Video: Huyu kama ni mkeo utamfanyaje?

Video: Huyu kama ni mkeo utamfanyaje?

Huyo mume hela Hana hapo hata sofa wala godoro hajanunua.
Kuna ndoa zinakufa kwa kuiga vitu kutoka nje. Na hata kama unaomba ushauri hakikisha unayemuomba ushauri ana ndoa kama yako na ana maisha kama yako. Kuna jamaa mke alikuwa anamsumbua kaka yake akamshauri awe anamshtua akili(anampiga makofi) mara moja moja. Hajui kuwa kaka yake ni tajiri na mkewe ni mama wa nyumbani. Yeye ana biashara ya duka na mkewe ni mtoto wa Jaji. Ile jamaa kumpiga mke kofi moja tu ndoa ikaisha. Jamaa amehangaika mpaka kwa maaskofu kusuluhisha. Mke washaondoka na watoto. Tusiige, ukikaa na mtu anakunywa naye bia unaona ni mwenzako kumbe mpo tofauti sana. Na pia mnaweza kuwa sawa kama marafiki lakini mkawa na ndoa tofauti.
 
Aaaah wapi wewe! Yule wa kwangu akijaribu huo upuuzi anajua kitakachomkuta. Kila siku nampaga risala na tahadhari.

Nyie mnaoweza kushare hongereni, mi hapana.
Ni kuachana tu kila mtu ashike hamsini zake. Unashare ila hujui.
 
Wanaume acheni haya mambo jamani yanaumiza sana!

Mwanaume kazingua mno, kumbe alimleta mchepuko wakafanya ushenzi mbele ya watoto?

Ila nimechekaaaa! Anayoyaongea huyo mwanamke kwa hasira yamenivunja mbavu.
Hasira hasara, sasa hayo makochi yamekosa nini??
 
Kweli kazingua, ila kuna wanawake wengine ni wastaarabu mpaka unashangaa. Kuna jamaa yetu alitualika kwenda kwake kula mbuzi choma siku ya Kumamosi (ilikuwa ni kawaida yetu). Huwa tunaanza na mchemsho wa nguvu, then vinywaji vikali tukiwa tunasubiria nyama choma.
Tunafika pale mida ya saa tano asubuhi tunakuta hali ya usalama ishachafuka. Kumbe asubuhi mke wake kaenda sokoni kununua viungo na mahitaji mengine, huku nyuma kamuacha jamaa na shemeji yake (rafiki ya mke wake) na vijana waliokuwa wanasaidia kuchinja na kuandaa nyama.

Jamaa kumbe kaachiwa gepu na hapo tayari walishaanza konyagi asubuhi na huyo shemeji mtu, wale vijana wachinjaji wanawachora tu (kumbuka mke ndiye aliwaomba waje kusaidia). Muda si mrefu jamaa na shemeji wakapelekana chumbani, madogo wakampigia mwanamke simu fasta akageuza na kupaki gari mbali kidogo. Anaingia anamkuta mme wake anapiga mashine (chumba cha wageni) na mlango wamerudishia tu.

Yule mwanamke kwa kusaidiana na wale vijana wakawafungia watuhumiwa mle ndani, tunafika pale jamaa kawa mpole kama sisimizi, nyama haikulika tena, tulibeba tu mikonyagi tukaondoka. Mpaka leo bado ni wanandoa na wanaishi kwa furaha tele, jamaa hata pombe akapumzika kabisa na kuwa mtu wa familia kweli kweli.
Daah! Huyo dada apewe maua yake aisee.
 
Back
Top Bottom