MandawaNaManenge
Member
- Jan 27, 2012
- 80
- 70
watu wamejaa miwivu tu. ooh hataolewa! kwani kuolewa ndio kuishi? watanzania sijui tumelogwa na nani?
Yaani Demba umenichimba nafsini. Mi nashangaa huu utumwa na myth za kuolewa sijui kupendwa eti credit. Jamani! So kupendwa nako kumebandikizwa (pegged) na upishi? Ndio maana watu wanang'ang'ania majikoni ili iwe rahisi hata kuweka limbwata! ( am scribbling this with a tear in my rib.. tehe).. Sawa kupika , labda ni vyema but sio bima ya ndoa wala mapenzi.
Na hata hivyo Vee kasema hapendi sio hawezi.
Na still, hata kama hapendi, ni choice yake. Fikra mgando tuziache.
Mbona zamaaaaani hizo za Ugagagigikoko, mwanamke aliyeweza kutembea vijiji nane kwenda ukweni kwa spidi sawa na mumewe au hata anaenda mwenyewe tu kusalimia ndie aliekuwa akionekana anafaa kuoa.
Leo nani anatembea na mmejikoki na vi -IST na viFunCargo vyenu?
Mbona mnanunua nyanya supermarket, hamlimi uani kwenu?
Wengine hadi mchicha mnanunua Shopperz kwanini usilime hata kwenye kigunia ukakijaza mchanga kama huna ua wa kuweka tuta!
Tusidanganyane wala kupelekeshana hapa na mawazo binafsi.
Pika kama unapenda , paka ina kama unapenda, piga pasi kama unapenda, tembea kwa mguu kwenda kazini kama unapenda. Vinginevyo, maisha ni yako, na chaguo ni lako.
Huwezi jua miaka mia ijayo hata kumeza mate itakuwa ni option maana kutakuwa na gadgets pia au watu mbadala wa kukumezea mate ili wewe ufanye mengine.
Jioni njema