28 September 2020
Nyamongo, Mara
Tanzania
TUNDU LISSU AHAIDI KULA SAHANI MOJA NA MAPOLISI WALIO WAPIGA MABOMU NYAMONGO MKOANI MARA
Watu wengi wamekufa hapa Nyamongo Tarime toka mwaka 2003 wengine walifungwa magerezani, wamepata ulemavu wa kila aina, kupoteza mashamba yao na migodi yao midogo kwa kisingizio cha uwekezaji. Miaka 17 iliyopita (2003) mgodi wa Nyamongo ulileta msiba mkubwa asema mgombea Tundu Lissu.
Serikali ya CCM ilishiriki katika madhila haya toka 2003 hadi leo 2020 halafu pia wanadiriki kuwapiga mabomu ya machozi. Atoa angalizo kwa Magufuli kuingilia mikutano ya CHADEMA na pia Kassim Majaliwa kufanya kampeni kinyume cha sheria ya Maadili ya Uchaguzi lakini Tume ya Uchaguzi ya Taifa haikemei wala kuiandikia barua CCM Mpya ya Magufuli.