Uzi wa vyakula tu

Hakuna kitu nilikuwa nachukia kama kuangalia maharage alafu ubaya tulikuwa tunapitia kwenye kuni hapo bimkubwa kabana hakuna cha housegirl wa mabinti kuchochea moto ni watoto wa kiume ndio kazi yenu had yaive alafu mm ndio nilikuwa mdogo Yan utapigwa na moshi hadi uchukie.
 

Ila umeshangundua wali wa kupikiwa kwenye kuni au mkaa mtamu sana,hata maharage ylopikwa kwa kuni
 
Sasa ole wako ukacheze halafu huku vijinga Vimeisha motoni[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787],maharage hayajaiva,na jioni ishafika[emoji16][emoji119]


Mimi Bi Mkubwa hadi leo anapikia kuni.
Mnaweza mpa hela ya mkaa na gesi
Anaweza nunua tu mkaa kidogo kwa ajili ya kupikia ubwabwa
Ila vyakula vyake vingi anapikia kwenye kuni.

Mkienda mnamjazia gesi,hapikii
Anaitunza[emoji1787]ili mradi apike kwa kuni.

Ana hekaheka yule mama[emoji119]
 
Old is gold
Vyakula vya kwenye kuni au mkaa vitamu mno ila kuni ziwe nzuri tu [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] sikuwa mbichi utalia
 
Old is gold
Vyakula vya kwenye kuni au mkaa vitamu mno ila kuni ziwe nzuri tu [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] sikuwa mbichi utalia
Chakula cha kuni kitamu snaa
Ila mimi sipendi kunuka moshi halafu nina aleji
Nikiingia tu kwenye kuni kwa kweli ni mtihani
Namwambia mm napikia gesi,atakuambia acha tu nitapika mwenyewe,
Yuko radhi akapike mwenyewe kwenye kuni kuliko utumie gesi yake.


Kuni mbichi[emoji119][emoji119] usiombe
Balaa lake[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Moshi mwingi na haziwaki
Kipindi cha masika sanasana ndio huwa kuni mbichi zinakuwa janga
 

Wamama wanapenda kupikia kuni
,mjin kuni unazipatia wapi? Vijijn sawa
 
Nzuri mi napenda cheesee ina ladha nzurii
Trudie umeona mkate nilotengeneza?nimejifunza insta Ila cake nimeshindwa sijui nakosea wapiii [emoji23][emoji23][emoji23] inakuwa ugali
Nimeona mkate umeutoa vizuri kweli hongera, keki inabidi ufwate vipimo bila vipimo inakuwa ugali. Na pia joto la kupikia inabidi liwe wastani iive vizuri.
Jaribu tena kupika kidogo kwa kufwata vipimo vyake
 
Safi sana ni vizuri mtoto ajue kazi zote,
Umenikumbusha kutumwa jamani ukiwa mdogo unatumwa kama mwehu [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] leta hiki fanya kile
Yaani tabu ya kutumwa hahaaa, sasa hivi ndio inamkuta mwanangu wa 4 yrs. Namtuma mpaka sasa hivi anajua kabisa chakula fulani kinahitaji hiki na hiki. Namuonea huruma ila ndio anajifunza
 
Kwenye oven
Jaribu hii unga nusu kg, butter robo kg, mayai 6_8 ya kisasa,baking powder vijiko vidogo 2 level,icing sugar robo kg , orange zest kiasi, orange juice vijiko 10.
Changanya unga na baking powder kisha chekecha,
Washa oven kabisa moto weka 150
Andaa chombo cha kupikia
Koroga cake yako kama inavyotakiwa
Bake sasa cake yako muda dakika 45 , usifungue fungue oven we itazame cake kupitia kioo baada ya dakika 45 fungua uchome na toothpick katikati uone kama imeiva kama bado ongeza dakika uendelee kusubiri iive, ikiiva subiri ipoe ndo ukate
 
Sawa nitafanya tena
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…