Issuna
JF-Expert Member
- Sep 3, 2014
- 3,203
- 7,628
Toba
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Toba
Yaani unashangaa halafu jibu hupatiNchi yenu ilivyo ya kisenge hivyo, export ishu muhimu ila ina bureacracy za kufa mtu yani.
Halafu unamsikia kolo mmoja anapiga mboyoyo zake nyuma ya MiC. "Vijana mnatakiwa mjiajiri!" Kumaanina zao! Yani kuna mambo yanatia hasira mno!Yaani unashangaa halafu jibu hupati
Kweli inauma sana nchi yenye kila neema lakini unashindwa kutoa kitu
Kuna nchi zimeamua kupanda mazao ambayo walikuwa hawana, yote hii ni kwa ajili ya baadhi ya wajinga
Sent from my SM-G570F using Tapatalk
Ndugu yangu haya machungu naumia kila siku kama ni opportunities nimeziacha hapo nyumbaniHalafu unamsikia kolo mmoja anapiga mboyoyo zake nyuma ya MiC. "Vijana mnatakiwa mjiajiri!" Kumaanina zao! Yani kuna mambo yanatia hasira mno!
Wakati goverment agency kadhaa zingeweza kuchukua wajibu wa ku supply hilo zao liliko soko la dunia hata kama wasingetupa hio dollar 550 kufidia gharama zao wangetupa hata $350 tu tungekuwa na very huge production maana ardhi sehemu kubwa iko wazi nchini!
Wanachofanya ni kufila vyanza vya mapato tu kwa kuimpose kodi bila kuweka mazingira mazuri ya kibiashara. Fuckk this shithole country!
Tuna viongozi wa kijinga sana yani. Kwanza hata si ujinga ni ubinafsi tu maana utakuta kuna wachache wananufaika na hizo oppotunities ila kuzipeleka kwa public ndio hawataki!Ndugu yangu haya machungu naumia kila siku kama ni opportunities nimeziacha hapo nyumbani
Kuna jamaa zangu wawili wanakata kata matunda na kupeleka kwenye mahoteli na airports wao wananunua soko kuu na wananiambia wanipe deal la matunda wao watautoa mzigo airport.
Nilikaa nawaangalia tu hata jibu la maana sikuwapa
Kuna watu wana roho mbaya hata shetani anawaogopa wakati yeye ndio anawatuma
Sent from my SM-G570F using Tapatalk
Hili halina ubishi kuna wakubwa wanavusha mipakani kila kukicha kwani haiwezekani fursa hizi wakanyimwa wengine bila maslahi makubwa kwa baadhi yaoTuna viongozi wa kijinga sana yani. Kwanza hata si ujinga ni ubinafsi tu maana utakuta kuna wachache wananufaika na hizo oppotunities ila kuzipeleka kwa public ndio hawataki!
Kampuni ziko kibao kuna kampuni moja Australia wananunua bila shida kuanzia kilo 50 na kuendelea maana zimekuwa adimu Duniani hivyo demand yake imeraise maradufu.
Sasa hivi muhimu ni kuwa na Vanilla, soko litakufuata ulipo Mkuu.
Sent using Jamii Forums mobile app
View attachment 1050596
UTANGULIZI
Zao la vanilla ni moja ya zao la viungo ambalo asili yake ni Kusini Mashariki ya Mexico na sehemu nyingine za Amerika ya Kati. Vanilla hulimwa katika nchi mbalimbali duniani. Nchi zinazolima kwa wingi ni pamoja na Madagascar, Comoro, Tahiti, Uganda, India na nchi nyingine za Amerika ya Kati.
Tanzania ni miongoni mwa nchi zinazolima vanilla katika Afrika. Zao hili lilianza kuingia nchini kutoka Uganda mnamo mwaka 1954 kupitia kwa mkulima mmoja wa kijiji cha Kiilima wilaya ya Bukoba Vijijini. Vanilla imeanza kulimwa kibiashara hasa katika mkoa wa Kagera mwaka wa 1992.
Katika mkoa wa Kagera, kilimo cha Vanilla kimehamasishwa zaidi na Chama cha Maendeleo Ya Wakulima kinachofahamika kama MAYAWA. Chama hiki kimekuwa kikihimiza uzalishaji na usindikaji wa Vanilla ambayo huuzwa kupitia kampuni zilizopo Uganda.
Mmea wa Vanilla huzaa maharage (mapodo) ambayo hukaushwa kwa njia maalum inayowezesha kupatikana kwa Kemikali inayoitwa Vanillini. Kemikali hiyo hutumika katika kuongeza laadha na harufu nzuri kwenye vyakula na vinywaji mbalimbali. Pia hutumika katika viwanda vinvyotengeneza Vipodozi na Dawa za matibabu ya binadamu.
Kwa matumizi ya kawaida, Vanilla huweza kutumika katika vinywaji kama Chai, Maziwa na kama kiungo kwenye mapishi ya Vyakula mbalimbali.
Maeneo mengine ya Tanzania yanayoweza kulima zao la vanilla ni pamoja na wilaya za Mbeya Vijijini, Tukuyu, Morogoro Vijijini, Mvomero, Muheza, Arumeru na Ukerewe.
UMBILE LA MMEA NA MAZINGIRA YANAYOFAA
Mmea wa Vanilla upo katika familia ya Okidi (Orchidaceae) ambayo ina genera zipatazo 700. Kati ya hizo, genera moja itwaayo vanilla ndio yenye umuhimu wa kiuchumi. Genera ya Vanilla ina aina au jamii zipatazo 110, kati ya hizo ni mbili ambazo huzalishwa kibiashara. Aina hizo ni Bourbon ya nchini Mexico na Tahitian ya visiwa vya Tahiti.
Soma: Aina mbali mbali za mbegu za mazao
Umbile la Mmea wa Vanilla
Mmea wa Vanilla ni rando teke linalotambaa ambalo ni la kudumu. Mmea huu hukua na kutambaa katika mti mwingine hadi kufikia urefu wa mita 10 hadi 15 na zaidi kutegemea na mazingira.
Mizizi
Mizizi ya mmea huu ni mirefu ina rangi nyeupe, myembamba yenye kipenyo cha milimita mbili. Mizizi hutokea kwenye fundo la shina lililo ndani ya udongo na hutambaa sambamba na tabaka la udongo wenye rutuba. Pia hutokea katika vifundo vya shina sambamba na majani ambayo hujishikiza katika miti ya kuegemea.
Shina
Shina la vanilla lina rangi ya kijani, refu lenye vifundo na kipenyo cha sentimeta moja hadi mbili. Nafasi kati ya fundo na fundo ni sentimita tano (5) hadi 15.
Majani
Majani yana rangi ya kijani iliyokolea, yenye umbile la bapa, lenye ncha, nene na kubwa. Huota kwa kupishana katika shina, yana urefu wa sentimita nane hadi 25 na upana wa sentimita mbili hadi nane, na yana rangi ya kijani iliyokolea.
Maua
Maua yana rangi mchanganyiko wa kijani na njano na kipenyo cha sentimita 10. Huota katika vifungu vyenye maua kati ya 18 hadi 30.
Matunda
Matunda yana umbile la podo la harage lenye rangi ya kijani likiwa changa. Hubadilika kuwa rangi ya njano, hatimaye kahawia kadri linavyokomaa. Podo lina urefu wa sentmeta 10 hadi 25, kipenyo cha sentimeta nane hadi 15 na lina mbegu ndogo sana ambazo huonekana linapokomaa.
Mazingira Yanayofaa katika Uzalishaji wa Zao la Vanilla
Mmea wa vanilla una asili ya msituni hivyo huhitaji kuoteshwa katika sehemu yenye kivuli na mvua ya kutosha. Ili zao hili liweze kukua vizuri linahitaji mazingira yafuatayo:
Mvua
Mmea wa Vanilla huhitaji kiasi cha mvua cha milimita 1250 hadi 2500 kwa mwaka. Pia zao hili huhitaji kipindi cha miezi mawili cha ukame ili kuweza kusisisimka na kutoa vitumba vya maua.
Joto
Zao hili hustawi vizuri katika maeneo yenye nyuzi joto 20 hadi 30 za Sentigredi. Pia huweza kustahimili nyuzi joto 32 za Sentigredi. Lakini hukua vizuri zaidi katika kiwango cha nyuzi joto 27 za Sentigredi.
Mwinuko
Zao hili hustawi vizuri katika maeneo yenye mwinuko wa mita 0 hadi 600 kutoka usawa wa bahari. Pia hustawi katika maeneo yenye mwinuko unaofikia mita 1500 katika nchi za joto (tropiki).
Udongo
Mmea wa vanilla una mizizi ambayo hutambaa katika sehemu ya juu ya udongo. Hivyo, huhitaji udongo mwepesi wa tifutifu, wenye rutuba ya kutosha na usiotuamisha maji.
Mwanga
Mmea wa vanilla huathirika kwa jua na husababisha kuungua kwa majani, hivyo huhitaji kivuli cha asilimia 50 hadi 75 ili uweze kukua vizuri. Kivuli kinaweza kupatikana kwa kupanda miti au kwa kutengenezwa kitaalamu.
UZALISHAJI WA ZAO LA VANILA
Vanilla huzalishwa kwa kupandikiza marando moja kwa moja shambani au kwa kukuzwa kwanza kwenye kitalu na baadaye kupandikizwa shambani. Kabla ya kupanda inatakiwa kuzingatia yafuatayo:
Uchaguzi wa Shamba
Shamba la kupanda vanilla inafaa liwe mahali pasipo na upepo mkali ili kuepuka kuanguka kwa miti ya kuegemea na kukatika kwa mimea. Ni muhimu kupanda miti ya kuzuia upepo ikiwa mahali hapo pana upepo mkali. Shamba hilo pia liwe na udongo usiotuamisha maji, mwepesi na ambao unaruhusu mizizi kupenya kwa urahisi.
Aidha, shamba lisiwe na magugu mabaya (kwa mfano kwekwe/sangare) ambayo hulazimu kutumia jembe mara kwa mara wakati wa palizi. Kutumia jembe huweza kusababisha kukatika au kuharibu mizizi na kuhatarisha ukuaji wa mmea.
Utayarishaji wa Shamba
Utayarishaji wa shamba huhusisha shughuli mbalimbali kama vile usafishaji wa shamba, utayarishaji wa mashimo na uwekaji wa mbolea.
Kusafisha Shamba
Shamba lisafishwe kwa kulima, kungíoa visiki, magugu mabaya na kutifua hadi kina kisichopungua sentimita 30.
Kutayarisha Mashimo
Mashimo yatayarishwe miezi miwili hadi mitatu sambamba na usafishaji wa shamba. Yawe na kina cha sentimita 30 na upana wa sentimita 60 hadi 90. Nafasi kati ya mstari na mstari iwe mita mbili na nusu hadi mita tatu na kati ya shimo na shimo iwe mita moja na nusu hadi mbili. Udongo wa juu utengwe na ule wa chini.
Uwekaji wa Mbolea
Mbolea za asili kama mboji, vunde au samadi ichanganywe vema na udongo wa juu na kujazwa kwenye shimo kwa kipimo cha debe moja hadi mbili kwa kila shimo.
Soma: mahitaji ya mbolea kwenye kilimo cha mahindi
Mifumo ya Upandaji
Zao la vanilla huweza kupandwa shambani kwa kutumia mifumo mikuu mitatu ifuatayo:
(i) Vanilla Pekee
Mfumo huu unahusisha upandaji wa mmea wa vanilla na miti ya kuegemea tu ambayo hutoa kivuli kwa mimea.
(ii) Vanilla na Migomba
Mfumo huu unawezesha kuotesha vanilla katika shamba la migomba, ambapo rando hupandwa pamoja na mti wa kuegemea ndani ya shamba la migomba. Na hivyo kukuwezesha kufanya kilimo cha migomba na vanilla katika shamba moja kwa wakati mmoja
(iii)Vanilla na Miti ya Kivuli
Katika mfumo huu vanilla huoteshwa katika shamba la miti ya kivuli, ambapo mmea hupandwa na miti ya kuegemea katikati ya miti ya kivuli.
Kumbuka: Mfumo wa pili na wa tatu unapendekezwa zaidi kutokana na matokeo yake mazuri.
Upandaji wa Miti ya Kuegemea (miega)
Miti ya kuegemea hupandwa miezi miwili hadi mitatu kabla ya kupanda rando la vanilla ili iweze kuchipua, kutoa kivuli na kuwa na uwezo wa kuhimili mimea.
(i) Sifa za Miega
Miti inayofaa kutumika kwa kuegemea iwe na sifa zifuatazo:
Miti yenye sifa hizo ni pamoja na mibono (Jatropha carcus) na Gilirisidia. Miti mingine inayoweza kutumika kwa kivuli na kuegemea ni pamoja na Erythrina spp na Bauhania spp.
- Uwezo wa kukua haraka bila kuathiri mmea wa vanilla.
- Uwezo wa kutoa kivuli kinachofaa.
- Uwezo wa kuchipua haraka inapopunguzwa.
- Uwezo wa kuchipua matawi kwa chini ili kupandishia marando kwa urahisi.
- Uwezekano wa kuoteshwa kwa urahisi.
(ii) Kupanda Miega ya Mibono
Miti inayotumika zaidi katika mashamba ya vanilla ni jamii ya Jatropha. Miti hii huoteshwa kwa kutumia mbegu au kipande cha tawi kwa umbali wa sentimita 30 kutoka katika shimo la kupandia vanilla. Tawi la mbono lenye urefu wa sentimita 120 hadi 150 hupandwa katika kina cha sentimita10 hadi 15.
Upandaji wa Vanilla
Mmea wa vanilla hupandwa mwanzoni mwa msimu wa mvua ili kuhakikisha upatikanaji wa unyevu ardhini. Hupandwa kwa kutumia rando lenye urefu wa kati ya sentimita 100 hadi 150 (futi tatu na nusu hadi tano) kutoka kwenye mmea unaokuwa vizuri, usio na magonjwa na wenye pingili ndefu. Rando lenye sifa hizo hukua haraka na kutoa maua mapema (miaka 2). Rando fupi halikui haraka na huchukua muda mrefu kutoa maua (miaka 2 hadi 3).
Kutayarisha Marando
Jinsi ya Kupanda
- Kata rando kwa kutumia kisu kikali kwa kufuata vipimo (sentimita 100 hadi 150).
- Ondoa majani matatu hadi matano katika sehemu ya chini ya rando itayofukiwa kwenye udongo.
- Ning’iniza rando lililokatwa kwenye kivuli kwa muda wa siku saba hadi 10 kabla ya kupanda ili kupunguza utomvu na kulipa nguvu ya kuchipua na kuhimili hali ya shambani.
Upandaji wa vanilla hufanywa kwa kutumia hatua zifuatazo:
Kumbuka:
- Andaa nyasi kavu (matandazo) ambazo zitatumika mara baada ya kupanda.
- Tengeneza kifereji chenye kina cha sentimita 10 hadi 12 katikati ya shimo lenye mbolea lililokwisha tengenezwa.
- Laza sehemu ya rando iliyotolewa majani katika kifereji hicho, acha sehemu yenye majani juu ya ardhi.
- Fukia rando kwenye kifereji kwa udongo na gandamiza taratibu ili lishikamane na udongo.
- Funga sehemu ya juu ya rando kwa kutumia kamba katika umbile la nane kwenye mti wa kuegemea.
- Weka matandazo kuzunguka kila shina lililopandwa.
Utunzaji wa Shamba
- Utaratibu huu wa kupanda hutumika katika aina zote za mifumo ya kuzalisha vanilla, na hutofautiana kwa nafasi za upandaji kati ya mfumo mmoja na mwingine.
- Shamba la vanilla pekee katika miaka ya mwanzoni, huweza kuchanganywa katikati ya mistari na mazao mengine ya muda mfupi kama mazao ya jamii ya mikunde.
Vanilla huhitaji kutunzwa vizuri ili iweze kukua vizuri na kutoa mavuno yenye ubora wa hali ya juu. Huduma muhimu katika uzalishaji wa vanilla ni kama ifuatavyo:
Kutengeneza Kivuli
Mmea wa vanilla huhitaji kivuli ili uweze kukua vizuri. Hivyo ni muhimu kupanda miti ya kivuli kabla ya kustawisha vanilla. Katika ukuaji wake kuanzia inapopandwa hadi inapokaribia kutoa maua huhitaji kivuli cha kutosha kinachoweza kuzuia jua kali na kuruhusu mwanga (asilimia 60 hadi 70).
Kipindi cha kusisimua kivuli kipunguzwe zaidi na kufikia asilimia 55 hadi 50. Kivuli kitengenezwe kwa kupunguza matawi ya miti ya miega na ya kivuli ili kupata kivuli kinachofaa.
Kumbuka: Kivuli kizito huathiri ukuaji wa mmea.
Kuweka Matandazo
Utandazaji wa nyasi ni muhimu katika shamba la vanila kutokana na tabia ya ukuaji wa mizizi ambayo huota katika kina cha sentimita 5 hadi 10, hivyo huhitaji kulindwa isiharibiwe. Matandazo yawekwe kuzunguka mashina ya mimea ili kuhifadhi unyevu, kuzuia uotaji wa magugu, na kulinda mizizi isiharibiwe wakati wa palizi.
Kumbuka: Matandazo yawe makavu na yasiwe na mbegu za magugu.
Palizi
Palizi hufanyika wakati wowote magugu yanapoota shambani. Inashauriwa kufanya palizi kabla ya mvua kunyesha ili mmea uweze kutumia maji ya mvua ipasavyo. Palizi ifanyike wakati wowote magugu yanapoota shambani, kwa kungíoa magugu kutumia mikono ili kuepuka kujeruhi mizizi jembe linapotumika.
Kuning’iniza Marando
Mmea wa vanilla uliokua vizuri huota matawi (marando) mengi na marefu. Marando hayo huelekezwa kwenye matawi ya miti ya kuegemea na kuningíinizwa. Rando linapofikia urefu wa sentimita 150 hadi 180 liningíinizwe katika matawi ya miega ili liendelee kukua kuelekea chini. Endapo kuna upepo mkali, marando yafungwe kwenye miega kwa muda ili yasivunjike.
Kulisha Marando
Kulisha marando ni kitendo cha kufukia ardhini sehemu ya kipande cha rando ili kiweze kutoa mizizi na kuongeza nguvu ya kuchukua chakula kutoka kwenye udongo. Kazi hii hufanywa baada ya rando lililoningíinizwa kurefuka sana kiasi cha kutambaa ardhini, katika hatua hii mmea huweza kuwa na umri wa miezi sita hadi tisa kutegemea na utunzaji.
Jinsi ya Kulisha
- Ondoa majani matatu hadi manne kwenye rando lililoingíinizwa na kurefuka sana.
- Fukia kwenye udongo, karibu na shina sehemu iliyoondolewa majani.
- Weka matandazo katika sehemu iliyofukiwa ili kuhifadhi unyevu.
- Funga sehemu ya juu ya rando katika mti wa kuegemea ili liendelee kukua.
- Marando mawili hadi mitatu yalishwe kwa wakati mmoja na mengine yaachwe kwa ajili ya kutoa maua na kupata marando ya kupanda.
Kumbuka: Kulisha kufanyike wakati wa mvua ili marando yaweze kutoa mizizi kwa urahisi. Kazi hii irudiwe kila wakati ili rando mama litakapokatika machipukizi yake yaendelea kukua.
Soma kilimo cha tangawizi
Kusisimua
Kusisimua ni kitendo cha kuufanya mmea kuwa katika hali ya kuweza kutoa maua. Kitendo hiki kifanywe wakati mmea ukiwa umefikia umri wa mwaka 1 na nusu au zaidi, na hufanywa wakati wa kiangazi ili kuepuka kupata matawi mengi badala ya vitumba vya maua. Mmea usiosisimuliwa hautoi maua au hutoa maua machache na kusisimua mapema kunaweza kuuchosha mmea.
Jinsi ya Kusisimua
Ukataji wa ncha huweza kufanyika kama ifuatavyo:
- Chagua matawi matatu hadi matano yanayoningíinia. Kusisimua matawi mengi kunaweza kuudhoofisha mmea au kuzaa maharage madogo.
- Kata ncha ya rando ili kuwezesha vitumba vya maua kukua na kuwa tayari kufunguka au kutoa maua.
- Kukata ncha ndogo (mdomo wa rando) kwa mkono. Hii hufanyika kwa rando fupi linaloningínia.
- Kukata rando kwa kisu kikali, kwa rando linaloningínia ambalo halijafikia urefu wa kupanda.
- Kukata rando kwa kisu kikali kwa rando refu linaloningíinia (lenye urefu wa kuweza kupandwa, sentimita100-150).
Uchavushaji
Ni kitendo cha kuunganisha chavua kutoka katika sehemu dume ya ua na kuweka katika sehemu jike ya ua, hufanyika baada ya maua kuchanua.
Uchanuaji wa Maua
Mmea wa Vanilla hutoa maua miezi miwili hadi mitatu baada ya kusisimuliwa. Maua huchanua kwa kipindi cha masaa matatu hadi manne kuanzia saa tatu asubuhi hadi saa saba mchana kwa muda wa miezi miwili hadi mitatu kutegemea unyevu uliopo kwenye udongo na kiwango cha Jua.
Ua huchanua kwa muda huo na hudondoka baada ya siku 1 ikiwa halikupata chavua. Hivyo ni muhimu uchavushaji ufanyike kwa haraka na kwa uangalifu mkubwa.
Jinsi ya Kuchavusha
Mmea wa vanilla, ili uweze kutoa matunda inabidi uchavushwe. Ua la vanilla kwa kawaida huchavushwa na nyuki jamii ya melapona ambao hawapo hapa nchini. Nyuki hao hupatikana Mexico na katika nchi nyingine za Amerika ya Kati. Hivyo uchavushaji hufanywa kwa mikono kwani umbile la ua haliruhusu nyuki wa aina nyingine kufanya uchavushaji.
Soma kilimo cha binzari
Uchavushaji hufanywa kwa kufuata hatua zifuatazo:
- Gawa petali ya ua la vanilla katika sehemu mbili kwa kutumia pini, sindano, au mwiba. Hakikisha vifaa hivyo ni safi.
- Kunjua sehemu jike ya ua (stigima) kwa kuelekea juu ili kuwezesha kulala sambamba kwenye sehemu dume ya ua (stameni).
- Unganisha stameni na stigima na kubana taratibu kwa dole gumba kwa nusu dakika ili kuruhusu chavua kuingia kwenye stigima.
Ua lililochavushwa vizuri, hubaki likiningíinia kwenye kikonyo chake. Ikiwa uchavushaji haukufanikiwa, ua hudondoka baada ya siku moja au mbili. Kiasi cha maua au mapodo nane hadi 12 yaachwe katika kila kitumba. Aidha vitumba vinne hadi nane viruhusiwe kukua katika kila rando na visizidi 20 kwa mmea.
Ndugu yangu mkulima hivi ndivyo vanilla inavyolimwa, ni shughuri nzito sana lakini inalipa sana, kama ilivyo kawaida: mvumilivu hula mbivu.
JAMANI KAMA HUNA MOYO USILIME HILI ZAO WENYE MAGONJWA YENU YA PRESHA BAKINI KWENYE MARAGE NA MAHINDI TU.
View attachment 1050596
UTANGULIZI
Zao la vanilla ni moja ya zao la viungo ambalo asili yake ni Kusini Mashariki ya Mexico na sehemu nyingine za Amerika ya Kati. Vanilla hulimwa katika nchi mbalimbali duniani. Nchi zinazolima kwa wingi ni pamoja na Madagascar, Comoro, Tahiti, Uganda, India na nchi nyingine za Amerika ya Kati.
Tanzania ni miongoni mwa nchi zinazolima vanilla katika Afrika. Zao hili lilianza kuingia nchini kutoka Uganda mnamo mwaka 1954 kupitia kwa mkulima mmoja wa kijiji cha Kiilima wilaya ya Bukoba Vijijini. Vanilla imeanza kulimwa kibiashara hasa katika mkoa wa Kagera mwaka wa 1992.
Katika mkoa wa Kagera, kilimo cha Vanilla kimehamasishwa zaidi na Chama cha Maendeleo Ya Wakulima kinachofahamika kama MAYAWA. Chama hiki kimekuwa kikihimiza uzalishaji na usindikaji wa Vanilla ambayo huuzwa kupitia kampuni zilizopo Uganda.
Mmea wa Vanilla huzaa maharage (mapodo) ambayo hukaushwa kwa njia maalum inayowezesha kupatikana kwa Kemikali inayoitwa Vanillini. Kemikali hiyo hutumika katika kuongeza laadha na harufu nzuri kwenye vyakula na vinywaji mbalimbali. Pia hutumika katika viwanda vinvyotengeneza Vipodozi na Dawa za matibabu ya binadamu.
Kwa matumizi ya kawaida, Vanilla huweza kutumika katika vinywaji kama Chai, Maziwa na kama kiungo kwenye mapishi ya Vyakula mbalimbali.
Maeneo mengine ya Tanzania yanayoweza kulima zao la vanilla ni pamoja na wilaya za Mbeya Vijijini, Tukuyu, Morogoro Vijijini, Mvomero, Muheza, Arumeru na Ukerewe.
UMBILE LA MMEA NA MAZINGIRA YANAYOFAA
Mmea wa Vanilla upo katika familia ya Okidi (Orchidaceae) ambayo ina genera zipatazo 700. Kati ya hizo, genera moja itwaayo vanilla ndio yenye umuhimu wa kiuchumi. Genera ya Vanilla ina aina au jamii zipatazo 110, kati ya hizo ni mbili ambazo huzalishwa kibiashara. Aina hizo ni Bourbon ya nchini Mexico na Tahitian ya visiwa vya Tahiti.
Soma: Aina mbali mbali za mbegu za mazao
Umbile la Mmea wa Vanilla
Mmea wa Vanilla ni rando teke linalotambaa ambalo ni la kudumu. Mmea huu hukua na kutambaa katika mti mwingine hadi kufikia urefu wa mita 10 hadi 15 na zaidi kutegemea na mazingira.
Mizizi
Mizizi ya mmea huu ni mirefu ina rangi nyeupe, myembamba yenye kipenyo cha milimita mbili. Mizizi hutokea kwenye fundo la shina lililo ndani ya udongo na hutambaa sambamba na tabaka la udongo wenye rutuba. Pia hutokea katika vifundo vya shina sambamba na majani ambayo hujishikiza katika miti ya kuegemea.
Shina
Shina la vanilla lina rangi ya kijani, refu lenye vifundo na kipenyo cha sentimeta moja hadi mbili. Nafasi kati ya fundo na fundo ni sentimita tano (5) hadi 15.
Majani
Majani yana rangi ya kijani iliyokolea, yenye umbile la bapa, lenye ncha, nene na kubwa. Huota kwa kupishana katika shina, yana urefu wa sentimita nane hadi 25 na upana wa sentimita mbili hadi nane, na yana rangi ya kijani iliyokolea.
Maua
Maua yana rangi mchanganyiko wa kijani na njano na kipenyo cha sentimita 10. Huota katika vifungu vyenye maua kati ya 18 hadi 30.
Matunda
Matunda yana umbile la podo la harage lenye rangi ya kijani likiwa changa. Hubadilika kuwa rangi ya njano, hatimaye kahawia kadri linavyokomaa. Podo lina urefu wa sentmeta 10 hadi 25, kipenyo cha sentimeta nane hadi 15 na lina mbegu ndogo sana ambazo huonekana linapokomaa.
Mazingira Yanayofaa katika Uzalishaji wa Zao la Vanilla
Mmea wa vanilla una asili ya msituni hivyo huhitaji kuoteshwa katika sehemu yenye kivuli na mvua ya kutosha. Ili zao hili liweze kukua vizuri linahitaji mazingira yafuatayo:
Mvua
Mmea wa Vanilla huhitaji kiasi cha mvua cha milimita 1250 hadi 2500 kwa mwaka. Pia zao hili huhitaji kipindi cha miezi mawili cha ukame ili kuweza kusisisimka na kutoa vitumba vya maua.
Joto
Zao hili hustawi vizuri katika maeneo yenye nyuzi joto 20 hadi 30 za Sentigredi. Pia huweza kustahimili nyuzi joto 32 za Sentigredi. Lakini hukua vizuri zaidi katika kiwango cha nyuzi joto 27 za Sentigredi.
Mwinuko
Zao hili hustawi vizuri katika maeneo yenye mwinuko wa mita 0 hadi 600 kutoka usawa wa bahari. Pia hustawi katika maeneo yenye mwinuko unaofikia mita 1500 katika nchi za joto (tropiki).
Udongo
Mmea wa vanilla una mizizi ambayo hutambaa katika sehemu ya juu ya udongo. Hivyo, huhitaji udongo mwepesi wa tifutifu, wenye rutuba ya kutosha na usiotuamisha maji.
Mwanga
Mmea wa vanilla huathirika kwa jua na husababisha kuungua kwa majani, hivyo huhitaji kivuli cha asilimia 50 hadi 75 ili uweze kukua vizuri. Kivuli kinaweza kupatikana kwa kupanda miti au kwa kutengenezwa kitaalamu.
UZALISHAJI WA ZAO LA VANILA
Vanilla huzalishwa kwa kupandikiza marando moja kwa moja shambani au kwa kukuzwa kwanza kwenye kitalu na baadaye kupandikizwa shambani. Kabla ya kupanda inatakiwa kuzingatia yafuatayo:
Uchaguzi wa Shamba
Shamba la kupanda vanilla inafaa liwe mahali pasipo na upepo mkali ili kuepuka kuanguka kwa miti ya kuegemea na kukatika kwa mimea. Ni muhimu kupanda miti ya kuzuia upepo ikiwa mahali hapo pana upepo mkali. Shamba hilo pia liwe na udongo usiotuamisha maji, mwepesi na ambao unaruhusu mizizi kupenya kwa urahisi.
Aidha, shamba lisiwe na magugu mabaya (kwa mfano kwekwe/sangare) ambayo hulazimu kutumia jembe mara kwa mara wakati wa palizi. Kutumia jembe huweza kusababisha kukatika au kuharibu mizizi na kuhatarisha ukuaji wa mmea.
Utayarishaji wa Shamba
Utayarishaji wa shamba huhusisha shughuli mbalimbali kama vile usafishaji wa shamba, utayarishaji wa mashimo na uwekaji wa mbolea.
Kusafisha Shamba
Shamba lisafishwe kwa kulima, kungíoa visiki, magugu mabaya na kutifua hadi kina kisichopungua sentimita 30.
Kutayarisha Mashimo
Mashimo yatayarishwe miezi miwili hadi mitatu sambamba na usafishaji wa shamba. Yawe na kina cha sentimita 30 na upana wa sentimita 60 hadi 90. Nafasi kati ya mstari na mstari iwe mita mbili na nusu hadi mita tatu na kati ya shimo na shimo iwe mita moja na nusu hadi mbili. Udongo wa juu utengwe na ule wa chini.
Uwekaji wa Mbolea
Mbolea za asili kama mboji, vunde au samadi ichanganywe vema na udongo wa juu na kujazwa kwenye shimo kwa kipimo cha debe moja hadi mbili kwa kila shimo.
Soma: mahitaji ya mbolea kwenye kilimo cha mahindi
Mifumo ya Upandaji
Zao la vanilla huweza kupandwa shambani kwa kutumia mifumo mikuu mitatu ifuatayo:
(i) Vanilla Pekee
Mfumo huu unahusisha upandaji wa mmea wa vanilla na miti ya kuegemea tu ambayo hutoa kivuli kwa mimea.
(ii) Vanilla na Migomba
Mfumo huu unawezesha kuotesha vanilla katika shamba la migomba, ambapo rando hupandwa pamoja na mti wa kuegemea ndani ya shamba la migomba. Na hivyo kukuwezesha kufanya kilimo cha migomba na vanilla katika shamba moja kwa wakati mmoja
(iii)Vanilla na Miti ya Kivuli
Katika mfumo huu vanilla huoteshwa katika shamba la miti ya kivuli, ambapo mmea hupandwa na miti ya kuegemea katikati ya miti ya kivuli.
Kumbuka: Mfumo wa pili na wa tatu unapendekezwa zaidi kutokana na matokeo yake mazuri.
Upandaji wa Miti ya Kuegemea (miega)
Miti ya kuegemea hupandwa miezi miwili hadi mitatu kabla ya kupanda rando la vanilla ili iweze kuchipua, kutoa kivuli na kuwa na uwezo wa kuhimili mimea.
(i) Sifa za Miega
Miti inayofaa kutumika kwa kuegemea iwe na sifa zifuatazo:
Miti yenye sifa hizo ni pamoja na mibono (Jatropha carcus) na Gilirisidia. Miti mingine inayoweza kutumika kwa kivuli na kuegemea ni pamoja na Erythrina spp na Bauhania spp.
- Uwezo wa kukua haraka bila kuathiri mmea wa vanilla.
- Uwezo wa kutoa kivuli kinachofaa.
- Uwezo wa kuchipua haraka inapopunguzwa.
- Uwezo wa kuchipua matawi kwa chini ili kupandishia marando kwa urahisi.
- Uwezekano wa kuoteshwa kwa urahisi.
(ii) Kupanda Miega ya Mibono
Miti inayotumika zaidi katika mashamba ya vanilla ni jamii ya Jatropha. Miti hii huoteshwa kwa kutumia mbegu au kipande cha tawi kwa umbali wa sentimita 30 kutoka katika shimo la kupandia vanilla. Tawi la mbono lenye urefu wa sentimita 120 hadi 150 hupandwa katika kina cha sentimita10 hadi 15.
Upandaji wa Vanilla
Mmea wa vanilla hupandwa mwanzoni mwa msimu wa mvua ili kuhakikisha upatikanaji wa unyevu ardhini. Hupandwa kwa kutumia rando lenye urefu wa kati ya sentimita 100 hadi 150 (futi tatu na nusu hadi tano) kutoka kwenye mmea unaokuwa vizuri, usio na magonjwa na wenye pingili ndefu. Rando lenye sifa hizo hukua haraka na kutoa maua mapema (miaka 2). Rando fupi halikui haraka na huchukua muda mrefu kutoa maua (miaka 2 hadi 3).
Kutayarisha Marando
Jinsi ya Kupanda
- Kata rando kwa kutumia kisu kikali kwa kufuata vipimo (sentimita 100 hadi 150).
- Ondoa majani matatu hadi matano katika sehemu ya chini ya rando itayofukiwa kwenye udongo.
- Ning’iniza rando lililokatwa kwenye kivuli kwa muda wa siku saba hadi 10 kabla ya kupanda ili kupunguza utomvu na kulipa nguvu ya kuchipua na kuhimili hali ya shambani.
Upandaji wa vanilla hufanywa kwa kutumia hatua zifuatazo:
Kumbuka:
- Andaa nyasi kavu (matandazo) ambazo zitatumika mara baada ya kupanda.
- Tengeneza kifereji chenye kina cha sentimita 10 hadi 12 katikati ya shimo lenye mbolea lililokwisha tengenezwa.
- Laza sehemu ya rando iliyotolewa majani katika kifereji hicho, acha sehemu yenye majani juu ya ardhi.
- Fukia rando kwenye kifereji kwa udongo na gandamiza taratibu ili lishikamane na udongo.
- Funga sehemu ya juu ya rando kwa kutumia kamba katika umbile la nane kwenye mti wa kuegemea.
- Weka matandazo kuzunguka kila shina lililopandwa.
Utunzaji wa Shamba
- Utaratibu huu wa kupanda hutumika katika aina zote za mifumo ya kuzalisha vanilla, na hutofautiana kwa nafasi za upandaji kati ya mfumo mmoja na mwingine.
- Shamba la vanilla pekee katika miaka ya mwanzoni, huweza kuchanganywa katikati ya mistari na mazao mengine ya muda mfupi kama mazao ya jamii ya mikunde.
Vanilla huhitaji kutunzwa vizuri ili iweze kukua vizuri na kutoa mavuno yenye ubora wa hali ya juu. Huduma muhimu katika uzalishaji wa vanilla ni kama ifuatavyo:
Kutengeneza Kivuli
Mmea wa vanilla huhitaji kivuli ili uweze kukua vizuri. Hivyo ni muhimu kupanda miti ya kivuli kabla ya kustawisha vanilla. Katika ukuaji wake kuanzia inapopandwa hadi inapokaribia kutoa maua huhitaji kivuli cha kutosha kinachoweza kuzuia jua kali na kuruhusu mwanga (asilimia 60 hadi 70).
Kipindi cha kusisimua kivuli kipunguzwe zaidi na kufikia asilimia 55 hadi 50. Kivuli kitengenezwe kwa kupunguza matawi ya miti ya miega na ya kivuli ili kupata kivuli kinachofaa.
Kumbuka: Kivuli kizito huathiri ukuaji wa mmea.
Kuweka Matandazo
Utandazaji wa nyasi ni muhimu katika shamba la vanila kutokana na tabia ya ukuaji wa mizizi ambayo huota katika kina cha sentimita 5 hadi 10, hivyo huhitaji kulindwa isiharibiwe. Matandazo yawekwe kuzunguka mashina ya mimea ili kuhifadhi unyevu, kuzuia uotaji wa magugu, na kulinda mizizi isiharibiwe wakati wa palizi.
Kumbuka: Matandazo yawe makavu na yasiwe na mbegu za magugu.
Palizi
Palizi hufanyika wakati wowote magugu yanapoota shambani. Inashauriwa kufanya palizi kabla ya mvua kunyesha ili mmea uweze kutumia maji ya mvua ipasavyo. Palizi ifanyike wakati wowote magugu yanapoota shambani, kwa kungíoa magugu kutumia mikono ili kuepuka kujeruhi mizizi jembe linapotumika.
Kuning’iniza Marando
Mmea wa vanilla uliokua vizuri huota matawi (marando) mengi na marefu. Marando hayo huelekezwa kwenye matawi ya miti ya kuegemea na kuningíinizwa. Rando linapofikia urefu wa sentimita 150 hadi 180 liningíinizwe katika matawi ya miega ili liendelee kukua kuelekea chini. Endapo kuna upepo mkali, marando yafungwe kwenye miega kwa muda ili yasivunjike.
Kulisha Marando
Kulisha marando ni kitendo cha kufukia ardhini sehemu ya kipande cha rando ili kiweze kutoa mizizi na kuongeza nguvu ya kuchukua chakula kutoka kwenye udongo. Kazi hii hufanywa baada ya rando lililoningíinizwa kurefuka sana kiasi cha kutambaa ardhini, katika hatua hii mmea huweza kuwa na umri wa miezi sita hadi tisa kutegemea na utunzaji.
Jinsi ya Kulisha
- Ondoa majani matatu hadi manne kwenye rando lililoingíinizwa na kurefuka sana.
- Fukia kwenye udongo, karibu na shina sehemu iliyoondolewa majani.
- Weka matandazo katika sehemu iliyofukiwa ili kuhifadhi unyevu.
- Funga sehemu ya juu ya rando katika mti wa kuegemea ili liendelee kukua.
- Marando mawili hadi mitatu yalishwe kwa wakati mmoja na mengine yaachwe kwa ajili ya kutoa maua na kupata marando ya kupanda.
Kumbuka: Kulisha kufanyike wakati wa mvua ili marando yaweze kutoa mizizi kwa urahisi. Kazi hii irudiwe kila wakati ili rando mama litakapokatika machipukizi yake yaendelea kukua.
Soma kilimo cha tangawizi
Kusisimua
Kusisimua ni kitendo cha kuufanya mmea kuwa katika hali ya kuweza kutoa maua. Kitendo hiki kifanywe wakati mmea ukiwa umefikia umri wa mwaka 1 na nusu au zaidi, na hufanywa wakati wa kiangazi ili kuepuka kupata matawi mengi badala ya vitumba vya maua. Mmea usiosisimuliwa hautoi maua au hutoa maua machache na kusisimua mapema kunaweza kuuchosha mmea.
Jinsi ya Kusisimua
Ukataji wa ncha huweza kufanyika kama ifuatavyo:
- Chagua matawi matatu hadi matano yanayoningíinia. Kusisimua matawi mengi kunaweza kuudhoofisha mmea au kuzaa maharage madogo.
- Kata ncha ya rando ili kuwezesha vitumba vya maua kukua na kuwa tayari kufunguka au kutoa maua.
- Kukata ncha ndogo (mdomo wa rando) kwa mkono. Hii hufanyika kwa rando fupi linaloningínia.
- Kukata rando kwa kisu kikali, kwa rando linaloningínia ambalo halijafikia urefu wa kupanda.
- Kukata rando kwa kisu kikali kwa rando refu linaloningíinia (lenye urefu wa kuweza kupandwa, sentimita100-150).
Uchavushaji
Ni kitendo cha kuunganisha chavua kutoka katika sehemu dume ya ua na kuweka katika sehemu jike ya ua, hufanyika baada ya maua kuchanua.
Uchanuaji wa Maua
Mmea wa Vanilla hutoa maua miezi miwili hadi mitatu baada ya kusisimuliwa. Maua huchanua kwa kipindi cha masaa matatu hadi manne kuanzia saa tatu asubuhi hadi saa saba mchana kwa muda wa miezi miwili hadi mitatu kutegemea unyevu uliopo kwenye udongo na kiwango cha Jua.
Ua huchanua kwa muda huo na hudondoka baada ya siku 1 ikiwa halikupata chavua. Hivyo ni muhimu uchavushaji ufanyike kwa haraka na kwa uangalifu mkubwa.
Jinsi ya Kuchavusha
Mmea wa vanilla, ili uweze kutoa matunda inabidi uchavushwe. Ua la vanilla kwa kawaida huchavushwa na nyuki jamii ya melapona ambao hawapo hapa nchini. Nyuki hao hupatikana Mexico na katika nchi nyingine za Amerika ya Kati. Hivyo uchavushaji hufanywa kwa mikono kwani umbile la ua haliruhusu nyuki wa aina nyingine kufanya uchavushaji.
Soma kilimo cha binzari
Uchavushaji hufanywa kwa kufuata hatua zifuatazo:
- Gawa petali ya ua la vanilla katika sehemu mbili kwa kutumia pini, sindano, au mwiba. Hakikisha vifaa hivyo ni safi.
- Kunjua sehemu jike ya ua (stigima) kwa kuelekea juu ili kuwezesha kulala sambamba kwenye sehemu dume ya ua (stameni).
- Unganisha stameni na stigima na kubana taratibu kwa dole gumba kwa nusu dakika ili kuruhusu chavua kuingia kwenye stigima.
Ua lililochavushwa vizuri, hubaki likiningíinia kwenye kikonyo chake. Ikiwa uchavushaji haukufanikiwa, ua hudondoka baada ya siku moja au mbili. Kiasi cha maua au mapodo nane hadi 12 yaachwe katika kila kitumba. Aidha vitumba vinne hadi nane viruhusiwe kukua katika kila rando na visizidi 20 kwa mmea.
Ndugu yangu mkulima hivi ndivyo vanilla inavyolimwa, ni shughuri nzito sana lakini inalipa sana, kama ilivyo kawaida: mvumilivu hula mbivu.
JAMANI KAMA HUNA MOYO USILIME HILI ZAO WENYE MAGONJWA YENU YA PRESHA BAKINI KWENYE MARAGE NA MAHINDI TU.
asante sana mkuuMaisha hayajawahi kuwa magumu hata siku moja bali ni sisi tu binadamu ndio tunakuwaga na mioyo migumu na tunashindwa kujipekecha sahihi ili kuendana na kasi ya Dunia.
Kasi ya Dunia ni kujua fursa zikoje kwa wakati sahihi na kisha kufanya maamuzi sahihi ili hatimae kila kitu kiende sawa sawia. Na hii yote inawezekana kama tukitafuta taarifa bila kuchoka na kuzifanyia kazi kwa wakati maana in this age of information, ignorance is rather your choice.
Hivyo ni choice ya watu wengi kutoji updates na kupata taarifa kwa wakati ili wapige hela zao kwa uzuri. Imagine wale watu waliopata taarifa mapema za M-pesa na kuzifanyia kazi wakati, walinufaika sana na M-Pesa kiuchumi... Achili mbali hiyo kuna Bitcoin wale watu walioijua tangu ilipokuwa changa mwaka 2011 huko ikiuzwa kwa dola $2 na wakachangamkia fursa leo hii ni mamilionea sababu Bitcoin ilishafikia dola $19000. Anyways, labda hii ya Bitcoin inaweza kuwa ngumu je unaikumbuka ile ya kuhama kutoka kwenye kanda za cassette kwenda kwenye CD... Wale waliochungulia fursa mapema walipiga hela nzuri tu kwa kuuza CD kwa bei wanayotaka. Hata lile ombwe la kuhamia kwenye simu za mkononi... Anko wangu alikuwa miongoni mwa watu wa mwanzoni kabisa kuchungulia hii fursa mapema then akapiga pesa ndefu sana.
Cha kuzingatia hapa ni kuifahamu fursa kwa undani zaidi mapema kabla ya wengine then uwezekano wa kuyaona maisha katika mwana bora zaidi hauepukiki.
Hapa ndipo linapokuja suala la kujua na kuifahamu kwa undani zaidi Neema ya vanilla iliyopanda bei maradufu zaidi ya madini ya silver ndani ya mwaka huu ambapo vanilla imeipiku silver ikiuzwa $600 na silver ikiuzwa dola $550, kupanda kwa bei kumesababishwa na kuongezeka kwa matumizi ya vanilla Duniani kwa kutengenezea madawa na pia kupungua kwa uzalishaji kwa mzalishaji mkuu wa vanilla Duniani ambayo ni nchi ya Madagascar.
Kwa hapa Tanzania kule Kagera kuna wakulima wa Vanilla ambayo wanaiuza Tsh 150,000/= kwa kilo. Then Kwenye soko la Dunia ndio inauzwa Tshs million1.5. Kama unataka kununua reja reja jipeche zaidi maeneo ya Kagera na kama unata kulima maeneo yenye hali ya hewa ya tropic ndio favourable conditions kwa hili zao.
Ukiwa na kilo 50 za Vanilla kwa bei ya million 1.5 kwa kilo utakuwa na jumla ya Tshs milioni 75 hapa ndipo jina lako linabadilika mtaani na unapewa jina jipya la Freemason, sio jina tu hata wewe unaanza kutembea umetanua mikono kama una majipu kwenye makwapa vile kwa ukwasi na kujiamini.
Information is power, And now you know.
I'm gone! [emoji188]
[emoji176]
Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna mama mmoja wa kiarusha analima vanila maeneo ya Tengeru....Aliniambia amepata soko Ulaya na inalipa sana..ngojea nimfuatilie zaidi
Imagine ushakopa bank unadaiwa sasa ?Toba
3.5k maana yake ni nini? Maana K husimama badala ya 000 mfano mtu akisema 50k hua ana maanisha 50,000 je hio 3.5k umekaanisha 3.5000 au 35,000?Nimelizungumzia sana hili la vanilla katika uzi mmoja humu
Tunanunua na kuuza lakini kwa bongo nilinyanyua mikono
Wauzaji wa Madagascar ni ku wire hela mzigo unapokea unaambiwa kabisa au ijia mwenyewe
Bei ndio hiyo mkuu lakini nashangaa kwetu kilo mwisho ilikuwa 3.5k tsh @kg
Lakini utapigwa bla bla nyingi
Sent from my SM using Tapatalk
3.5k maana yake ni nini? Maana K husimama badala ya 000 mfano mtu akisema 50k hua ana maanisha 50,000 je hio 3.5k umekaanisha 3.5000 au 35,000?
Poa mkuu yani ilinichanganya sana kuielewaSorry mkuu nilimaanisha 350,000
Au inaweza kuwa 350k
Ntairekebisha