Video ya Rais wa Sudan Kusini akitokwa na haja ndogo yazua maswali kuhusu afya za viongozi

Video ya Rais wa Sudan Kusini akitokwa na haja ndogo yazua maswali kuhusu afya za viongozi

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Katika tukio lisilo la kawaida, Rais wa Sudan Kusini, Salva Kiir mwenye miaka 71 ameonekana akitokwa na haja ndogo wakati wa hafla ya Kitaifa na wimbo wa Taifa ukipigwa. Kitendo hicho kinaibua maswali kuhusu hali za kiafya za viongozi wengi duniani kuendelea kukaa madarakani hata baada ya umri wao kuwa mkubwa na wengine wakiwa na afya zisizoridhisha.

Mwaka huu 2022, pia mgombea wa Urais nchini Nigeria Bola Ahmed Adekunle Tinubu mwenye miaka 70 alionekana akiwa na mfuko maalumu wa kuhifadhia mkojo wakati wa mchakato wa kuanza kampeni hali iliyopelekea wananchi kuhoji kuhusu afya yake na majukumu anayotaka kugombea.

 
Kuna watu wanapenda ku ng'ang'ania madaraka

Unakuta umri ushaenda ila yeye yumo, afya ni mgogoro yeye yumo

Hatu huyu wakwetu SAA 100 mwaka 2025 apumzike tu, kwani mpaka kufikia Januari 27 mwaka 2025 atakuwa na miaka 65 ukiongeza na miaka 5 ya awamu ya pili anayo ing'ang'ania kuwa atagombea atatoka akiwa na miaka 70

Na pia kama sasa nchi ni ngumu kwake ndo ataiweza kweli katika umri wa miaka 65 hadi 70 (umri wa ubibi)
 
Back
Top Bottom