Valuation Calculator for Used Motor vehicles and CRSP List - TRA WANAKISIA BEI ZA MAGARI?


shukrani boss hapo nimekusoma vizuri saaaana mkuu.....
 
Jamani na mimi naomba msaada nimeagiza kagari kangu cc1490 ya mwaka 2003 kwa usd 2000 cif gari ndio ipo njiani je Nitalipia kodi sh ngapi?
 
hii ni bila ya hiyo CIF hapo juu?

nisaidie na mimi

Alteza ya kawaida
2001
cc 1900
F.O.B 2000 $

itacost kiasi gani?
 

asante mdau
 
hiyo sheet yao ya excel ni very open its a matter of plug and play.
wasiwasi wangu kama wengine walivyoweka humu ni jinsi wanavyoweka hizo price za hayo magari. Kuna mengi sana ni changa la eyes. Na kama list ipo kwa nini wakatae kuitumia wao wenyewe?
Nadhani ifike mahali tuanze kupelekana mahakamani ili watu wawajibike. U can not preach A and expect to live B. What's the exception?
Wizi tu. Sioni kama kuna mashiko sana kuwa na mkeka halafu hawautumii wao wenyewe wanakurupuka kufanya kivyao vyao. Ila pia nahisi watu wengi hawajui kama hii mikeka ipo ndo maana wanabambikiwa sana makodi yasiyokuwepo.
Yana mwisho haya yote lakini
 
TRA hawasomeki kiukweli. Calc zao haziendani na uharisia hata uduchu. Bora kununua gari iliyokwama kama hela yako niya kupima
 
ndugu zangu nataka kuagiza range rover 4.6 ya February 2000 FOB £2,995 ni kiasi kama tshs
6,901,200/=ushuru itakuwa bei gani!samahani kwa usumbufu wadau.ASANTENI.
 
Wha about Subaru Forester ya mwaka 2000 wakuu,inaweza gharimu ngapi kimahesabu ya kodi za Tra
 

TRA kuna matatizo sana,wanalalamikiwa sana but hawana nia ya kijirekebisha au kutoa elimu kwa wateja wao...badala yake elimu inayotolewa ni ya kulipa kodi ila namna gani ukadiriaji wa kodi unafanyika ni wao wenyewe.
 
TRA wanahitaji maandamano, nimenunua gari kwa shilingi 11,300000 kodi wanasema 11,350,000. Calculator inaonyesha nahitaji kulipa kodi ya 4,580,000 inakuwaje jamaniiii! nifanyaje????
 

Twende taratibu mkuu hapo kwenye nyekundu, kwa hiyo TRA wanaestablish bei za magari katika mchakato wa kukokotoa kodi wanatumia retail price, kwa maana bei ya gari pamoja na kodi (KODI IPI) wakati kodi ndiyo wanakokotoa?
 
Kama ntakuwa nimewaelewa TRA ni kwamba hiyo gharama ni ya gari mpya yani MSRP= manufacturer suggested retail price. Hiyo sio FOB au CIF. Kwasasa wanatumia mtindo wa kushuka thamani ( depreciation). Hivyo ukiagiza toyota RAV4 ya mwaka 2005 wao wataangalia bei ya toyota RAV4 ya mwaka 2013 yani kitu kipya kabisa mtengenezaji anauza shilingi ngapi yani MSRP ni ngapi.
MSRP wanaitoa kwasababu makampuni yanayotengeneza magari hayauzi moja kwa moja kwa mteja, wanawapa ma dealer wauze sasa wewe ukienda kwa dealer na ameongeza em 10 tafuta dealer alieongeza em 7.
HOJA YAKO: ukiambiwa angalia gari inayoendana na RAV4 kama yako haiko kwenye list ingia kwenye mtandao google linakotengenezwa hilo la kwako MSRP ni ngapi? Kama ukikuta ni $23,000 angalia hiyo inaendana na gari gani vingine unaweka kama cc, mwaka nk unapata kodi
 

Ikitokea bei uliyonunulia ni kubwa kuliko iliyo kwenye list ya tra, bei uliyonunulia inatumika.
 

Namini ni wajibu sasa wa uongozi wa JF kufanya utaratibu wa kuwaalika hawa maafsa humu pindi inapobidi maana hali ni mbaya kuna maswali mengi kwa wizara zote, polisi, TRA na taasisi nyingine.
Mkuu Invisible tafadhali anagalia unachoweza kufanya.
 
Last edited by a moderator:
TRA wanahitaji maandamano, nimenunua gari kwa shilingi 11,300000 kodi wanasema 11,350,000. Calculator inaonyesha nahitaji kulipa kodi ya 4,580,000 inakuwaje jamaniiii! nifanyaje????
Fedhuli Tafadhali tuambie ni gari gani na ni la mwaka gani?
 
Last edited by a moderator:
Kuna jamaa yangu aliwahi kuniambia maafisa wa TRA wanamiliki wao na jamaa zao yard za kuuza magari hapa TZ kwa hiyo wanachojaribu kufanya ni kupandisha sana kodi ili ku discourage watu wasiagize magari nje ili wanunue yaliyoko kwenye yard zao wapate faida,hii nchi ubinafsi utawala.
 
TRA kuna matatizo sana,wanalalamikiwa sana but hawana nia ya kijirekebisha au kutoa elimu kwa wateja wao...badala yake elimu inayotolewa ni ya kulipa kodi ila namna gani ukadiriaji wa kodi unafanyika ni wao wenyewe.

Bora wangefanya tulipie kama sasa tunavyolipia MVehicle License KWA Mpesa itapunguza ukwapuaji wao waliouzoea
 
TRA wanahitaji maandamano, nimenunua gari kwa shilingi 11,300000 kodi wanasema 11,350,000. Calculator inaonyesha nahitaji kulipa kodi ya 4,580,000 inakuwaje jamaniiii! nifanyaje????


TRA ni mzigo kwa maendeleo ya Tanzania, hiyo calculator yao haina ukweli hata kidogo, hata ukifuata vipi inavyoelekeza ukifikisha gari mchezo tofauti. Shame on them
 
Twende taratibu mkuu hapo kwenye nyekundu, kwa hiyo TRA wanaestablish bei za magari katika mchakato wa kukokotoa kodi wanatumia retail price, kwa maana bei ya gari pamoja na kodi (KODI IPI) wakati kodi ndiyo wanakokotoa?

Wauza magari mapya hapa tanzania, TOYOTA, DT Doby na wengine si wanayalipia kodi magari yao na kuweka profit magrni yao? Hivyo bei zilizowekwa ni za retai price kwa gari jipya ambalo lishalipiwa kodi na kuwekwa profit margin. Unapotoa hiyo margin na kodi zilizolipia unapata thamani ya gari likiwa jipya kabla ya kulipiwa kodi. Baada ya hapo ndo yanakuwa depreciated kufuatana na umri ili kupata thamani ya kulitoza kodi kwa wakati huu.
Hope utakuwa umenisoma
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…