Umesahau kuniambia dakika ngapi kukoroga siag na sukar na mayai dakika ngapiTafuta mzani
Na tin ya kupikia,sufuria huwa hazitoi keki yenye shape nzuri.
Recipe yule mdau Patra31 aliweka Jana.
Mixer siyo lazima uwe nayo.
Waweza tumia mwisho tu.
Hata mm sina mixer.
Sasa inabidi uandae moto
Kama ni oven inatakiwa uipashe iwe na moto
Au kama unatumia jiko la mkaa,
Unaandaa moto,unachukua sufuria kubwa sana unaweka mchanga kidogo,unaupika motoni.
Andaa tin yako mapema,unapaka siagi na unanyunyiza unga ili kuzuia keki kukakamia chini .
Unaanza sasa kuchanganya ingredients zako;
*Anza na siagi pamoja na sukari.
Hapa sasa ndipo pa muhimu..inatakiwa uchanganye kwa nguvu huu mchanganyiko hadi ugeuke kuwa na rangi nyeupe.
*Unaanza weka mayai
Unaweka moja baada ya jingine.
Kila ukiweka moja,unakoroga,unaongeza unakoroga
Hivyohivyo hadi unamlize.
*Anza kuweka unga wako
Hakikisha unga unauchekecha mapema.
Unaweka kidogo kidogoo.
Huu mchanganyiko wa unga usiupige sana kama ule wa siagi na sukari
Wenyewe tunachanganya tu kidogo..kama una mixer ,unaweka low speed.
Weka ladha matone kiasi tu.
Mimi huwa naongeza na vineger kijiko kimoja.
Kisha weka baking powder,koroga kiasi,
Usiache huu mchanganyiko ukae muda mrefu
Ukimaliza tu,unahamishia kwenye tin .
Igonge tin chini kama mara 3,kuondoa hewa hewa.
Usipogonga ndio zile keki unakuta Ina matobo.
Iweke tin ndani ya lile sufuria lenye mchanga wa moto .
Funika,weka moto juu.
Hakikisha moto hauwi mwingi sana wala mdogo sana.
Kama unatumia oven unaweka.
Usifunue funue keki Yako,inaweza kunywea.
Baada ya muda kama nusu saa hivi keki itakuwa tayari.
Inategemea na kasi yako ya mkono.Umesahau kuniambia dakika ngapi kukoroga siag na sukar na mayai dakika ngapi
Na kwanin keki hupasuka sababu ni nin?Inategemea na kasi yako ya mkono.
Ukikoroga kwa nguvu na haraka ,basi hata mchanganyiko wako utabadili rangi haraka.
Kwahiyo kasi ya mtu ndiyo itadetermine atumie muda mwingi au mchache.
Kichwa ndo sehemu ya samaki nisiyoipenda
Kuna watu mna makusudiView attachment 2514941
Cha jion ila itakuwa soup tu
Hata mim sipendiKichwa ndo sehemu ya samaki nisiyoipenda
Imradi tu tupate njaa[emoji39]
Oven lita 48 210,000 hadi 180,000Mkaa
Sina Oven
Keki hupasuka kutokana na sababu mbalimbaliNa kwanin keki hupasuka sababu ni nin?
Nikinunua oven nataka ninunue kubwa itakayoweza kupika na zike cup cakes ndogo ndogo na nyingi .Oven lita 48 210,000 hadi 180,000
SawaKeki hupasuka kutokana na sababu mbalimbali
Ukiweka moto mwingi au ukazidisha baking powder
Au siagi na mayai umepiga sana.
Inatakiwa tupige sana ndiyo lakini isiwe too much na muda mrefu kupita kiasi.
Mayai ukiweka mojaUmesahau kuniambia dakika ngapi kukoroga siag na sukar na mayai dakika ngapi
Nyama kharam [emoji23][emoji847][emoji847][emoji847]
View attachment 2517199
Sema kwa biashara nunua oven ya gas au ya umeme na generator, vinginevyo utakuja pata hasaraNikinunua oven nataka ninunue kubwa itakayoweza kupika na zike cup cakes ndogo ndogo na nyingi .
Pia nitanunua nikishaanza rasmi biashara.
Sasahivi acha nikomae tu na mkaa.
Uzuri oven haina complications kama mkaa.
Nikiweza kwenye mkaa, hata Kwenye oven nitaweza.