Uzoefu wa biashara ya juisi ya miwa; Changamoto na ushauri

Uzoefu wa biashara ya juisi ya miwa; Changamoto na ushauri

Ndugu wana Jamvi Poleni na majukumu ya hapa na Pale. Naomba ushauri wenu kuhusu biashara ya kuuza juice ya Miwa kwa Mikoa ya Pwani.Ningependa kujua changamoto zake na Faida inayopatikana lakini pia Mashine inayotumia Umeme kukamua Miwa inauzwa wapi na ni shilingi ngapi....?
Naomba kuwasilisha Wadau.
Mm ninayo made in India. Ni original kabisa utaifurahia. Mwanza nilitumia za tz zilinishinda.
 
Ninayo Dar. Iko complete pamoja na meza ya huduma, na fan ya kufukuzia inzi. Bei poa Tshs:1.5m
Nitafute kwa namba 0754377397 na 0789531559
 
Nami ninatafuta hiyo mashine mwenye kujua bei zake atusaidie hapa,isiyotumia umeme yaan ya mkono,inayotumia umeme na inayotumia diesel

Sent from mTalk
 
Ninayo Dar. Iko complete pamoja na meza ya huduma, na fan ya kufukuzia inzi. Bei poa Tshs:1.5m
Nitafute kwa namba 0754377397 na 0789531559
***
kwa utendaji huu wa sasa kwa Sikh waweza pata net ya 30,000/ kama faida.
 
Unataka uwawekee wasukuma juice ya miwa mwatulole au nyankumbu....mhhhh wale wamezoea kumenya miwa k mdomo na kutafuna sijui kama watalipa
Nyankumbu[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] .Watu wanatafuna miwa kama gomba.
 
Wakuu heshma kwenu,naomba kujua kama biashara ya juice ya mua inalipa maana nna vimilion vyangu vitatu jamaa wananishauri ninunue mashine ya kukamua juice ya mua inalipa..Kejeli ruksa pia
 
Hyo biashara ni location tu aseeh...ukipatia location utapiga hata elf 70-80 kwa siku...tatizo ni kupata location site tu....vingine vinafata....
 
Hyo biashara ni location tu aseeh...ukipatia location utapiga hata elf 70-80 kwa siku...tatizo ni kupata location site tu....vingine vinafata....
Nashkuru mkuu naomba anaejua pia eneo ambalo ni potential anipe taarifa,lkn pia kupitia biashara hiyo ntaajiri vijana wenzangu maana mimi nipo ktk ajira rasmi ila kuacha pesa bank naumia maana zunatumika kuwanufaisha wenyewe
 
Tafuta pakujibanza maeneo ya k.koo hasa parking za daladala au sehem kwenye mama ntilie wengi.
Ukipata mashine ya kisasa nenda vyuoni km UD pale uombe leseni kwenye uongozi wa wanafunzi.

Maeneo km tandika, buguruni, manzese na sehem yenye muingiliano mkubwa ndio potential kwa biashara yako.

Ila zingatia usafi katika biashara hii.
 
Inalipa ila kwanza uwe msafi tu maana kama usipokua msafi wateja wako watakua wapita njia tu na sio watu na familia zao wanaonunua mpaka lita tano hasa kipindi cha mfungo wa Ramadhani
 
Ahsanteni sana kwa michango yenu mmenifungua sana ila nipo ktk process yakupata eneo huku nikikamilisha mchakato wakununua hiyo mashine, soon mambo yakikamilika tu ntakuja tena kuomba kukutanishwa na kijana mwenye uwezo wakuiendesha biashara hii, anaeamini kua ujasiriamali ndio njia ya kujipatia kipato halal
 
Back
Top Bottom