Vigezo gani anavitumia DC wa wilaya ya Ubungo, Hassan Bomboko kuvamia kumbi za starehe na nyumba za wageni kukamata watu anaodai ni makahaba?

Shida anataka kutumia approach ya Makonda ya IRON HAND.. yule jamaa ana kipaji na nyota ya kipekee.. na ni MWANASAYANSI mzuri sana wa SIASA anajua wapi pa kupiga wapi pa kushika.

Makonda ukimfatilia ishu kama hizi wala hana huo muda, mfano watu walimbeza kuwakumbatia WADUDU.. sijui kama naeleweka hapa.

Leo RAIS katoa dongo ktk hotuba yake kawasema hao Ma- RC na DC.
 
NDIO TATIZO LA VYEO VYA KUPEANA BAADA YA KUPIGA KAZI KWA AJILI YA KUIJENGA CV YAKO, WEWE UNA FANYA KAZI ILI KAMERA ZIKUONE SASA KWA AKILI YAKE AMEWAKAMATA ATAWASHITAKI KWA SHERIA IPI?

Tanzania hakuna sheria inazuia ukahaba, isipokuwa sheria inakataza mapato yatokanayo na ukahaba.
 
Siungi mkono ukahaba lakii jamani anachokifanya huyu kijana kinatengeneza udhalilishaji wa hali ya juu..Viongozi mliopo juu yake muonnyeni huju mtu anawaharibia.Asitafute Kiki za Bw. Makonda.Makonda ana jihusisha na issues ambazo ninawagusa wananchi zikiwemo dhuluma na manyanyaso.Na ndiyo maana kila anapofika anapokelewa kwa shangwe na nderemo..
Viongozi aina ya ya dc wa Ubungo huwa wanapatikanaje ?.RC Chalamila huu ni Mkoa wako .Pamoja na ucheshi wako lakini Mkoa unapakwa masizi.
 
Watajulia wapi hayo ndugu wakati hao ni vijana wa mwendo Kasi mama anatuletea? Wakati mwingine unajiuliza hivi huyu nae analipwa mshahara Kwa Kodi za wananchi wakiwemo na hao anaowashutumu ni makahaba na anajiona kabisa Yuko kazini? Sijui Hawa viongozi wa sampuli hii wanaokotwa wapi
 
Hivi vile vienjio vinavyotetea haki za binadamu na haki za wanawake vimepotelea wapi kwenye hili? Mbona Kwa ishu ya makonda walikurupuka na makamera na matamko hili nalo hawaoni? Au halina maslahi?
 
Nikiwa mvulana nimemaliza form 6 natoka zangu club kufurahi nikakutana na defenda wakanizoea eti mzululaji nikawauliza uzulalaji maana Nini, wakabaki wanaduwaa wakaniachia haraka.
Tatizo police na hawa wateule elimu ni ndogo sana wanafanya mambo ya aibu hadi unajiuliza hivi matatizo yote hapo ubungo DC ameshindwa ku control tatizo la taka anahangaika na mtu timamu aliyeamua kuchanua mapaja Kwa hiari yake
 
Waliofungua lodges na bar nao wakafanye biashara gani? Unaenda kukamata malaya barabarani halafu unamsingizia mwenye bar kuwa ndiye anayewafuga? Does it make sense
Waafrica tupo kama mbuni tunaficha kichwa mchangani wakati matako yako nje!

Takwimu za TACAIDS zinaonyesha maambukizi ya virus vya HIV vinaonfezeka kwa kasi sana! Hasa kwa vijana wadogo ambao ndio nguvu kazi ya taifa! Na hao malaya wanaojiuza awachagui rika wanauzia hata watoto wadogo!!

Na pia gest nyingi zimegeuzwa kama ofisi za hao malaya! Wanalipa vyumba wanavitumia kwa ajili ya kufanyia uasherati!

Hivi mnataka tuwe na taifa la namna gani? Ambalo vijana wengi ndio victim wa ugonjwa wa ukimwi?
 
Tena naona serikali imechelewa sana kuchukua hatua.
 
Guests house nyingi zina condom za bure
 
Wangekuwa wanapiga doria halmashauri kucheki Kama Kodi zetu zunatumika sawa. Ile report ya cag ingekuwa unafuatiliwa Ila wao wamekaa sijui wanataka wapate hongo
Viko vyombo kwa ajili ya hiyo kazi lakin si sababu ya kuignore matatizo mengine. Serikali ni omnipresent
 
Anataka watu wakabake watoto wa shule. Hajui kwamba hao makahaba wanasaidia kupunguza ubakaji
 
Hivi vyeo vilikuwa vya kikoloni, katiba mbovu. Hakuna vetting yoyote ya maana ni kuteua TU hata wehu huko mtaani!
 
Anataka watu wakabake watoto wa shule. Hajui kwamba hao makahaba wanasaidia kupunguza ubakaji

Mwambie ukweli huyu pimbi hajielewi na hajui chochote! Mtoto wake akibakwa akili zitamjia sawasawa!
 
Hata mimi nimeiona hiyo video naona hili jambo halijakaa poa, swali fikirishi je nikweli kwamba hakuna mtu ambaye anaweza akalala na mke wake wa ndoa kwenye nyumba ya kulala wageni?, Swali jingine je wale wanao tumia magari kufanya ngono hawaoni? La mwisho je yeye hajwawahi kwenda na pisi Kali kwenye vyumba vya kulala wageni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…