Uzinduzi wa shamba la miti Chato kesho, Rais Magufuli kuwa mgeni Rasmi

Uzinduzi wa shamba la miti Chato kesho, Rais Magufuli kuwa mgeni Rasmi

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
E021B95C-0CDE-4388-B19D-DDF0AF8C3EB9.jpeg


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika hafla ya kuzindua Shamba la Miti Chato kesho Januari 27, 2021 katika eneo la Butengo, Wilaya ya Chato, Mkoani Geita.

Wananchi maeneo husika pamoja na wananchi wote mnakaribishwa kuhudhuria hafla hii ya kihistoria kwa nchi yetu. Hafla hii inatarajiwa kuanza saa kumi na mbili asubuhi.

SHAMBA la Miti Chato ni miongoni mwa mashamba ya Serikali yaliyoanzishwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) katika mwaka wa fedha 2017/18.

JANUARI 12, 2021 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Damas Ndumbaro alitangaza Chato kuwa Kitovu cha uhifadhi na utalii katika Kanda ya Ziwa alipokuwa katika ziara ya kikazi shambani hapo.

Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2017/2018(miaka minne iliyopita) shamba hili limepandwa jumla ya miche 7,449,255 kwenye hekta 2,682(sawa na ekari 6,705).

Miti.jpg
 
Ni jambo jema maana litahamasisha wananchi kupanda miti kwenye maeneo yao?
 
Hapa kikwete alikuwa analaumiwa kufungua shule msoga. Watanzania hawaishi malalamiko
 
Mimi kesho nazindua ufugaji wa samaki karibuni sana

Hapa kikwete alikuwa analaumiwa kufungua shule msoga. WaTZ hawaishi malalamiko
 
Hapa kikwete alikuwa analaumiwa kufungua shule msoga. WaTZ hawaishi malalamiko
Mkuu hatujakuuliza mbona unajishtukia
 
Hapa kikwete alikuwa analaumiwa kufungua shule msoga. WaTZ hawaishi malalamiko
Usiseme watz sema machadema
 
Hapa kikwete alikuwa analaumiwa kufungua shule msoga. WaTZ hawaishi malalamiko
Mkuu, wengi wa watu wa Kitanzania, hawajawahi kujua wakitakacho hivyo, wewe wasikupe homa.
 
Ni jambo jema, hongera kwa TSF, ni vyema mapori mengi ya asili yapandwe miti ya kisasa ya kibiashara mengi yamebaki vichaka.
 
Back
Top Bottom