Vanessa Mdee ndio msanii bora wa kike kwa sasa, Jide kakabidhi kijiti rasmi

Sijakuelewa mkuu..unataka kusema bifu la jide na clouds ndo lililomuweka jide juu kimuziki ama??

Kwa kipindi kile yes bifu ilimrudisha kwenye chati,kabla ya bifu alikuwa ashaanza kufifia,sahivi kafifia tena maana katoa nyimbo kama 3 zote hazijafanya vizuri
 
Namkubali sana v-money..ila naamini hata yeye ukimuuliza kuwa ye ni mkali kuliko jide atakwambia hapana...

hujamuelewa mtoa mada, ni kama kwenye mpira Thibaut Courtois wa Chelsea anapompigisha bench Peter Cech, hii haimaanishi kwamba Courtois ni bora kuliko Cech bali kwa wakati huu Courtois yuko vizuri kuliko Cech, Cech heshima yake inabakia palepale kama Legend wakati Courtois ndo yupo kwenye mda wa kuutafuta ulegend (ingawa anaweza asiufikie).Mwisho wa siku unaweza kujaji nani ni bora kila mmojawapo atapofikia mwisho wa career yake. Sorry kama sio shabiki wa soka ntakuwa nimekuacha
 
Kipindi kipi boy?? Bifu la jide na clouds ni la muda mrefu.au.unazungumzia baada ya jide juzi juzi hapa kuongea kwenye media?
 
Lady Jaydee ni Legendary.... Vannessa anafanya vyema lakini mileage za Lady Jaydee na mafanikio yake kwa miaka 15 mfululizo ktk muziki si sawa kumfananisha na huyo dogo. Labda tuwe specific nini tunashindanisha.
 

U don't nid to be srry bro..we r on the same page..ila binafsi sidhani kama courtois yuko vizuri kivileee kuliko cech..nadhani chelsea wana future nae ukizingatia kuwa bado ni mdogo,ndo mana wanampa game nyingi ili azidi kugain experience..so mfano wako nashindwa kuuwianisha na mada husika
 
ndo maana yake

Kama ndo hivyo sidhani kama ni sahihi..ukinambia bifu la clouds limemweka juu kimziki nashindwa kuelewa boss..wote tunajua impact ya clouds kwenye music industry bongo..sasa ukinambia kubaniwa kwa jide na clouds fm(mabingwa wa kupiga promo ambao wanaweza kukuaminisha kuwa nyeusi ni nyeupe na ukaamini) ndo kumemfanya awe juu kimziki ntaitaji maelezo kidogo..nwei labda nikubaliane na ww kwa muda kuwa bifu la juzi kati limembusti,ila Jay dee amekuwa akifanya vizuri toka kitambo sana..huko nyuma nini kilikuwa kinambusti??
 
Kwa kipindi kile yes bifu ilimrudisha kwenye chati,kabla ya bifu alikuwa ashaanza kufifia,sahivi kafifia tena maana katoa nyimbo kama 3 zote hazijafanya vizuri

Kwa mtazamo wako unahisi nyimbo kama yahaya na joto hasira ziliitaji bifu ili ziwe hit??
 
Kwa mtazamo wako unahisi nyimbo kama yahaya na joto hasira ziliitaji bifu ili ziwe hit??

Hizo nyimbo ni matokeo ya bifu hivyo huwezi kuzitenganisha na bifu. Me #kende nimemuelewa. Ni kuwa kabla ya hizo nyimbo 2 jide ashaanza kusahaulika kwenye game mpaka alipoingia kwenye bifu akapata cha kuimba... zaid alikua akipiga live band kama akina Banana na TID pale Nyumbani Loungh. Baada ya Nyimbo hizo Mbili za Mipasho kuwananga SebaMaganga,Ruge na Kusaga keshatoa nyingine kama 3 lakini hazijahit. Hata hizo live band zimefulia kwakua hana jipya kila ukienda pale MOG pamenyauka mda wote monday hadi sunday. Hata wasanii wenzie wanamkimbia.

Ni juzi tu watu walijitahidi kuhudhulia kwan wengi walikua Team Kiba.

Vanessa Toka alipochomoka na kwenye featuring ya ommy mpaka wa leo anazidi kupanda kwanini tusiseme kwa sasa kamfunika jayd?

Jide hivi sasa kabaki u-legendary ila kimziki v kamfunika. Tatizo bongo tuna kasumba ya kukariri historia na kuifanya ionekane iko hai muda wote.
 

Mkuu nimetaka kujua uzuri wa wimbo..haijalishi ni mipasho au vipi..unachotaka kusema bifu ndo limefanya nyimbo ionekane nzuri au??..hiyo yahaya hadi watt wadogo walikuwa wanaimba..nao hao walikuwa wanajua wimbo katungiwa mtu fulani?
 
Achen kumshusha jamani jide..jide atabak kua jide hakuna wa kumafananisha nae..wanakuja wasanii wa kike wengi wanavuma mfn kina linah.rachel,maua nk lkn bado jide anabak kua jide wengine wanapotea tu
 
Lady Jaydee ni Legendary.... Vannessa anafanya vyema lakini mileage za Lady Jaydee na mafanikio yake kwa miaka 15 mfululizo ktk muziki si sawa kumfananisha na huyo dogo. Labda tuwe specific nini tunashindanisha.

Vannesa hampati jide kwa chochote, watakua wanamuonea tu, kibongo bongo kwa mademu bado sana kumfikia jide
 

Jide atabaki kuwa jide tu, nitajie hao wasanii wenye angalau vibanda vya kuuzia chips kumzidi jide, jide alishashindikana, ni bora useme vee anapita kwenye nyayo za jide ila sio kumpita, izo ni ndoto, vee hamgusi jide kwa lolote
 

Aya sasa, huyu mtu ni wa kumfananisha na vibwengo kama akina vee? Matusi hayo tena wamuombe msamaha jide, ni dharau sana
 

AHahahahahahaj hahahaha dah nimekupenda buree, eti Vanessa atafute kijiti chake, dah we mbaya sana, umetisha, watuachie comando wetu, hawamuwezi miaka miaa
 
Mkuu vanesa amechukua tuzo wimbo bora wa chipukizi rnb 'closer' kili music mwaka jana, though bado hawez kukaa meza moja na jide, ila ni msanii mzuri pia

Yes, vannesa anafanya vzur, ila huwez mfananisha na jide ata robo, jide muziki wake unasikilizwa from tandale to masaki to east africa,v money bado hajateka soko la uswazi kihivyo ambapo ndipo kuna mashabiki wengi, so she has a long way to go
 
Acha jide aitwe queen of music eact africa..kuna song kashirikishwa na msanii wa kenya atemidva bonge la song jide kafunika mbaya..na kitu kipya kingine chatarajiwa kuja kamshirikisha mazet yule wa ktk song la njalo na uhuru
 

Jide ni chuma cha reli, vannesa ajipange tu kutoka kivyake ila level za jide atazisikia kwenye bomba, wamekuja wasanii wenye sauti kama kasuku ila wamedunda kwa jide, inshort wamuache kabisaaaa
 
Acha jide aitwe queen of music eact africa..kuna song kashirikishwa na msanii wa kenya atemidva bonge la song jide kafunika mbaya..na kitu kipya kingine chatarajiwa kuja kamshirikisha mazet yule wa ktk song la njalo na uhuru

Toka nianze kumjua jide kwa kweli, hajawahi kutoa nyimbo mbaya, anajua kuimba na anajua nini watu wanataka, inshort jide kabarikiwa kwa namna yake, sauti yake sio nzuri sanaaaaa but anajua kuitumia vyema kukonga nyoyo za mashabiki, yule mwanamke ni hatar, muache tu ajite anaconda
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…