Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 2,833
- 1,301
VIJANA KUNUFAIKA NA FURSA ZA MAFUNZO YA UZOEFU WA KAZI NA UANAGENZI.
Katibu wa Uhamasishaji na Chipukizi Taifa Cde. Victoria Mwanziva amefika Wizara ya Vijana, Kazi na Ajira na kukutana na Mkurugenzi wa Ajira na ukuzaji ujuzi Ndugu. Ally Msaki;
Lengo likiwa ni kuona namna gani vijana wananufaika na mipango mikakati ya serikali kwa vijana. Maeneo yaliyozungumziwa ni;
- Mafunzo ya Uzoefu ya kazi
- Internship Training
- Apprenticeship training, Uanagenzi (Mafunzo ya Uanagenzi)
- Recognition of Prior Learning Skills
Katibu wa Uhamasishaji na Chipukizi UVCCM Taifa pia ametembelea Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na kukutana na Naibu Waziri Mhe Deogratius Ndejembi lengo likiwa ni kutathimini kwa pamoja nafasi ya kijana katika utumishi wa Umma.