OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 53,868
- 121,001
Leo ni uzinduzi rasmi wa Simba Week, tuna mambo mengi kwenye wiki hii.
"Msimu huu tunarudi kwa nguvu, tunarudi kutetea ubingwa wetu na slogan yetu ni WE ARE UNSTOPPABLE - HATUSHIKIKI – HATUZUILIKI.- CEO Barbara
Zoezi la usajili bado linaendelea. Wiki ijayo timu yetu ya digital itaanza kutangaza wachezaji wengine.- CEO Barbara.
Kesho mtajua tofauti ya mdhamini na msaada. Tutakuwa na tukio na mdhamini wetu mpya, kampuni ya M-Bet."
"Wachezaji ambao tunawasajili sio wa sandakalawe, ni wachezaji muhimu kwenye vikosi vyao hivyo kunakuwa na ugumu kuwapata, inabidi kuzungumza na vilabu vyao ili kuwashawishi."- Meneja wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano, Ahmed Ally.
Mwenyekiti wa klabu ya Simba, Murtaza Mangungu amesema jezi za timu hiyo msimu wa 2022/23 zitazinduliwa wiki hii na zitatengezwa Ulaya badala ya Asia.