Uchaguzi 2020 VIDEO: Wachambuzi wa siasa Kenya washangazwa na muundo wa uchaguzi wa Tanzania, wasema walitoka huko kitambo sana

Uchaguzi 2020 VIDEO: Wachambuzi wa siasa Kenya washangazwa na muundo wa uchaguzi wa Tanzania, wasema walitoka huko kitambo sana

Kama ni matatizo yetu tuyajadili wenyewe, siyo mtu anatuletea mambo ya Kenya kama rejea ya mafanikio na majivuno yao bandia. Nayaita bandia kwa sababu wakenya kila wakati wanajiona eti wako bora kuliko sisi wakati kisiasa wako hovyo kabisa. Baada ya Rwanda, ndo pekee waliouwana ktk ukanda huu kwa sababu za uchaguzi. Bahati mbaya sana sisi, kama unavyoona akina dikteta2020 anamwita mtu ni mchambuzi wakati hana lolote! Mafanikio ni mfumo siyo kuandikwa tu ktk katiba. Z'bar tume ilipalaganyika pamoja na kwamba ilikuwa na uwakilishi wa vyama vyote vikuu!

Hapa kwetu mambo yako hovyo kabisa na tunaostahili kulalama ni sisi wananchi. Hawa wanasiasa wetu wa upinzani wako hovyo maana ndo wamekuwa Bungeni miaka yote wakifanya show off. Wanalalama ili sisi wananchi tuwasaidie kurudi Bungeni, wakifika hatuwasikii wakitia presha juu ya mambo ya msingi. Leo hii tusingekuwa na mkuu wa mkoa au wilaya anayejihusisha na siasa za CCM. Wako kimya wakihangaikia kusikika Bungeni kwa matusi nk. ili uchaguzi ukifika warudishwe.

Mtu kama Lissu nilitegemea apambane na mambo kama hayo na jumuiya ya kimataifa, badala yake yeye ana mwanasheria anayemlinda, yeye akiwa nje ya nchi; zoezi la kijinga kuliko yeye mwenyewe anavyoamini. Yaani ashinde wakati majimbo yako chini ya wakurugenzi, usalama uko chini ya mkuu wa wilaya, na mkuu wa wilaya ni mkuu wa usalama wilayani? Halafu unategemea vitisho na kujivuna eti tutawapeleka mahakamani! Trash!
Lissu hakuwepo kwa sehemu kubwa ya awamu hii na wa kulaumu sio yeye bali ni waliobaki nyuma ndio walifanya kosa kubwa ambalo sasa linawagharimu kuhusiana na tume ya uchaguzi.

Kwa vyovyote vile baada ya uchaguzi mkakati sasa lazima uwe ni katiba mpya itakayotoa fursa ya nchi kupata pia na tume huru ya uchaguzi ili tuachane na chaguzi za kihuni na hata ikilazimu nchi kuwekewa vikwazo, tuwekewe tu. It's worth it.
 
Lissu hakuwepo kwa sehemu kubwa ya awamu hii na wa kulaumu sio yeye bali ni waliobaki nyuma ndio walifanya kosa kubwa ambalo sasa linawagharimu kuhusiana na tume ya uchaguzi.

Kwa vyovyote vile baada ya uchaguzi mkakati sasa lazima uwe ni katiba mpya itakayotoa fursa ya nchi kupata pia na tume huru ya uchaguzi ili tuachane na chaguzi za kihuni na hata ikilazimu nchi kuwekewa vikwazo, tuwekewe tu. It's worth it.
Binafsi nayaona malalamiko ya Lissu kama kilio cha mtoto. Yeye ni mwanasheria anayejivunia kazi yake. Anakuja akielewa mazingira ya uchaguzi halafu anaanza kulalamikia mfumo. Hata kama ni mchezo lazima uhakikishe sheria na vigezo vyote viko sawa ndo uingie uwanjani.

Haikuwa lazima kujiingiza kwenye kampeni, ukitegemea utatia presha uwe ni wa haki wakati set-up haiko kwenye haki. Wenzake wako majimboni wanakoweza bahatisha, yeye anahangaikia kitu asichoweza kupata. Hata ashangiliwe namna gani, ataishia kuumiza koo tu na kutukana, maana naye bahati mbaya sana hajui kuchagua maneno ya jukwaani. Lazima atapigwa tu!
 
Hao jamaa wana demokrasia sana, Tanzania hii nani anaweza kuongea hivyo tofauti na Lissu.

Hayo maswala anayoongelea huyo mbunge mbona ni yale yale ya ufisadi na hata huku tunayo, mtu anatwaa pesa za umma kwenda kujengea uwanja wa ndege kwao na ukiuliza unaletewa wasiojulikana.

Kama Kenya ni sawa na Colombia je Tanzania ina tofauti gani huku kuna watu hadi leo haijulikani walipo.

Yanayofanyika katika mashirika kama Air Tanzania hakuna anayejua na hata kwenye ujenzi wa bwawa la Stieglar Gorge na hata reli ya Standard Gauge, tunaambiwa ni siri ya Magufuli na mpwa wake. Hamna kitu hapo.
Munapenda kukataa kufikiri tu. Anayejenga uwanja wa ndege kwao unalinganisha na anayepora ardhi yeye na familia yake? Linagnisha na waliojichukulia viwanda, walioamua kuunda makampuni ya usafirishaji na mafuta, hao akina GSM, nk. hawa wmaetumia pesa za umma kwa faida na familia zao.
 
Munapenda kukataa kufikiri tu. Anayejenga uwanja wa ndege kwao unalinganisha na anayepora ardhi yeye na familia yake? Linagnisha na waliojichukulia viwanda, walioamua kuunda makampuni ya usafirishaji na mafuta, hao akina GSM, nk. hawa wmaetumia pesa za umma kwa faida na familia zao.
Wote wahalifu tu, acha unafiki.
 
Pale Kenya sasa hivi ni kama hamna mkubwa! Kila mtu ni kambare! Wamejaa ukabila, hayo ndio waliyoendelea hakuna kingine.

Fikiria uchaguzi bado miaka 2 lakini ofisi ya Rais Kenyata ina mgogoro wa kugombea madaraka ya 2022.

Inanikumbusha kati Kikwete na Lowassa kabla Kikwete hajamaliza muda wake
 
kenya kuna binadamu kamili wanaojitambua,huku kwetu tuna binadamu sokwe
Kweli kabisa mkuu, naona hapa walikuwa bado masokwe kama sisi!
images.jpg
download.jpg
 
Yawezekana kabisa sisi Tanzania ndio tukawa tumebaki na mfumo huu wa ki analogia wa Tume yetu ya uchaguzi duniani. Yaani Rais anateua ma-kamishina wote wa tume, afu yeye aliyewateua ni mgombea... patam hapo.
 
Sawa lakini mimi pia nimeonyesha nawao pia wanachangamoto.
Tume huru itakuja tu kwa hapa Tanzania ni swala la muda tu.
ila kwa Kenya siasa za ukabila wanalo na linawatafuna sana.
Iko hivi, kwanza niseme nakuelewa sana mkuu but nilitaka nikwambie hivi, suala la ukabila ni mtambuka na ni suala la individuals, ni gumu sana kuliondoa, kwetu pia lipo tena sana. Refer lile tukio la uvunjwaji wa nyumba za Morogoro road mwanzoni mwa awamu hi na kilicho sitishwa uvunjwaji wa nyumba za namna hiyo hiyo kule Mwanza, unaikumbuka ile statement iliozuia nyumba za Mwanza zisivunjwe? Ukabila. Suala la tume HURU ni suala la watu waliokwenda shuleni tu na kujua tu hivi, "kulingana na elimu yetu, hili na sawa na hili sio sawa" but ukabila upo kwenye DAMU, hautoki. Jaribu kukaa karibu na Mjaluo, Mhaya, Mnyakyusa na Mchaga uone, hata angesoma vipi, hi kitu haitoki. Au jaribu kua karibu na Watutsi uone, hawa ukabila upo kwenye DAMU, kuutoa ni ngumu sana
 
Hatukusikia kwamba kuna wagombea wa vyama fulani walioenguliwa wasigombee wala hatukusikia mawakala wamepigwa na kuondolewa vituoni.

Pia hatukuona ofisi za vyama zikivamiwa na vyombo vya dola ili kupora makompyuta na kufungwa kwa nguvu ili wasijumlishe matokeo wala hatuona wakuu wa mapolisi wakiwambia wagombea wa vyama fulani kwamba hamuwezi kushinda.

Pia hatukuona vyombo vya habari vikilazimishwa kuandika habari za chama fulani peke yake wala hatukuona mapolisi wakitorosha masanduku ya kura kutoka kwenye vituo vya kupigia kura wala hatukuona tume ya uchaguzi ikiwapiga marufuku wagombea fulani kuendelea na kampeni kwa muda fulani.

Tanzania bado sana kuja kufanya uchunguzi wenye hadhi ya kuitwa uchaguzi bado tuko kwenye uhuni tu unafanywa na ccm na vyombo vyake vya dola.
 
Hii nchi yetu TZ ina wasomi wa ajabu sana! Sasa unaleta vyama vingi lakini katiba inabakia ileile ya chama kimoja halafu utegemee uchaguzi uwe huru na haki? Tatizo liko kwa yule mwenye ufunguo wa chumba chenye KEKI. Upinzani lazima uchonge ufunguo mbadala na utumie mbinu ya kuweza kukifikia kitasa chenyewe "KATIBA MPYA"; hata ikibidi wapitie dirishani!
 
Hii nchi yetu TZ ina wasomi wa ajabu sana! Sasa unaleta vyama vingi lakini katiba inabakia ileile ya chama kimoja halafu utegemee uchaguzi uwe huru na haki? Tatizo liko kwa yule mwenye ufunguo wa chumba chenye KEKI. Upinzani lazima uchonge ufunguo mbadala na utumie mbinu ya kuweza kukifikia kitasa chenyewe "KATIBA MPYA"; hata ikibidi wapitie dirishani!

CCM mnaanza kutuchokonoa, mna nini nyie, yaani mshaona uchaguzi wa juzi wa Kenya, mnaanza kutaka na sisi tufanye au tuwe na Tume ya Uchaguzi kama ya Kenya.. Ujue kila nchi ina mambo yake, shukuruni sana CCM imesimama imara labda leo ungekuta nchi yetu ni kama Congo, Rwanda, Sudan, Somalia, Kenya ya ukabila na umwagaji damu ya 2007, Egypt, Libya au Syria au Central Africa, etc, nchi nyingi hali ni mbaya sana sbb vyama vyao vimeua nchi zao.

Leo umekaa na una furaha na amani, unafanya biashara zako utakavyo, huduma kadhaa serikali ya CCM inapatia wananchi wake, ila yote huoni, nyie mnaangalia Tume Huru ya Uchaguzi, hivi mlijua Tume huru ya Uchaguzi ndio kila kitu, ndio maendeleo ya yetu, ndio mwarobaini wa matatizo yetu? Jibu ni hapana kabisa.

So narudia ishukuru sana kila siku CCM, ukiweza fika nchi mbalimbali Africa hali ni mbaya sana sbb ya uongozi mbaya sana wa mtutu wa bunduki, wananchi wao wanaishi kama wanyama, kisa amani haipo na utawala ni wa kidikteta kabisa, narudia tena sbb hujui tu ndio maana unaandika, ishukuru daima na milele CCM.
 
Back
Top Bottom