Wasanii wa muziki wa Bongo Fleva nchini, Abdul Naseeb maarufu kama Diamond Platinumz na Faustina Charles maarufu kama Nandy, mapema leo hii wamewasili katika ofisi za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), kufuatia kusambaa mitandaoni kwa video zao wakiwa faragha zilizodaiwa kukosa maadili.
Hata hivyo hivi karibuni Waziri wa Habari, Sanaa, Michezo na Utamaduni, Harrison Mwakyembe aliagiza kukamatwa kwa wasanii hao kwa ajili ya upelelezi kisha kufikishwa mahakamani kujibu mashitaka yanayowakabili ya kukiuka maadili na kusambaza video hizo chafu.
Tazama Video hapa chini ikionesha Diamond na Nandy wakiwasili TCRA.
Diamond akijitetea na Kuomba msamaha
======
Wasanii wa bongo fleva, Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz’na Faustina Charles ‘Nandy’ wamewasili katika ofisi za Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA).
Wasanii hao wanaitikia wito wa TCRA ikiwa ni siku chache baada ya kusambaa kwa video zao zinazokiuka maadili.
Nandy aliwasili TCRA saa 5:48 asubuhi leo Aprili 19 na Diamond aliwasili saa 6:15 mchana. Diamond alisindikizwa na menejimenti yake ikiongozwa na Said Fella.
Hivi karibuni, Waziri wa Habari, Sanaa na Utamaduni, Dk Harrison Mwakyembe alizungumza bungeni kuwa wasanii hao walikamatwa na kuhojiwa kuhusu kusambaa kwa video zinazokiuka maadili.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa alithibitisha kuwahoji wasanii hao.
Hata hivyo hivi karibuni Waziri wa Habari, Sanaa, Michezo na Utamaduni, Harrison Mwakyembe aliagiza kukamatwa kwa wasanii hao kwa ajili ya upelelezi kisha kufikishwa mahakamani kujibu mashitaka yanayowakabili ya kukiuka maadili na kusambaza video hizo chafu.
Tazama Video hapa chini ikionesha Diamond na Nandy wakiwasili TCRA.
Diamond akijitetea na Kuomba msamaha
======
Wasanii wa bongo fleva, Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz’na Faustina Charles ‘Nandy’ wamewasili katika ofisi za Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA).
Wasanii hao wanaitikia wito wa TCRA ikiwa ni siku chache baada ya kusambaa kwa video zao zinazokiuka maadili.
Nandy aliwasili TCRA saa 5:48 asubuhi leo Aprili 19 na Diamond aliwasili saa 6:15 mchana. Diamond alisindikizwa na menejimenti yake ikiongozwa na Said Fella.
Hivi karibuni, Waziri wa Habari, Sanaa na Utamaduni, Dk Harrison Mwakyembe alizungumza bungeni kuwa wasanii hao walikamatwa na kuhojiwa kuhusu kusambaa kwa video zinazokiuka maadili.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa alithibitisha kuwahoji wasanii hao.