Video: Wanajeshi wa Urusi wapokea kichapo kwa kugoma kwenda kupigana Ukraine

Unaambiwa heri uchomwe kisu au unywe sumu unaweza wahishwa hospital ukapona ila sio HIMARS. Hiki chombo kimebadili taswira nzima ya vita.
HIMARS na kile kikosi cha Drone zinawachanganya sana Warusi. Ndo maana wamehamia kwenye vita ya ballistic missile wanazorusha kutokea Baharini na huko Urusi.

Mpaka wanatumia janja ya kurusha fake missile nyingi ili ku overwhelm air defense systems za ukraine.
 
Heri ya kuachia ngazi ya Urais lakini sio kwa hiko anachofanya kugharimu taifa zima.
Madikiteta wote duniani wanaangalia maslahi yao siyo ya Taifa. Putin hawezi kuachia madaraka hata angebaki yeye na kikundi chake.

Tuliona yaliyofanywa na Dikteta uchwara wetu. Alikuwa tayari kupiga risasi watu, kuwaua, kuwatupa baharini, kunyang'Anya watu mali zao na maovu mengine, kisa wanamkosoa au kupinga mambo ya kijinga aliyokuwa anafanya. Sembuse Dikteta kamili (Putin) unatarajia aachie madaraka.
 
Mbaya zaidi adui yako ana moto balaa, ana mashine za kisasa. Hiyo HIMARS unaambiwa ni balaa tupu, bado US hajapeleka F14, F18 au F35 huko.
Ipelekwe F35 Putin si anaharisha usiku kucha siku akipata hiyo taarifa.

ukiimarishwa ulinzi wa anga la Ukraine vita inaisha. Mkakati wa NATO na USA sasa hivi ni kuimarisha ulinzi wa anga. Maana kwa frontline Urusi alishatepeta. NASAMS na IRIS-T na long range missile za HIMARS zikifika zote zilizoahidiwa mchezo unaisha.
 
You nailed it
 
Kwann ukafe kwa ujinga wa putin si apeleke watoto wake wakapigane. Ufe watoto wako atalea nani. Sometimes vita huwa ni matakwa ya kiongozi mpumbavu na sio uhitaji wa nchi.
Bila shaka hujawahi kupitia hata jkt. Oh sawa nikueleweshe. Jeshi huapa kulinda katiba, kumlinda Rais, na kulinda ardhi na maslahi ya taifa popote. Pia huapa kupokea amri kutoka kwa rais wao muda wote wa utumishi.
Ni kosa la jinai kukataa kupigana inapotolewa amri na mkuu wa nchi. Eti ukatae kupigana kisa familia yako ataitunza Nani ukifa?
Nb.
Kijeshi Hili lipo kote kukataa kupigana kosa lake Ni shaba iwe ulaya, Marekani au Iran.
 

Sio kila amri unatii, inaruhusiwa kughairi kama amri ina ukichaa, leo hii Putin aibuke ghafla atoe amri ya kushambulia Ulaya kwa manyuklia, nakuhakikishia atapigwa risasi na mejenerali wake maana wananajua kitakachofata ni Urusi kufutwa kwenye uso wa dunia.
 
Kama hujui jambo Bora unyamaze. Si kila amri zinazotolewa na Rais kwa majeshi lazima zitekelezwe. Rais akikurupuka bila kufuata utaratibu hawawezi kutekeleza amri yake. Rais hutoa amri kwa majeshi kwa utaratibu maalum, ni baada ya Baraza la usalama kuidhinisha ndo atatoa amri ya hali ya hatari au vita. Mambo mengine huitaji kuridhiwa na bunge ndo utekelezaji wake uanze.

At individual capacity mwanajeshi anaweza kukataa kwenda vitani na akatoa sababu zake za msingi. Hawezi kupigwa shaba, bali utapelekwa court marshal na utahukumiwa kwa mujibu wa taratibu za kijeshi ikiwemo kufukuzwa kazi na siyo kuuawa kama unavyodai.

Makosa ya kupigwa risasi labda kama unataka kupindua nchi, na yanayoendana na hayo.
 

Na ndio maana Putin amekua akijificha kwenye mgongo wa special operation, maana akiita jina "full invasion", itamletea matatizo ndani ya nchi.
 
Na ndio maana Putin amekua akijificha kwenye mgongo wa special operation, maana akiita jina "full invasion", itamletea matatizo ndani ya nchi.
Maana yake kwenye Baraza la usalama au waliudanganya umma kuwa ni special military operation ya siku 3 tu, siyo vita.

Waliudanganya umma kuwa special military operation ni kwa ajili ya Donetsk na Luhansk ambazo zilijitangaza kuwa ni Jamhuri.
 
Kwa mara ya kwanza nimekugongea like. Kumbe ukivua gamba you are so objective!
 
Ulivyojibu ndo umezidi kujiexpose kuwa una fikra mgando.
 
Mashabiki wa putin humu ndani mwanzo wa vita walisema HIMARS si kitu, wakasema haiwezi kukomboa hata nusu heka.

Leo hii kinachoendelea huko kinatisha.
 
Tuna upeo unaofanana. Licha ya kumpamba kooote Jiwe, hakuna Rais nliyemuona mkatili na asiye na akili hata chembe kama jamaa.
 
Na hawawezi kuzipeleka wale, walisema wanataka kuona vita ikichukua muda mrefu zaidi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…