Video: Paul Makonda na harakati za hila za kuulinda mfumo wa serikali tawala ya CCM ulioshindwa. Atafanikiwa au anasukuma anguko lake?

Uzima Tele

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2023
Posts
1,270
Reaction score
2,822
Your browser is not able to display this video.

This video is Courtesy of SK Media Online TV.

=====================================================
KWA UFUPI;

1. Paul Makonda ni Katibu wa Idara ya Itikadi na Uenezi ndani ya CCM. Yupo barabarani anatembea nchi mzima hata sasa kwa kinachoitwa "ziara ya kuimarisha uhai wa chama..."

2. Ukifuatilia hotuba zake ktk mikutano yake, utaona kwa uwazi kabisa nyuma ya pazia sura ya Mtendaji mkuu wa serikali (Rais Samia Suluhu Hassan) na sio sura ya kiongozi wa idara ndogo tu ndani ya Chama Cha Mapinduzi - CCM yaani Idara ya Itikadi na Uenezi.

Mtu anaweza jiuliza, huyu mtu anafanya hivi kwa makusudi, kwa bahati ya kutojua au ana baraka za boss wake M/kiti CCM taifa na Rais wa JMT?

Ni Kwa sababu maagizo yake ni maigizo tu. Hakuna Mtendaji makini wa serikali atayatilia maanani na kuyatekeleza. Ni kwa sababu hayatoki kwa mtu sahihi kwa mtiririko wa utendaji wa kiserikali..

Mtu anajiuliza Yuko wapi Rais mwenyewe? Yuko wapi VP, Dr Phillip Mpango? Yuko wapi PM, Mwl Kassimu Majaliwa? Wako wapi mawaziri wa kisekta ili kushughulika na matatizo na changamoto za nchi? Je, ya Paul Makonda ni kiashiria cha nchi na taifa kukosa uongozi makini na thabiti? Bila shaka hili la mwisho laweza kuwa jibu..!!

3. Kwa hili kila mtu anajiuiza kuikoni huko CCM kwa maigizo haya? Mifumo sahihi haitendi kazi tena au ndio kuchoka kwenyewe huku? Na kwanini Rais Samia Suluhu Hassan, VP Dr Phillip Mpango na PM Mwl Kassimu Majaliwa wanamtanguliza huyu mtu kupiga kelele ambazo kiuhalisia hazitakuwa na matokeo yoyote kwa wananchi?

4. Fuatilia uchambuzi wa jambo hili toka Kwa mwandishi wa habari mkongwe na nguli Ansbert Ngurumo ktk video ili ujue uongo, hadaa, hila na maigizo ya serikali ya CCM kupitia watu wake wa ajabu ajabu..
 
Kote alikopita amepata muitikio mkubwa na watu wamerejesha Imani Yao Kwa chama na Serikali.

Sijasikia Wala kuona mahala amesema ccm oyee au Samia oyee watu wakatukana au kuacha Kuitika.

Chadema hofu na kiwewe Cha nini?
 
Kote alikopita amepata muitikio mkubwa na watu wamerejesha Imani Yao Kwa chama na Serikali.

Sijasikia Wala kuona mahala amesema ccm oyee au Samia oyee watu wakatukana au kuacha Kuitika.

Chadema hofu na kiwewe Cha nini?
Wanaitikia kwa lazima, kila mkoa wakuu wa idara wa halmashauri na taasisi wote wanalazimishwa kuambatana naye, unadhani wataacha kuitikia?
 
Kote alikopita amepata muitikio mkubwa na watu wamerejesha Imani Yao Kwa chama na Serikali.

Sijasikia Wala kuona mahala amesema ccm oyee au Samia oyee watu wakatukana au kuacha Kuitika.

Chadema hofu na kiwewe Cha nini?

Zaidi ya nusu ya wanaokusanyika kwenye mikutano yake wanapatikana kwa nguvu ya Dola. Kwa Chama kilichoko madarakani muda mrefu tena kwa shuruti, hakishindwi kupata watu kwa njia yoyote ile Ili kuhadaa umma kuwa wanakubalika. Na huko kote wanahutubia tu bila kujibu maswali magumu. Sana sana wanachofanya ni kustage watu ili walete kero ambazo watajifanya kuzitatua Ili kuhadaa wajinga.
 
Kote alikopita amepata muitikio mkubwa na watu wamerejesha Imani Yao Kwa chama na Serikali.

Sijasikia Wala kuona mahala amesema ccm oyee au Samia oyee watu wakatukana au kuacha Kuitika.

Chadema hofu na kiwewe Cha nini?
Hoja hapa ni HILA na ULAGHAI na sio mwitikio wa watu..

Watu hata ukiandaa mazingira ya kuwachinja na kuwala nyama kwa kutumia hila na udanganyifu wa ahadi za kutatua matatizo yao, watakuja tu lakini mwisho wa siku watajua kuwa kumbe walidangamywa..!!

Na unachokisema hapa ndio hasa ujumbe wa makala hii. Yaani CCM Kwa kumtumia Paul Makonda inatumia hila na udanganyifu kuwahadaa na kuwadanganya wananchi kwa ahadi za uongo. Haya ya Paul Makonda ni maneno matupu. Hakuna kitakachobadilika. Unabisha? Basi subiri..

Na unafikiri nini itakuwa reaction ya wananchi wakija kujua kuwa walidangamywa? Anguko kuu la CCM huku architecture akiwa ni Paul Makonda na Samia Suluhu Hassan..!
 
Hivi kauli ya kile anachokifanya Makonda kuitwa "maigizo" imethibitishwa vipi?!

Na kwasababu hii kauli mostly nimeona ikitolewa na wapinzani, sio kwamba wameamua kutoa jibu rahisi la kisiasa ili kufifisha kile anachofanya Makonda?

Kwasababu kwa mtazamo wangu, ili jambo fulani lithibitishwe kwamba lilikuwa maigizo, basi ni lazima kwanza tuupe muda nafasi ili kuthibitisha hivyo, lakini sio kusema ni maigizo kwasababu watendaji wanaohojiwa na Makonda hawatafanya kile wanachoagizwa.

Hilo ni wrong, au kama ulishaongea na watendaji wahusika wakakujibu hivyo, lakini kama hukuwahi kuongea nao, basi hilo ni jibu uliloamua kujichagulia kwa manufaa yako, possibly ya upande wako wa upinzani.

Nasema hivyo kwasababu, tumeona Makonda akimpigia Mchengerwa juzi, na Mchengerwa nae akaanza kufanyia kazi kile alichoambiwa na Makonda.

Sasa mpaka kufikia hapo naona kuna haja kwa upinzani kuangalia namna nzuri ya kupambana na Makonda, na sio kumtungia majibu mepesi ambayo kiuhalisia hayapo, au kumtukana matusi ya nguoni, find a proper way guys.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Wameshikwa na kiwewe hao Wapinzani achana nao
 
walisema hawatamjibu Makonda ety sio level yenu ngoja dawa imwingie huyo soga la Ulaya walidhani kumuondoa Magufuli ndio wataingia madarakani moto wa Makonda ni hatari zaidi ya ule wa Magufuli
 
Huyu ngurumo muhuni tu
 
Mkuu Tindo, hunitendei haki kuniweka mimi katika kundi hili la hawa machawa mazagazaga!.
P
Unastahili kuwepo kwenye kundi Hilo. Zipo sababi kadhaa, lakini Moja kubwa ni Ile Imani Yako kuwa "CCM itatawala milele!" Ccm itajimaliza yenyewe, na visababishi itakuwa ni uroho wa madaraka ndani ya chama, wizi , ufisadi na fitina.
 
Makonda anakanyaga mafuta mpaka mwisho,

weak opposition iko surprised 🐒
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…