Vijana Msijidanganye: Ukiamua kujiajiri ni lazima uwe na nidhamu ya kazi (Self-Discipline) mara kumi (10) zaidi ya ulivyoajiriwa ndio utafanikiwa

Vijana Msijidanganye: Ukiamua kujiajiri ni lazima uwe na nidhamu ya kazi (Self-Discipline) mara kumi (10) zaidi ya ulivyoajiriwa ndio utafanikiwa

Kujiajiri Kuna changamoto nyingi kuliko kuajiriwa...wewe angalia hata maprofessor wengi wa TZ wanavyogombania vyeo huko siasani
Unafikiri hawajui Kuna kujiajiri??
Mie kilichonishinda kwenye kujiajiri ni ushirikina tu mkuu....Mambo ya kwenda kwa sangoma kuchanjwa chale za makalio siyawezi kwa kweli[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Namkumbuka rafikk yangu Alie nifundisha nidhamu ya kujiajiri huyu mwamba siku nyingine anafunga ofisi saa 6 usiku na anaamka saa 12 kamili ni kazi kazi, nilipiga nae kazi muda mfupi lakin nikawa nawaonea wivu walio ajiriwa wanapata muda wa kuinjoy na familia ila sisi wajuba bila kujinyima uhuru hakuna kitu tunaingiza...
Hivyo naunga hoja kuwa kujiajiri siyo kuwa huru la sivyo biashara itakushinda
 
Kweli kabisa ndugu Infantry Soldier kujiajiri ni kama upo vitani na inatakiwa ushinde vita.

Bila nidhamu kujiajiri kutakushinda. Kunaa kukata tamaa, kurudishwa nyuma, kuaibika, kudhihakiwa mwanzoni aka vitani. Hadi uje kufanikiwa umepigana sana na viunzi.
Chochote kinataka self discipline eg. Hata kula
 
Mambo ya kwenda kwa sangoma kuchanjwa chale za makalio siyawezi kwa kweli
emoji1787.png
emoji1787.png
emoji1787.png
Hahahahahaaaa mkuu una vituko sana inaonekana. Nimejikuta nacheka peke yangu ndani ya daladala...
 
Namkumbuka rafikk yangu Alie nifundisha nidhamu ya kujiajiri huyu mwamba siku nyingine anafunga ofisi saa 6 usiku na anaamka saa 12 kamili ni kazi kazi, nilipiga nae kazi muda mfupi lakin nikawa nawaonea wivu walio ajiriwa wanapata muda wa kuinjoy na familia ila sisi wajuba bila kujinyima uhuru hakuna kitu tunaingiza...
Hivyo naunga hoja kuwa kujiajiri siyo kuwa huru la sivyo biashara itakushinda
Ni sheedah yaan hasa mishe ziyumbe kdgo
 
Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa jamiiforums.

Ndugu zangu vijana msijidanganye;

Ukiamua kujiajiri ni lazima uwe na nidhamu ya kazi (Self-Discipline) mara kumi (10) zaidi ya ulivyoajiriwa ndio utafanikiwa.

Nimeamua kutoa ushauri huu kwa maana kwamba, juzi nilikuwa nimepanda daladala ya kutoka Mnazi Mmoja huku Dar nikawa ninaelekea Kigogo kwenda kumsalimia rafiki yangu mmoja hivi, classmate wa Secondary School, aliyefiwa na baba yake weeks chache zilizopita.

Sasa mimi nilikuwa nimekaa siti ile ya nyuma kabisa maeneo ya dirishani kwa maana ndio pande zangu hizo ninazopendaga mimi, then kiti kinachofuata mbele yangu walikuwa wamekaa wasichana/wadada wawili ambao wanaonekana ni University graduates wa miaka ya hivi karibuni (mimi ni University Graduate wa miaka 11 iliyopita) alafu walikuwa wametoka kazini ila kuna changamoto moja ilikuwa imewakera wakawa wanapiga story kwa sauti kidogo bila kujua kama mimi ninawasikia.

Wale akina dada wakawa wanaambizana kuwa ni bora wajiajiri tu kwa maana kuajiriwa ni utumwa. Ukijiajiri unakuwa na nafasi kubwa sana ya kujitawala na unakuwa free sana kujipangia mambo yako uingie kazini saa ngapi na utoke muda gani tofauti na kuajiriwa katika ofisi za watu wengine ambao wanakupangia kila kitu cha kufanya.

Mimi ninaomba kuchukua wasaa huu kutuma salamu zangu za pole sana kwa vijana wenye akili kama za hawa akina dada wanaofikiri kwamba kujiajiri sio utumwa.

Ndugu zangu kujiajiri ni utumwa na kama unataka kuacha kazi ya kuajiriwa na kutaka kujiajiri kwa kudhani kwamba ukifungua biashara yako hautakiwi kuwa na nidhamu ya kazi, basi ni bora hiyo pesa uende uka-bet kwa mhindi labda zali linaweza kuwa lako ukafanikiwa lakini usifungue biashara yako.

Nidhamu ya kazi kwa aliyeajiriwa ni ile ile kwa hata wewe unayetaka kujiajiri. Usifikiri eti kwa kuwa wewe ndio boss basi ukitaka kuingia kazini hata saa 5 asubuhi basi sawa tu kwa kuwa biashara yako. Hapana ndugu yangu. Unapojiajiri wewe ndiye unayepaswa kuonesha nidhamu ya hali ya juu sana kazini ili uwe mfano wa kuigwa kwa wafanya kazi wako.

Wewe kama top boss ndiye unayepaswa kuwa panctual, yaaani kama reporting time ni saa 2 asubuhi, basi wewe ikifika tu saa 1:30, upo kazini. Kama hairuhusiwi kutupa takataka hata karatasi sakafuni boss ndiye anayepaswa kuwa wa kwanza kuonesha hilo na sio vinginevyo

Kijana kama unataka kuacha kuajiriwa na kuanza biashara yako kwa kufikiri eti ukiwa na chako ndio unapaswa kukosa nidhamu ya kazi, you are wrong na tafuta mambo mengine ya kufanya. Nakushauri nenda hata uka-bet. Yangu mimi ni hayo tu.

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.

Ni kweli, ila kujiajiri kuna uwezo, if you do more it will pay more and if smart, eventually hautakuwa busy maana watu watakuwa wanakufanyia and so less work!

Do not challenge, I speak from experience!
 
Nina uzoefu so sio propaganda, mara ya kwanza is very consuming but as time goes I nashuka!

E:g Mimi naweza Anza kazi saa 4 usiku mpaka 8, then nalala, Kesho naamka saa 5, then free, mfanyakazi hayupo flexible!

Do not challenge, I speak from experience!
Mbona kama vile umejihami na hili neno Do not challenge katika ile comment yako number 69?

Au ninaonekama kama vile ni mtu mwenye mentality ya kupenda kubishana bishana sana?
 
Back
Top Bottom