Video na Picha: Ushahidi kuhusu yaliyotokea kwa Jaji Warioba wakati na baada ya vurugu, Ubungo Plaza

Video na Picha: Ushahidi kuhusu yaliyotokea kwa Jaji Warioba wakati na baada ya vurugu, Ubungo Plaza

Mleta mada umevurugwa tena umevurugukiwa kabisaaa! Paul Makonda alikuwa hamsaidii Amon Mpanju. Kama alikuwa ana NIA ya dhati ya kumsaidia basi angelisimama mbele yake ili asidhulike. Paul Makonda alimtumia Amon Mpanju kama KINGA YA KUJINUSURU na kipigo baada ya kuanzisha FUJO NA KUNDI LAKE. Picha inajieleza bayana. Alafu, kwa hao vijana unaosema walikuwa wanaonyesha Mabango yao yenye jumbe mbali mbali, kuna UHUSIANO gani wa kusimama na kupiga kelele za CCM.. CCM.. CCM na kuonyesha mabango yao huku wakiwa wanapanda na kusimama juu ya viti? Je, hiyo ndo namna ya kufikisha ujumbe? Jipange upya kabisaa ndo uje hapa mwehu wewe! Hata hivyo kichapo alikipata na bado vijana wanaoipenda Tanzania yao wako tayari KUZAA NAE WAKIMTIA MIKONONI.
 
Sindano inamuuma sana huyu mgonjwa ssm. Tutaendelea kumdunga tu Hatakama ni ya sumu
 
Jamiiforums is where we dare to talk openly!

[video=youtube_share;x6JAoKzSbsE]http://youtu.be/x6JAoKzSbsE[/video]
Kwa mwananchi yoyote ambaye hajafungwa kimawazo na kifikra, angalia vizuri hii video kwenye dakika ya 1:18 ili yale uliyoambiwa uchanganye naya kwako kuhusu tuhuma zinazoelekezwa kwa Paulo Makonda!.

Pix-1.JPG


Mtoa mada katika mdahalo wa kujadili Katiba Inayopendekezwa, Jaji Joseph Warioba akitoa mada kabla ya mkutano huo kuvunjika katika ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es Saam.
DSC_2016.JPG

Jaji Joseph Warioba akitoa mada katika kongamano kabla ya vurugu kutokea.
Pix-2.JPG

Baadhi ya vijana walioingia na mabango ndani ya ukumbi wa mkutano wakionyesha mabango yao.
Pix-4.JPG

Jaji Joseph Warioba akiangalia usalama wake kabla ya kuondolewa na mlinzi wake katika ukumbi wa Ubungo Plaza ambapo mdahalo wa kuijadili Katiba Inayopendekezwa ulikuwa ukifanyika kabla ya kuvunjika.


Pix-3.JPG

Mlinzi wa Jaji Joseph Warioba (kushoto) akimkinga kwa mikono ili asipate madhara baada ya kuanza vurugu katika mdahalo wa kujadili Katiba Inayopendekezwa.


Pix-5.JPG

Aliyekuwa mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Humphrey Polepole akiongea na mmoja wa vijana aliyekuwa na jazba mara baada ya kutokea kwa vurugu katika mdahalo wa kujadili Katiba Inayopendekeza.

Pix-6.JPG

Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF), Joseph Butiku (katikati) akisindikizwa kuingia katika chumba cha VIP mara baada ya kuvunjika kwa mdahalo wa kujadili Katiba Inayopendekezwa.


DSC_2069.JPG


DSC_2072.JPG

Baadhi ya vijana wakionyesha mabango yenye ujumbe mbali mbali
DSC_2135.JPG

Paulo Makonda akimsaidia mlemavu wa macho, Amon Mpanju baada ya vurugu kuanza kutokea ndani ya ukumbi wa Ubungo Plaza.
DSC_2163.JPG


DSC_2181.JPG

Baadhi ya viti vilivyotumika kama silaha na kinga kwenye vulugu

DSC_2263.JPG

Jaji Warioba akitoka katika ukumbi huku akisindikizwa na askari kanzu.
DSC_2268.JPG

Jaji Warioba akisindikizwa na makachero wa Polisi baada ya kuvunjika kwa mdahalo wa Katiba Inayopendekezwa
Pix-4.JPG

Hii hapa hajaika kwanini?
 

Attachments

  • Warioba.jpg
    Warioba.jpg
    87.7 KB · Views: 330
Alama za nyakati zipi while Wamehost huo mkutano kama raia wengine ila wao walikua na nia ya kuwahabarisha watu wajue undani wa katiba na sio kupelekwa. Naomba muwe mnafikiria na sio kuongea tu mana kila mwananchi ana uhuru wake na yeye kautumia huo uhuru ili kuwahamasisha watanzania wasome well katiba na kuielewa na si kuburuzwa.

Mnaboa watu kama nyie na ndio mana nchi haipigi hatua kwa sababu ya watu wenye mawazo mgando kama wewe
 
huyo kijana makonda angeangalia akina twabwe hiza wapo wapi siku hizi na
 
Kama hukubaliani na hoja anayotoa mwenzako dawa ni kutoa hoja mbadala yenye nguvu zaidi au kujiondoa kwenye majadiliano naye. Kuanzisha vurugu kwa sababu tu hukubaliani na hoja za mwenzako ni kiwango cha china kabisa cha kufikiri. Kwa lugha sahihii ni unyani.
 
Nakubaliana na wewe kwa kiasi kikubwa sana, ule ulikuwa mdahalo huru unao accommodate fikra na mitazamo tofauti. Haukupaswa kujikita kwenye upande au kundi fulani, tafsiri ninayoipata ni kwamba kuna kundi fulani tu ndio lilipaswa kuhudhuria na kujadili, sifikiri kama ni sawa kujikita katika misimamo fulani bila kuwapa fursa ya kutoa maoni au kuonyesha imani zao watu wanaoamini tofauti na sisi. Msingi mkuu kabisa wa ustaarabu ni pamoja na uvumilivu, kuvumilia kusikia au kuona mambo tusiyopenda kuyasikia au kuyaona.

Ninafikiri kwa kuwa mdahalo uliandaliwa na taasisi inayohudumia watanzania wote, isingekuwa sawa kuhodhiwa na baadhi yetu huku tukiwafungia wapinzani wetu nje, inaleta picha ya kudhoofisha demokrasia jambo ambalo haliwezi kuleta afya kisiasa.
Hakukuwa pia na sababu ya upande mwingine pia kuingia na mabango na kuyatoa ukumbini. Nina hakika kungekuwa na muda wa mjadala ambapo pande zote Wangetoa maoni yao kuliko walivyotenda.
 
Taifa letu litaangamizwa na unafiki na uwongo wa baadhi ya watu wanaofaidika au wanaodhani watafaidika na matokeo ya unafiki na uwongo wao.

Ukweli hutafutwa.

Ukweli huweka huru kila binadamu anayeutafuta na kuupata.

Hotel ina CCTV, ukumbi pia una CCTV.

Ukweli hutumia ngazi wakati uwongo hupanda lift.

Kuna baadhi ya wananchi wanawaza katika mlengo wa hisia, wanaongozwa kwa hisia na wanaishi kwa hisia.

Ukweli umeanza kutufikia kwa sasa.

vp mbona hujaweka ile makonda akimpiga mkuu
 
a country iliyojaa ignorants... mtu na akili zake anatumia violence kiasi hicho what for?? Honestly kuna measures nyingi sana watu wangechukua maana hii ya kurushiana viti haisaidii chochote, n even worse ni ile walikua wanarushiana wao kwa wao... Hahaha! i pity these guys!
 
mi nilishuhudia jamaa anarusha mateke kama checknoris , lile teke lingempata makonda haki ya mungu leo tungekuwa tunazungumza mengine. tushukuru tu mungu wote wazima
 
a country iliyojaa ignorants... mtu na akili zake anatumia violence kiasi hicho what for?? Honestly kuna measures nyingi sana watu wangechukua maana hii ya kurushiana viti haisaidii chochote, n even worse ni ile walikua wanarushiana wao kwa wao... Hahaha! i pity these guys!

Ndiyo wasomi wetu hawa.Sijui bongo zao zinakuwa zimeingia maji.
 
hao vijana walioleta fujo ni wasaliti na maadui wa taifa. kama serikali haitawachukulia hatua, si wanaonekana kwa sura, wanajulikana tunao huku mtaani, kwanini tusiwafuate hukuhuku mtaani tuwale kabang ili iwe fundisho kwa vijana wengine wanaotumiwa? nchi hii ya kipumbavu sana.

kweli kabisa
 
Makonda uliwahi kuwadanganya watu Moshi kuwa wewe ni mlokole lakini wapi, tumekujua sasa. Mtu asiyewaheshimu hata wazee.
 
Back
Top Bottom