi wa vyakula hivyo basi Mara moja moja jiongeze tu kula vyakula hivyo.
5. Pika na tumia chai ya viungo asili kama mdalasini, iliki, karafuu, mchaichai nk. Usichukulie poa ati vinauzwa kwa Tsh mia.
6. Kivumbasi.. Mwinura mkubwa .. Kashwagara. Tumia mmea huo kupikia chai pia . mikoa mingine kiungo kikuu cha chai ni mwinura mkubwa. Wengine hutumia kivumbasi kupikia kahawa za kutafunwa. Faida sana.
7. Epuka uzinzi na ulevi, mashetani hupitia sana hapa, ukiachana na VISASI vya wanadamu vitokanavyo na stress za mapenzi.
8. Mara moja moja tumia maji bahari kujikogesha mwili wako. Usijisingizie ati bahari iko mbali nawe, usafiri upo sehemu zote.
9. Nenda katika ibada yako kanisani au msikitini kulingana na imani yako.. Hats kama ni nyumbani kwako, usimsahau Mungu.
10. Usimnyenyekee shetani hata siku moja ati ''yaani nimehangaika kote ila sijapata tiba..nimeamua kuacha'' .. Unajipa madhambi ya bure wewe.
11. Kachungulie, usiache muda mrefu ukapita bila kwenda KUNAKO ili '' kujifuatilia mwenyewe'' utafahamu mengi yaliyokuzunguka.
12. Tumia mboga za majani aina nyingi uwezavyo. Utakuta jamii moja wanatumia, nyingine hawatumii. Ukiwa umenisoma hapa basi jitahidi ule, mfano katika jamii moja ni mboga, kwingine ni chakula cha sungura. Nakwambia we kula mboga hizo.
Hayo ni baadhi tu, ikiwa mwilini mwako una uchawi, unaweza ukauondoa japo unaweza usitambue hilo. Pia kama kuna jini mchafu mwilini mwako utamuadhibu na kumuhangaisha. Uwezekano ni mkubwa sana akaukimbia mwili wako.
Cha msingi na sekondari, fuatilia ili usafishe mwili wako kuondoauchawi, masheitwani, kunusi na nuksi, ufungue liziki zako na vifungo vingine na kung'arisha nyota na update kazi ili maisha yaendelee. Kumbuka maisha haya ni yako binafsi (mwili, roho na nafsi) ni vyako na havina mbadala (spea). Jihangaikie mwenyewe. ULIZA CHOCHOTE, NITAKUJIBU.