Uzi wa ushahidi wa mambo ya kusikitisha katika uchaguzi mkuu wa 2020

Mikoani huko kamatakamata inatisha. Kuna wananchi weengi wamo korokoroni kwa ama kutokukubaliana au kuhoji wizi na figisu za ccm kwenye uchaguzi
Mkuu, hii ni kiujumla mno; haisaidii kitu chochote.

Tunataka ushahidi. Hawa walioko korokoroni hawana majina au hata sehemu waliko hazijulikani?
 
Aisee haya mambo ni ya aibu kubwa mno!!
 
Mkuu, hii ni kiujumla mno; haisaidii kitu chochote.

Tunataka ushahidi. Hawa walioko korokoroni hawana majina au hata sehemu waliko hazijulikani?

Kaka kule inbox umegoma kunipa mrejesho!
 
Mkuu, hii ni kiujumla mno; haisaidii kitu chochote.

Tunataka ushahidi. Hawa walioko korokoroni hawana majina au hata sehemu waliko hazijulikani?
Mkuu, Kama una uwezo wa kufanya chochote fuatilia mkoa wa Mara (hasa Tarime na Rorya), Simiyu na Singida. Utashangaa sana.

Pia, ukiacha Dar, naskia maeneo mengine mengi ni hivo hivo.

Wale unaskia wanakimbia usifikiri wanaigiza
 
Ongeza - karatasi za kura zilizobaki kwenye vituo baada ya upigaji kura, wasimamizi waliambiwa, wazipige upande wa CCM na kuingiza kwenye masanduku ya kura.
Vituo vyote vya kupigia kura Tanzania wasimamizi wakuu walielekezwa kuongeza kura kwa ccm.
 

Jamaa aliniudhi sana na kuniangusha. Tumepiga kura wote kisha akanishawishi eti nitafute wenzangu kama 100 tupige kelele na kuandamana kama hatuna akili atanipa shillingi laki mbili., kumbe alishapanga tukio akamatwe aje kusingizia anataka kuuliwa ili akaishi Ulaya.Kwa kweli Lissu wewe ni msaliti, nataka hela zangu.
 
Ushahidi mwepesi kwa tuhuma nzito!! Acheni propaganda za kuchafua nchi wakati mnajua kabisa masuala haya yamejaa URONGOOO na GHILIBA kubwa!

Hata Rais Trump analalamika ila Kwa ushahidi mweupe na jinsi Mahakama ilivyoukataa tusubiri tuone Rais Biden akipelekwa ICC!

Queen Esther
 
Marekani ingekuwa kama Tanzania, Trump angetumia mahakama, NEC, jeshi, polisi, Mamlaka ya Anga, makampuni ya simu, TISS, TCRA, nk kubaki madarakani. Ungekuwa na akili hata kidogo, ungejua kuwa kwa vile Marekani siyo Tanzania, Trump anaondoka.
 
Kodi za wananchi waliodhulumiwa haki yao
Ni ziaid ya UCHAFUZI ,Bilioni zaidi ya 500 serikali imepoteza kwenye UTOPOLO Huu wa Tar 27 na 28 Oct 2020.
 
Mkuu unataka watu waweke ushahidi ili wasulubiwe baada ya kuanika ushahidi?
 
Nowdays jf is not where we dare to talk openly... Tuliamini hapa n sehemu ya kutoa ya moyoni yasiyoweza kutolewa in other platforms but saivi wanayazuia!! Its real bad!
 
Maneno mengi ushahidi sufurii. Tunaita porojo.
 
Ni ubabe wa kutisha...Natumia kodi yenu, mda wenu na attention yenu kwenye matokeo ya kura zenu kumbe sio zenu,anayebisha anaharibu amani anapigwa anateswa na ikibidi anauawa. Tunaona kila siku watu wazikwa,sijui wengine wanaamini wataishi Miele.....
 
Mkuu acha urongo basi
 
Mkuu, Kama una uwezo wa kufanya chochote fuatilia mkoa wa Mara (hasa Tarime na Rorya), Simiyu na Singida. Utashangaa sana.

Pia, ukiacha Dar, naskia maeneo mengine mengi ni hivo hivo.

Wale unaskia wanakimbia usifikiri wanaigiza
Hapana. Mimi sisemi kuna kuigiza kwa wanaokimbia. Wanaokimbia wanajulikana na ni ushahidi usiopingika. Wanachokimbia kinajulikana na yeyote mwenye akili timamu isipokuwa hawa waliolewa waliomo humu JF na kwingineko.

Uzi huu ni muhimu sana. Unapoandika hapa kama ulivyoandika hata katika mistari mitatu uliyobandika hapo juu, huo sio ushahidi hata kidogo; hayo ni kama majungu tu.

"Mikoa ya Mara, Simiyu na Singida", wote hao hata mmoja tu asijulikane kabisa taarifa zake kwa usahihi?

Sasa usije ukadhani ninakukatalia kwamba watu hao hawapo, lakini kutaja tu mikoa bila hata ya taarifa zozote zinazowahusu watu hao, huo sio ushahidi. Hata hao wanaofanya maovu haya wanapenda sana taarifa za kijumlajumla sana kama hizi, kwa sababu haziwabani kivyovyote.

Watu wanaowekwa gerezani, kwa mamia, hata mmoja bila kutajwa jina na mkasa wake ukaelezwa na kueleweka..., huo sio ushahidi.
 
Kaka kule inbox umegoma kunipa mrejesho!
Utaniwia radhi ndugu yangu. Huko huwa napaepa kama ukoma; huwa siingii kamwe huko.
Naomba unielewe, na sio kwamba nakutilia mashaka mkuu wangu.

Tuendelee tu huku huku. Msimamo wako nauelewa barabara, na sina shaka nao.

Najua kuna siku moja tutaelezana yote bila ya shaka tunayoshindwa kuyaeleza bayana sasa hivi. Siku hiyo ipo tu inakuja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…