Video: Jengo la Shule lenye ghorofa 5 lililojengwa miaka 85 iliyopita likihamishwa kama lilivyo katika mji wa Shanghai, China

Video: Jengo la Shule lenye ghorofa 5 lililojengwa miaka 85 iliyopita likihamishwa kama lilivyo katika mji wa Shanghai, China

Parody

Member
Joined
Sep 13, 2020
Posts
24
Reaction score
69
Tazama jengo la shule lililojengwa zaidi ya miaka 85 iliyopita likihamishwa zima zima kama lilivyo katika mji wa Shanghai, China, kwa kutumia teknolojia iliyopewa jina "Mashine Inayotembea"



Jengo hilo lililopo katika eneo la Wilaya ya Huangpou lilijengwa mwaka 1935 kwa ajili ya Shule ya Msingi Lagena, na limeondolewa ili kupisha ujenzi wa majengo mapya ya ofisi, ujenzi unaotarajiwa kukamilika mwaka 2023.

Kuhamishwa kwa jengo hilo kulifanikiwa baada ya Wahandisi kuchimba kuzunguka jengo hilo kisha kuweka mashine (robots) zaidi ya 198, hasa katika nguzo zinazoshikilia jengo hilo, na kufanikiwa kulibeba na kulisogeza umbali wa mita 62 kutoka eneo lililokuwepo awali ndani ya muda wa siku 18!

Hatua hiyo ni sehemu ya serikali ya China kuhifadhi majengo ya asili yenye historia ya nchi hiyo.

Chanzo: CNN
 
Sema tume ingia kwe 18 za mabeberu tukichomoka nina badili jina humu dawa yetu ina chemka ipo nyuzi joto 60 mda huu
The world is moving to the east blaza nyie endeleeni kutetemeka na hao wazungu pori zilipendwa
 
Tazama jengo la shule lililojengwa zaidi ya miaka 85 iliyopita likihamishwa zima zima kama lilivyo katika mji wa Shanghai, China, kwa kutumia teknolojia iliyopewa jina "Mashine Inayotembea"

View attachment 1616062

Jengo hilo lililopo katika eneo la Wilaya ya Huangpou lilijengwa mwaka 1935 kwa ajili ya Shule ya Msingi Lagena, na limeondolewa ili kupisha ujenzi wa majengo mapya ya ofisi, ujenzi unaotarajiwa kukamilika mwaka 2023.

Kuhamishwa kwa jengo hilo kulifanikiwa baada ya Wahandisi kuchimba kuzunguka jengo hilo kisha kuweka mashine (robots) zaidi ya 198, hasa katika nguzo zinazoshikilia jengo hilo, na kufanikiwa kulibeba na kulisogeza umbali wa mita 62 kutoka eneo lililokuwepo awali ndani ya muda wa siku 18!

Hatua hiyo ni sehemu ya serikali ya China kuhifadhi majengo ya asili yenye historia ya nchi hiyo.

Chanzo: CNN
Mashine inayotembea ... bongo tunatembeza mashine... ooh mwanaume mashineeee
 
Mngekuwa mnahamasisha watu wawapigie kura huko mtaani kwa bidii kama mnavyorusha vijimaneno humu kweli mngechukua nchi. Dozi imewaingia
 
Yani Tanzania tumejaza Vilaza tu kila idara, huko mambele ukiwa mbumbuu unaeza ukauliwa..huku Tz ni vikao vya chama namna ya kuiba kura
Mbona huzungumzii vikao vya chadema vya kutafuna ruzuku na kushindwa hata kujenga ofisi ya chama HQ? Au nyani haoni kundule?
Ngoja nikuache kwenye.

NB: Mapato ya chadema 2015 - 2020 yalikuwa ni zaidi ya Bil 5. Ruzuku pamoja na michango wa wabunge wao 70.
 
hata technology iliyotumika mwaka huu kuiba kura inastaajabisha kwani sijawahi kuona!!!
 
Back
Top Bottom