Vibahasha vya khaki vinavyozuia harakati na kuua ndoto za vijana

Vibahasha vya khaki vinavyozuia harakati na kuua ndoto za vijana

Joined
Sep 10, 2013
Posts
335
Reaction score
478
Ndoto kubwakubwa za wanasiasa na wanataaluma vijana zimeuawa na vihela vidogo vidogo visivyojaa hata bahasha ndogo.

Kwa wanasiasa vijana wameamua kutumikishwa na wakongwe wa siasa na kazi yao kubwa ni kutumwatumwa kama vijakazi ingawa wanapakwa mafuta kwa mgongo wa chupa na kuitwa majina mazuri mazuri ya uongo.

Kazi yao kubwa Hawa vijana ni kutengeneza fitina na kutukana waliotumwa kuwatukana,wamekuwa kama vijibwa vidogo vidogo vinavyoamuriwa mbwekee huyu au yule bila kuhoji kwa nini.

Utavikuta Dodoma wakati wa bunge utafikiri ni madreva au mautingo wa magari, hulala kwenye hotel cheap cheap huku vikiwinda mademu kwa ajili ya mabosi wao,vina akiri lakini vimeamua kuwa Vijinga,

Kundi la pili ni la wanataaluma,wanalipwa mishahara viduchi sana mwisho wa mwezi,vinabebeshwa mizigo mizito kama punda lakini wanauwezo wa kuanzisha biashara au kufungua ofisi zao kubwa maishani na kujenga taasisi kubwa duniani.

Kama ilivyo kwa punda awekewavyo karoti mbele yake na kuburuta mzigo mzito ili aifikie karoti na akiipata huitafuna yote bila kuacha akiba kisha huwekewa nyingine tena ndivyo ilivyo kwa waajiriwa hawa na vibahasha vya mwisho wa mwezi.

Katika kundi hili la wanataaluma naumizwa zaidi na waandishi wa habari vijana ambao mchana kutwa utawaona wanavyopigwa vumbi na jua kwenye mabenchi ya ofisi za wakubwa kutafuta habari,ukweli ni kwamba hawatafuti habari bali vibahasha vya kaki vyenye elfu thelathini ili waandike sifa za uongo kwa mafisadi na walarushw hao.

Taarifa za ukweli ziko vijijini ambako kuna mateso ya kila aina,matukio ya kutisha ambayo wakiyaandika na kuyaripoti yatawakuza sana sana,shida huko hakuna bahasha ukiwaita watakuuliza bahasha..bahasha...bahasha,ndiyo maana watazeekea kwenye mabenchi ya wakubwa.Hawako tayari kusota,kutembea kwa miguu,kulala na njaa ili wakue na kutimiza ndoto Zao.
 
Kamanda, ukiachilia mbali taaluma walizo nazo watu pia kuna ukosekanaji mkubwa wa ufahamu, mwanasiasa yeyote awe CCM, CDM,NCCR, ACT n.k anapokuendea wewe kijana na kukupa jukumu fulani jiulize maswali kadhaa, jiridhishe kwanza kabla ya kuanza kujiingiza katika malengo ya wanasiasa. Kulinda utu wako ni bora zaidi kuliko hela za kwenye bahasha ya kaki.
 
Kamanda, ukiachilia mbali taaluma walizo nazo watu pia kuna ukosekanaji mkubwa wa ufahamu, mwanasiasa yeyote awe CCM, CDM,NCCR, ACT n.k anapokuendea wewe kijana na kukupa jukumu fulani jiulize maswali kadhaa, jiridhishe kwanza kabla ya kuanza kujiingiza katika malengo ya wanasiasa. Kulinda utu wako ni bora zaidi kuliko hela za kwenye bahasha ya kaki.
"Kulinda utu wako ni bora zaidi kuliko hela za kwenye bahasha ya khaki"great quote
 
Wewe ni wa kupuuzwa tu, unafanya usanii, huna dhamira ya kweli.
 
Huo ndo ukweli, vijana wengi hawatimizi ndoto zao kwa sababu ya umasikini wao na kutojiamini katika mambo mbalimbali. Pia wamegawanywa kimakundi kama hawa ccm, hawa cdm, nk vijana hawajajitambua vizuri nguvu yao mbele ya jamii na taifa lao kiujumla!
 
Kamanda angalia Sifa ulizozipata kwenye harakati zako ndani ya CDM huko kanda ya Ziwa hadi kupewa jimbo la kalenga wakati wa kampeni zisije haribikia hapa JF. JF sio sawa na Jukwaani ukishika MC basi wengine kimya kwa mwendo huu nakupa miezi mitano.
 
Huo ndo ukweli,
vijana wengi hawatimizi ndoto zao kwa sababu ya umasikini wao na
kutojiamini katika mambo mbalimbali. Pia wamegawanywa kimakundi kama
hawa ccm, hawa cdm, nk vijana hawajajitambua vizuri nguvu yao mbele ya
jamii na taifa lao kiujumla!

Umenena kaka
 
Back
Top Bottom