Uzima Tele
JF-Expert Member
- Jan 20, 2023
- 1,270
- 2,822
- Thread starter
-
- #21
Pole sana Kwa kuingizwa kundi moja na Lucas mwashambwa na MamaSamia2025 na ChoiceVariable na chiembe na Tlaatlaah na Etwege na wengine kibao.Mkuu Tindo, hunitendei haki kuniweka mimi katika kundi hili la hawa machawa mazagazaga!.
P
Hata hivyo, wewe Pascal Mayalla bado ni chawa tu japo unaweza usie yule wa "mazagazaga" bali yule chawa mwenye akili timamu maana kuna wakati huwa unajiongeza ili kuficha tabia za chawa..
Back to the topic;
Una maoni gani juu ya uchambuzi huu wa Ansbert Ngurumo?
Is Paul Makonda engineering his own downfall subsequently to your CCM?
Umeuona udanganyifu na hila za CCM katika eneo moja tu la treni ya SGR?
Hivi inawezekana vipi viongozi wa serikali waandamizi kuanzia Rais hadi mawaziri kuwa waongo wa kutoa ahadi zaidi 10 katika jambo moja tu kuhusu kuanza kwa huduma za usafiri wa treni ya SGR kati ya DSM na Morogoro tu na bado hakuna hata moja iliyotimizwa?
Hivi kwa mtazamo wako, serikali ya viongozi wa namna hii inakuwa na uhalali gani kuendelea kuwepo? Tuendelee kuiamini? Ina uadilifu wowote?
Hili ni eneo moja tu. Njoo kwenye umeme. For more than 35yrs ni uongo na ulaghai mtindo mmoja..!
Ni ngumu sana kupiga hatua za kimaendeleo chini ya mfumo wa utawala unaolea na kubeba viongozi wajinga, wazembe na wasiowajibika kwa kiwango hiki!!