Uchaguzi 2020 VIDEO: Wachambuzi wa siasa Kenya washangazwa na muundo wa uchaguzi wa Tanzania, wasema walitoka huko kitambo sana

Sasa mbona mnapoteza nguvu na rasilimali zenu juu ya kitu ambacho mnajua kabisa hakina haki?
 
kumbuka kila nyumba ina sebule yake Na kila kabila lina desturi zake, hata hivyo hakuna walichotuzidi kwa sasa licha kubadili katiba mara 2 ni fujo tupu
 
Shida kubwa ya nchi yetu ni chama tawala, hawajiamini hivyo kupelekea kutoa maaumuzi mabovu kila Leo kila siku miaka yote, mfano Tundu lissu alipofika Geita siku ya kampeni yake , CCM kwa hofu kubwa mchana walipita na kipaza sauti wakiwa watangazia vijana, kina mama na kina baba wote waccm wafike office za ccm mchana eti lengo lao ni kujaribu kupunguza idadi ya wana nchi wengi kuhudhuria mkutano wa lissu, hata baada ya msafara wa lissu kuingia Kati Kati ya mji umati mkubwa wenye mapenzi na lissu wakawa upande wa kushoto , huku upande wa kulia wana ccm wakajaa wakawa wanaimba chagua magufuli kinyume na sheria za uchaguzi, hiyo ni siku ya Lissu iweje CCM waandamane? kwa hiyo fujo nyingi 80% zina ratibiwa na ccm lakini tume haiwezi kuchukua hatua maana wanaogopa kufukuzwa, tume sio huru.
CCM waavuruga uchaguzi halafu wana sema lissu anatukana, hivi kusema uwanja wa ndege chato umejengwa kinyume na matakwa ya wengi ni kutukana? kusema mpwa wa magufuli kutoa pesa na mayanga mke mwenza wa magufuli kujenga tender nyingi ni kutukana? Magufuli sio mungu wala sio mkamilifu kusemwa ni kawaida,asiongoze nchi kama familia yake, ccm asilimia kubwa bad wana mawazo ya kale ambayo hayana mshiko kwa wakati huu.
 
Hawa ni wachambuzi wa kisasa nchini Kenya wakishangazwa na namna Tanzania ilipo bado kwenye ukoloni japo ni wa watu weusi.

Hawa hawawezi kuchambua siasa za Kenya kwa kulinganisha na Tanzania kuliko PLO Lumbumba; hawa ni wababaishaji tu. Msikie Lumbumba alivyosema hapa


Barrick walikuja kwa Magufuli na kuomba msamaha "Mea culpa, mea culpa, mea Maxima Culpa" halafu kuna mtu anasema tuwaachia machimbo wajifanyie watakavyo?
 
Chadema kupewa pesa na serikali ya CCM ni takwa la kisheria,ndivyo hivyohivyo Rais wa jumuhuli ya muungano kuteuwa mwenyekiti wa tume ya uchaguzi.
 
kwa kweli kuna vitu vinatia aibu inakuwa kama nchi haina wasomi. wenzetu wanatuona kama tupo zama za manyani
 
Siasa za Kenya ni za ubaguzi wa kikabila.

Kenya wapambane kwanza waondoe hili kabla ya wao kukosoa wengine.
hii ndo akili za CCM,unakwepa hoja kijinga kabisa. hoja ni tume,usitutoe kwenye mstari. au hoja ya tume majibu yake ni ukabila?
 
Kenya na siasa za kugawana madaraka,viongozi wao wapo kwa ajili siasa za kupeana ulaji,tokea hiyo katiba mpya wana jipya gani kutufanya tuwaige?
 
hii ndo akili za CCM,unakwepa hoja kijinga kabisa. hoja ni tume,usitutoe kwenye mstari. au hoja ya tume majibu yake ni ukabila?
Nimeukuta katikati mjadala huu ingawa kwenye uzi mwingine wa subject hii nilicomment....hivi huko Kenya kuna demokrasia gani wanayoringia?! Tanzania tunayo demokrasia na tume huru...huko Kenya kuna demokrasia gani?! Hivi kweli Kenya wana tume huru?! Kama ni hivyo mbona Kila uchaguzi ukimalizika huwa ni mapambano ya silaha chanzo kimojawapo kikiwa ni tume inayodaiwa kuwa ni huru?! Tangu lini Kenya kukawa na demokrasia?! Hao wachambuzi was Kenya ni wajinga na wapumbavu pamoja na ushenzi...demokrasia Kenya?! Tangu lini?! Hiyo ni demokrasia ya wenye nacho ...familia chache nchini Kenya zinamiliki karibu nusu ya ardhi ya Kenya na kuwaacha wakenya kwa mamilioni wakiwa hawana hata mita moja ya mraba ya ardhi...familia ya kiongozi mmoja maarufu was Kenya inamiliki maelfu kwa maelfu ya ekari za ardhi...yaani karibu 1/7 ya ardhi ya Kenya inamilikiwa na familia moja...hakuna chombo Cha habari Cha Kenya kinachohoji Hilo..demokrasia gani hiyo...yaani wakenya badala ya kujadili Mambo yao wanaleta uchochezi huku katika kipindi hiki nyeti Cha uchaguzi?! Huo ni uchokozi na pia uchochezi...demokrasia gani wanayoringia. Kenya...kwenye Corona viongozi wait wamekopa hell na zimeliwa na wachache Bila hata aibu huku wakenya kwa mamilioni wakiliazimishwa kujifu gia ndani na kuteseka kwa njaa...stupid...hiyo ndiyo demokrasia?!
 
Pale Kenya sasa hivi ni kama hamna mkubwa! Kila mtu ni kambare! Wamejaa ukabila, hayo ndio waliyoendelea hakuna kingine.

Fikiria uchaguzi bado miaka 2 lakini ofisi ya rais Kenyata ina mgogoro wa kugombea madaraka ya 2022
Unahamisha mada. Mada ni kuwa Rais kuteua Tume ya Uchaguzi huku naye ni mgombea ni jambo halikubaliki siku nyingi kwenye demokrasia
 
Kasoro unazozisema hazihusu mada. Mada ni kuwa Tume ya Uchaguzi isiteuliwe na rais au serikali, sababu moja kati ya zile za kidemokrasia ni kuwa na yeye ni mgombea. Tuseme ukweli tu, hili lilipitwa na wakati siku nyingi. Hata Katiba iliyopendekezwa bila kura za UKAWA iliondoa kasoro hii. Ni uongozi huu tu ndio unafurahia kasoro hii. Wewe unasikika kama mtu ujuaye mambo ya kisasa. Fanya mengine, utetezi wa hii kasoro haukufai
 
Pale Kenya sasa hivi ni kama hamna mkubwa! Kila mtu ni kambare! Wamejaa ukabila, hayo ndio waliyoendelea hakuna kingine

Fikiria uchaguzi bado miaka 2 lakini ofisi ya rais Kenyata ina mgogoro wa kugombea madaraka ya 2022
kenya kuna binadamu kamili wanaojitambua,huku kwetu tuna binadamu sokwe
 
Niliyoyazungumza ndiyo mada yenyewe...mada ni tume huru na demokrasia..huko Kenya ni Nani anateua hiyo tume inayodaiwa ni huru?! Composition ya wanaoteua ikoje?! Na composition ya walioteuliwa ikoje?! Suala hapa siyo Nani anateua?! Issue hapa no utendaji wa tume na impartiality katika utendaji...je, hiyo tume ya Kenya iko impartial?! To what extent?! Kama iko impartial ni vipi Kila baada ya uchaguzi kunakuwa na shida na hata mapambano ya silaha na mamia kuuawa?! Hujui kuwa viongozi wa Kenya waliwahi kushirakiwa kwenye mahakama ya kimataifa baada ya uchaguzi?! I hate watu wanaozungumzia demokrasia wasijue maana ya demokrasia...do you think in Kenya media iko free?! To what extent?! Do you think media Kama the Daily Nation itakosoa miradi ya Aghakan? People are talking of democracy and they mean liberal democracy. Do you think liberal democracy is feasible in Africa in each and every aspect?!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…